Tuesday, September 02, 2014

NDEGE YA KENYA YAANGUKA TANZANIA


Masalia ya ndege ya Kampuni ya Safari Express Limited iliyoanguka katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kuua watu watatu jana.
Ndege ya Kampuni ya Safari Express Limited imeanguka katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kuwateketeza watu watatu waliokuwamo ndani.
Ndege hiyo yenye namba za usajili 5Y-SXP iliruka kutoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza Jumapili saa 1:26 usiku ikielekea Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta (JKIA) Kenya ambako ilitakiwa kutua saa 2:36 usiku.
Meneja Uhusiano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa), Paschal Shelutete alikiri ndege hiyo kuanguka kwenye hifadhi hiyo na walikuwa katika harakati za kuitafuta.
Mkaguzi Mkuu wa Ajali za Ndege nchini, kutoka Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi, David Nyamwihura alisema ajali hiyo ilitokea takriban maili 20 kutoka Serengeti, katika eneo la Kogatembe na watu wote watatu waliokuwamo wamefariki dunia.
Meneja wa Udhibiti wa JKIA, Clever Davor aliliambia gazeti la Daily Nation la Kenya kuwa ndege hiyo ilipoteza mawasiliano na rada ya uwanja huo ikiwa imeruka angani urefu wa futi 14,000. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BOKO HARAM WAUTEKA MJI MUHIMU NIGERIA

Wanajeshi wa serikali ya Nigeria.
Kundi la Boko haram limefanya mashambulizi katika mji wa Bama na kusababisha mauaji ya watu wengi huku wengine wakitoroka.
Wanamgambo hao waliuteka mji wa Bama ,ambao ni wa pili kwa ukubwa katika jimbo la Borno siku ya Jumatatu baada ya jaribio la awali la kutaka kuuteka mji huo kuzimwa na vikosi vya serikali.
Akizungumza na BBC ,wakaazi wamethibitisha kuwa mji huo umetekwa na kundi hilo na kwamba maelfu ya watu sasa wameachwa bila makao.
Mamlaka ya Nigeria bado haijatoa tamko lolote kuhusu shambulizi hilo.
Taarifa zinasema kuwa watu wengi wametoroka wakiwemo wanajeshi.
Zana za kivita zinazotumiwa na wapiganaji wa Boko Haram
Hapo awali jeshi la Nigeria lilitoa ripoti kuonyesha kuwa mpaka sasa limewaua wapiganaji 70 wa Boko Haram ,kutokana na mapigano kati ya kikundi hicho na wanajeshi Kaskazini -Mashariki mwa mji wa Bama.
Boko Haram walifika mapema asubuhi katika mji huo kwa magari ya kivita.Taarifa kutoka katika mji huo zinaeleza kwamba mashambulizi yalianzishwa na vikosi vya jeshi la Nigeria.
Msemaji wa kundi hilo la Boko Haram ameelezea hali ya mji huo kwa sasa kuwa wakaazi wa mji wa Bama wamekimbilia katika mji mwingine wa Borno na Maiduguri .
Nalo shirika la Amnesty International limetoa takwimu kuwa raia wapatao milioni nne wamekufa mwaka huu katika mgogoro huo kati ya Boko Haram na vikosi vya ulinzi vya Nigeria.

KIONGOZI WA AL-SHABAB ASHAMBULIWA

Haijulikani ikiwa Ahmed Abdi Godane aliuawa kwenye shambulizi hilo
Wanajeshi wa Mreakani wamefanya mashambulizi ya angani dhidi ya msafara wa magari ya mmoja wa viongozi wa kundi la Al Shabaab nchini Somalia.
Haijulikani ikiwa kiongozi wa kundi hilo, Ahmed Abdi Godane aliuawa kwenye shambulizi hilo lililofanyika umbali wa kilomita 240 kusini ya mjini mkuu Mogadishu.
Mwandishi wa BBC anasema kuwa wanajeshi wa Marekani walionekana wakishuka katika eneo hilo kwa helikopta na kuchukua miili ya wapiganaji waliouawa.
Msemaji wa idara ya ulinzi ya Marekani, (Rear Admiral John Kirby) alisema bado inadurusu matokeo ya shambulizi hilo.
Baadhi ya taarifa zinasema kuwa wapiganaji waliwakamata wakazi walioshukiwa kutoa taarifa kwa Marekani.

Na BBC

Thursday, August 28, 2014

TUHUMA NZITO KWA MAWAZIRI


 “Tunalipa wajumbe wanaohudhuria bungeni, kama hilo linatendeka lazima nilifuatilie. Ninachosema kama kuna waziri amelipwa na hayupo itabidi aturejeshee hiyo fedha. Lakini hili tatizo ni gumu kwa sababu mtu analipwa na tunajua yupo kumbe pengine hajaingia katika vikao,”

Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), limedai kuwa baadhi ya mawaziri na manaibu wao wamekuwa wakilipwa posho za kuhudhuria vikao vya Bunge Maalumu la Katiba hata wanapokuwa hawapo bungeni.

