Sunday, April 10, 2016
NDANDA KOSOVO AFARIKI DUNIA
Msanii
mkongwe kwa miondoko ya dansi nchini, ambaye aliwahi kuwa katika bendi ya FM
na baadae kuanzisha yake iliyofahamika kwa jina la Stono Musica au
jina linguine Wajela Jela, Ndanda Kosovo amefariki dunia. Like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz
Katika
taarifa ambayo imetufikia imeeleza kuwa marehemu amefariki jana asubuhi
katika hospitali ya taifa ya Muhimbili alipokuwa amelazwa alipokuwa
amelazwa akisumbuliwa na vidonda vya tumbo. Mungu ailaze roho ya marehemu peponi, Amin.
YANGA YATOKA SARE NA AL AHLY
Mchezo
wa Ligi ya Mabingwa Afrika, hatua ya 16 kati ya wawakilishi pekee wa
Tanzania katika mashindano hayo, Yanga ya Tanzania na wageni Al Ahly ya
Misri umemalizika katika uwanja wa taifa kwa timu hizo kutoka sare ya
goli moja kwa moja.
Katika
mchezo huo, Al Ahly ilikuwa ya kwanza kupata goli kupitia kwa mchezaji
wake Amr Gamal na dakika chache baadae Yanga kusawazisha baada ya
mchezaji wa Al Ahly, Ahmed Hegazy kujifunga dakika ya 16 ya mchezo huo
ambapo mpaka mchezo unamalizika, Yanga 1 na Al Ahly 1
WADHAMINI WA UEFA CHAMPIONS LEAGUE WAJITUPA SOKA LA BONGO
Shirikishio la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeishukuru kampuni ya
bia ya Heineken ambao ni wadhamini wakuu wa michuano ya Ligi ya Mabingwa
barani Ulaya (UEFA) kwa kujitolea kufanya ukarabati wa viwanja vitatu
vya mpira wa miguu vilivyopo jijini Dar es salaam.
Katika barua ya Meneja Mkuu wa Heineken nchini Tanzania, Michael
Mbugu kwenda kwa wakurugenzi ya Manispaa wilaya za Ilala na kinondoni,
nakala yake kutumwa kwa Rais wa TFF, imeeleza mdhamini ameelekeza nguvu
zake kwenye kukarabati baadhi ya viwanja nchini ili viwe katika hali
nzuri na salama ili kukuza vipaji vya vijana kwenye mchezo wa soka.
Heineken imelenga kuboresha dhamira yake ya kushirikiana na jamii
sehemu mbalimbali kwa kuchangia ukarabati wa viwanja vya TP Manzese kata
ya Sinza, Sigara Segerea kata ya Tabata Sigara na uwanja wa Magunia
Msasani uliopo kata ya Msasani.
Kufanya ukarabati wa viwanja hivyo kutatoa nafasi kwa vijana wa
maeneo ya Ali Maua, Darajani, Sweet Corner na Kijiweni (uwanja wa TP
Manzese), Macho, Kisiwani, Msasani na Msikitini (uwanja wa Magunia),
Barakuda, Tabata, Senene, Mwembeni, Chang’ombe, Kinyerezi na Segera
(uwanja wa Sigara) kufanya mazoezi na kuendeleza vipaji vya mpira wa
miguu.
Aidha TFF inazipongeza Halmashauri za Manispaa za Ilala na Kinondoni
kwa kupata nafasi ya kufanyiwa ukarabati viwanja vyao na kampuni ya
Heineken, na kuziomba mamlaka hizo kuvitunza viwanja hivyo ili viweze
kutumiwa na vijana wa kike na kiume katika mchezo wa mpira wa miguu. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
CRISTIANO RONALDO AANDIKA REKODI MPYA LA LIGA
Cristiano Ronaldo amekuwa mchezaji wa kwanza kufunga mabao 30 ndani
ya misimu sita ya La Liga baada ya Madrid kuichapa Eibar kwa bao 4-0
kwenye mchezo wa ligi. Karim Benema ambaye anapambana na majeruhi ya goti pamoja na Gareth
Bale walipumzishwa wakati Madrid inasubiri mchezo wa marudiano siku ya
Jumanne wa klabu bingwa Ulaya dhidi ya Wolfsburg.
