Thursday, August 07, 2014

MBUNGE CHADEMA ATINGA BUNGENI...!!!

Mbunge wa Viti Maalumu, Chadema  Leticia Nyerere akiwa kwenye viwanja vya bunge jana mjini Dodoma. 

Mjumbe mwingine wa Bunge la Katiba kutoka Kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) jana alionekana kwenye Viwanja vya Bunge na alisaini za mahudhurio.
Mjumbe aliyeonekana jana, Leticia Nyerere wa viti maalumu, Chadema, anafanya idadi ya wajumbe waliotinga kwenye viwanja hivyo hadi sasa kufikia watatu baada ya Chiku Abwao (viti maalumu Chadema) kuonekana juzi na Clara Mwatuka (viti maalumu CUF) kuonekana Jumapili.
Nyerere hakuwa akihudhuria vikao baada ya Ukawa kutangaza kususia Bunge mwezi Aprili na jana hakupatika kuzungumzia suala hilo.
Kuonekana kwa mjumbe hao kunaweza kutafsiriwa kuwa ni kubomoka kwa ngome za Vyama vya Chadema, NCCR na CUF vinavyounda umoja huo kwani tangu awali walikubaliana kutoshiriki shughuli za Bunge hadi pale watakapofikia makubaliano ya hoja zao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

POLEPOLE: 'ANAYEZUIA MIJAALA YA KATIBA AMEPOTEZA SIFA YA KUWA RAIS'

Aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Hamphrey Polepole akizungumza kwenye mjadala wa wazi kuhusu Katiba mpya, uliofanyika jijini Dar es Salaam jana.

Aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole amesema makongamano na mijadala inayohusu Katiba mpya yataendelea kwa sababu ni ya lazima pia ni haki ya kikatiba.
Akizungumza kwenye Kongamano la Katiba lilioandaliwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) jana, Polepole alisema mtu anayezuia wananchi kuendelea kuzungumzia Katiba amepoteza sifa za kuwa kiongozi wa nchi.
Huku akishangiliwa na washiriki wa kongamano hilo, Polepole alisema Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi ya kidemokrasia, inayoheshimu haki za binadamu na utawala wa kiraia. Hivyo inashangaza kusikia kuna kiongozi anajaribu kuwafunga mdomo wananchi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAPENZI YA KWELI: WAAGA DUNIA PAMOJA BAADA YA MIAKA 62...!!!

Don na Maxine Simpson wakiwa hospitalini
Amini Usiamini mapenzi ya kweli bado yapo humu duniani!
Kisa kimoja ambacho kimedhibitishia wengi baada ya wapenzi wawili waliooana na kuishi pamoja kwa takriban miaka 62 walipoaga dunia pamoja.
Don na Maxine Simpson walikuwa wakazi wa mji wa Bakersfield, ulioko jimbo la California, Marekani waliaga dunia saa nne baada ya kushikana mikono hospitalini na kuahidiana penzi lao halitafifia kamwe hata mauti iwapate.
Walikuwa wamelazwa hospitalini kufuatia hali duni ya afya inayotokana na umri wao mkubwa.
Don na Maxine Simpson wakiwa bukheri wa afya
Lakini punde alipoaga Maxine na mwili wake ukaondolewa chumbani walikokuwa wamelazwa pamoja na mumewe Don, zilipata saa nne tu uchungu ulipomzidi Don na akakata roho iliwaendelee kupendana na mkewe ahera.
Mjukuu wao Melissa Sloan aliiambia runinga ya KERO-TV Kuwa Don alimhusudu sana nyanya yake yaani Maxine tangu alipomtupia jicho mnamo mwaka wa 1952 walipokutana katika mashindano ya Bowling.
Wapenzi hao wawili waliooana mwak huohuo na hawajawahi kuachana tangu hata katika mauti.
''Babu yangu alikuwa anatamani kuishi na nyanya yangu na hata baada ya wawili hao kuanza kuugua kutokana na umri wao mkubwa waliwaomba wasimamizi wa hospitali walimolazwa wasiwatenge.''
Don alikuwa na miaka 90 huku mke wake akiwa na miaka 87.
Don na Maxine Simpson walipokutana
''Babu yangu alihudumu kama mwanajeshi katika jeshi la Marekani naye bibi alikuwa ni muuguzi haswa walipokuwa huko Ujerumani ambapo waliwahi kuishi kwa muda mrefu.''alisema mjukuu wao Melissa.
Wamemuacha nyuma mtoto mmoja wa kiume na wajukuu watano.
Je unaamini kuna penzi la kweli ?
Tuwachie jibu lako katika mtandao wetu wa facebook BBCSwahili.com na pia kwenye tweeter @bbcswahili. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

