Sunday, June 07, 2015

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 07, 2015 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC03387
DSC03388

Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.DSC03389

NYAMA YA PUNDA YASINDIKWA NCHINI...!!!

SERIKALI imekiri kuruhusu uanzishwaji wa kiwanda cha kusindika nyama ya punda kilichopo mkoani Dodoma.

Imekiri hivyo baada ya Mbunge wa Ole, Rajab Mbarouk Mohamed (CUF), kuibua hoja hiyo juzi (ijumaa) jioni wakati wa kupitisha makadirio ya bajeti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa mwaka wa fedha 2015/2016.

Katika hoja yake, alitaka kujua juhudi zilizofanywa na Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi (TFDA), kukagua viwanda vya usindikaji wa chakula ikiwa ni pamoja na kiwanda hicho. Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

BARCELONA YAWACHAPA JUVENTUS 3-1

http://jambotz8.blogspot.com/p/blog-page_26.html
Barcelona walitawazwa mabingwa wa Ulaya kwa mara ya tano baada ya kuichapa Juventus mabao matatu kwa moja katika mechi kali ya fainali iliochezwa katika uwanja wa Olimpiki wa Berlin.
Barcelona walikuwa wa kwanza kufunga kupitia Ivan Rakitic kunako dakika ya nne ya mwanzo wa kipindi cha kwanza.
Hata hivyo Alvaro Morata alisawazisha .Lakini Luis Suarez alifunga bao jingine baada ya kipa Gianluigi Buffon kuutema mpira naye nyota Neymar akafunga udhia baada ya gusa ni guse kati yake na Messy.
http://jambotz8.blogspot.com/p/blog-page_26.html
Katika mechi hiyo Andre Iniesta ndiye aliyetangazwa mchezaji bora.Hii inamaanisha kwamba Barcelona wameshinda mataji matatu ikiwemo lile la Copa Del Rey,La liga na la vilabu bingwa barani Ulaya.

Mechi hiyo pia ilikuwa ya mwisho kwa kiungo wa wakati wa Barcelona Xavi Hernandez ambaye anaondoka kilabu hiyo baada ya kuichezea kwa mda mrefu. Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ANGALIA PICHA 10 ZA MASTAA WA MPIRA WALIPOKUWA WATOTO

messi
Lionel Messi wa sasa na wakati akiwa mtoto
ronaldo
Cristiano Ronaldo wa sasa na wakati akiwa mtoto.
Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, na usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Friday, June 05, 2015

SOMA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 05, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC03316
DSC03317
DSC03318
Nunua gari kwa bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

IDADI YA WALIOFARIKI GHANA YAFIKIA 175


Ghana moto
Takriban watu 175 wamefariki kufiakia sasa kufuatia moto uliotokea katika kituo kimoja cha mafuta katika mji mkuu wa Ghana Accra.

Moto huo uliozuka siku ya jumatano usiku ulianza wakati wakaazi wa mji huo walipokuwa wakikabiliana na siku mbili za mvua kubwa ambayo imewaacha raia wengi bila makaazi pamoja na stima.


Ghana moto
Mafuriko hayo yaliathiri juhudi za uokozi na huenda yalisababisha moto kulingana na mwandishi wa BBC Sammy Darko mjini Accra. Tayari Ghana imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo hivyo.


Ghana moto
Mlipuko huo ulitokea hapo jana wakati mamia ya watu walipokuwa wamejihifadhi katika kituo hicho cha mafuta kutokana na mvua kubwa zinazonyesha. Rais wa Ghana, John Mahama amesema janga hilo halitajirudia tena.

Ghana moto 
Bwana Mahama amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mji mkuu, Accra alipotembelea eneo la tukio. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

RAHEEM STRLING KUELEKEA OLD TRAFFORD

Raheem Sterling
Mshambuliaji wa Liverpool Raheem Sterling huenda akaelekea katika kilabu ya Manchester United ,hatahivyo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 ana wasiwasi kuhusu athari za uhamisho huo hususan kutokana na ushindani mkali uliopo kati ya klabu hizo mbili.

