Saturday, October 04, 2014

MIAKA 15 YA KUMBUKUMBU YA KIFO CHA BABA WA TAIFA MWL. J. K. NYERERE

Mwalimu J. K. Nyerere na aliyekuwa Rais wa Msumbiji marehemu Samora Machel.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OKTOBA 04, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WABUNGE KUANDAMANA NA KENYATTA ICC


Rais Uhuru Kenyatta akiwasili katika mahakama ya kimataifa ya ICC

Idadi kubwa ya wabunge nchini Kenya wanajiandaa kuandamana na Rais Uhuru Kenyatta katika mahakama ya kimataifa ya ICC,Uholanzi ambako anatarajiwa kuhudhuria kikao maalum kuhusiana na kesi inayomkabili katika mahakama hiyo.
Kenyatta ametakiwa kufika mbele ya mahakama hiyo tarehe nane mwezi huu huku kiongozi wa mashitaka Fatou Bensouda akilalamika kuwa Kenya imekataa kushirikiana na mahakama hiyo kuhusiana na ushahidi dhidi ya Kenyatta.
Mapema wiki hii, mahakama hiyo ya ICC ilitupilia mbali ombi la Rais Kenyatta, la kutaka kikao hicho cha Octoba 8 kuhairishwa au aruhusiwe kutumia video. Majaji wa Mahakama hiyo walimuagiza Uhuru kufika binafsi mbele yao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TOFAUTI YA DINI YAVUNJA NDOA INDIA

Ndoa ya kihindi
Maafisa wa polisi katikati mwa India wamefutilia mbali harusi kati ya mwanamume mkristo na mwanamke wa kihindu baada ya shinikizo kutoka kwa makundi ya kihindu yenye mrengo wa kulia.
Wanandoa hao wawili kutoka Madhya Pradesh walitoroshana na kuoana katika sherehe ya kihindu bila ruhusa ya familia ya msichana.
Baada ya makundi hayo ya Kihindu kupinga hatua hiyo na kutishia kushambulia majengo ya serikali,maafisa wa polisi katika eneo hilo waliwasaka wapenzi hao na kuwalazimisha kuachana.
Waandishi wanasema kuwa hatua hiyo ya makundi ya kihindu imekuwa ya kawaida katika jimbo hilo katika siku za hivi karibuni. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MESSI AKUTWA NA KESI YA KUKWEPA KULIPA KODI

messi
Nyota wa Barcelona Lionel Messi anakabiliwa na kesi ya kukwepa kodi,majaji nchini Hispania wamethibitisha tuhuma hizo.
Ikumbukwe Messi alikuwa akikabiliwa na tuhuma za ukwepaji kulipa kodi kwa muda sasa.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Friday, October 03, 2014

KURA MBILI ZAPITISHA RASIMU YA KATIBA INAYOPENDEKEZWA

http://jambotz8.blogspot.com/

Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Deo Sanga akisakata muziki katikati ya Ukumbi wa Bunge hilo baada ya kutangazwa kwa matokeo ya kura zilizopigwa kupitisha Rasimu ya Mwisho ya Katiba inayopendekezwa mjini Dodoma jana.


Dodoma/Dar. Licha ya upinzani kutoka makundi kadhaa ya wananchi, Bunge la Katiba jana lilihitimisha kazi yake kwa kupitisha Katiba inayopendekezwa baada ya kupata theluthi mbili za wajumbe wa kila upande wa Muungano.

Matokeo hayo yaliyohitimisha mchakato huo, yalifanikishwa kwa tofauti ya kura mbili za wajumbe katika baadhi ya ibara na nyingine kwa kura moja tu, ikimaanisha kuwa iwapo kura hizo mbili zingekosekana hadithi ingekuwa tofauti.

 Kutangazwa kwa matokeo hayo kuliwafanya wajumbe walioshiriki mchakato hadi hatua ya mwisho baada ya wenzao wa kundi la Ukawa kususia, kulipuka kwa furaha, nyimbo, tambo, vijembe na vigelegele huku wakijimwaga ukumbini kusakata dansi.