James Rodriguez alianza kuzifungua nyavu za Eibar kwa mkwaju wa mpira
wa adhabu ndogo kabla ya Lucas Vazquez hajapachika bao la pili. Hadi mapumziko tayari Madrid ilikuwa mbele kwa magoli 4-0 huku
Ronaldo akitumbukia nyavuni kupiga bao la tatu akiunganisha pasi ya Jese
ambaye naye alipiga bao na kukamisha idadi ya magoli 4-0.
Real inakumbuka kichapo cha magoli 2-0 kutoka kwa Wolfsburg wakati
ikijiandaa na mchezo wao wa marudiano kwenye uwanja wa Bernabeu huku
kocha wa klabu hiyo Zinedine Zidane kiweka wazi kwamba, endapo
watashindwa kufuzu kwa hatua ya nusu fainali basi msimu wao utakuwa
umemaliza.
Kikosi cha Zidane kwa sasa kipo nyuma ya vinara wa ligi hiyo (Barca)
kwa pointi nne nyuma kikisimama nafasi ya tatu nyuma ya Atletico Madrid. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
Saturday, April 02, 2016
MAKONDA ATANGAZA NEEMA KWA BODABODA
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amekutana na waendesha bodaboda na kuahidi kushugulikia kero zinazowakabili ikiwemo kuondoa vikwazo vya wao kuingia katikati ya jiji.
Aidha, amewaahidi kuwapatia pikipiki kwa marejesho ya Sh25,000 kwa wiki kwa muda maalum kabla ya kuwaachia kabisa.
Kwa mantiki hiyo, Makonda amewataka kufanya usajili upya na kusajili vituo vyao ili watambulike kisheria huku akisema atawapatia mavazi maalum 'reflectors' kama utambulisho.
Awali, mmoja wa waendesha bodaboda hao, Daud Laurian alimsomea RC Makonda risala iliyoainisha matatizo yao ikiwemo zuio la ya jiji kutokana na agizo la aliyekua mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mecky Sadick Machi 3, 2014.
Waendesha hao wamehaokikishia Makonda kuwa raia wema katika suala zima la ulinzi iwapo Jeshi la Polisi Kanda Maalum litawachukulia kama ndugu zao na marafiki.
KONDAKTA ALIETISHIA KUMUUA MAGUFULI ASHTAKIWA
Kondakta wa daladala amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na shtaka la kutishia kumuua Rais John Magufuli.
Hamim Seif (42) mkazi wa Mwananyamala Ujiji, alidaiwa kutenda kosa hilo Machi 10 mwaka huu katika baa ya Soweto, maeneo ya Makumbusho jijini Dar es Salaam.
Wakili wa serikali Keneth Sekwao aliambia mahakama Alhamisi kuwa mshtakiwa, akiwa katika baa hiyo, alitishia kumuua Dkt Magufuli kwa maneno kwa njia ya kujitoa mhanga.
“Kwa haya mambo anayoyafanya Rais Magufuli, mimi nimo tayari kujilipua kwa kujitoa mhanga ili kumuangamiza,” alinukuliwa na Wakili Sekwao. Mshtakiwa alikana shtaka hilo
Hakimu Mkazi, Hellen Liwa aliweka wazi dhamana ya mshtakiwa huyo na kumtaka kutafuta wadhamini wawili, kutoka taasisi ya Serikali inayotambulika, ambao watasaini hati ya dhamana ya Sh2 milioni.
Alishindwa kutimiza masharti ya dhamana na akawekwa rumande hadi 14 Aprili kesi ikatapotajwa tena.
BOKO HARAM WAAPA KUTOSALIMU AMRI
Abubakar Shekau kiongozi wa Boko Haram
Wapiganaji wa kundi la Boko Haram wametoa kanda mpya ya video wakiapa kuendeleza vita vya kutaka uongozi wa sheria za kiislamu.
'Lazima mujue kwamba hakuna ukweli, hakuna majadiliano,hakuna kusalimu amri'', alisema mtu mmoja aliyejifunika uso na kuzungumza kwa lugha ya hausa.