Hatahivyo Liverpool imesema kuwa haiko tayari kufanya biashara na wapinzani wao wakuu kutoka Kaskazini Magharibi. Mkufunzi wa kilabu ya Manchester United Luois Van Gaal anavutiwa na kasi ya mchezaji huyo na uwezo wake wa kuwaponyoka mabeki.

Sterling amekataa ombi la kitita cha pauni laki moja kutoka kwa Liverpool akisema kuwa anataka kuondoka na kukichezea kilabu ambacho kina uwezo wa kushinda mataji. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

SERENA ATINGA FAINALI FRENCH OPEN 2015

Serena William,mchezaji tenis nambari moja duniani akifurahia ushindi.
Serena Williams amefanikiwa kutinga fainali za michuano ya tenis ya French Open. Licha ya kujisikia kuumwa Serena aliweza kupambana vikali na kumbwaga mpinzani wake Timea Bacsinszky kwa seti 4-6 6-3 6-0 na kufuzu kucheza fainali za mwaka huu.

Serena nambari moja duniani kwa wanawake sasa atapambana na Lucie Safarova katika mchezo wa fainali kesho, Jumamosi. Serena amekuwa akiumwa kipindi chote cha michuano hiyo, kiasi kwamba anasema hakutarajia kushinda katika mchezo huo.

Serena anajaribu kushindi taji la tatu la michuano hiyo ya French Open na taji la ishirini la michuano mikubwa. Mapema katika uwanja wa Philippe Chatrier, Safarova wa 13 kwa ubora alimtupa nje MSerbia Ana Ivanovic na kuwa mwanamke wa kwanza wa Czech kufika fainali za michuano hiyo katika uwanja wa Roland Garros katika kipindi cha miaka 34.
Kwa upande wa Wanaume, fainali zitafanyika Jumapili hii. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

Tuesday, June 02, 2015

AL-SHABAAB WADAIWA KUVITEKA VIJIJI KENYA

Alshabaab
Hofu kubwa imetanda Kaskazini mwa nchi ya Kenya,baada ya kuwepo kwa taarifa kwamba kundi la wapiganaji wa Al shabaab Limeviteka vijiji kadhaa katika mpaka wa Kenya na somalia.
Mamia ya wakaazi wameyatoroka makaazi yao kufuatia taarifa za kuwepo kwa wapiganaji wa Alshabaab wapatao thelathini.
Shule nne zinaripotiwa kufungwa.
Naibu kamishna wa kaunti ya Mandera amenukuliwa akisema kwamba wamepokea ripoti za kuwepo kwa wapiganaji hao na watawaandama na kulidhibiti eneo hilo. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

MLIPUKO WA BOMU WAUA WATU 20 NIGERIA

Mlipuko nchini Nigeria
Takriban watu 20 wamefariki kutokana na mlipuko wa bomu katika mji wa kaskazini mashariki wa Maiduguri nchini Nigeria.
Mji huo ulikuwa umeshambuliwa saa za alfajiri siku ya jumanne na washukiwa wa kundi la Boko haram .
Saa chache baadaye ,mlipuaji wa kujitolea muhanga alijilipua katika soko la kuuza ngombe la Gamboru ndani ya mji huo kulingana na walioshuhudia.
Wakati wa kuapishwa kwake rais mpya wa Nigeria Muhammadu Buhari alisema kuwa anayahamisha makao makuu ya kijeshi katika vita dhidi ya wapiganaji hao kutoka mji mkuu wa Abuja hadi Maiduguri. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

Thursday, May 28, 2015

MWANASHERIA KENYA AJITOSA KUMUOA MTOTO WA OBAMA...!!!

Rais Barrack Obama wa Marekani akiwa na mtoto wake Malia. 

