Friday, July 24, 2015

WAJUMBE WA CCM WAPATA AJALI, MMOJA AFARIKI


Mtu mmoja amefariki Dunia baada ya basi Dogo aina ya toyota HIACE, lililokuwa limewabeba wajumbe wa chama cha mapinduzi wa kata ya Milanzi kwenye manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa, waliokuwa kwenye kampeni za kura za maoni za udiwani kuacha njia na kupinduka, ambapo pia ajali hiyo imeacha majeruhi kumi na moja.

Akiongea na waandishi wa habari kwenye Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Rukwa mjini Sumbawanga, mwenyekiti wa CCM wa kata ya milanzi Bw. Edgar Mwanandenje ambaye ni miongoni mwa majeruhi hao, amesema walikuwa wakitokea kwenye mchakato wa kampeni ya kura za maoni katika kata yao, ndipo dereva wa basi hilo dogo alipolazimisha kuipita kwa kasi pikipiki aina ya bajaj iliyokuwa mbele yao, na kupoteza mwelekeo kabla ya kupinduka. 

Katibu wa ccm wilaya ya sumbawanga mjini Bw Gabriel Kiula akiongelea juu ya ajali hiyo,amemtaja aliyepoteza maisha kuwa ni Didas Mwanisenga aliyekuwa mjumbe wa kamati ya siasa ya kata ya milanzi, huku kamanda wa polisi wa mkoa wa Rukwa Bw. Jacob Mwaruanda akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

EU YAJADILI KUKATA MISAADA BURUNDI


Bendera ya Burundi

Muungano wa Ulaya EU umeanza kikao maalum kujadili uwezekano wa kukata msaada wake nchini Burundi. Inakisiwa kuwa fedha kutoka muungano huo unafikia zaidi ya nusu ya bajeti nzima ya Burundi ya kila mwaka. 

Mkuu wa masuala ya kigeni wa Muungano wa EU Federica Mogherini, ameelezea wasiwasi wake juu ya ghasia zilizototokea nchini humo kabla ya kufanyika uchaguzi wa rais, na ametilia shaka iwapo serikali itakayoundwa baada ya uchagzui huo itakuwa wakilishi ya taifa nzima. 

Upande wa uchaguzi ulisusia kura hiyo iliyofanywa siku ya Jumanne. Matokeo rasmi yanatarajiwa kutangazwa Ijumaa hii Uamuzi wa Rais Pierre Nkurunzinza kuwania urais kwa muhula wa tatu umetajwa kwenda kinyume na mkataba waliosaini mjini Arusha miaka kumi na tano iliyopita, ambao ulimaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka mingi.

Ghasia zimezuka nchini humo tangu rais Pierre Nkurunzinza kutangaza kuwania kiti hicho ambapo zaidi ya watu laki moja wamikimbia nchi hiyo huku makumi ya maelfu wengine wakiuawa katika maandamano. Juhudi kadhaa za kuleta upatanishi kati ya makundi hasimu zimeambulia patupu.

BUHARI "MAREKANI INAWASAIDIA BOKO HARAM"


Rais Mahammadu Buhari akiwa na mwenyeji wake Obama alipokua ziarani nchini Marekani wiki hii.

Marekani "inawasaidia na kuchochea " kundi la wanamgambo wa kiislam wa Boko Haram kwa kukataa kutoa silaha kwa Nigeria, ni kauli ya rais wa Nigeria Mahammadu Buhari.

Sheria ya Marekani inazuia serikali kuuza silaha kwa nchi ambazo zinashindwa kushughulikia ipasavyo masuala ya haki za binadamu.

Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari alikutana na rais Barack Obama Jumatatu kuomba msaada zaidi. Boko Haram limewauwa watu 10,000 tangu mwaka 2009 na limewateka mamia ya wasichana na wanawake.

Thursday, July 23, 2015

MATOKEO YA KURA ZA MAONI UBUNGE CHADEMA MBEYA NA MAJIMBO MENGINE

http://jambotz8.blogspot.com/

http://jambotz8.blogspot.com/

YANGA SC YAZINDUKA, YAWAPIGA 3-0 TELECOM, MSUVA NA TAMBWE WAKOSA PENALTI

Yanga imerejea katika michuano ya Kagame baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Telecom ya Djibout katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Jana.

