Thursday, February 09, 2017

TUNDU LISSU AGOMA KULA

Wakati Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu akigoma kula hadi afikishwe mahakamani, wakili wake amepeleka maombi Mahakama Kuu kuomba apewe dhamana baada ya polisi kuendelea kumshikilia kwa siku ya tatu.

Wakili wa mbunge huyo, Peter Kibatala alisema mteja wake amefikia hatua hiyo, baada ya Jeshi la Polisi linalomshikilia kumnyima dhamana bila sababu.

“Hakuna sababu za msingi za kumnyima dhamana na tangu jana Lissu hajala na amesema hatakula hadi afikishwe mahakamani,” alisema Kibatala na kuongeza:

“Kosa analodaiwa kulifanya lilifanyika Januari 4 na hadi Februari 6 ni mwezi, kama ni muda wa kuchunguza kosa hata hati ya mashtaka ingekuwa tayari,” alisema Kibatala.

Alisema mteja wao (Lissu) analalamikia kuanzia ukamatwaji wake ulipoanza, alipokamatwa eneo la Bunge bila Spika kuwa na taarifa.

Kibatala alisema polisi waliokwenda kumkamata aliwatambua njiani na alikamatwa bila kuwapo kibali cha kukamata (arrest warrant).

MAREKANI KUMSAKA MTOTO WA OSAMA BIN LADEN

Marekani imemtaja Hamza ambaye ni mtoto wa kiume wa Osama Bin Laden katika orodha ya Magaidi.

Taarifa kutoka wizara ya ulinzi zinasema Hamza Bin Laden akiwa katika umri wa miaka ishirini amekuwa kiongozi makini wa kundi la Al Qaeda ambao ni wapiganaji wa kundi lililoanzishwa na baba yake.

Taarifa zinasema amekuwa makini katika suala hilo kwa kufuata nyayo za baba yake kwa kujiunga na jihadi na kusambaza ujumbe wa sauti kwa niaba ya kundi la Al Qaeda na kuchochea mashambulizi dhidi ya nchi za Magharibi.

Kwa sasa Atazuiliwa kufanya biashara na wananchi wa Marekani na mali zake zitataifishwa.

Kiongozi mkuu wa usalama wa kundi la Al Qaeda Ibrahim al-Banna ametajwa katika orodha hiyo pia.

Marekani itatoa ofa ya dola Million tano kwa atakayesadia kukamatwa kwa al-Banna.

Wednesday, February 08, 2017

MNYAA ATIMULIWA UANACHAMA WA CUF

Chama cha Wananchi (CUF) kimemtimua uanachama Mohamed Habibu Mnyaa, huku mwenyewe akidai bado ni mwanachama halali.

Mnyaa amefukuzwa na mkutano mkuu wa tawi la Chanjaani, Jimbo la Mkoani kisiwani Pemba, uliohudhuriwa na wajumbe 112 kati ya 113.

Taarifa iliyotolewa na Katibu wa tawi la Chanjaani, Kombo Mohamed Maalim, ilisema Mnyaa alifukuzwa kutokana na kukiuka katiba ya chama hicho Ibara ya 12 (6)(7)(16).

Alisema miongoni mwa mambo aliyofanya ni kuwa na mwenendo usiofaa wa kuwagawa wanachama, kueneza taarifa za upotoshaji dhidi ya viongozi na chama, kufanya vitendo vya hujuma za kutaka kukidhoofisha chama, kudharau na kushindwa kuhudhuria na kutoa ushirikiano kwa tawi lake kila alipotakiwa kufanya hivyo.

Akizungumzia hatua hiyo, Mnyaa ambaye amewahi kuwa mbunge wa Mkanyageni kwa vipindi viwili mwaka 2005-2015 alisema hukumu ya kufukuzwa kwake imechukuliwa katika tawi ambalo siyo lake, kwa kuwa alishalihama tangu mwaka jana.

WAFANYABIASHARA WA POMBE ZA KIENYEJI WATAKIWA KUWA NA LESENI

Wafanyabiashara wa Pombe za Kienyeji wanatakiwa kuwa na leseni ya kufanya biashara hiyo ambayo hutolewa na Halmashauri.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jafo ameyasema hayo, Mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Najma Giga juu ya Serikali imejipangaje kukabiliana na tatizo la ulevi wa kupita kiasi kwa pombe za kienyeji pamoja na sheria ya vileo ya mwaka 1969 kuwa ya zamani hivyo kutokidhi mabadiliko ya hali halisi ya vileo.

“Pombe za kienyeji zimeanishwa katika kifungu cha 2 cha tafsiri katika Sheria ya Vileo, Sura ya 77 ambapo kwa mujibu wa sheria hiyo, wafanyabiashara wote wanatakiwa kuwa na leseni ambayo inatolewa na Halmashauri,” alifafanua Jafo.