Mwanasheria kijana nchini ametuma ombi la kumuoa mtoto wa Rais Barack Obama anayeitwa Malia.
Mwanasheria Felix Kiprono alisema jana kwamba yupo tayari kutoa ng’ombe 50, kondoo 70 na mbuzi 30 ikiwa ni mahari ya kumposa mtoto huyo.
Alisema kuwa analazimika kufanya hivyo ili kutimiza ndoto yake ya muda mrefu ya kumuoa mtoto wa Rais Obama.
“Nimevutiwa kumchumbia Malia tangu mwaka 2008,” alisema Kiprono baada ya kuhojiwa na gazeti la The Nairobian. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

ODAMA: NAOGOPA MSAADA WA MASHARTI...!!!

Odama
Jennifer Kyaka ‘Odama

MWIGIZAJI mwenye mvuto katika filamu za Bongo, Jennifer Kyaka ‘Odama’, amesema anaogopa marafiki wa kiume kwa kuwa huwa na masharti magumu pindi wanapotoa msaada.
“Wasanii wa kiume kwangu sipendi kwa kuwa huwa na masharti kuliko marafiki wa kike ambao husaidia bila masharti ya ajabu,” alisema.
Aliongeza kwamba, marafiki wa kike anakuwa huru kuwaeleza shida na matatizo yake kuliko wa kiume ndiyo maana hiyo ni sababu yake nyingine ya kutopenda marafiki wa kiume kama anavyopenda marafiki wa kike. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

SOMA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MEI 28, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC03017
DSC03018
DSC03019
Nunua gari bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

"NATAKA KUWA MCHEKESHAJI" INSPEKTA HAROON

INSPECTOR.
Haruna Kaena ‘Insepkta Haroun’

UNALIKUMBUKA kundi la Gangwe Mobb, hapo lazima utamtaja Haruna Kaena ‘Insepkta Haroun’ na Luten Kalama, wawili hao baada ya kutengana kila mmoja akawa anafanya kazi binafsi lakini sasa Inspekta Haroun ameibuka na kudai kwamba anataka kuwa mwigizaji wa vichekesho.
Inspekta Haroun aliyetamba na wimbo wa ‘Mtoto wa Geti Kali’ aliendelea kueleza kwamba fani anazozipenda ni muziki na kuigiza vichekesho.
“Mimi msanii hivyo natakiwa niwe mbunifu, nisibweteke na kazi, fani moja na kwa sasa napenda kuwa mwigizaji wa vichekesho kwa kuwa napenda kazi hiyo na ninaiweza,” alijinadi.
Msanii huyo aliwahi kushirikishwa katika vipengele vya uigizaji katika kipindi cha vichekesho kilichokuwa kikirushwa na televisheni ya Clouds. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

WABUNGE WAMKAANGA MAGUFULI

Waziri wa Ujenzi, Dk John Pombe Magufuli 

Waziri wa Ujenzi, Dk John Pombe Magufuli amekuwa hapati wakati mgumu anapowasilisha bajeti ya wizara hiyo, lakini hali ilikuwa tofauti jana wakati wabunge walipoungana kueleza hofu yao katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa barabara kutokana na madeni ya makandarasi.
Wabunge hao walidiriki kueleza kuwa kuna ufisadi katika ununuzi wa kivuko cha Bagamoyo na wengine kueleza kuwa miradi iliyotajwa kwenye hotuba ya bajeti ilishatekelezwa miaka ya 80 na 90.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kamati ya Miundombinu kuhusu bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2015/2016 iliyosomwa na Makamu Mwenyekiti, Profesa Juma Kapuya, deni linalodaiwa na makandarasi ni kati ya Sh850 bilioni na Sh900 bilioni.
“Kamati haijaridhishwa kabisa na hali hii kwani deni hili sasa ni kubwa kuzidi hata bajeti inayotengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya wizara hii, jambo ambalo linafanya bajeti hii kuonekana ni kiini macho tu,” alisema Profesa Kapuya.
Kambi ya Upinzani
Katika taarifa yake, Kambi ya Upinzani Bungeni (KUB) ilimshutumu Waziri Magufuli kwa kuandika hotuba ndefu ili kuwachanganya wabunge, huku hotuba hizo zikitaja hata miradi ya barabara zilizojengwa miaka ya 80 na 90.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...