Tuesday, October 25, 2016

MABUSHA TATIZO LA WENGI JIJINI DAR

UTAFITI uliofanywa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii unaonyesha kuwa wakazi wa Mkoa wa Dar es salam 6800 tayari wamepata athari ya matende na mabusha. 

 Akizungumza katika zoezi hilo Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dk Grace Magembe alisema mpaka sasa tayari watu 104 kwa Mkoa wa Dar es Salaam wameshafanyiwa upasuaji wa mabusha. 

Alisema kutokana na idadi kubwa ya wagonjwa wa mabusha Jijini Dar es Salaam wanatarajia kuwafanyia upasuaji wagonjwa 1000. 

Akizungumza wakati wa ugawaji wa dawa za kinga tiba ya Matende, Minyoo na Mabusha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, alisema kuwa kiwango hicho ni kikubwa sana kwa wakazi wa dar es salaam kwani mpaka sasa watanzania milioni 2.7 wameathirika na magonjwa yasiyopewa kipaumbele ikiwemo ngiri maji pamoja na matende hususani vijijini. 

Alisema zoezi la utoaji wa dawa za kinga tiba litatolewa bure ambapo zaidi ya watanzania milioni 4.5 wanatarajiwa kupata kinga tiba hizo. 

 “Kinga tiba imeanza kutolewa Oktoba 25 hadi 29 kwa watu wenye umri kuanzia miaka 5 na kuendelea kwa kumeza dawa za Mectizan na Albendazole za kukinga na kutibu magonjwa ya minyoo tumbo,mabusha na matende,” alisema Makonda.

FORBES: RAIS MAGUFULI KUWANIA TUZO YA FORBES YA MTU MASHUHURI

Ikiwa ni mwaka mmoja tangu kufanyika kwa uchaguzi mkuu,Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli ameteuliwa kuwania tuzo la Forbes la mtu mashuhuri wa mwaka.

 Jarida hilo la biashara limemtambua rais Magufuli kwa umuhimu wake katika kuimarisha uchumi wa taifa. Wengine walioteuliwa kuwania tuzo hiyo ni pamoja na Benki ya Capitec nchini Afrika Kusini, Rais wa Mauritania, Mtetezi wa haki za umma nchini Afrika Kusini na raia wa Rwanda. 
Mwaka uliopita tuzo hilo lilichukuliwa na mfanyibiashara wa Tanzania Mohammed Dewiji.

Chanzo: BBC Swahili

Sunday, October 02, 2016

MSANII WA JAMAICA ALIYEJICHORA TATTOO YA MAGUFULI....!!!

Las Laciano

Mwanamziki wa Jamaica Las Laciano aliyewahi kutamba na nyimbo kadhaa, ikiwemo "its me against jah" amejichora tatoo ya rais kutokea Africa anayemkubali, ambaye ni rais wa Tanzania Mh. Dr. John Magufuli. 

Sababu ni kuwa ndo rais muwajibikaji, anayeona mbele hatishiwi na matatizo ya mpito ila anatishiwa na matatizo ya muda mrefu kama rushwa, urasimu na uzembe kazini. Mheshimiwa Magufuli ameendelea kugonga kimataifa na anazidi kukubalika.

Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz.
https://m.facebook.com/jambotz/

Wednesday, September 21, 2016

TAZAMA PICHA ZAIDI ZA NDEGE MPYA YA TANZANIA




Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz.

NDEGE MPYA YA ATCL YAWASILI NCHINI, YA PILI ITATUA WIKI IJAYO

Ndege mpya ya kwanza iliyonunuliwa na Serikali kwa ajili ya kutumiwa na Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) imetua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam ikitokea nchini Canada ilikotengenezwa. 

Ndege hiyo aina ya Bombadier Q400 NextGen imetua majira ya saa 6:15 Mchana na kisha kupatiwa heshima maalum ambayo hutolewa kwa ndege yoyote mpya inayotua katika nchi yake (Water Salute). 

Baada ya kupokewa ndege imeegeshwa katika eneo la ndege za jeshi (Airwing Ukonga). Akizungumza baada ya kuwasili kwa ndege hiyo Katibu Mkuu Uchukuzi Dkt. Leonard Chamriho amesema ndege ya pili inatarajiwa kuwasili baada ya wiki moja na kwamba baada ya kuwasili ndege ya pili ndipo yatafanyika mapokezi rasmi, yatakayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa tarehe itakayotangazwa baadaye.

Tuesday, September 20, 2016

PICHA ZAIDI ZA AJALI YA BUS LA NEW FORCE ILIYOTOKEA MKOANI NJOMBE



Watu 12 wamefariki dunia katika ajali ya basi la kampuni ya New Force lililokuwa likisafiri kutoka Dar kwenda Songea jana, katika watu waliofariki kati yao wanaume ni 4 na wanawake 8. Huku majeruhi wakiwa 19. Zoezi la uokozi lilimalizika majira ya saa 8 usiku.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...