Akitangaza matokeo hayo, Naibu Katibu wa Bunge hilo, Dk Thomas Kashililah alisema hali ya upigaji kura ilikuwa ni nzuri na kila kura za kila upande zilitosheleza na kutoa uhalali wa Katiba inayopendekezwa kupelekwa kwa wananchi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PINDA: "KATIBA IPATIKANE KABLA YA RAIS MPYA"


Bunge Maalumu la Katiba, kabla ya kuahirishwa kwake 

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amesema atafurahi kuona mchakato mzima wa Katiba ukikamilika kabla rais mpya hajapatikana katika Uchaguzi Mkuu ujao, pendekezo ambalo ni kinyume na makubaliano baina ya Rais Jakaya Kikwete na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) kuwa upigaji wa kura ya maoni ufanyike baada ya Uchaguzi Mkuu 2015.

Akizungumza Bungeni baada ya kupewa nafasi na Mwenyekiti wa Bunge la Katiba, Samuel Sitta kutoa shukrani, Pinda alipendekeza kura ya maoni ipigwe sambamba na Rais ili kiongozi ajaye afanye kazi ya kutekeleza matakwa ya Katiba hiyo.

Alisema rais ajaye anaweza kuwa na ajenda zake, hivyo ni muhimu kumaliza kazi yote na kumkabidhi Katiba ambayo imekamilika ili aitekeleze.

“Nampongeza sana mwenyekiti kwa kufanya kazi nzuri ya kuhakikisha Katiba inayopendekezwa inapatikana kwa wakati na kwa kuzingatia maoni ya wananchi,” alisema Waziri Mkuu Pinda.

Alichojifunza

Pinda alieleza kuwa katika mchakato huo wa Mabadiliko ya Katiba, amejifunza mambo makuu manne, kubwa likiwa ni kutii sauti ya wengi, kwani ni sauti ya Mungu. Alisema wingi wao bungeni ni kiashiria cha uwepo wa sauti ya Mungu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WANAFUNZI 40 MEXICO WAPOTEA

http://jambotz8.blogspot.com/
Mamia ya wanafunzi nchini Mexico katika jimbo la Guerrero wameandamana katika mji mkuu wa jimbo la Chilpancingo kulalamikia kutoweka kwa zaidi ya wanafunzi wenzao arobaini wiki iliyyopita.
Wanafunzi hao wanasemekana kuwa mwisho walionekana kusombwa katika magari ya polisi kufuatia maandamano walioshiriki wakilalamikia ubaguzi katika ajira ya walimu wa maeneo ya vijijini.
Polisi walifyatua rissasi kwenye basi na kwa waandamaji na kuua watu sita na wengine 17 kujeruhiwa.
Maafisa ishirini na wawili wa polisi wanashikiliwa na kwa kutuhuma za kufyatua risasi.
Ndugu ya waliouawa wanaosaidiwa na polisi waliingia mlango kwa mlango katika eneo la Iguala wakiwa wameshikilia picha za wapendwa wao na kutafuta eneo ambalo miili ya ndugu zao ilipofichwa. Serikali ya jimbo hilo imetoa dola 75,000 kwa yeyote atakayetoa taarifa kueleza wanafunzi hao walipo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WANAFUNZI WA HONG KONG KUKUTANA NA SERAKALI

http://jambotz8.blogspot.com/
 
Viongozi wa wanafunzi huko Hong Kong wamekubali kukutana na upande wa serikali kujadili malalamiko yao siku tano baada ya maandamano makubwa ya kupigania demokrasia.
Hiyo inafuatia mwaliko kutoka kwa mkuu wa utawala wa Hong Kong CY Leung. Alitoa taarifa hiyo muda mfupi kabla ya kumalizika kwa muda wa mwisho uliowekwa na wanafunzi hao waliotishia kuvamia majengo ya serikali iwapo mkuu huyo hatajiuzulu.
Muda wa mwisho uliowekwa na wanafunzi hao umemalizika salama.
Bwana Leung amesema atabakia madarakani na kuwaonya waandamanaji kuwa watapata matatizo iwapo watavamia majengo ya serikali.
Kumekuwa na makabiliano makali katika eneo la majengo ya serikali ambapo waandamanaji wamekuwa wakiendelea kudai uchaguzi wa haki mwaka 2017. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 03, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MIAKA 15 YA KUMBUKUMBU YA KIFO CHA BABA WA TAIFA MWL. J. K. NYERERE

Kutoka kushoto ni Marehemu Habib Halala, Mzee Paul Soizgwa, JK Nyerere, Brig. Hashim Mbita, Mzee Benjamin Mkapa, siku kumi kabla ya JK kustaafu uraisi 1985.  Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Thursday, October 02, 2014

HAWA NDIO WAKE WA MARAIS WA AFRIKA WANAOTIKISA...!!!

