Tuesday, February 09, 2016

MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA POLE KWA MKE WA PINDA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemtumia salamu za pole Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu Mama Tunu Pinda aliyepatwa na ajali ya gari, iliyotokea jana tarehe 08 Februari, 2016 akiwa safarini kutoka Dodoma kwenda Dar es salaam.

Ajali hiyo imetokea katika eneo la Mkundi lililopo katika Manispaa ya Morogoro ambapo gari aliyokuwa akisafiria Mama Tunu Pinda, ilipinduka baada ya kumgonga mwendesha pikipiki aliyeingia ghafla barabarani.

Katika salamu hizo alizozituma kupitia kwa Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda, Rais Magufuli amesema amepokea kwa mshtuko taarifa za kutokea kwa ajali hiyo na amemuombea Mama Pinda na Majeruhi wengine kupona haraka.

"Kupitia kwako Mheshimiwa Waziri Mkuu Pinda, naomba unifikishie pole nyingi kwa mkeo Mama Pinda kwa kuumia katika ajali hii, na namuomba Mwenyezi Mungu awaponye majeruhi wote ili waweze kuendelea na shughuli zao za kila siku" alisema Rais Magufuli.

Mama Tunu Pinda anaendelea kupata matibabu Jijini Dar es salaam, na hali yake inaendelea vizuri.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dodoma
09 Februari, 2016

MAGAZETI YA LEO JUMANNE FEBRUARI 09, 2016


DSC00926 DSC00927 DSC00928 

Like page yetu ya facebook Jambo Tz

Friday, February 05, 2016

HAYA NDIO MAGARI MAPYA YA POLISI UGANDA


 Magari Maalum ya Jeshi la Polisi la Uganda yakiwa yamewasili Bandari ya Mombasa Nchini Kenya, tayari kwa safari ya kuelekea Kampala.

Jeshi la Polisi la Uganda limejiimarisha zaidi kipindi hiki cha kampeni na hasa siku ya Uchaguzi utakaofanyika hivi karibuni.


MAGUFULI: MIMI SI KICHAA WALA DIKTETA

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Magufuli.


RAIS Dk. John Magufuli amesema anapochukua hatua yeye si kichaa, si dikteta, si shetani wala si mnyama, ila ni mpole, lakini amefika mahali lazima afanye hivyo kwani ndani ya Serikali yanafanyika mambo ya ajabu.

Kauli hiyo aliitoa jana jijini Dar es Salaam katika kilele cha Siku ya Sheria nchini, alipokuwa mgeni rasmi kwa mara ya kwanza katika uzinduzi wa Mwaka wa Mahakama tangu alipoapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Alisifu kazi kubwa inayofanywa na Idara ya Mahakama, huku akitangaza uamuzi wa gharama za kurusha matangazo ya moja kwa moja ya Bunge zaidi ya Sh bilioni nne ni bora zikawasaidia wananchi.

“Ninapochukua hatua mimi si mnyama, si dikteta, si shetani, ni mpole kweli, lakini inafika mahali lazima nifanye, yanayofanyika serikalini ni mambo ya ajabu sana, nataka kutoa sadaka yangu, inawezekana hata nikifa naweza kuwa rais wa malaika,” alisema.

Alipongeza kazi kubwa inayofanywa na mahakama huku akibaki kujiuliza kwanini katika maadhimisho ya siku yao hawarushi matangazo yao moja kwa moja kupitia luninga.

“Mnafanya kazi kubwa, nilipofika niliuliza kwanini hii siku yenu hamrushi ‘live’, nikajibiwa fedha za kurusha ‘live’ zinapelekwa kuwahudumia wananchi.

UBELGIJI VINARA VIWANGO VYA UBORA FIFA


 Ubelgiji imeendelea kukaa katika nafasi ya kwanza kwenye viwango vya ubora vya FIFA kwa muhjibu wa viwango viliyotolewa Alhamisi.

Katika kumi Bora imebaki vile vile bila mabadiliko huku Mabingwa wa Dunia, Germany, wakiwa Nafasi ya 4.

Ivory Coast imeporomoka hadi Nafasi ya 9 kwa bara la afrika na sasa ipo Nafasi ya 28 Duniani ikifuatiwa na Cape Verde ambayo ipo Nafasi ya 33 baada ya kupanda Nafasi huku Algeria ikiwa Nafasi ya 36 baada ya kushuka Nafasi 8.