MBUNGE WA CCM AHOJI 'UTAJIRI' WA MAKONDA BUNGENI

Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Kasheku ameendeleza ‘vita’ yake dhidi ya Paul Makonda, akisema yupo tayari kusaidia vyombo vya dola kukamata vigogo wa dawa za kulevya na kuhoji ukimya wa mawaziri watatu dhidi ya kile alichodai utajiri wa mkuu huyo wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Awali, Kasheku ambaye ni maarufu kwa jina la Msukuma, alitoa tuhuma dhidi ya Makonda juzi, alipotaka kujua wafadhili wa safari za mkuu huyo wa mkoa nje ya nchi na sababu za kubagua watuhumiwa wa biashara ya dawa za kulevya kwa kutaja baadhi na kuwaacha wengine, huku mawaziri wakisita kuchukua hatua.

Alitoa tuhuma hizo bungeni baada ya Makonda kuagiza watu 12, wakiwemo wasanii maarufu wa muziki na filamu, kuripoti Kituo Kikuu cha Polisi cha Dar es Salaam, akiwatuhumu kuhusika na utumiaji au biashara ya dawa za kulevya.

Jana, Msukuma aliibuka na hoja nzito zaidi akihoji sababu za mawaziri kutochukua hatua na pia kutaja baadhi ya mali alizopata Makonda katika kipindi kifupi alichoshika madaraka ya mkuu wa mkoa baada ya kuwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni pia kwa muda mfupi.

Mbunge huyo alitoa tuhuma hizo nzito muda mfupi baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu, wakati alipotumia kanuni ya 68 (7) kuomba mwongozo kutoka kwa Naibu Spika, Tulia Ackson.

WAANDISHI WA HABARI WAKAMATWA, WAHOJIWA NA POLISI

Waandishi wa habari wawili jana walikamatwa na kuhojiwa katika Kituo cha Polisi cha Usa River mkoani Arusha, huku aliyetoa amri ya kukamatwa kwao akizua utata.

Wakati taarifa za awali zikidai ni amri ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti, yeye alikana kuhusika na agizo hilo.

Waliokamatwa ni Bahati Chume mwandishi wa kujitegemea wa gazeti la Mwananchi Mkoa wa Kilimanjaro na Dorine Alois kutoka kituo cha Sunrise Radio cha jijini Arusha.

Waandishi hao walikamatwa walipokuwa wakifuatilia habari ya mgogoro kwenye machimbo ya kokoto katika Kijiji cha Kolila mpakani mwa wilaya za Arumeru na Hai.

Mnyeti alipoulizwa alikana kutoa amri hiyo akisema yeye hana ugomvi na waandishi wa habari.

Saturday, February 04, 2017

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI FEBRUARI 04, 2017 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


Tu-follow instagram @jambotz. Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz.

TAZAMA PICHA 30 BORA ZA OBAMA KATI YA MILLION 2 ALIZOPIGWA KATIKA KIPINDI CHA MIAKA NANE


Pete Souza katika kipindi cha miaka 8 amempiga picha zaidi ya million 2 rais mstaafu wa Marekani. Pete ambae alikuwa mpiga picha wa familia ya Obama aliambatana nae rais huyo kwa kipindi chote cha miaka nane ya uongozi wake.
Tu-follow instagram @jambotz. Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz.

Sunday, January 29, 2017

TAZAMA PICHA ZA ZOEZI LA UOKOAJI KWA WALIOFUKIWA NA KIFUSI GEITA.

Wachimbaji wote 15 waliofukiwa na kifusi katika mgodi wa RZ Geita wameokolewa asubuhi ya leo. Jambo Tz inawapa pole na kuwaombea wapone haraka ndugu wote waliokumbwa na ajali hii.

MBUNGE APENDEKEZA BIMA KWA WANYWAJI WA POMBE

Mbunge mmoja nchini Kenya amewasilisha mswada bungeni kuzishinikiza kampuni zinazouza pombe kutoa asilimia ndogo ya faida yao kuwadhamini wanywaji ambao wataathirika na pombe hiyo.

Mbunge Gideon Mwiti anataka watengenezaji wa pombe kutoa kati ya asilimia 5 na 10 ya mapato wanayopata kwa kampuni za bima ili kuwafidia watu ambao wataathirika na pombe ama hata kupata ajali kwa kuwa walevi kulingana na gazeti la Daily Nation nchini humo.

Mswada huo pia unapendekeza kwamba iwapo mtu atafariki kutokana na athari za kunywa pombe ,kampuni hizo za pombe zilazimike kufidia familia yake.

Bw Mwiti pia amezishutumu kampuni za pombe kwa kushindwa kukuza pombe zisizo na madhara kwa afya, kwa mujibu wa ripoti hiyo.