 
Ana Paula Dos Santos.
alizaliwa1964, ni mke wa Rais wa Angola, Jose Eduardo Dos Santos, Paula ni mwanamitindo wa zamani, anasifika kwa uzuri na kujua kuvaa.
Mama Salma Kikwete.
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, alizaliwa 1963, anatajwa kuwa katika orodha ya wake wazuri wa marais wa Afrika, anasifika kwa mavazi yake ya kitenge.
Margaret Wanjiku Kenyatta.
Ni mke wa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, anatajwa kuwa na tabasamu zuri ingawa nywele zake zenye rangi ya kijivu ni kivutio kikubwa. Kazaliwa Mwaka 1963.
 
Hinda Deby Itno.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TAARIFA TOKA BUNGE LA KATIBA DHIDI YA MWANASHERIA MKUU WA ZANZIBAR


Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman akisindikizwa kutoka ndani ya ukumbi wa Bunge Maalum leo mjini Dodoma na Askari Polisi.
Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman (mwenye Kaunda suti ya kijivu) akisindikizwa kutoka nje ya viwanja vya Bunge Maalum la Katiba leo mjini Dodoma na Askari Polisi mara baada ya kushutumiwa na baadhi ya Wajumbe wa Zanzibar. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

NAFASI ZA AJIRA WIZARA YA MAMBO YA NDANI {UHAMIAJI}

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi anatangaza nafasi za kazi zifuatazo katika Idara ya Uhamiaji kwa Raia wote wa Tanzania wenye sifa. 

1. KOPLO WA UHAMIAJI Nafasi 114 - (Nafasi 100 kwa ajili ya Tanzania 
Bara na Zanzibar na nafasi 14 maalum kwa ajili ya Zanzibar tu) 
A. SIFA ZA MWOMBAJI: 
(i) Awe Raia wa Tanzania mwenye umri kuanzia miaka 25 hadi 30. 
(ii) Awe amehitimu kidato cha sita na kufaulu masomo ya Kiingereza, Kiswahili, Historia, Jiografia, Kifaransa, Hisabati ambapo masomo mawili kati ya hayo yawe katika kiwango cha “Principal”. 
(iii) Awe pia na mojawapo ya sifa zifuatazo:
• Cheti cha Sheria; 
• Cheti cha Kompyuta; 
• Cheti cha Ufundi (FTC) kwenye fani ya umeme na mitambo 
(iv) Waombaji wenye ujuzi wa mojawapo ya lugha zifuatazo (Kifaransa, Kichina, Kijerumani, Kiarabu au Kihispania) watafikiriwa kwanza. 
(v) Aidha, Mwombaji aliyepitia mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa atapewa kipaumbele. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA CHAMA CHA ACT-TANZANIA KUHUSU ZITTO KABWE

 Zitto Kabwe
--
ALLIANCE FOR CHANGE AND TRANSPERANCY. 
--
Ndugu wanahabari kumekuwa na utaratibu wa habari zinazoupotosha umma wa watanzania kuhusu chama chetu cha ACT-Tanzania.

Katika gazeti la mwanahabari toleo na 117 la tarehe 29/09/2014 katika ukurasa wake wa mbele iliandikwa "MKAKATI WA KUKIPA NGUVU CHAMA CHA KIPYA CHA ZITTO KABWE WAVUJA".

Act-Tanzania tunaeleza kuwa ni chama cha watanzania wote kisichokuwa na mmilki wake na tunaunganishwa na misingi kumi ya chama pamoja na Itikadi yetu ya Demokrasia jamii.

Act-Tanzania tunatambua uwezo na mchango wa kisiasa na ujenzi wa demokrasia ya vyama vyingi nchini uliotolewa na Mheshimiwa Zitto Kabwe mbunge wa Kigoma Kaskazini.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...