Friday, March 04, 2016

MAGUFULI "MAJIPU YAKINISHINDA SINA SABABU YA KUENDELEA KUWA RAIS"

RAIS Dk. John Magufuli, amesema kama atashindwa kutumbua majipu dhidi ya wazembe na wabadhirifu serikalini, hana sababu ya kuendelea kushika wadhifa huo.

Amesema endapo hali hiyo ikitokea ni bora arudi nyumbani kwake akalale, kwa sababu lengo lake la kuwapatia wananchi Tanzania mpya, litakuwa halijatimia.

Rais Dk. Magufuli aliyasema hayo jana, wakati wa hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya Arusha-Holili yenye urefu wa kilometa 234.3, itakayogharimu Sh bilioni 209.3
“Ndugu zangu kazi hii ni ngumu, wapo watu ambao hawataki mimi na Serikali yangu kuwatumbua, nitapambana hadi nihakikishe ninafanikiwa.

“Na iwapo nitashindwa hakuna sababu ya mimi kuendelea kuwa Rais wa nchi hii, ni bora nirudi nyumbani kwangu kulala,” alisema. Like page yetu ya facebook Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MACHI 04, 2016

20160304_053145
20160304_053212
20160304_053230 
Like page yetu ya facebook Jambo Tz

ALIYEDAI HAKUNA 'MUNGU' ASHITAKIWA

Mwanamume aliyeandika kwamba hakuna Mungu katika majibizano mtandaoni ameshtakiwa kusini mwa Urusi. Viktor Krasnov aliripotiwa kwa polisi na wanaume wawili waliokasirishwa na lugha aliyoitumia wakati wa majibizano katika mtandao wa kijamii wa Kirusi wa VKontakte mwaka 2014.

Mtandao huyo hufanana sana na Facebook na ni maarufu sana. Ameshtakiwa Stavropol kwa kosa la "kutusi hisia za waumini”. "Matusi” kama hayo yaliharamishwa kisheria mwaka 2013 baada ya kesi ya Pussy Riot. Wakati wa majibizano hayo, Bw Krasnov anadaiwa pia kupuuzilia mbali Biblia na kusema ni “mkusanyiko wa hadithi za kubuni za Wayahudi”.

Wataalamu wa lugha waliunga mkono msimamo wa Bw Krasnov kwamba maandishi yake yalikuwa “matusi kwa waumini” hao. Kwa mujibu wa sheria ya Urusi, akipatikana na hatia, anaweza kufungwa jela mwaka mmoja na kutozwa faini ya hadi $4,083) au kufanyishwa kazi ngumu saa 240. Like page yetu ya facebook Jambo Tz.

RATIBA YA LIGI KUU TANZANIA BARA WEEKEND HII

Wachezaji wa Timu ya Yanga
 
Ligi kuu ya Tanzania itaendelea tena mwisho wa wiki hii kwa nyasi za viwanja mbalimbali kuwaka moto. Hapo kesho katika dimba la taifa Jijini Dar es Salaam kutachezwa mchezo wa wababe wawili wa soka Azam Fc watakaowakabili vinara wa ligi hiyo Yanga.
Wachezaji wa Timu ya Simba 

Huku African Sport wakiwa nyumbani katika uwanja wa mkwakwani kukipiga na Majimaji.
Toto Africans,watakua katika uwanja wa Kirumba, kupepetana na Ndanda FC. Kagera Sugar wao watakuwa na kibarua kizito dhidi ya Mgambo JKT.

Kikosi cha JKT Ruvu kitawaalika Mwadui Fc, toka Mkoani shinyanga wakati Wajelajela wa Tanzania Prisons watakua wenyeji wa Stand United, nao wakata miwa wa Mtibwa watapimana ubavu na Coastal Union.

Jumapili utapigwa mchezo mmoja ambapo Wekundu wa Msimbazi watakuwa na kibarua kizito cha kuwakabili Mbeya City mchezo utakaochezwa kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Like page yetu ya facebook Jambo Tz.

UGANDA NDIO TIMU BORA AFRIKA MASHARIKI

Timu ya taifa ya Uganda

Timu ya taifa ya Cape Verde 
 
Cape Verde wametua kileleni mwa orodha ya Fifa ya uchezaji kandanda barani Afrika ya mwezi Machi. Huo ni ufanisi mkubwa kwa taifa hilo linalojumuisha visiwa kadha vidogo kaskazini magharibi mwa Afrika.

