Monday, August 10, 2015

WAALIOMUUA JENERALI NSHIMIRIMANA WAKAMATWA

Kiongozi wa mashtaka nchini Burundi amesema kuwa watu kadhaa wanaoshukiwa kutekeleza mauaji ya jenerali Adolphe Nshimirimana wamekamatwa. Hata hivyo Afisa huyo anasema kuwa viongozi waliopanga njama ya kumua jenerali huyo wangali wanasakwa.
Kufuatia mauaji ya kiongozi huyo wa kikosi cha ulinzi wa rais wa Burundi Pierre Nkurunziza, Mwanaharakati maarufu wa haki za kibinaadamu nchini humo alipigwa risasi na kujeruhiwa vibaya na watu waliokuwa katika pikipiki .

Pierre Claver Mbonimpa alishambuliwa katika mji mkuu wa Burundi, Bujumbura mapema wiki hii. Mbonimpa amekuwa mkosoaji mkubwa wa tangazo la rais Nkurunziza ya kuwania muhula wa tatu.
Hadi kufikia sasa haijajulikana ni nani aliyekuwa amelenga kumtoa uhai.
Wakati huohuo taharuki imetanda katika mji mkuu wa Bujumbura baada ya milio ya risasi kusikika katika maeno kadha ya mji huo usiku wa kuamkia leo.

Hakuna taarifa zaidi ila habari zinasema huenda wanajeshi kadhaa wameuawa na wengine kujeruhiwa. Inaelezwa milio hiyo ya risasi ilisikika baada ya gari moja kutoka ofisi ya Rais wa nchi hiyo kuchomwa moto.
Burundi imekabiliwa na ghasia tangu hatua ya rais Nkurunziza mnamo mwezi Aprili kutaka kuwania muhula wa tatu. Wapinzani wamedai kwamba hatua hiyo ni kinyume na katiba huku jaribio la mapinduzi likifeli mnamo mwezi Mei.

Uchaguzi wa urais ulifanyika mwezi uliopita ambapo bwana Nkurunziza alishinda lakini ulisusiwa na upinzani.

Friday, August 07, 2015

SOMA MAGAZETI YA LEO AGOSTI 07, YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
. .
Asante kwa kutembelea blog hii, endelea kuwa nasi, like page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

CHENGE AKIRI KUPOKEA SH. 1.6 BILLION

Mh. Andrew Chenge 

Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge amekiri mbele ya Baraza la Maadili kupokea Sh1.6 bilioni kutoka Kampuni ya VIP Enginering and Marketing Limited, zikiwa ni malipo ya kutoa ushauri.

Pia, alihoji kama kuna tatizo kutumia taaluma yake ya sheria kuzishauri kampuni binafsi na kujipatia fedha.
Chenge ambaye alitoa utetezi wake jana saa 7:30 mchana, alisema hakulipwa fedha hizo kwa sababu ni kiongozi wa umma, bali kwa kutoa ushauri.
Alisema aliingia mkataba na kampuni hiyo wa kutoa ushauri wa kisheria dhidi ya Kampuni ya Mechmer ambazo ni kampuni binafsi zilizokuwa na mgogoro. Asante kwa kutembelea blog hii, endelea kuwa nasi, like page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

MTIKISIKO: NI BAADA YA PROF. LIPUMBA KUJIENGUA UENYEKITI CUF

Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim
Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba akiaga waandishi wa habari baada ya kuwatangazia kujivua wadhifa huo katika mkutano alioufanya Dar es Salaam jana.

Hakuna neno jingine linalofaa kuelezea hali ilivyo ndani ya Ukawa zaidi ya “mtikisiko” baada ya Profesa Ibrahim Lipumba kuamua kujivua uenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) wakati mkakati wa vyama vya upinzani kushirikiana kutaka kushika dola ukiwa umeshika kasi.

Uamuzi wa Profesa Lipumba, mmoja wa waasisi wanne wa Ukawa-Umoja wa Katiba ya Wananchi unaoundwa na vyama vinne vya Chadema, CUF, NCCR Mageuzi na NLD-,unamaanisha anapoteza wadhifa wake wa mwenyekiti mwenza wa umoja huo ambao umeamua kushirikiana kwenye Uchaguzi Mkuu kwa kusimamisha mgombea mmoja kuanzia ngazi ya urais hadi udiwani atakayeungwa mkono na vyama hivyo.
Wengine walioongoza harakati za kuasisi Ukawa ni Freeman Mbowe, ambaye ni mwenyekiti wa Chadema, James Mbatia wa NCCR-Mageuzi na Emmanuel Makaidi wa NLD. Asante kwa kutembelea blog hii, endelea kuwa nasi, like page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.

Thursday, August 06, 2015

BAYERN MUNICH MABINGWA WA AUDI


Kikosi cha Bayern munich

Miamba ya soka la Ujerumani Bayern Munich wametwaa ubingwa wa michuano ya Audi mwaka 2015.

Bayern wakicheza katika uwanja wao Allianz Arena Jijini Munich, wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya klabu ya Real Madrid ya Hispania.