Ujumbe huo unajiri baada ya kanda ya video isiojulikana mwezi uliopita kumuonyesha kiongozi wa Boko Haram Abubakar Shekau akionekana dhaifu swala linaloongeza uvumi kwamba mda wake katika uongozi wa kundi hilo unaelekea ukingoni.
Katika kanda hiyo ya video kuna watu wamesimama na bunduki za AK-47 mbele ya magari.
Sunday, March 27, 2016
Friday, March 25, 2016
Tuesday, March 22, 2016
MWALIMU ANAEHITAJI KUBADILISHANA KITUO
TANGAZO: Mimi ni mwalimu wa secondary nipo halmashauri ya Tandahimba nahitaji mwalimu wa kubadilishana nae Mbeya kutoka Iringa, Morogoro, Pwani au tuwasiliane kwa no. 0655591881.
Monday, March 21, 2016
SHEIN ASHINDA URAIS KWA ASILIMIA 91.4
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Jecha Salim Jecha amemtangaza Rasmi Mgombea urais wa CCM Dr. Ali Mohammed Shein kuwa mshindi wa kiti cha urais wa Zanzibar akiwa na kura 299.982 sawa na asilimia 91.4.
Sunday, March 13, 2016
Friday, March 11, 2016
HATIMAE MAGUFULI AWAPA SAFARI YA NJE MAWAZIRI WAWILI
Tangu Novemba 5 wakati Dk John Magufuli alipoapishwa, ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Waziri wa Mambo ya Nje, Balozi Augustine Mahiga pekee waliotoka nje ya nchi, lakini jana Rais aliwaruhusu mawaziri wengine wawili kusafiri nje.
Rais Magufuli alizuia safari za nje siku chache baada ya kuapishwa akisema watumishi wa umma watakaokuwa wakitaka kwenda nje watalazimika kuomba kibali kutoka Ikulu, ikiwa ni mkakati wake wa kudhibiti matumizi ya fedha za Serikali.
Tangu wakati huo, safari za nje kwa watumishi wa umma zimekuwa za nadra na mawaziri wamekuwa wakifanya ziara za kwenda mikoani kufuatilia utendaji na utoaji wa huduma kwa wananchi. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
MBOWE: NAWALETEA KATIBU MKUU MAKINI
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amevunja ukimya na kusema atawasilisha jina makini la mrithi wa nafasi ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa.
Akizungumza mjini hapa jana, baada ya kumalizika kikao cha kwanza cha Kamati Kuu, Mbowe alisema sifa za kiongozi anayepaswa kushika wadhifa huo zinafahamika.
Alisema wajumbe na wanachama wa Chadema watarajie kumpokea mtu makini ambaye jina lake atalipendekeza kisha kupigiwa kura na wajumbe wa Baraza Kuu kesho. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
MAREKANI YAMFILISI MTANZANIA MUUZA UNGA
SERIKALI ya Marekani juzi ilitangaza kutaifisha mali za bilionea Mtanzania, Ali Khatib Haji Hassan, maarufu Shikuba pamoja na mtandao wake wa kimataifa wa biashara ya dawa za kulevya.
Shikuba ambaye ni mfanyabiashara maarufu Dar es Salaam, anamiliki msururu wa biashara kama vile maduka ya kubadili fedha (bureau de change), kampuni za ulinzi, majumba na utitiri wa magari ya kifahari.
Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Fedha ya Marekani kupitia ofisi yake ya Udhibiti wa Mali Haramu za Raia wa Kigeni (OFAC), Shikuba na taasisi yake wameangukia katika sheria za nchi hiyo za kudhibiti mapapa wa unga wa kigeni (Kingpin Act).
Mbali ya sababu za kisheria, Marekani imesema bilionea huyo amekuwa akitumia faida haramu kutokana na biashara zake chafu kuhonga maofisa wa Serikali ya Tanzania ili asikamatwe na kushtakiwa. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
TRUMP NA RUBIO WATOFAUTIANA KUHUSU UISLAMU
Mgombea wa urais
kupitia tiketi ya chama cha Republican Marco Rubio amemshtumu Donald
Trump kwa kusema kuwa Uislamu unachukia Marekani katika mjadala uliokuwa
moja kwa moja runingani.