Katika mechi yake ya kwanza ya michuano hiyo, Yanga ilianza kwa kupoteza kwa mabao 2-1 dhidi ya Gor Mahia huku mshambuliaji wake Donald Ngoma akilambwa kadi ya nyekundu.

Malimi Busungu ndiye shujaa baada ya kufunga mabao mawili huku Geofrey Mwashuya, akifunga bao la tatu.

BENTEKE AHAMIA LIVERPOOL RASMI


Christian Benteke

Timu ya Livepool imekamilisha kumsajili rasmi mshambuliaji mwenye asili ya Jamuhuri ya Kidemokrasia wa kongo Christian Benteke kutoka Aston Villa kwa kitita paundi milion 32.5. 

Benteke alikubali mkataba wa muda mrefu na kuwa mchezaji wa pili kununuliwa kwa gharama kubwa huko England.

Mshambuliaji huyo raia wa Ubelgiji ameifunga magoli 49 katika mechi 101 alizocheza kwenye timu yake ya zamani ya Aston Villa.

Wednesday, July 22, 2015

KURA ZAANZA KUHESABIWA BURUNDI


Rais Pierre Nkurunziza

Shughuli ya kuhesabu Kura imeanza nchini Burundi kufuatia uchaguzi wa urais ambao umeshutumiwa na wengi nchini humo na hata kimataifa.

Rais Pierre Nkurunzinza anatarajiwa kupata ushindi mkubwa kwa muhula wa tatu huku upinzani ukisusia kabisa kura hiyo.

Huku hayo yakijiri Marekani na Uingereza wamekashifu kura hiyo wakisema kuwa haikuwa ya huru na haki. Marekani kwa upande wake imependekeza kugawana madaraka huku ikitishia kuchukua hatua dhidi ya Burundi iwapo muafaka hautapatikana.

Tuesday, July 21, 2015

UCHAGUZI UMEEANZA NCHINI BURUNDI


Uchaguzi wa urais umeanza Burundi

Baada ya ghasia na maandamano ya miezi kadhaa, hatimaye raia nchini Burundi sasa wamefika katika vituo vya kupiga kura ili kumchagua rais wao. Watu wawili wameuwawa usiku wa kuamkia leo katika mji mkuu Bujumbura.

Foleni zimeonekana katika vituo vya kupigia kura

KESI YA RAIS WA ZAMANI WA CHAD YAAHIRISHWA HADI SEPTEMBA

Rais wa zamani wa Chad arejeshwa kortini 

Kesi ya kihistoria dhidi ya Kiongozi wa zamani wa Chad Hissene Habre iliyokuwa imerejeshwa mahakamani leo nchini Senegal sasa imeahirishwa hadi mwezi Septemba.

Mahakama imetoa muda huo kwa wakili wapya wa kiongozi huyo wa zamani wa kimla kujiandaa kwa kesi inayomkabili ya makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu, ukatili na uhalifu wa kivita.

Bwana Habre ambaye amekataa kuitambua mahakama hiyo alikataa kuzungumza mahakamani huku akiwashauri wakili wake wasimwakilishe mahakamani.

KITIMTIM MICHUANO YA KLABU BINGWA ULAYA

Michuano ya Klabu Bingwa Ulaya inaendelea tena hii leo kwa timu zile zinacheza round ya kwanza ambapo Dila Gori ya Geogia itakuwa na kibarua kigumu itakapoumana vikali na Partizan Belgrade ya Serbia.

Huku FC Pyunik ya Armenia ikikutana uso kwa uso na Molde ya Norway.

Milsami ya Boldova itapimana nguvu na Ludo Bulgaria.

Mechi nyingine za Klabu Bingwa barani Ulaya hapa chini Dila Gori v Partizan Belgrade 13:30

FC Pyunik v Molde 15:00

Milsami Orhei v Ludo Razgd 16:00

HJK Helsinki v FK Ventspils 17:00

Maccabi Tel Aviv v Hibernians FC 18:30

Lincoln Red Imps v FC Midtjylland 19:00

Vardar v Apoel Nic 19:00

Zalgiris v Malmö FF 19:10

Crusaders FC v Skenderbeu Korce 19:45

Monday, July 20, 2015

NCHIMBI AENGULIWA KWENYE KINYANG'ANYIRO CHA UBUNGE...!!!

Dr. Emmanuel Nchimbi

KAMATI ya Siasa ya chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Songea Mjini imetupilia mbali fomu ya mgombea UBUNGE Dr. Emmanuel Nchimbi kwa madai kuwa fomu hiyo haikuwa na vigezo na kusababisha kushindwa kuijadili baada ya mgombea kutokuwepo kwenye kikao hicho.