Bao la ushindi la Bayern lilifungwa Dakika ya 88 na mshambuliaji Robert Lewandowski,alieunganisha mpira wa adhabu uliopigwa na Douglas Costa.

Katika mchezo wa kumsaka mshindi wa tatu Tottenham Hotspur waliwachapa AC Milan kwa mabao 2-0 kwa mabao ya Nacer Chadli, Dakika ya 8, na Thomas Carroll, Dakika ya 71.

FIORENTINA YAICHAPA CHELSEA KWAO


Kocha wa Chelsea Jose Mourinho

Klabu ya soka ya Fiorentiana ya Italia imewachapa mabingwa wa ligi ya England Chelsea kwa bao 1-0.

Bao pekee la ushindi la Fiorentina ama maarufu kama Viola liliwekwa kimiani na beki Gonzalo Rodríguez raia wa Argentina katika Dakika ya 34 baada ya Kipa wa Chelsea Begovic kutema Shuti la Alonso Mendoza.

Mchezo huu ni wa mwisho wa kirafiki kwa klabu ya Chelsea inayonolewa na Kocha Jose Mournho kabla ya kuanza kwa kipute cha ligi kuu ya Engalnd hapo Augusti 8. Ambapo wataanza utetezi wa ubingwa wao kwa kucheza Mechi yao ya kwanza dhidi ya timu ya Swansea City.

Sunday, August 02, 2015

ANGALIA PICHA YA MH. MAGUFULI AKIWA NA MIAKA 15

Mh. Dr. John Pombe Magufu

Hii picha yake hapa chini ni ya miaka 40 iliyopita akiwa Mwanafunzi wa kidato cha kwanza Katoke Seminari March 1975.

Monday, July 27, 2015

RAIS OBAMA AWASILI NCHINI ETHIOPIA


Rais Barack Obama wa Marekani hatimaye amefika nchini Ethiopia katika ziara yake ya pili ya nchi za Afrika.

Ni mara yake ya kwanza tangu aongoze taifa la Marekani akiwa rais kuhutubia wanachama hamsini na mbili wa umoja wa Afrika katika makao makuu yake yaliyoko Addis ababa.

Mazungumzo yao yakiwa yamelenga kutafuta suluhu ya kutokomeza migogoro ya vita za wenyewe kwa wenyewe sudan ya kusini. 

Rais Obama, aliwasili nchini Ethiopia akiwa anatokea mjini Nairobi ambako aliwaambia wakenya kuwa amna kikomo cha kile wanachokihitaji na kusisitiza kwa kutoa angalizo katika athari za ukabila na rushwa. 

Tamaduni mbaya kama unyanyasaji wa kijinsia, ndoa za kulazimishwa, tohara kwa watoto wa kike na kutopeleka watoto shuleni.

MSANII BOBBI KRISTINA AFARIKI DUNIA


Bobbi Kristina afariki Dunia

Bobbi Kristina Brown, mtoto wa marehemu Whitney Houston ambaye alikuwa gwiji wa muziki wa R&B, amefariki dunia baada ya kupoteza fahamu kwa muda wa miezi sita tangu alipokutwa taabani kwenye bafu lake na pindi alipofikishwa hospitalini na kukutwa na matatizo kwenye ubongo.

Bobbi amekufa akiwa na umri wa miaka 22,huku akivutiwa kuwa muigizaji na muimbaji mahiri na mwenye ubora wa aina yake. Msemaji wa familia Kristen Foster amesema Bobbi amefariki akiwa amezungukwa na familia yake, ''hatimaye yuko salama sasa kwenye mikono ya Mwenyezi Mungu,tunawashukuru wote walioungana nasi katika maombi na kuonesha upendo kwa miezi michache iliyopita''.

Bobbi ambaye alikuwa amepoteza fahamu tangu akutwe ameanguka kwenye bafu lake panapo tarehe 31 januari mwaka huu na kuwekwa kwenye matibabu huku akiwa amekosa ufahamu na mpaka kifo chake kumkuta alikuwa hajapata fahamu bado.

Inakumbukwa kuwa miaka mitatu iliyopita mama yake Bobbi,alikutwa pia kwenye bafu lake amepoteza fahamu baada ya kupitliza kiwango cha dawa za kulevya na pombe mwishowe kufa. Bobbi alikuwa mtoto pekee wa Whitney Houston na Bobby Brown,magwiji wa muziki wa miondoko ya R &B.

Sunday, July 26, 2015

MLIPUKO WAUA WATU 10 SOMALIA


Takriban watu 10 wameuawa katika mlipuko huo

Takriban watu 10 wameuawa kufuatia mlipuko mkubwa uliotokea katika hoteli moja katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu.

Mwandishi wa BBC katika mji huo anasema kuwa lori moja lilitumiwa kushambulia hoteli ya Jazeera karibu na uwanja wa ndege wa taifa hilo. Wajumbe wa kimataifa wamekuwa wakiishi katika hoteli hiyo ambayo imelengwa katika siku za nyuma.

