Wednesday, February 08, 2017

MBUNGE WA CCM AHOJI 'UTAJIRI' WA MAKONDA BUNGENI

Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Kasheku ameendeleza ‘vita’ yake dhidi ya Paul Makonda, akisema yupo tayari kusaidia vyombo vya dola kukamata vigogo wa dawa za kulevya na kuhoji ukimya wa mawaziri watatu dhidi ya kile alichodai utajiri wa mkuu huyo wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Awali, Kasheku ambaye ni maarufu kwa jina la Msukuma, alitoa tuhuma dhidi ya Makonda juzi, alipotaka kujua wafadhili wa safari za mkuu huyo wa mkoa nje ya nchi na sababu za kubagua watuhumiwa wa biashara ya dawa za kulevya kwa kutaja baadhi na kuwaacha wengine, huku mawaziri wakisita kuchukua hatua.

Alitoa tuhuma hizo bungeni baada ya Makonda kuagiza watu 12, wakiwemo wasanii maarufu wa muziki na filamu, kuripoti Kituo Kikuu cha Polisi cha Dar es Salaam, akiwatuhumu kuhusika na utumiaji au biashara ya dawa za kulevya.

Jana, Msukuma aliibuka na hoja nzito zaidi akihoji sababu za mawaziri kutochukua hatua na pia kutaja baadhi ya mali alizopata Makonda katika kipindi kifupi alichoshika madaraka ya mkuu wa mkoa baada ya kuwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni pia kwa muda mfupi.

Mbunge huyo alitoa tuhuma hizo nzito muda mfupi baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu, wakati alipotumia kanuni ya 68 (7) kuomba mwongozo kutoka kwa Naibu Spika, Tulia Ackson.

WAANDISHI WA HABARI WAKAMATWA, WAHOJIWA NA POLISI

Waandishi wa habari wawili jana walikamatwa na kuhojiwa katika Kituo cha Polisi cha Usa River mkoani Arusha, huku aliyetoa amri ya kukamatwa kwao akizua utata.

Wakati taarifa za awali zikidai ni amri ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti, yeye alikana kuhusika na agizo hilo.

Waliokamatwa ni Bahati Chume mwandishi wa kujitegemea wa gazeti la Mwananchi Mkoa wa Kilimanjaro na Dorine Alois kutoka kituo cha Sunrise Radio cha jijini Arusha.

Waandishi hao walikamatwa walipokuwa wakifuatilia habari ya mgogoro kwenye machimbo ya kokoto katika Kijiji cha Kolila mpakani mwa wilaya za Arumeru na Hai.

Mnyeti alipoulizwa alikana kutoa amri hiyo akisema yeye hana ugomvi na waandishi wa habari.

Saturday, February 04, 2017

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI FEBRUARI 04, 2017 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


Tu-follow instagram @jambotz. Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz.

TAZAMA PICHA 30 BORA ZA OBAMA KATI YA MILLION 2 ALIZOPIGWA KATIKA KIPINDI CHA MIAKA NANE


Pete Souza katika kipindi cha miaka 8 amempiga picha zaidi ya million 2 rais mstaafu wa Marekani. Pete ambae alikuwa mpiga picha wa familia ya Obama aliambatana nae rais huyo kwa kipindi chote cha miaka nane ya uongozi wake.
Tu-follow instagram @jambotz. Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz.

Sunday, January 29, 2017

TAZAMA PICHA ZA ZOEZI LA UOKOAJI KWA WALIOFUKIWA NA KIFUSI GEITA.

Wachimbaji wote 15 waliofukiwa na kifusi katika mgodi wa RZ Geita wameokolewa asubuhi ya leo. Jambo Tz inawapa pole na kuwaombea wapone haraka ndugu wote waliokumbwa na ajali hii.

MBUNGE APENDEKEZA BIMA KWA WANYWAJI WA POMBE

Mbunge mmoja nchini Kenya amewasilisha mswada bungeni kuzishinikiza kampuni zinazouza pombe kutoa asilimia ndogo ya faida yao kuwadhamini wanywaji ambao wataathirika na pombe hiyo.

Mbunge Gideon Mwiti anataka watengenezaji wa pombe kutoa kati ya asilimia 5 na 10 ya mapato wanayopata kwa kampuni za bima ili kuwafidia watu ambao wataathirika na pombe ama hata kupata ajali kwa kuwa walevi kulingana na gazeti la Daily Nation nchini humo.

Mswada huo pia unapendekeza kwamba iwapo mtu atafariki kutokana na athari za kunywa pombe ,kampuni hizo za pombe zilazimike kufidia familia yake.