Kaimu Mwenyekiti wa Jukata, Hebron Mwakagenda alisema jana: “Mawaziri na manaibu ambao ni wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba walioko mjini Dodoma wanapokuwa na safari za kikazi huaga kwa Waziri Mkuu lakini jambo la kushangaza ni kuendelea kulipwa posho wakati hawapo.”

Alisema hali hiyo husababisha Bunge hilo kuendelea kuwalipa posho kupitia akaunti zao za benki lakini wakiwa hawapo Mjini Dodoma. Mwakagenda alisema mawaziri hao wanapotoka kwenda kwenye shughuli mbalimbali za kiserikali nako hulipwa posho. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MTOTO WA MIAKA 9 AMUUA MWALIMU WAKE KWA BUNDUKI

Screen Shot 2014-08-28 at 7.07.03 AM
Hiki ni kipande cha video ya mfunzo hayo kabla ya tukio.

Unaweza kushtushwa na umri mdogo wa mtoto mwenyewe aliekua anafundishwa kufyatua risasi kwenye bunduki, hii imetokea Arizona nchini Marekani ambapo mtoto wa miaka 9 ndio kichwa cha habari kwenye mafunzo ya kutumia submachine gun iliyotengenezwa Israel.
Mtoto huyu wa kike anaetokea New York alikua kwenye mapumziko na matembezi kama mtalii kwenye mji wa Arizona ambako pia ndio alichukua time yake ya ziada kujifunza kutumia bunduki lakini kwa bahati mbaya risasi ikafyatuka na kumjeruhi mwalimu wake aitwae Charles Vacca mwenye umri wa miaka 39 ambae alifariki baadae hospitalini.
Screen Shot 2014-08-28 at 7.34.27 AM 
Wakati tukio linatokea mtoto huyu alikua na wazazi wake ambapo tovuti ya bullets and burgers imesema watoto kati ya miaka 8 na 17 wanaweza kufyatua risasi kama iwapo tu watakua chini ya uangalizi wa Mzazi au Mwalimu.
Hii sio mara ya kwanza kwa tukio kama hili, ilishawahi kutokea mwaka 2008 ambapo mtoto wa miaka 8 alijiua kwa bahati mbaya kwa risasi kwenye onyesho la bunduki hukohuko Marekani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WANAWAKE WA BAWACHA WAMCHUKULIA FOMU HALIMA MDEE


Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (kushoto) akifuta machozi huku akiwa ameshika fomu za kuwania nafasi ya Uenyekiti wa Bazara la Wanawake wa Chadema (Bawacha) alizokabidhiwa na baadhi ya wanakwake makao makuu ya Chama hicho jijini Dar es Salaam  jana. 


Vigogo wa Baraza la Wanawake la Chadema (Bawacha), watachuana katika kinyang’anyiro cha kuwania uenyekiti wa baraza hilo baada ya jana baadhi ya wanawake kujitokeza kumchukulia fomu Mbunge wa Kawe, Halima Mdee.

Mbunge huyo anaungana na Mbunge wa Viti Maalumu, Chiku Abwao na wanachama wengine, Lilian Wasira na Sophia Mwakagenda ambao nao wamesharejesha fomu kuwania nafasi hiyo inayoshikiliwa na Suzan Lyimo.

Mwisho wa kuchukua na kurejesha fomu ni Agosti 30 na uchaguzi unatarajiwa kufanyika Septemba 11, mwaka huu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MACHIFU WAOMBA UTAWALA WAO UREJESHWE


Makamu mwenyekiti wa Bunge la Katiba, Samia Hassan Suluhu (kulia) akimsikiliza mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Umoja wa Machifu Tanzania, Chifu John Mgemela wa Magu (katikati) na Chifu Ndutu Ndaturu wa Bariadi waliotembelea ofisini kwake bungeni Dodoma juzi kutaka mapendekezo yao umoja huo yaingizwe kwenye Katiba mpya. 


Umoja wa machifu nchini juzi uliwasilisha mapendekezo yao katika Bunge la Katiba ukitaka yaingizwe kwenye Katiba inayotungwa.

Machifu hao wamependekeza kurudishwa kwa utawala wa Kichifu na Kitemi ili kutoa nafasi ya kurekebishwa kwa jamii ambayo kwa maoni yao imeanza kupoteza mwelekeo.

Mapendekezo ya viongozi hao wa jadi, yalipokelewa na makamu mwenyekiti wa Bunge hilo, Samia Suluhu Hassan ambaye aliwaahidi kuyafanyia kazi.