Ripota wetu anasema kuwa ni moja ya mashambulizi mabaya kuwahi kushuhudiwa mjini Mogadishu. Anasema kuwa magari ya ambulansi yameanza kuokota miili.

14 WAFA KATIKA SHAMBULIO CAMEROON


Watu 14 wameuawa jana usiku katika shambulizi la bomu lililotekelezwa na Boko Haram

Watu 14 wameuawa jana usiku katika shambulizi la bomu lililofanyika kwenye jumba moja la starehe katika mji wa Maroua Kaskazini mwa Cameroon.

Siku chache baada ya kutokea kwa mashambulizi mawili ya bomu katika mji mkuu wa eneo hilo kulingana na habari kutoka kwa maafisa wa usalama. Afisa mmoja wa jeshi lililopelekwa katika eneo hilo kupambana na Boko Haram ndiye aliyetoa habari hiyo kwa siri.

Shambulizi hilo lilifanyika saa mbili kasorobo jana usiku saa za Afrika Mashariki wakati mwanaume mmoja alirusha bomu ndani ya baa katika wilaya ya Ponre kulingana na afisa huyo wa jeshi ambaye hakutaka kutajwa. Wakazi walijaribu kumfuata lakini aliwarushia grunedi kuwafukuza.

Saturday, July 25, 2015

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JULAI 25, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
.
.
Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

WEMA SEPETU ALA ‘NGUMI’ ZA USO UBUNGE SINGIDA

Wema
Msanii maarufu wa filamu nchini, Wema Abraham Sepetu amepigwa chini katika kura za maoni kugombea ubunge wa viti maalum Singida.
 
Aysharose Mattembe ndiye ameibuka kidedea akimtupa kwa mbali Madam Wema aliyeshika nafasi ya nne.
11228022_1051907251486527_8461334309566372025_n 
Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

ZLATAN YUKO TAYARI KUKIPIGA MAN UNITED, ILA ANAHOFIA JAMBO MOJA


2ABD88C600000578-0-image-a-66_1437751952554
Mshambuliaji msumbufu na mwenye majivuno, Zlatan Ibrahimovic maarufu kama ‘Cadabra’ amesema angependa kuichezea Manchester United siku moja lakini anahofia ‘ngumi’ za kila siku na kocha Louis Van Gaal.

Akiwajibu waandishi wa habari kama yuko tayari kujiunga na mashetani hao wekundu, Cadabra alisema angeweza kuchezea United lakini anahofia ugomvi wa kutoisha baina yake na Louis Van Gaal.

Zlatan na Van Gaal hawakuwa na mahusiano mazuri tangu wakiwa Ajax miaka ya 1990’s lakini moto uliwaka zaidi baada ya Zlatan kumtaja Van Gaal kama ‘pampasi’ katika kitabu chake.

Wawili hao hawana urafiki na kwamba hawawezi kuiva chungu kimoja. Hisia zimekuwa ni nyingi miongoni mwa mashabiki mara baada ya kocha Louis Van Gaal kutangaza kwamba atafanya usajili wa kushitukiza wa mshambuliaji siku za usoni.

Hata hivyo Cadabra nahodha wa Sweden anahusishwa na tetesi za kujiunga na AC Milan ya nchini Italia. Habari zinasema Zlatan amechoshwa na quality ya ligi nchini Ufaransa na sasa anafikiria kuihama klabu yake ya Paris St. Germain. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

HATIMAYE WAYNE ROONEY AMJIBU VAN GAAL

2AD1593000000578-3173794-image-m-25_1437770313268
Wayne Rooney amesema yuko tayari kuwa mfungaji bora wa Manchester Unites kwa mara nyingine na amewapa changamoto wenzake ya kuandika Historia msimu ujao.
 
Nyota huyo wa England alicheza namba nyingi msimu uliopita chini ya Louis van Gaal na ikifika wakati akashushwa mpaka kiungo cha chini.
 
Kwasasa Rooney anataka kucheza namba anayoipenda yaani namba 9 na amesema yuko tayari kufunga magoli.
 
“Niko tayari kubadili akili yangu na kuwa moja ya wafungaji wa magoli,” Amesema nyota huyo wa zamani wa Everton ambaye msimu uliopita aliifungia United magoli 12.
 
“Nataka kucheza nafasi ya mshambuliaji ambapo nadhani ninaweza kufunga, naamini naweza kulitekeleza hilo”
Rooney performed a number of roles for Manchester United last term but is keen to play as a number nine
Msimu wa 2009-10 na 2011-12, Rooney alifunga magoli 34 kwenye mashindano yote akicheza nafasi ya mshambuliaji wa kati na kama atarudishwa nafasi hiyo anaweza kufanya vizuri.
 
Siku za karibuni, kocha wa Man United, Louis van Gaal alisema anatarajia kumtumia Rooney kama mshambuliaji wa kati msimu ujao na maneno haya ya Wayne ni majibu kwa bosi wake. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...