Bw Mwiti pia amezishutumu kampuni za pombe kwa kushindwa kukuza pombe zisizo na madhara kwa afya, kwa mujibu wa ripoti hiyo.

Thursday, January 26, 2017

WACHIMBAJI 14 WAFUNIKWA NA KIFUSI GEITA

Picha na maktaba.

Wachimbaji wadogo 14 kutoka mgodi wa dhahabu wa RZ uliopo Kata ya Nyarugusu mkoani Geita wamefukiwa na kifusi cha udongo baada ya kutokea maporomoko kwenye moja ya shimo walilokuwa wanachimba

Watu hao ni raia 13 Watanzania na raia mmoja wa China. Tukio hilo limetokea saa 9 usiku leo wakati wachimbaji hao wakiendelea na shughuli ya uchimbaji katika mgodi wa RZ unaomilikiwa na wachina.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Ezekiel Kyunga ametembelea eneo la tukio na kuona shughuli za uokozi zikiendelea na kuagiza nguvu ziongezwe

Tayari kampuni za madini ya dhahabu GGM, Kahama na Busolwa wameombwa kuongeza nguvu.

Wednesday, January 25, 2017

ECOWAS WABAINI KEMIKALI YA SUMU IKULU YA GAMBIA

Rais mstaafu wa Gambia Yahya Jammeh

Askari wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (Ecowas) wamegundua kemikali ya sumu kali iliyokuwa imetegwa kwenye vyumba vya Ikulu.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Ecowas kupitia gazeti la Freedom la Gambia, kemikali hiyo ilitegwa kwa lengo la kuua mtu yeyote atakayeingia ndani ya Ikulu hiyo.

Kutokana na hali hiyo, kiongozi mpya wa Gambia, Adama Barrow anatakiwa kuendelea kukaa Senegal kwa usalama wake huku uchunguzi ukiendelea kufanyika.

CUF WAMGEUKIA JENERALI MWAMNYANGE

Kikao cha kutathmini uchaguzi mdogo wa Jimbo la Dimani  cha  Chama cha  Wananchi (CUF), kimekusudia kumwandikia barua ya malalamiko Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (JWTZ), Jenerali Davis Mwamunyange wakidai wanajeshi walishiriki kuleta hofu.

Hata hivyo, jeshi hilo limekana madai ya CUF likisema ni uzushi.

Madai hayo yalitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui alipozungumza kwa simu na mwandishi wetu kuhusu uamuzi wa kikao hicho kilichofanyika jana Unguja chini ya uenyekiti wa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad na kuhudhuriwa na wajumbe 14.

Alidai kikao hicho kilichojadili mwenendo mzima wa uchaguzi kuanzia kampeni, kilifikia uamuzi wa kuandika barua ya malalamiko kwa Jenerali Mwamunyange wakidai wanajeshi walionekana wakizunguka mitaani katika jimbo, siku ya kuamkia uchaguzi na siku ya kupigakura.

FUMANIZI FEKI ZATIKISA MOSHI NA ARUSHA

(picha na maktaba) 

Utapeli wa aina yake unazidi kutikisa mikoa ya Kilimanjaro na Arusha baada ya kuibuka matukio ya kupangwa ya kufumania watu wenye heshima katika jamii kwa lengo la kujipatia fedha.

Siku za karibuni kumekuwa na mlolongo wa matukio hayo, yakiwalenga viongozi wa kiroho, wanandoa na vigogo wenye nyadhifa serikalini.

Uchunguzi ulibaini utekelezaji wa matukio hayo huambatana na vitisho kwa walengwa, ikiwamo kuwapiga picha na baadaye kutakiwa kutoa fedha kati ya Sh milioni 5 na Sh milioni 15 ili tukio hilo lisichapishwe kwenye vyombo vya habari.

Wake au waume za watu, viongozi wa dini na watendaji serikalini ndiyo walengwa wakuu wa matukio hayo, kwa kuwa ndiyo wenye hofu ya kuvunjiwa heshima kwenye jamii.

Chanzo: Mwananchi.

IVORY COAST YATUPWA NJE YA AFCON

Wachezaji wa Morocco wakishangilia.

Bingwa mtetezi wa michuano ya kombe la mataifa ya afrika tembo wa Africa Ivory Coast, wametupwa nje ya michuano ya mwaka huu baada ya kuchapwa kwa bao 1-0 na Simba wa Atlas Moroco

Goli pekee liliowaondoa miamba hao wa soka wa Afrika mashindanoni lilifungwa na Rachid Alioui katika dakika ya 64 ya mchezo.

Nayo timu ya Jamuhuri ya kidemocrasia ya Congo ilitambia Togo kwa kuichapa kwa mabao 3-1 na hivyo kufuzu hatua ya robo fainali wakiwa vinara kwa kundi C kwa alama 7 huku Moroco wakiwa nafasi ya pili kwa alama 6.