Wamefanikiwa kuwapita mabingwa wa Afrika wa mwaka 2015 Ivory Coast ambao wameshuka hadi nambari mbili. Cameroon pia wameimarika, na kuingia katika orodha ya 10 bora na kuwaondoa Guinea.

Licha ya kushinda Kombe la Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wameshuka nafasi moja hadi nambari 58. Miongoni mwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, Uganda inaongoza ikiwa nambari 67, ikifuatiwa na Rwanda (85), Kenya (103), Tanzania (125), Burundi (129) na Sudan Kusini (140). Like page yetu ya facebook Jambo Tz.

"ARSENAL HATUJIAMINI" SANCHEZ

Alexi Sanchez 
Kiungo wa kati wa Arsenal Alexis Sanchez amesema kuwa Arsenal haina imani kwamba itashinda ligi ya Uingereza baada ya kushindwa mara mbili mfululizo na Manchester United na Swansea. The Gunners walipoteza 3-2 katika uwanja wa Old Trafford na 2-1 nyumbani dhidi ya Swansea na hivyobasi kuwa pointi sita nyuma ya viongozi wa ligi Leicester.

''Mara nyingine tunakosa motisha kwamba tayari tumeshinda 1-0 tunapoelekea uwanjani'',aliiambia Directiv Sport kabla ya mechi dhidi ya United.''Tunakosa ile ari kwamba tunaweza kuwa mabingwa''. Sanchez aliongea: Iwapo tutaingia katika uwanja na ari ya kuwa mabingwa ,kushinda ligi ama hata kombe la vilabu bingwa Ulaya,tunaweza kuafikia hilo.

''Ninakumbuka mechi dhidi ya Manchester United mwaka uliopita.Wachezaji walikuwa na motisha ya kushinda taji tulipoingia uwanjani.Tuliwashinda katika dakika 20 na kupata 3-0.Tulikuwa na ari na kujiamini siku hiyo''. Arsenal imeshinda mara tatu pekee kutoka mechi 11 katika mashindano yote na wako katika nafasi ya tatu katika ligi.

Tuesday, March 01, 2016

DAKTARI ASIMAMISHWA KAZI KISA LAKI MOJA

Baada ya kufichua uozo katika bandari tatu kubwa hapa nchini, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amehamia katika afya baada ya kumsimamisha kazi daktari wa kitengo cha upasuaji katika Hospitali ya Ligula, Fortunatus Namahala kwa madai ya kumuomba mgonjwa rushwa ya Sh100,000.

Waziri Mkuu alichukua hatua hiyo jana alipotembelea hospitali hiyo ya mkoa na kukabiliwa na Tatu Abdallah ambaye alidai kwamba alilazimika kuuza shamba lake la ekari 2.5 ili apate Sh100,000 kwa ajili ya upasuaji wa baba yake.

“Februari Mosi nilimleta baba yangu hapa nikaambiwa anatakiwa kufanyiwa upasuaji. Nikaandikiwa ninunue dawa za Sh85,000 hapo nje kwenye duka la dawa pia uzi wa kushonea kwa Sh25,000. Lakini pia daktari akasema anataka Sh100,000 ya kwake. Lakini hadi Februari 7 hakufanyiwa huo upasuaji,” alidai.

'SERIKALI YA AWAMU YA NNE ILIJAA KULEANA' JANUARY MAKAMBA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, January Makamba amesema uwajibikaji katika utawala wa Serikali ya Awamu ya Nne haukuwa wa kuridhisha kwa sababu kulikuwa na utamaduni wa kuoneana haya, kujuana, kusitiriana na kutoogopa.

Amesema hayo yalikuwa yakitokea kwa kuwa waliokuwa wakifanya makosa hawakuwa wakichukuliwa hatua na hivyo kujengeka utamaduni wa watu kutoogopa, lakini sasa utawala mpya umeonyesha kuchukua hatua dhidi bila ya woga.

Makamba, ambaye aliingia tano bora ya mbio za urais ndani ya CCM kabla ya kuangushwa kwenye kikao cha Halmashauri Kuu, alitoa kauli hiyo juzi katika mahojiano maalumu na Mwananchi ofisini kwake jijini Dar es Salaam juzi.

Thursday, February 18, 2016

Saturday, February 13, 2016

MWANAMKE ALIYEWAPORA SILAHA MAJAMBAZI APEWA ZAWADI NA JESHI LA POLISI

http://jambotz8.blogspot.com/
Sophia Manguye akisaini mara baada ya kukabidhiwa zawadi yake.
Mwanamke aliyepambana na jambazi na kufanikiwa kumnyang’anya bunduki aina ya SMG, Sophia Manguye (46), amepewa zawadi ya Sh 500,000 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Tarime/Rorya, Gemini Mushy.

