Saturday, August 13, 2016

MAALIM SEIF AMTEMBELEA MH. NDUGAI

Ujumbe wa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad umemtembelea Spika wa Bunge, Job Ndugai nyumbani kwake Salasala Dar es Salaam kumjulia hali baada ya kutoka India alikokwenda kuchunguzwa afya yake.

Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza Rais Mstaafu wa Serikali ya Zanzibar, ameambatana na Kaimu Mwenyekiti wa CUF, Severina Mwijage, Naibu Katibu Mkuu CUF Tanzania Bara, Magdalena Sakaya na Naibu Katibu Mkuu mstaafu, Julius Mtatiro.
 
Ndugai amemhakikishia Maalim Seif kuwa hali yake kiafya imeimarika sana.

Sunday, July 10, 2016

JE, WAMJUA MNYAMA MWENYE WIVU KUPITA KIASI....??!

Nyegere ni moja kati ya wanyama wenye wivu sana hapa duniani. Chakula chake kikubwa ni asali, yeye hupanda juu ya mzinga wa asali na kuujambia, baada ya mashuzi yake nyuki wote hulewa na yeye kupakua asali na masega yake na kula. Mwili wake una ngozi ngumu sana kiasi hata nyuki akimuuma hakuna chochote kinatokea.

Nyegere ni mnyama mwenye wivu na mapenzi makubwa sana kwa jike lake, hutembea nyuma ya jike huku akiwa ameziba sehemu za siri za jike, hata jani tu likiigusa sehemu ya siri ya jike litararuliwa na kupokea kichapo cha hatari, maana wivu wake ni kuwa jani laitakuwa "limefaidi utamu" wa jike.
Nyegere anaweza kununua ugomvi mpaka kijiji cha sita, walina asali ndio waathirika wakubwa wa hasira za Nyegere, anaweza kuujambia mzinga akala kidogo asali na kupeleka kwa mke, mlina asali akifika na kupakua, nyegere ana uwezo ya kufuatilia harufu ya aliyeiba asali yake mpaka nyumbani, na akifika anavunja mlango na kuingia ndani na kumvamia mwizi wa asali yake (ukizingatia milango ya vijijini si imara). Watu wengi vijini wameuwawa kwa namna hii. Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz. Pia tu-follow instagram @jambotz.

Friday, June 24, 2016

MAOMBI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU 2016/2017

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inapenda kutoa taarifa kwa Umma na wadau wake wote kuwa inatarajia kuanza kupokea maombi ya Mikopo kwa mwaka wa masomo 2016 /2017 kuanzia tarehe 27 Juni 2016 hadi tarehe 31 2016.

Katika kipindi hicho waombaji wa mikopo watarajiwa wanapaswa kusoma mwongozo wa utoaji mikopo na ruzuku (GUIDELINES AND CRITERIA FOR ISSUANCE OF STUDENTS’ LOANS AND GRANTS FOR THE 2016/2017 ACADEMIC YEAR) uliopo kwenye tovuti hii ya Bodi ili kufahamu sifa za mwombaji na taratibu kufuata kabla ya kuomba mikopo kwa njia ya mtandao.

Utoaji wa Mikopo unaongozwa na Sheria ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya juu Na. 9 ya 2004 (kama ilivyorekebishwa) hususani vifungu vyake vya 16 na 17.
Kwa taarifa hii, waombaji wote wa mikopo wanatakiwa kusoma mwongozo huo kabla ya kujaza maombi ya mikopo na wazingatie kuwa tarehe ya mwisho ya kuomba mikopo ni Julai 31, 2016.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...