Moroco na Jamuhuri ya kidemocrasia ya Congo wanafuzu katika kundi hilo la huku Ivory Coast na Togo zikitupwa nje ya michuano hiyo.

Tuesday, January 24, 2017

MAALIM SEIF "NIMESHAMALIZANA NA JECHA"

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad 
  
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamada mesema ameshamalizana na mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha na haoni umuhimu wa kuzungumzia wala kumjibu, kwa sababu atampa sifa asizostahili.

Akihojiwa katika kipindi cha Funguka cha kituo cha televisheni cha Azam TV juzi, Jecha alisema hakumshirikisha Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein katika kufuta matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2015 visiwani humo.

Jecha alifuta matokeo hayo Oktoba 28, 2015, siku ambayo alitakiwa atangaze mshindi wa uchaguzi wa rais, huku ZEC ikiwa imeshatangaza matokeo ya majimbo 31 na mengine tisa yaliyosalia yakiwa yameshahakikiwa.

Alitangaza uchaguzi mpya Machi 20, 2016 ambao ulisusiwa na CUF na Dk Shein kuibuka mshindi.

DC AMSWEKA NDANI DIWANI WA CHADEMA

 
Mkuu wa Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu, Joseph Chilongani amemweka rumande Diwani wa Bukundi, Joseph Masibuka (CHADEMA ) kwa tuhuma za kubomoa nyumba 20 za wananchi kwa madai ya kujengwa katika eneo lake.

Hata hivyo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Jonathan Shanna alisema jana kuwa wanachunguza madai hayo kubaini kama kuna kosa ili hatua za kisheria zichukuliwe.

Shanna aliwapongeza wananchi kutojichukulia sheria mkononi wakati wa ubomoaji wa nyumba hizo wilayani hapa.

Kubomolewa kwa nyumba hizo na kampuni ya udalali, kumesababisha zaidi ya kaya 100 kukosa makazi.

Hata hivyo, Chilangoni aliwataka wananchi kurejea kwenye makazi yao na kwamba gharama za ujenzi zitafanywa na diwani huyo.

Baadhi ya wakazi hao walisema nyumba za nyasi na magodoro yalichomwa moto wakati wa ubomoaji.

Saturday, January 21, 2017

BABU WA LOLIONDO KURUDI UPYA NA KIKOMBE....!!!

Mchungaji Ambilikile Mwasapile

Mchungaji Ambilikile Mwasapile bado yupo na shughuli zake za kutoa kikombe cha dawa anayodai inatibu magonjwa  yote yanayomkabili binadamu.

Hata hivyo, baada ya ukimya wa muda mrefu babu ameibuka na kuitaka kwa mara nyingine Serikali kuboresha miundombinu ya Loliondo kwa kuwa kuna mambo makubwa yanakuja kutokana na maono anayoonyeshwa.

Akizungumza nyumbani kwake katika Kijiji cha Samunge, Tarafa ya Sale jana, Mchungaji Mwasapile alisema watu waliokuwa wanakwenda kwa wingi miaka iliyopita wamepungua sana na sababu ni kuwa idadi kubwa ya walipokea uponyaji wakati huo.

Mchungaji huyo mstaafu alisema wito anaoutoa kwa Serikali kuboresha miundombinu unatokana na mambo makubwa anayoonyeshwa yatakayokuja wakati ambao Mungu ameupanga.

YAHYA JAMMEH AKUBALI KUNG'ATUKA MADARAKANI

Kiongozi wa muda mrefu nchini Gambia Yahya Jammeh, anasema kuwa ataondoka madarakani baada ya kukataa kukubali kushindwa.

Katika tangazo kwenye runinga, Jammeh alisema kuwa hakuna haja ya hata tone moja la damu kumwagika.

Taangazo hilo linakuja saa kadha baada ya mazungumzo kati ya bwana Jammeh na wapatanishi wa Afrika Magharibi. Hata hivyo hakuna taarifa zaidi kuhusu yale yayoafikiwa.

Bwana Jammeh alishindwa kwenye uchaguzi wa mwezi Disemba na mrithi wake Adama Barrow tayari amesha apishwa.
Gambia: Jammeh 'akubali k

Bwana Barrow amekuwa akiishi katika taifa jirani la Senegal kwa siku kadha. Wanajeshi kutoka nchi za magharibi mwa Afrika ikiwemo Senegal wametumwa nchini Gambia wakitisha kumtimua bwana Jammeh madarakani.

Uamuzi wa bwana Jammeh kuondoka ulikuja kufuatia mazungumzo na marais wa Guinea na Mauritania.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...