Friday, March 04, 2016

UGANDA NDIO TIMU BORA AFRIKA MASHARIKI

Timu ya taifa ya Uganda

Timu ya taifa ya Cape Verde 
 
Cape Verde wametua kileleni mwa orodha ya Fifa ya uchezaji kandanda barani Afrika ya mwezi Machi. Huo ni ufanisi mkubwa kwa taifa hilo linalojumuisha visiwa kadha vidogo kaskazini magharibi mwa Afrika.

Wamefanikiwa kuwapita mabingwa wa Afrika wa mwaka 2015 Ivory Coast ambao wameshuka hadi nambari mbili. Cameroon pia wameimarika, na kuingia katika orodha ya 10 bora na kuwaondoa Guinea.

Licha ya kushinda Kombe la Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wameshuka nafasi moja hadi nambari 58. Miongoni mwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, Uganda inaongoza ikiwa nambari 67, ikifuatiwa na Rwanda (85), Kenya (103), Tanzania (125), Burundi (129) na Sudan Kusini (140). Like page yetu ya facebook Jambo Tz.

Mataifa yanayoshika mkia Afrika n Somalia, Eritrea na Djibouti, yote yakiwa nambari 204.
Duniani, Ubelgiji wanaongoza wakifuatwa na Argentina. Like page yetu ya facebook Jambo Tz.

Hii hapa ndiyo orodha ya Fifa ya mataifa bora Afrika Machi:

  1. Visiwa vya Cape Verde
  2. Ivory Coast
  3. Algeria
  4. Ghana
  5. Tunisia
  6. Senegal
  7. Misri
  8. DR Congo
  9. Congo
  10. Cameroon

Orodha ya 10 bora duniani

  1. Ubelgiji
  2. Argentina
  3. Uhispania
  4. Ujerumani
  5. Chile
  6. Brazil
  7. Ureno
  8. Colombia
  9. England
  10. Austria

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...