Bwana Rubio ambaye anakabiliwa na
ushindani wa maisha yake katika jimbo la Florida siku ya Jumanne amesema
kuwa Uislamu una tatizo la itikadi kali lakini akaongezea kuwa Waislamu
wengi wanapenda Wamerekani.
''Marais hawawezi kusema kile wanachotaka ,kuna madhara'',alisema huku raia wakimpigia makofi. Wagombea hao wanne wa chama cha Republican walisikia maombi kutoka kwa viongozi wa chama hicho kuwa na mjadala wa amani.
Ikilinganishwa
na mjadala uliopita ambao ulikabiliwa na na matusi ya kibinafsi mjadala
huu ulikuwa na muongozo mzuri huku wagombea wote wakitoa malengo ya
sera zao.
''Kufikia sasa siamini vile tumekuwa watulivu hapa'',bwana Trump alinukuliwa akisema. Lakini
katika swala la Uislamu,kulikuwa na tofauti kubwa kati ya Trump na
wagombea wengine huku wenzake wote wakitofautiana naye kwamba familia za
magaidi ziangamizwe. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
SIMBA YARUDI KILELENI YAINYUKA NDANDA 3-0
TIMU ya soka ya Simba jana ilirejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kishindo baada ya kuinyuka Ndanda FC mabao 3-0 katika mchezo uliopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Matokeo ya ushindi wa jana yameiwezesha Simba kufikisha pointi 51 na
kuwashusha mahasimu wao wa jadi Yanga hadi nafasi ya pili, wakiwa
wamejikusanyia pointi 50 huku Azam FC wakibaki nafasi tatu na pointi 47.
Simba wamerejea kileleni kwa kuwazidi mahasimu wao Yanga kwa pointi moja, lakini Wanajangwani hao wapo nyuma kwa mchezo mmoja kutokana na kushuka dimbani mara 21 huku wapinzani wao wakicheza mara 22. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
Simba wamerejea kileleni kwa kuwazidi mahasimu wao Yanga kwa pointi moja, lakini Wanajangwani hao wapo nyuma kwa mchezo mmoja kutokana na kushuka dimbani mara 21 huku wapinzani wao wakicheza mara 22. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
Thursday, March 10, 2016
UTUMBUAJI MAJIPU WAOKOA BILLION 700/=
KASI
ya kuzuia ukwepaji kodi za Serikali uliofanywa kwa kipindi cha miezi mitatu na
utawala wa Rais Dk. John Magufuli kwa ‘kutumbua majipu’ umeokoa wastani wa Sh
bilioni 700.
Katika
utawala wa Serikali iliyopita ya awamu ya nne, wastani wa makusanyo ya kodi kwa
kiwango cha juu kwa mwezi yalikuwa Sh bilioni 900, lakini baada ya kuingia kwa
awamu hii kumekuwapo na ongezeko la zaidi ya Sh bilioni 700 kwa miezi mitatu ya
Desemba hadi Februari.
Akitangaza
ongezeko hilo kwa waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kaimu Kamishna Mkuu
wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata, alisema katika kipindi cha
Desemba 2015, pia TRA iliweza kuvuka lengo kwa kukusanya kiasi cha zaidi ya Sh.
trilioni 1.4 sawa na ongezeko la wastani wa Sh. bilioni 490 kwa mwezi.
Alisema
kiasi hicho ni kikubwa kikilinganishwa na wastani wa makusanyo kwa mwezi Julai
hadi Novemba mwaka jana ambapo ilikuwa ni Sh. bilioni 900 kwa mwezi. Like page
yetu ya facebook Jambo Tz
'NITAFANYA KAZI NA ALI KIBA BILA VIKWAZO' HARMONIZE
LICHA ya tetesi kwamba wasanii wawili wa muziki wa Bongo Fleva, Ali
Kiba na Nasibu Abdul ‘Diamond’, kutoonyesha nia ya kushirikiana katika
muziki wao, msanii anayetamba na wimbo wa ‘Bado’, Rajabu Ibrahimu
‘Harmonize’, amesema yupo tayari kufanya kazi na Ali Kiba bila kikwazo
chochote.
Msanii huyo alisema Ali Kiba ni msanii wa Tanzania na ni msanii mzuri
katika muziki hivyo kufanya naye ‘kolabo’ ni kitu cha kawaida kama
wasanii wengine anavyofanya nao.