Wakizungumza mbele ya vyombo vya habari jana, Chifu John Mgemela wa Magu na Agnes Ntuzu wa Bariadi, walisema maoni hayo yalitokana na mapitio ya Rasimu ya Katiba inayoendelea kuboreshwa na Bunge hilo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

“Tunataka Katiba ieleze wazi kuwa sera na sheria zitakazotungwa zihakikishe kunakuwa na tume ya taifa ya utamaduni itakayoanzishwa kisheria kusimamia masuala ya utamaduni,”a lisema Chifu Mgemela.

Alisema ni vyema Katiba ijayo ikatoa fursa kwa machifu na watemi kutambulika katika mfumo rasmi wa uongozi wa jamii, ili wasaidie kudhibiti mwenendo wa jamii ambao kwa sasa umepoteza mwelekeo kimaadili.

Akipokea mapendekezo hayo, Suluhu alisema ingawa Bunge hilo halifanyi kazi ya iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya kukusanya maoni, hawawezi kukataa kuwapokea wananchi wanaopeleka mapendekezo yao.

Alisema muda mfupi baada ya kukutana na machifu hao, ratiba ilikuwa inaelekeza kuwa kamati ndogo ya uongozi wa Bunge hilo ikutane na miongoni mwa kazi ambazo zingefanywa ni kujadili mapendekezo yaliyopokelewa.

Alisema ikiwa mapendekezo hayo yatakubalika, maoni hayo yatawasilishwa kwenye kamati zote za Bunge hilo zinazoendelea kupitia na kujadili Rasimu ili yafanyiwe kazi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS AGOSTI 28, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WANAMGAMBO KUCHUKULIWA HATUA LIBYA


Harakati za kijeshi Libya
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio linalotoa wito wa kusitisha mapigano nchini Libya haraka iwezekanavyo na kuweka vikwazo dhidi watu wanaohusika na ghasia zinazoendelea nchini humo kati ya makundi ya wanamgambo wanaopingana.
Balozi wa Libya katika Umoja wa Mataifa ameliita azimio hilo kama "msingi", lakini ameonya kuwepo kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Orodha ya watakaokabiliwa na vikwazo vya uchumi bado haijaamuliwa.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeshtushwa na kuongezeka kwa mapigano katika ya makundi ya wanamgambo na vikundi vya kijeshi.
Mapigano ya karibuni yamejikita katika uwanja wa ndege wa kimataifa, Tripoli, ambao kwa sasa unadhibitiwa na wanamgambo kutoka Misrata na miji mingine yakiwa chini ya mwavuli wa "Mapambazuko ya Libya", ikiwa ni pamoja na makundi mengine ya kiislam. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ARSENAL YAFUZU UEFA 2014

Mchezaji wa Arsenal(kushoto) akipambana na mchezaji wa Basiktas(kulia). Arsenal ilishinda 1-0
Asernal imefuzu kucheza fainali za kombe la UEFA kwa msimu wa 17 mfululizo baada ya kuichabanga Besiktas ya Uturuki kwa jumla ya goli 1-0.Katika mchezo wa awali wiki moja iliyopita, timu hizo zilitoka sare ya kutofungana.
Hata hivyo, mchezaji mpya aliyejiunga na Arsenal msimu huu, Alexis Sanchez ndiye aliyeiwezesha Asernal kusonga mbele baada ya kufunga goli la kwanza tangu ajiunge na Arsenal akitokea Barcelona mwezi mmoja uliopita.
Sanchez aliyenunuliwa kwa kitita cha pauni milioni 35 kutoka Barcelona kwa kipindi chote cha mchezo alihaha kutafuta goli, ambapo katika dakika moja ya nyongeza katika kipindi cha kwanza cha mchezo aliweza kutumbukiza kimiani goli pekee kwa Arsenal na kufuzu kutoka hatua ya makundi kucheza fainali za UEFA kwa mwaka huu.
Arsenal ilipata nafasi za kumaliza mchezo mapema, lakini wachezaji wake Santi Cazorla na Alex Oxlade-Chamberlain walipoteza nafasi nyingi za wazi walizopata.
Zikiwa zimebaki dakika 15 kumaliza mchezo kipindi cha pili, Arsenal ilipata pigo baada ya mlinzi wake wa kulia Mathieu Debuchy alitolewa nje kwa kadi nyekundu kutokana na kuonyeshwa kadi mbili za njano. Lakini Arsenal waliendelea kupambana hadi dakika ya mwisho ya mchezo.
Timu nyingine zilizofuzu kucheza fainali za UEFA kwa mwaka huu katika michezo ya Jumatano usiku ni Athletic Bilbao iliyopata ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya Napoli. (Jumla 4-2), Bayer 04 Leverkusen 4, FC Copenhagen 0, jumla(7-2). Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Ludogorets Razgrad 1 - 0 Steaua Bucharest
Malmö FF 3 - 0 FC Red Bull Salzburg

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...