Tuesday, November 01, 2016

WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE KUANZA MITIHANI LEO, WAZIRI AONYA UDANGANYIFU

 
Wanafunzi wa kidato cha nne wakimsikiliza naibu waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo mara baada ya kukagua maandalizi ya mtihani wa kidato cha nne unaofanyika Leo. 
 

Naibu waziri ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akiagana na wanafunzi wa  shule ya sekondari Msalato mara baada ya kuzungumza nao.

Naibu waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo, amefanya ziara kwenye shule mbalimbali mjini Dodoma kuangalia maandalizi kwa ajili ya mtihani wa kidato cha nne unaoanza Leo nchini.

Katika ziara yake kwenye Shule ya sekondari Jamhuri, Kiwanja cha ndege na Msalato, Jafo amewaonya walimu na wanafunzi hao nchini kuepukana na vitendo vya udanganyifu.

Akizungumza na walimu na wanafunzi katika shule hizo, Jafo amesema katika mtihani huo hawatarajii kuwepo na udanganyifu kwa kuwa wamejifunza kupitia mtihani wa darasa la saba ambapo kumekuwepo na tabia ya walimu kujificha chooni ili kuwasaidia wanafunzi.
Amesema shule zitakazofanya fanya hivyo zitakuwa zimepoteza thamani yake. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

WANAWAKE WANAOFANYA NGONO BILA KINGA WANAUWEZEKANO MKUBWA WA KUPATA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI

Naibu waziri wa Afya Maendeleo ya jamii wazee jinsia na Watoto Dkt. Hamis Kigwangala akiwa anazungumza na waandishi wa habari wanawake kuhusu tatizo la Saratani ya shingo ya Kizazi, katika Ukumbi wa Olasiti Lodge Jijini Arusha, aliyepo kushoto kwake ni Dkt. Mathew Kasumuni kutoka hospital ya Mountmeru iliyopo jijini Arusha.
Waandishi wa habari wanawake wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu waziri wa Afya Maendeleo ya jamii wazee jinsia na Watoto Dkt. Hamis Kigwangala, Aliyepo kushoto kwake ni Dkt. Mwanahamis Ghembe kutoka Mountmeru Hospital.

Naibu waziri wa Afya Hamisi Kigwangala amesema kuwa wanawake wanaoshiriki tendo la ndoa bila kinga wapo hatarini kupata virusi vinavyoitwa HPV vinavyosababisha   Saratani ya mlango wa kizazi.

Kigwangala amesema wanawake wanaofanya ngono bila kinga wanaweza kupata saratani ya mlango wa kizazi, ambapo husababishwa kwa kufanya ngono bila kinga,huambukizwa  kwa kujaamiana. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 1, 2016 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

20161101_041402

20161101_041409

20161101_041420

Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

Thursday, October 27, 2016

SERIKALI YATANGAZA MATOKEO YA DARASA LA SABA 2016

Serikali imetangaza matokeo ya mtihani wa darasa la 7 kwa mwaka 2016 ambapo ufaulu umeongezeka kwa asilimia 2.52 na shule iliyoongoza kitaifa ni shule ya Msingi Kwema ya mkoani Shinyanga. 

Mtihani huu ulifanyika tarehe 7 na 8 mwezi Septemba mwaka huu. Kutazama matokeo hayo bofya hapa.

Wednesday, October 26, 2016

MAGAZETI YA LEO JUMATANO OCTOBA 26, 2016 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

20161026_041718
20161026_041734
20161026_041746

Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

MPIGIE KURA RAIS MAGUFULI ASHINDE TUZO ZA MTU MASHUHURI ZA FORBES

Rais John Magufuli ni miongoni mwa watu mashuhuri barani Africa waliopendekezwa kuwania tuzo ya FORBES AFRICA PERSON OF THE YEAR 2016.

Mpaka sasa rais Magufuli anaongoza kwa 80% ya kura zote zilizopigwa. Unaweza kumpigia kura yako hapa.

Share na wenzio.

Tuesday, October 25, 2016

MABUSHA TATIZO LA WENGI JIJINI DAR

UTAFITI uliofanywa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii unaonyesha kuwa wakazi wa Mkoa wa Dar es salam 6800 tayari wamepata athari ya matende na mabusha. 

 Akizungumza katika zoezi hilo Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dk Grace Magembe alisema mpaka sasa tayari watu 104 kwa Mkoa wa Dar es Salaam wameshafanyiwa upasuaji wa mabusha. 