“Mimi sijui kiukweli kama kuna bifu kati ya Diamond na Ali Kiba kwa
sababu sijawahi kumsikia Diamond akimzungumzia Ali Kiba kwamba wana
ugomvi,” alisema Harmonize.
Harmonize ambaye hivi karibuni alijinadi kutoanzisha uhusiano wa
kimapenzi, anazidi kujizolea umaarufu kutokana na nyimbo zake tatu
ukiwemo ‘Aiyola’, ‘Kidonda Changu’ na ‘Bado’ huku akizidi kujipanga kwa
mambo mengine makubwa yatakayokuja kupitia kampuni ya wasafi
anayoifanyia kazi. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
MKWASA ATAJA SABABU ZA KUMUITA KAZIMOTO
KOCHA mkuu wa timu ya Taifa ya soka ‘Taifa Stars’, Boniface Mkwasa, amesema uwezo mkubwa aliokuwa nao kiungo wa Simba,
ndio umemfanya amuite kwenye kikosi chake kitakachocheza na Chad, Machi
23 kwenye mchezo wa kufuzu fainali za mataifa ya Afrika (Afcon),
utakaochezwa mji wa Djamena, nchini Chad.
Mkwasa alimjumuisha mchezaji huyo kwenye kikosi chake hicho chenye jumla ya wachezaji 25, licha ya kuwa tayari ameshatangaza kuacha kuichezea timu ya Taifa ili kutoa nafasi kwa wachezaji wengine.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii jana, Mkwasa alisema, Mwinyi ameonyesha mchango mkubwa kwenye timu yake ya Simba na ndio sababu iliyompelekea kumjumuisha kwenye kikosi chake ambacho kulingana na ratiba ilivyobana anahitaji kuwa na wachezaji wenye uzoefu mkubwa ili kuweza kupambana na Chad kwani hawana muda mrefu wa kujiandaa.
“Hizo taarifa za kuwa amestaafu kuichezea timu ya Taifa sijazipata hivyo haikuwa kikwazo kwangu kumuita, lakini pia bado ana kiwango kizuri ni kijana mkongwe na amekuwa na mchango mkubwa kwenye timu yake, bado ana nafasi kubwa ya kulisaidia Taifa lake,” alisema. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
Mkwasa alimjumuisha mchezaji huyo kwenye kikosi chake hicho chenye jumla ya wachezaji 25, licha ya kuwa tayari ameshatangaza kuacha kuichezea timu ya Taifa ili kutoa nafasi kwa wachezaji wengine.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii jana, Mkwasa alisema, Mwinyi ameonyesha mchango mkubwa kwenye timu yake ya Simba na ndio sababu iliyompelekea kumjumuisha kwenye kikosi chake ambacho kulingana na ratiba ilivyobana anahitaji kuwa na wachezaji wenye uzoefu mkubwa ili kuweza kupambana na Chad kwani hawana muda mrefu wa kujiandaa.
“Hizo taarifa za kuwa amestaafu kuichezea timu ya Taifa sijazipata hivyo haikuwa kikwazo kwangu kumuita, lakini pia bado ana kiwango kizuri ni kijana mkongwe na amekuwa na mchango mkubwa kwenye timu yake, bado ana nafasi kubwa ya kulisaidia Taifa lake,” alisema. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
LIVERPOOL KUCHUANA NA MAN U EUROPA
Mkufunzi wa timu ya Liverpool Jurgen
Klopp ameitaja mechi ya Alhamisi ya kombe la Europa kati ya Liverpool
na Manchster United kuwa mechi kubwa sana.
Liverpool wanaikaribisha Anfield timu ya Manchester United ikiwa ni mkutano wao wa kwanza Ulaya.
Hatahivyo
Klopp anasema :''kila siku kombe la Europa linafurahisha.Ni Mechi kubwa
sana.Ijapokuwa sio kubwa zaidi katika kazi yangu kama mkufunzi wa
Liverpool lakini ni muhimu sana''.
Manchester United imeshinda makombe 3 ya bara Europa hivi karibuni ikiwa 2008,huku Liverpool ikilibeba kombe hilo mara tano.