Akizungumza asubuhi ya leo ofisini kwake katibu wa CCM wa Wilaya hiyo Juma Mpeli alisema kuwa mpaka jana majira ya saa kumi jioni fomu za kugombea ubunge jimbo la Songea Mjini zilipokelewa tisa (9) lakini fomu moja ya Dr. Nchimbi ilikuwa imechukuliwa na mmoja wa wakazi wa Songea na ikalejeshwa siku hiyo hiyo ikiwa imejazwa.

Alisema kuwa fomu hiyo ya mgombea ilishindikana kujadiliwa kwa kuwa mgombea mwenyewe Dr. Nchimbi hakuwepo kwenye kikao ambacho wagombea wote waliitwa kujadiliwa kadri ya maelezo waliyoyatoa kwenye fomu ya kugombea ubunge kwenye jimbo hilo.

MAN U KUTOONGEZA WASHAMBULIAJI

Kocha Mkuu wa Manchester United Louis Van Gaa

 Kocha mkuu wa Manchester United Louis Van Gaal ametamba kuwa hatanunua mwingine kwani alio nao kwa sasa wanatosha wakiongozwa na Wayne Rooney.

Pamoja na Wayne Rooney washambuliaji wengine waliobaki ni Javier Hernandes Chicharito, na James Wilson baada ya mshambuliaji mpachika magoli Robin Van Persie kujiunga na Fenerbahce ya Uturuki hivi karibuni na Radamel Falcao mkopo wake kumalizika.

Van Gaal anatarajia kumtumia Rooney kama mshambuliaji pekee pale mbele ambapo atasaidiwa na Mephis Depay aliyesajiliwa wakati wa majira ya joto kutoka PSV Eindhovenya Uholanzi. Van Gaal anatamba kuwa Depay anaweza kuwa mshambuliaji wa katikati tofauti na alivyokuwa akitumika wakati alipokuwa PSV.

Saturday, July 18, 2015

WAZEE WA KIMILA MONDULI WAMUANGUKIA LOWASSA

Wazee wa kimila wa jamii ya wafugaji wa Kimaasai (Malaigwanan) kutoka Wilaya ya Monduli wamemuomba waziri mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa kubaki na kuendelea kuwa kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa sababu ndicho kilichomlea na anakijua.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Monduli kwa niaba ya Malaigwanan, Mzee Joseph Mesopiro kutoka Kata ya Sepeko wilayani humo alisema viongozi wa mila wanakusudia kutuma ujumbe maalumu kwa Lowassa kumshauri asihame CCM kama baadhi ya watu aliowaita wapambe wanavyomshauri.

“Sote Monduli tumesononeka kwa jinsi vikao vya chama vilivyomtendea mbunge wetu. Bado tunampenda kama ambavyo tunakipenda chama chetu. Tunaamini ataendelea kubaki CCM na kupigania ushindi wa chama katika uchaguzi ujao,” alisema Mzee MMesopiro

TUNAWATAKIA EID MUBARAKA WATU WOTE



Leo ni sikukuu kubwa sana duniani... ina maana kubwa sana kwa waislam na watu wote duniani.

Kwakulijua hili Jambo Tz tunachukua nafasi hii kuwatakia sikukuu njema watanzania wote na dunia kwa ujumla.

OBAMA KUTOTEMBELEA KIJIJI CHA BABA YAKE

Barack Obama

#ObamainKenya ndilo neno linalotawala mitandao ya kijamii nchini Kenya huku rais huyo akitarajiwa kulitembelea taifa hilo.

Hata hivyo wakaazi wa kijiji cha Kogelo ambapo babaake Obama alizaliwa na kulelewa sasa hawatalazimika kufanya maandalizi ya aina yoyote kufuatia ziara hiyo baada ya balozi wa Marekani nchini Kenya Robert Godec kusema kuwa rais huyo hatozuru kijiji cha Kogelo.

''Ana mda mchache sana kwa hivyo basi atakuwa nairobi pekee'', alisema bwana Godec akizungumza na runinga ya KTN.

Bibiye Obama Sarah Obama alikuwa amejiunga na wakaazi wa Kogelo akimtaka Obama kuwatembelea kulingana na ripoti za kituo cha habari cha Capital fm.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...