Timu nyingine katika ishirini bora ni Ubeligiji, Argentina, Uhispania, Ujerumani na Chile.

20 bora katika viwango vya Fifa.

1 Ubelgiji

2 Argentina

3 Uhispania

4 Ujerumani

5 Chile

6 Brazil

7 Portugal

8 Colombia

9 England

10 Austria

11 Uruguay

12 Switzerland

13 Ecuador

14 Uholanzi

15 Italy

16 Romania

17 Wales

18 Croatia

19 Hungary

20 Uturuki

Friday, January 22, 2016

UCHAGUZI ZANZIBAR KURUDIWA MACHI 20

Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) imetangaza tarehe ya marudio ya uchaguzi visiwani humo baada ya matokeo ya uchaguzi uliopita kufutwa.

Uchaguzi huo sasa utafanyika Jumapili tarehe 20 Machi. Tangazo hilo limefanywa na mwenyekiti wa ZEC Jecha Salim Jecha. Bw Jecha amesema tarehe hiyo iliamuliwa na tume baada ya mkutano hapo jana.

"Uchaguzi huo utahusisha uchaguzi wa Rais, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani na hakutakuwa na uteuzi mpya wa wagombea wala mikutano ya kampeni," amesema Bw Jecha.

"Wagombea wote walioteuliwa hapo awali wataendelea kuwa wagombea katika uchaguzi huu."

Chama cha Wananchi (CUF) kimekuwa kikipinga kurudiwa kwa uchaguzi. Chama hicho mapema mwezi huu kilionya kwamba hatua hiyo inaweza kusababisha vurugu. Viongozi wa chama hicho walisusia maadhimisho ya Siku ya Mapinduzi wiki iliyopita.

Chama tawala, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilikuwa tayari kimewashauri wanachama wake visiwani wajiandae kwa marudio ya uchaguzi, tangazo lililoshutumiwa vikali na viongozi wa CUF.

ANGALIA PICHA ZA RAIS DR. MAGUFULI AKIWA KATIKA VAZI LA JESHI...!!!

http://jambotz8.blogspot.com/

http://jambotz8.blogspot.com/
Amiri Jeshi Mkuu, Rais Dr. Magufuli akiwasikiliza wananchi kwa makini alipopita maeneno ya Sanawali kuwasalimia wakati akielekea Wilayani Monduli.

Thursday, January 21, 2016

MAGUFULI AMTEUA KIKWETE KUWA MKUU WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM

Rais wa Tanzania Dkt John Magufuli amemteua Rais mstaafu Dkt Jakaya Kikwete kuwa mkuu wa chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Tangazo la uteuzi huo limetolewa na katibu mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue.

Uteuzi huo umeanza kutekelezwa tarehe 17 Januari.

Balozi Nicholas Kuhanga amekuwa akishikilia wadhifa huo kama kaimu, kwa mujibu wa tovuti ya chuo kikuu hicho.

ANGALIA PICHA ZA RAIS DR. MAGUFULI AKISHONA NGUO KWA CHEREHANI...!!!


 Rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli akionesha umahiri wake wa kutumia Cherehani na kushona nguo za wafanyakazi wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kuvifahamu vitengo mbalimbali na watumishi wake wa  Ikulu jijini Dar es salaam jana Januari 20, 2016.

Saturday, January 16, 2016

UKAWA YASHINDA KITI CHA UMEYA KINONDONI

Diwani wa Kata ya Ubungo kupitia chama cha demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Boniface Jacob ameshinda kiti cha Umeya wa Manispaa ya kinondoni kwa jumla ya kura 38 kati ya 58 zilizo pigwa.

Boniface alikuwa akichuana na mgombea mwenzake ambaye ni mtoto wa kada wa Chama cha Mapinduzi Benjamin Sitta ambaye alikuwa mgombea udiwani katika jimbo la Kawe na hqkufanikiwa kushinda.

Friday, January 08, 2016

WAZIRI ACHUKIZWA NA MADARAJA YA UFAULU

VITA ya kupambana na utendaji kazi usiokuwa na tija kwa Taifa kwa watendaji wengi wa taasisi za Serikali imezidi kushika kasi baada ya Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, kumtaka Katibu wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), Dk. Charles Msonde kumwandikia maelezo ya kitaalamu yaliyosababisha kubadilishwa kwa mfumo wa upangaji viwango vya ufaulu kutoka wa madaraja (Division) hadi wastani wa pointi (GPA).