Mkufunzi
wa Manchester United Louis Van Gaal amesema kuwa wale wanaomkosoa kwa
kushushwa katika kombe la Europa hawaelewi huku Klopp akisema kuwa
anaamini mechi hiyo itasisimua mashabiki katika uwanja wa Anfield.
Saturday, March 05, 2016
Friday, March 04, 2016
MAGUFULI "MAJIPU YAKINISHINDA SINA SABABU YA KUENDELEA KUWA RAIS"
RAIS Dk. John Magufuli, amesema kama atashindwa kutumbua majipu dhidi
ya wazembe na wabadhirifu serikalini, hana sababu ya kuendelea kushika
wadhifa huo.
Amesema endapo hali hiyo ikitokea ni bora arudi nyumbani kwake
akalale, kwa sababu lengo lake la kuwapatia wananchi Tanzania mpya,
litakuwa halijatimia.
Rais Dk. Magufuli aliyasema hayo jana, wakati wa hafla ya kuweka jiwe
la msingi la ujenzi wa barabara ya Arusha-Holili yenye urefu wa
kilometa 234.3, itakayogharimu Sh bilioni 209.3
“Ndugu zangu kazi hii ni ngumu, wapo watu ambao hawataki mimi na
Serikali yangu kuwatumbua, nitapambana hadi nihakikishe ninafanikiwa.
“Na iwapo nitashindwa hakuna sababu ya mimi kuendelea kuwa Rais wa nchi hii, ni bora nirudi nyumbani kwangu kulala,” alisema. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
ALIYEDAI HAKUNA 'MUNGU' ASHITAKIWA
Mwanamume aliyeandika kwamba hakuna Mungu katika majibizano mtandaoni ameshtakiwa kusini mwa Urusi. Viktor
Krasnov aliripotiwa kwa polisi na wanaume wawili waliokasirishwa na
lugha aliyoitumia wakati wa majibizano katika mtandao wa kijamii wa
Kirusi wa VKontakte mwaka 2014.
Mtandao huyo hufanana sana na Facebook na ni maarufu sana. Ameshtakiwa Stavropol kwa kosa la "kutusi hisia za waumini”. "Matusi” kama hayo yaliharamishwa kisheria mwaka 2013 baada ya kesi ya Pussy Riot. Wakati
wa majibizano hayo, Bw Krasnov anadaiwa pia kupuuzilia mbali Biblia na
kusema ni “mkusanyiko wa hadithi za kubuni za Wayahudi”.
Wataalamu wa lugha waliunga mkono msimamo wa Bw Krasnov kwamba maandishi yake yalikuwa “matusi kwa waumini” hao. Kwa
mujibu wa sheria ya Urusi, akipatikana na hatia, anaweza kufungwa jela
mwaka mmoja na kutozwa faini ya hadi $4,083) au kufanyishwa kazi ngumu
saa 240. Like page yetu ya facebook Jambo Tz.
RATIBA YA LIGI KUU TANZANIA BARA WEEKEND HII
Wachezaji wa Timu ya Yanga
Ligi kuu ya Tanzania itaendelea tena mwisho wa wiki hii kwa nyasi za viwanja mbalimbali kuwaka moto. Hapo
kesho katika dimba la taifa Jijini Dar es Salaam kutachezwa mchezo wa
wababe wawili wa soka Azam Fc watakaowakabili vinara wa ligi hiyo Yanga.
Huku African Sport wakiwa nyumbani katika uwanja wa mkwakwani kukipiga na Majimaji.
Toto
Africans,watakua katika uwanja wa Kirumba, kupepetana na Ndanda FC.
Kagera Sugar wao watakuwa na kibarua kizito dhidi ya Mgambo JKT.
Kikosi
cha JKT Ruvu kitawaalika Mwadui Fc, toka Mkoani shinyanga wakati
Wajelajela wa Tanzania Prisons watakua wenyeji wa Stand United, nao
wakata miwa wa Mtibwa watapimana ubavu na Coastal Union.
Jumapili
utapigwa mchezo mmoja ambapo Wekundu wa Msimbazi watakuwa na kibarua
kizito cha kuwakabili Mbeya City mchezo utakaochezwa kwenye uwanja wa
Taifa Dar es Salaam. Like page yetu ya facebook Jambo Tz.
Subscribe to:
Posts (Atom)