BOKO HARAM WASHAMBULIA CAMEROON

Wapiganaji wa Boko haram
Watu wanaodaiwa kuwa ni kundi la Boko Haramu wameshambulia raia na wanajeshi kaskazini mwa Cameroon ambapo watu kumi wanasadikiwa kufariki dunia.
Shambulio hilo linakuja baada ya shambulio jingine la hivi karibu ambapo wapiganaji wa kundi hilo walivuka mpaka kutoka Nigeria na kufanya mashambulizi kadhaa kwa wiki za hivi karibuni nchini Cameroon.
Tayari majeshi kutoka katika ukanda huo yameahidi kupambana na wapiganaji hao wa Boko Haramu walioua watu 4000 wasio na hatia kwa mwaka huu pekee.

Ni shambulizi la mchana la kusikitisha. Waendesha piki piki wanadaiwa kuwa ni wapiganaji wa Boko Haram waliolenga kukishambulia kijiji caha Zigague kaskazini mwa Cameron.
Walimshambulia kiongozi wa jadi wa baadae kurushiana risasi na kundi la wanajeshi wa Jeshi la Cameroon. Mwanajeshi mmoja aliuawa pamona na raia nane.
Kundi hilo pia lilishambulia kituo cha polis.
Katika siku za hivi karibu wapiganaji wa Boko Haramu wamekuwa wakifanya mashambulizi katika nchi ya Cameroon. Kumekuwa na matukio kadhaa ya utekaji nyara jambo lilosukuma jeshi kuanza mapambano ya angani.
Mashambulizi mengi yanayofanywa Boko Haramu yamekuwa yakielekezwa nchini Nigeria ambapo mashirika ya kutetea haki za binadamu yanasema zaidi ya watu 4000 wameuawa kwa mwaka huu pekee.
Karika siku za hivi karibuni, Camerooni, Nigeria, Chad na Niger zilikubalina kuunda jeshi la pamoja la kanda hiyo ili kupambana na wapiganaji hao wa Boko Haramu. Hata hivyo Cameoroon wakati inatafuta namna ya kupambana Boko haram kunaongeza hali isiyo tabirika ya kuongezeka kwa mashambulizi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MASOGANGE AHOJIWA ZAIDI YA MASAA 10 'AIRPORT'

http://jambotz8.blogspot.com/
Kikosi Kazi cha Polisi cha Kuzuia Dawa za Kulevya nchini kimemhoji kwa zaidi ya saa 10, msanii Agnes Gerald ‘Masogange’ kuhusiana na tuhuma za kukamatwa na dawa aina ya crystal methamphetamine huko Afrika Kusini, Julai mwaka jana.
Kamanda wa Polisi Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Gedfrey Nzowa alisema jana kuwa Masogange alianza kuhojiwa juzi usiku baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam akitokea Afrika Kusini.
Nzowa alisema baada ya kuhojiwa, Masogange aliruhusiwa na kwamba yupo huru, ameachiwa bila masharti yoyote.
Kamanda wa Polisi wa Uwanja wa Ndege, Hamisi Selemani naye alithibitisha kuhojiwa kwa msanii huyo akisema: “Hapa kuna kikosi kazi, kila mmoja alimhoji kwa wakati wake lakini kwa upande wa polisi tulimpekua na kumhoji lakini tumemwachia.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS AGOSTI 07, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, August 06, 2014

BINTI ALIYEGOGWA KWA BAHATI MBAYA NA MTOTO WA RAIS OBAMA ATOA KALI YA MWAKA...!!!

Mtoto wa kike wa rais wa  Marekani, Maria Obama mwenye umri wa miaka 16 alimgonga kwa bahati mbaya msichana aliyefahamika kwa jina la Bridget Truskey walipokuwa katika tamasha kubwa la muziki la Lollapalooza nchini Marekani. 
Msichana huyo amewashangaza watu baada ya kuonesha kufurahishwa sana na tukio hilo  kutokana na umaarufu wa Maria Obama.
Truskey ametweet sentensi kadhaa kuonesha furaha yake huku maelezo yakionesha kuwa haamini kilichotokea.
“I got (accidentally) kicked by Malia Obama today at Lollapalooza. No lie. Malia. Obama. It was awesome. #lollapalooza.”  Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WARIOBA: BUNGE LITAPOTEZA FEDHA NYINGI ZA WANANCHI...!!!

Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wakiwa ndani ya Ukumbi wa Bunge hilo baada ya kuanza kwa vikao vyake mjini Dodoma jana. 

Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema kuendelea vikao vya Bunge Maalumu la Katiba bila kuwapo maridhiano baina ya pande zinazovutana na upande mmoja ukibaki nje ya Bunge, ni sawa na kutumia vibaya fedha za Watanzania.
Amesema kauli kwamba akidi ya wajumbe wa Bunge hilo imetimia na vikao vinaweza kuendelea haiwezi kuzaa Katiba itakayokubaliwa na wananchi wote na ni tofauti na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba inavyoeleza katika sehemu ya kufanya uamuzi.
Akizungumza katika mahojiano na mwandishi wetu ofisini kwake Dar es Salaam jana, Jaji Warioba alisema, “Kama uwezekano wa kukutana upo, kwa nini Bunge liendelee kutumia fedha wakati mnajua kuwa mwisho hamtafikia uamuzi? Jambo la msingi ni kujitahidi kuafikiana na Bunge liwe na wajumbe wote.”
Kauli ya Warioba imeungwa mkono na Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba wakati akichangia hoja ya mabadiliko ya kanuni ya Bunge hilo kwa kulitaka bunge hilo kujitathimini iwapo baada ya mjadala litaweza kufikia uamuzi, ili kuepuka matumizi mabaya ya fedha za walipakodi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PINDA: TUNGEJUA TUNGEAMUA AINA YA MUUNGANO KWANZA

Waziri Mkuu Mizengo Pinda PICHA|MAKTABA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amesema kama Serikali ingejua, ingeanza kwa kura za maoni ya wananchi kuamua aina ya muungano wanaoutaka, kabla ya kuendelea na mchakato wa Katiba.
“Tungejua kama hali ya aina hii itajitokeza, basi tungeanza na kura ya maoni, tungewauliza wananchi kama wanautaka muungano na kama ndiyo, basi uwe wa aina gani au serikali ngapi, mtu angesema moja, mbili, tatu na kadhalika,” alisema Pinda jana kwenye Viwanja vya Bunge mjini hapa.
Pinda alikuwa akijibu swali kuhusu hatima ya Bunge Maalumu kutokana na wajumbe wa Bunge hilo ambao ni wanachama wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kususia vikao hivyo wakishinikiza kile walichokiita kujadiliwa kwa rasimu iliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba na siyo vinginevyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

YANGA SC WAIBUKA NA KUIPA MAKAVU ‘LAIVU’ CECAFA, WASEMA INALICHIMBIA SOKA KABURI


benomarcio

Katibu Mkuu wa Young Africans Bw Beno Njovu akiongea na waandishi wa habari leo makao makuu ya klabu ya Yanga, kushoto kwake ni Kocha Mkuu Marcio Maximo na afisa habari Baraka Kizuguto
Uongozi wa klabu ya Young Africans leo umefanya mkutano na waandishi wa habari juu na kusema kilichofanywa na waandaji wa michuano ya Kombe la Vilabu Bingwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kuiondoa timu isishiriki ni cha kushangaza sana na kinadidimiza soka kwa ujumla.
Katibu Mkuu wa Young Africans Bw Beno Njovu amesema walipata barua ya mwaliko wa kushiriki mashindano tarehe 25/7/2014 na kudhibitisha kushiriki michuano hiyo kwa kuandika barua iliyokwenda TFF na kisha wao kuiwasilisha kwa CECAFA.
“Baada ya kudhibitisha kushiriki michuano hiyo tuliambiwa na CECAFA tutume orodha ya wachezaji na viongozi ambao watasafiri kuelekea nchini Rwanda kwenye michuano hiyo ili waweze kuandaa tiketi za ndege na sehemu ya malazi kitu ambacho tulitimiza” alisema Beno. 
Lakini katika hali ya kushangaza jana tulipokea barua kutoka TFF ikisema CECAFA imetuondoa kwenye mashindano hayo kwa kushindwa kukidhi vigezo na kuiteua timu ya Azam kuchukua nafasi yetu “aliongeza Beno.”