Pia amemtaka kumweleza sababu zilizowafanya kuongeza mtihani (Continuous Assesment) kwa wanafunzi wa kujitegemea ili ajiridhishe pamoja na viongozi wengine wa wizara iwapo mabadiliko hayo yana tija kwa Taifa au la.

Profesa Ndalichako alitoa agizo hilo jana wakati akizungumza kwenye kikao cha menejimenti ya baraza hilo.

MKAPA AJITOSA KUMSAIDIA MAGUFULI

Rais Dk John Magufuli akizungumza na Rais Mstaafu wa Awamu ya tatu Benjamin William Mkapa Ikulu jijini Dar. Picha na Ikulu

Rais mstaafu Benjamin Mkapa amesema yuko tayari kufanya kazi yoyote na kutoa ushirikiano wake kwa serikali ya Rais John Magufuli endapo atahitajika.

Mkapa aliyeambatana na Waziri Mkuu Mstaafu Joseph Warioba ametoa kauli hiyo jana punde baada ya kukutana na Rais John Magufuli Ikulu, Dar es Salaam.

“Rais Mstaafu Mkapa pia amemhakikishia Rais Magufuli kuwa yuko tayari kutoa ushirikiano wakati wote ama kufanya kazi yoyote endapo atahitajika kufanya hivyo,” taarifa iliyotolewa na Ikulu jana mchana imeeleza.

SAMATTA, AUBAMEYANG WATISHA TUZO ZA AFRIKA

Mwanasoka raia wa Tanzania anayechezea TP Mazembe ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Mmbwana Ally Samatta amenyakua tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika anachezea ndani ya bara la Afrika. Huku tuzo ya mwanasoka bora barani Afrika ikienda kwa Pierre-Emerick raia wa Gabon anayesakata kabumbumbu katika klabu ya Borusia Dotmund nchini Ujerumani.

Tuzo hizo za kila mwaka zinazotolewa na Shirikisho la soka barani Afrika almaarufu kama CAF zimetolewa usiku kuamkia Ijumaa mjini Abuja nchini Nigeria.

Kwa upande wa timu ya wanawake ya mwaka tuzo imekwenda kwa timu ya Cameroon

YANGA YATINGA NUSU FAINALI MAPINDUZI CUP

Mabingwa wa Tanzania Bara Timu ya Yanga, imefanikiwa kutinga hatua ya Nusu fainali kufuatia ushindi wa Bao 2-1 dhidi ya Mtibwa mabao ambayo yamefungwa na wachezaji Aboubakar na Malimi Busungu na kuwa kinara wa kundi B la michuano ya kombe la Mapinduzi baada ya kujikusanyia jumla ya pointi 7.

Katika mchezo mwingine wa mapema kutinga hatua ya nu Nusu Fainali Timu ya Mafunzo imeichapa Azam FC 2-1 kwa ushindi usio na faida kwa timu hiyo baada ya kutupwa nje ya mashindano hayo kwa uchache wa pointi.

Yanga sasa watacheza Nusu Fainali na Mshindi wa Pili wa Kundi A na Mtibwa Sugar kukutana na Mshindi wa Kundi hilo.

Kundi A linamaliza Mechi zake leo Ijumaa kwa Timu ya Jamhuri kuchuana na URA na Simba ikicheza na JKU huku kila Timu ikiwa ina nafasi kutinga Nusu Fainali ikipata matokeo mazuri ingawa Sare kwa Simba itawafikisha Nusu Fainali wakati URA na Jamhuri zikihitaji ushindi.

Thursday, January 07, 2016

MTOTO WA KARUME ASHAURI SHEIN KUKAA PEMBENI

Mwanasheria wa kujitegemea nchini, Fatma ofisinakizungumzaini Dar es Salaam jana. Picha na Florence Majani

Dar es Salaam: Mwanasheria wa kujitegemea nchini, Fatma Karume amemshauri Rais wa Zanzibar, Ali Mohamed Shein kuachia madaraka.

“Dk Shein lazima aondoke kwa sababu kuendelea kubaki madarakani ni kuwanyang’anya Wazanzibari haki yao ya msingi,” alisema Fatma ambaye ni mtoto wa aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Fatma alisema kuwa mzozo wa Zanzibar umesababishwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salum Jecha kutangaza kufutwa matokeo yote ya Uchaguzi Mkuu visiwani humo wakati hana mamlaka kisheria kufanya hivyo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...