Alisema kutokana na idadi kubwa ya wagonjwa wa mabusha Jijini Dar es Salaam wanatarajia kuwafanyia upasuaji wagonjwa 1000. 

Akizungumza wakati wa ugawaji wa dawa za kinga tiba ya Matende, Minyoo na Mabusha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, alisema kuwa kiwango hicho ni kikubwa sana kwa wakazi wa dar es salaam kwani mpaka sasa watanzania milioni 2.7 wameathirika na magonjwa yasiyopewa kipaumbele ikiwemo ngiri maji pamoja na matende hususani vijijini. 

Alisema zoezi la utoaji wa dawa za kinga tiba litatolewa bure ambapo zaidi ya watanzania milioni 4.5 wanatarajiwa kupata kinga tiba hizo. 

 “Kinga tiba imeanza kutolewa Oktoba 25 hadi 29 kwa watu wenye umri kuanzia miaka 5 na kuendelea kwa kumeza dawa za Mectizan na Albendazole za kukinga na kutibu magonjwa ya minyoo tumbo,mabusha na matende,” alisema Makonda.

FORBES: RAIS MAGUFULI KUWANIA TUZO YA FORBES YA MTU MASHUHURI

Ikiwa ni mwaka mmoja tangu kufanyika kwa uchaguzi mkuu,Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli ameteuliwa kuwania tuzo la Forbes la mtu mashuhuri wa mwaka.

 Jarida hilo la biashara limemtambua rais Magufuli kwa umuhimu wake katika kuimarisha uchumi wa taifa. Wengine walioteuliwa kuwania tuzo hiyo ni pamoja na Benki ya Capitec nchini Afrika Kusini, Rais wa Mauritania, Mtetezi wa haki za umma nchini Afrika Kusini na raia wa Rwanda. 
Mwaka uliopita tuzo hilo lilichukuliwa na mfanyibiashara wa Tanzania Mohammed Dewiji.

Chanzo: BBC Swahili

Sunday, October 02, 2016

MSANII WA JAMAICA ALIYEJICHORA TATTOO YA MAGUFULI....!!!

Las Laciano

Mwanamziki wa Jamaica Las Laciano aliyewahi kutamba na nyimbo kadhaa, ikiwemo "its me against jah" amejichora tatoo ya rais kutokea Africa anayemkubali, ambaye ni rais wa Tanzania Mh. Dr. John Magufuli. 

Sababu ni kuwa ndo rais muwajibikaji, anayeona mbele hatishiwi na matatizo ya mpito ila anatishiwa na matatizo ya muda mrefu kama rushwa, urasimu na uzembe kazini. Mheshimiwa Magufuli ameendelea kugonga kimataifa na anazidi kukubalika.

Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz.
https://m.facebook.com/jambotz/

Wednesday, September 21, 2016

TAZAMA PICHA ZAIDI ZA NDEGE MPYA YA TANZANIA




Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz.

NDEGE MPYA YA ATCL YAWASILI NCHINI, YA PILI ITATUA WIKI IJAYO

Ndege mpya ya kwanza iliyonunuliwa na Serikali kwa ajili ya kutumiwa na Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) imetua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam ikitokea nchini Canada ilikotengenezwa. 

Ndege hiyo aina ya Bombadier Q400 NextGen imetua majira ya saa 6:15 Mchana na kisha kupatiwa heshima maalum ambayo hutolewa kwa ndege yoyote mpya inayotua katika nchi yake (Water Salute). 

Baada ya kupokewa ndege imeegeshwa katika eneo la ndege za jeshi (Airwing Ukonga). Akizungumza baada ya kuwasili kwa ndege hiyo Katibu Mkuu Uchukuzi Dkt. Leonard Chamriho amesema ndege ya pili inatarajiwa kuwasili baada ya wiki moja na kwamba baada ya kuwasili ndege ya pili ndipo yatafanyika mapokezi rasmi, yatakayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa tarehe itakayotangazwa baadaye.

Tuesday, September 20, 2016

PICHA ZAIDI ZA AJALI YA BUS LA NEW FORCE ILIYOTOKEA MKOANI NJOMBE



Watu 12 wamefariki dunia katika ajali ya basi la kampuni ya New Force lililokuwa likisafiri kutoka Dar kwenda Songea jana, katika watu waliofariki kati yao wanaume ni 4 na wanawake 8. Huku majeruhi wakiwa 19. Zoezi la uokozi lilimalizika majira ya saa 8 usiku.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...