Friday, March 04, 2016

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MACHI 04, 2016

20160304_053145
20160304_053212
20160304_053230 
Like page yetu ya facebook Jambo Tz

ALIYEDAI HAKUNA 'MUNGU' ASHITAKIWA

Mwanamume aliyeandika kwamba hakuna Mungu katika majibizano mtandaoni ameshtakiwa kusini mwa Urusi. Viktor Krasnov aliripotiwa kwa polisi na wanaume wawili waliokasirishwa na lugha aliyoitumia wakati wa majibizano katika mtandao wa kijamii wa Kirusi wa VKontakte mwaka 2014.

Mtandao huyo hufanana sana na Facebook na ni maarufu sana. Ameshtakiwa Stavropol kwa kosa la "kutusi hisia za waumini”. "Matusi” kama hayo yaliharamishwa kisheria mwaka 2013 baada ya kesi ya Pussy Riot. Wakati wa majibizano hayo, Bw Krasnov anadaiwa pia kupuuzilia mbali Biblia na kusema ni “mkusanyiko wa hadithi za kubuni za Wayahudi”.

Wataalamu wa lugha waliunga mkono msimamo wa Bw Krasnov kwamba maandishi yake yalikuwa “matusi kwa waumini” hao. Kwa mujibu wa sheria ya Urusi, akipatikana na hatia, anaweza kufungwa jela mwaka mmoja na kutozwa faini ya hadi $4,083) au kufanyishwa kazi ngumu saa 240. Like page yetu ya facebook Jambo Tz.

RATIBA YA LIGI KUU TANZANIA BARA WEEKEND HII

Wachezaji wa Timu ya Yanga
 
Ligi kuu ya Tanzania itaendelea tena mwisho wa wiki hii kwa nyasi za viwanja mbalimbali kuwaka moto. Hapo kesho katika dimba la taifa Jijini Dar es Salaam kutachezwa mchezo wa wababe wawili wa soka Azam Fc watakaowakabili vinara wa ligi hiyo Yanga.
Wachezaji wa Timu ya Simba 

Huku African Sport wakiwa nyumbani katika uwanja wa mkwakwani kukipiga na Majimaji.
Toto Africans,watakua katika uwanja wa Kirumba, kupepetana na Ndanda FC. Kagera Sugar wao watakuwa na kibarua kizito dhidi ya Mgambo JKT.

Kikosi cha JKT Ruvu kitawaalika Mwadui Fc, toka Mkoani shinyanga wakati Wajelajela wa Tanzania Prisons watakua wenyeji wa Stand United, nao wakata miwa wa Mtibwa watapimana ubavu na Coastal Union.

Jumapili utapigwa mchezo mmoja ambapo Wekundu wa Msimbazi watakuwa na kibarua kizito cha kuwakabili Mbeya City mchezo utakaochezwa kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Like page yetu ya facebook Jambo Tz.

UGANDA NDIO TIMU BORA AFRIKA MASHARIKI

Timu ya taifa ya Uganda

Timu ya taifa ya Cape Verde 
 
Cape Verde wametua kileleni mwa orodha ya Fifa ya uchezaji kandanda barani Afrika ya mwezi Machi. Huo ni ufanisi mkubwa kwa taifa hilo linalojumuisha visiwa kadha vidogo kaskazini magharibi mwa Afrika.

Wamefanikiwa kuwapita mabingwa wa Afrika wa mwaka 2015 Ivory Coast ambao wameshuka hadi nambari mbili. Cameroon pia wameimarika, na kuingia katika orodha ya 10 bora na kuwaondoa Guinea.

Licha ya kushinda Kombe la Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wameshuka nafasi moja hadi nambari 58. Miongoni mwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, Uganda inaongoza ikiwa nambari 67, ikifuatiwa na Rwanda (85), Kenya (103), Tanzania (125), Burundi (129) na Sudan Kusini (140). Like page yetu ya facebook Jambo Tz.

"ARSENAL HATUJIAMINI" SANCHEZ

Alexi Sanchez 
Kiungo wa kati wa Arsenal Alexis Sanchez amesema kuwa Arsenal haina imani kwamba itashinda ligi ya Uingereza baada ya kushindwa mara mbili mfululizo na Manchester United na Swansea. The Gunners walipoteza 3-2 katika uwanja wa Old Trafford na 2-1 nyumbani dhidi ya Swansea na hivyobasi kuwa pointi sita nyuma ya viongozi wa ligi Leicester.

''Mara nyingine tunakosa motisha kwamba tayari tumeshinda 1-0 tunapoelekea uwanjani'',aliiambia Directiv Sport kabla ya mechi dhidi ya United.''Tunakosa ile ari kwamba tunaweza kuwa mabingwa''. Sanchez aliongea: Iwapo tutaingia katika uwanja na ari ya kuwa mabingwa ,kushinda ligi ama hata kombe la vilabu bingwa Ulaya,tunaweza kuafikia hilo.

''Ninakumbuka mechi dhidi ya Manchester United mwaka uliopita.Wachezaji walikuwa na motisha ya kushinda taji tulipoingia uwanjani.Tuliwashinda katika dakika 20 na kupata 3-0.Tulikuwa na ari na kujiamini siku hiyo''. Arsenal imeshinda mara tatu pekee kutoka mechi 11 katika mashindano yote na wako katika nafasi ya tatu katika ligi.

Tuesday, March 01, 2016

DAKTARI ASIMAMISHWA KAZI KISA LAKI MOJA

Baada ya kufichua uozo katika bandari tatu kubwa hapa nchini, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amehamia katika afya baada ya kumsimamisha kazi daktari wa kitengo cha upasuaji katika Hospitali ya Ligula, Fortunatus Namahala kwa madai ya kumuomba mgonjwa rushwa ya Sh100,000.

Waziri Mkuu alichukua hatua hiyo jana alipotembelea hospitali hiyo ya mkoa na kukabiliwa na Tatu Abdallah ambaye alidai kwamba alilazimika kuuza shamba lake la ekari 2.5 ili apate Sh100,000 kwa ajili ya upasuaji wa baba yake.

“Februari Mosi nilimleta baba yangu hapa nikaambiwa anatakiwa kufanyiwa upasuaji. Nikaandikiwa ninunue dawa za Sh85,000 hapo nje kwenye duka la dawa pia uzi wa kushonea kwa Sh25,000. Lakini pia daktari akasema anataka Sh100,000 ya kwake. Lakini hadi Februari 7 hakufanyiwa huo upasuaji,” alidai.

'SERIKALI YA AWAMU YA NNE ILIJAA KULEANA' JANUARY MAKAMBA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, January Makamba amesema uwajibikaji katika utawala wa Serikali ya Awamu ya Nne haukuwa wa kuridhisha kwa sababu kulikuwa na utamaduni wa kuoneana haya, kujuana, kusitiriana na kutoogopa.

Amesema hayo yalikuwa yakitokea kwa kuwa waliokuwa wakifanya makosa hawakuwa wakichukuliwa hatua na hivyo kujengeka utamaduni wa watu kutoogopa, lakini sasa utawala mpya umeonyesha kuchukua hatua dhidi bila ya woga.

Makamba, ambaye aliingia tano bora ya mbio za urais ndani ya CCM kabla ya kuangushwa kwenye kikao cha Halmashauri Kuu, alitoa kauli hiyo juzi katika mahojiano maalumu na Mwananchi ofisini kwake jijini Dar es Salaam juzi.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...