Mwanamke huyo ambaye aliomba Serikali kumpa silaha ili kujilinda, alisema kuwa hajaridhika na zawadi hiyo kwa kuwa kama asingemmudu jambazi huyo watu wengi wangepoteza maisha.
http://jambotz8.blogspot.com/
Hata hivyo, Mushy alimwomba Manguye kupokea kiasi hicho japokuwa ni kidogo kwa kuwa ni zawadi kutoka ofisi yake. Like page yetu ya facebook Jambo Tz

UTAFITI: UMAARUFU WA MAGUFULI WAONGEZEKA LOWASSA WASHUKA...!!!

Matokeo ya utafiti mpya uliofanywa mapema mwezi huu yanaonyesha kuwa umaarufu wa Rais John Magufuli umeongezeka kufikia asilimia 74.5, akimuacha mbali mpinzani wake wa karibu kwenye Uchaguzi Mkuu, Edward Lowassa.

Magufuli alishinda mbio za urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, akipata asilimia chache kuliko wagombea wengine kutoka CCM, lakini amejiongezea umaarufu kutokana na hatua ambazo amekuwa akichukua tangu alipoapishwa Novemba 5, 2015.

Katika uchaguzi huo, Dk Magufuli alipata kura milioni 8.8 sawa na asilimia 58.47, akifuatiwa na Lowassa aliyepata kura milioni 6.07, sawa na asilimia 39.97. Like page yetu ya facebook Jambo Tz

PICHA YA DEREVA WA BASI LA SIMBA MTOTO ENZI ZA UHAI WAKE

http://jambotz8.blogspot.com/
Fred Venance enzi za uhai wake.

Huyu ndiye aliyekuwa dereva wa bus la Simba Mtoto lililopata ajali juzi . Taarifa zinasema ametoka kufunga ndoa Jumapili iliyopita tu. Baba wa kijana huyu ni dereva wa bus la Tashriff.
http://jambotz8.blogspot.com/

http://jambotz8.blogspot.com/
Like page yetu ya facebook Jambo Tz
http://jambotz8.blogspot.com/
http://jambotz8.blogspot.com/
Watu 11 akiwamo mama, mwanawe na mjukuu wake wamekufa papohapo na wengine 34 kujeruhiwa katika ajali ya basi la kampuni ya Simba Mtoto lililogongana uso kwa uso na lori. Familia iliyopatwa na janga hilo ni ya mwandishi wa habari mwandamizi wa Redio ya Mlimani, Hamis Dambaya aliyefiwa na mkewe, Raya Said, mtoto wake Nargis Hamis na mama mkwe wake ambaye jina lake halikutambuliwa mara moja. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
Watu 11 akiwamo mama, mwanawe na mjukuu wake wamekufa papohapo na wengine 34 kujeruhiwa katika ajali ya basi la kampuni ya Simba Mtoto lililogongana uso kwa uso na lori. Familia iliyopatwa na janga hilo ni ya mwandishi wa habari mwandamizi wa Redio ya Mlimani, Hamis Dambaya aliyefiwa na mkewe, Raya Said, mtoto wake Nargis Hamis na mama mkwe wake ambaye jina lake halikutambuliwa mara moja

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI FEBRUARI 13, 2016

DSCN0208 DSCN0209 DSCN0210
Like page yetu ya facebook Jambo Tz

UFISADI WA SHILINGI MILIONI 20 WAZUA TAFRANI MSIKITINI JIJINI DAR ES SALAAM


Waumini wa dini ya Kiislam wakizozana nje ya Msikiti wa Masjidi Pelapela uliopo eneo la Mtakuja Vingunguti jijini Dar es Salaam katika swala ya Ijumaa leo mchana, baada ya kutokea tafrani ya waumini hao dhidi ya viongozi wao ambao wanatuhumiwa kutafuna fedha zaidi ya sh.milioni 20 walizochanga kwa ajili ya ujenzi wa msikiti mpya.
Muumini wa Msikiti huo, Mbarouk Mohamed Makame (kushoto), akizungumza kuhusu fedha hizo zinazodaiwa kutumiwa vibaya na viongozi wao. Kulia ni mmoja wa wazee wa msikiti huo, Mzee Selasela.
 Mzee Selasela akionesha dari la msikiti huo lililochakaa ambapo fedha hizo zinazodaiwa kutumiwa vibaya na viongozi wao zingesaidia kuufanyia ukarabati. Like page yetu ya facebook Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...