Thursday, January 26, 2017

WACHIMBAJI 14 WAFUNIKWA NA KIFUSI GEITA

Picha na maktaba.

Wachimbaji wadogo 14 kutoka mgodi wa dhahabu wa RZ uliopo Kata ya Nyarugusu mkoani Geita wamefukiwa na kifusi cha udongo baada ya kutokea maporomoko kwenye moja ya shimo walilokuwa wanachimba

Watu hao ni raia 13 Watanzania na raia mmoja wa China. Tukio hilo limetokea saa 9 usiku leo wakati wachimbaji hao wakiendelea na shughuli ya uchimbaji katika mgodi wa RZ unaomilikiwa na wachina.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Ezekiel Kyunga ametembelea eneo la tukio na kuona shughuli za uokozi zikiendelea na kuagiza nguvu ziongezwe

Tayari kampuni za madini ya dhahabu GGM, Kahama na Busolwa wameombwa kuongeza nguvu.

Wednesday, January 25, 2017

ECOWAS WABAINI KEMIKALI YA SUMU IKULU YA GAMBIA

Rais mstaafu wa Gambia Yahya Jammeh

Askari wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (Ecowas) wamegundua kemikali ya sumu kali iliyokuwa imetegwa kwenye vyumba vya Ikulu.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Ecowas kupitia gazeti la Freedom la Gambia, kemikali hiyo ilitegwa kwa lengo la kuua mtu yeyote atakayeingia ndani ya Ikulu hiyo.

Kutokana na hali hiyo, kiongozi mpya wa Gambia, Adama Barrow anatakiwa kuendelea kukaa Senegal kwa usalama wake huku uchunguzi ukiendelea kufanyika.

CUF WAMGEUKIA JENERALI MWAMNYANGE

Kikao cha kutathmini uchaguzi mdogo wa Jimbo la Dimani  cha  Chama cha  Wananchi (CUF), kimekusudia kumwandikia barua ya malalamiko Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (JWTZ), Jenerali Davis Mwamunyange wakidai wanajeshi walishiriki kuleta hofu.

Hata hivyo, jeshi hilo limekana madai ya CUF likisema ni uzushi.

Madai hayo yalitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui alipozungumza kwa simu na mwandishi wetu kuhusu uamuzi wa kikao hicho kilichofanyika jana Unguja chini ya uenyekiti wa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad na kuhudhuriwa na wajumbe 14.

Alidai kikao hicho kilichojadili mwenendo mzima wa uchaguzi kuanzia kampeni, kilifikia uamuzi wa kuandika barua ya malalamiko kwa Jenerali Mwamunyange wakidai wanajeshi walionekana wakizunguka mitaani katika jimbo, siku ya kuamkia uchaguzi na siku ya kupigakura.

FUMANIZI FEKI ZATIKISA MOSHI NA ARUSHA

(picha na maktaba) 

Utapeli wa aina yake unazidi kutikisa mikoa ya Kilimanjaro na Arusha baada ya kuibuka matukio ya kupangwa ya kufumania watu wenye heshima katika jamii kwa lengo la kujipatia fedha.

Siku za karibuni kumekuwa na mlolongo wa matukio hayo, yakiwalenga viongozi wa kiroho, wanandoa na vigogo wenye nyadhifa serikalini.

Uchunguzi ulibaini utekelezaji wa matukio hayo huambatana na vitisho kwa walengwa, ikiwamo kuwapiga picha na baadaye kutakiwa kutoa fedha kati ya Sh milioni 5 na Sh milioni 15 ili tukio hilo lisichapishwe kwenye vyombo vya habari.

Wake au waume za watu, viongozi wa dini na watendaji serikalini ndiyo walengwa wakuu wa matukio hayo, kwa kuwa ndiyo wenye hofu ya kuvunjiwa heshima kwenye jamii.

Chanzo: Mwananchi.

IVORY COAST YATUPWA NJE YA AFCON

Wachezaji wa Morocco wakishangilia.

Bingwa mtetezi wa michuano ya kombe la mataifa ya afrika tembo wa Africa Ivory Coast, wametupwa nje ya michuano ya mwaka huu baada ya kuchapwa kwa bao 1-0 na Simba wa Atlas Moroco

Goli pekee liliowaondoa miamba hao wa soka wa Afrika mashindanoni lilifungwa na Rachid Alioui katika dakika ya 64 ya mchezo.

Nayo timu ya Jamuhuri ya kidemocrasia ya Congo ilitambia Togo kwa kuichapa kwa mabao 3-1 na hivyo kufuzu hatua ya robo fainali wakiwa vinara kwa kundi C kwa alama 7 huku Moroco wakiwa nafasi ya pili kwa alama 6.

Moroco na Jamuhuri ya kidemocrasia ya Congo wanafuzu katika kundi hilo la huku Ivory Coast na Togo zikitupwa nje ya michuano hiyo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...