FRANK LAMPARD ANAWEZA KUFIKIA REKODI YA KUCHEZA MECHI 1,000 AKIWA MANCHESTER CITY

_76387466_frank_lampard_chelsea_getty
FRANK James Lampard, mwenye miaka 36, mpaka sasa amecheza mechi 973 kwa klabu na nchi yake katika maisha ya soka.
Anahitaji mechi 27 tu kufika digiti nne na kitu hicho anaweza kufanya kupitia michuano ya ligi kuu soka nchini England baada ya kujiunga na Manchester City kwa mkopo kutoka klabu ya New York City mwezi huu.
Kiungo huyo mkongwe ataitumikia Man City mpaka mwezi Januari mwakani ambapo ataende NYCFC kujiandaa na michuano ya ligi kuu nchini Marekani.
Atakuwepo kwa michezo 23 ya ligi kuu, mechi sita za ligi ya mabingwa, ataanza kombe la Capital One na FA na mechi ya Ngao ya Hisani itakayopigwa siku ya jumapili.
Lampard ambaye bado hajastaafu soka la kimataifa, ana nafasi kubwa ya kuongeza mechi zake 106 alizocheza kwa timu ya taifa baada ya kurudi ligi kuu.
Lampard ndiye mchezaji aliyecheza mechi nyingi zaidi kwa taifa lake. Pia alicheza England B na alicheza mara 19 katika timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 19.
Kiungo huyo alicheza mechi 187 akiwa na Westaham, klabu yake ya kwanza na alicheza mechi 11 akiwa kwa mkopo Swansea kabla ya kwenda kucheza mechi 649 katika miaka 13 aliyocheza Chelsea, na kujiweka katika nafasi ya tatu ya kucheza mechi nyingi klabuni hapo nyuma ya Peter Bonetti na mchezaji anayeshikilia rekodi Ron Harris.
Mchezaji wa mwisho wa England kufikisha mechi 1,000 katika timu ya wakubwa alikuwa kocha msaidizi wa Manchester United, Ryan Giggs ambapo alifikisha idadi hiyo mwaka 2013 kwenye mechi za ligi ya mabingwa dhidi ya Real Madrid.
Kocha wa sasa wa Fleetwood, Graham Alexander, ambaye aliichezea Scunthorpe United, Luton Town, Preston North End na Burnley alifikisha mechi 1,00 mwezi aprili 2011.

Tuesday, August 05, 2014

MJUMBE WA UKAWA ATINGA BUNGENI...!!!

Bunge  

Wakati wajumbe wa Bunge la Katiba wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakiendelea na msimamo wa kususia vikao vinavyotarajiwa kuanza leo mjini Dodoma, mmoja wa wajumbe wake jana aliripoti bungeni na kujiandikisha.
Mjumbe huyo, Clara Mwatuka ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), alionekana katika Viwanja vya Bunge saa 6:30 mchana akiwa ameongozana na wabunge kadhaa wa CCM wakiwamo Livingstone Lusinde (Mtera) na Jerome Bwanausi (Lulindi).
CUF ni moja ya vyama vinavyounda Ukawa, pamoja na Chadema na NCCR Mageuzi na tayari viongozi wakuu wa vyama hivyo, Profesa Ibrahim Lipumba, Freeman Mbowe na James Mbatia wametangaza kwamba wajumbe wote wanaotokana na umoja wao hawatashiriki vikao vya Bunge hilo.
Mwatuka baada ya kujaza fomu maalumu za kujiandikisha, alielekea lango la Magharibi na kuingia kwenye gari la Bwanausi.
Awali, alipoulizwa kwenye Viwanja vya Bunge kuhusu kuwapo kwake Dodoma, alikataa kuzungumza lakini alikiri kujiandikisha bungeni.
Baadaye alipoulizwa imekuwaje akajiandikisha ilhali uongozi wa chama chake umesema hawatashiriki, Mwatuka alijibu: “Kwa hapo ni mapema sana kuzungumzia suala hilo, nitazungumza kesho (leo) kule bungeni ukinitafuta.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE AGOSTI 05, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ISRAEL NA HAMAS KUSIMAMISHA MAPIGANO?

Mwanajeshi wa Israel
Israel na Hamas yamekubaliana kufuata maombi ya Misri ya kusimamisha mapigano kwa siku tatu huko Gaza, kuanzia leo jumanne asubuhi.
Israel inasema kuwa itakubaliana na mpango huo bila ya masharti yoyote.
Nayo Misri inasema kuwa muafaka huo unafaa kufuatiwa na mazungumzo ya amani yenye nia ya kuboresha kabisa usalama.
Majeshi ya Israeli awali yalirejelea operesheni kali zaidi huko Gaza, baada ya kumalizika kwa makataa ya saa saba ya kukomesha mapigano. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BENKI YA DUNIA YASAIDIA EBOLA

Wahudumu wa afya katika tahadhari ya kukabiliana na Ebola
Benki ya Dunia imetangaza kutoa msaada wa hadi dola milioni mia mbili, kutoka mfuko wa dharura wa msaada, ili kuzisaidia mataifa matatu ya Afrika magharibi kukabiliana na ugonjwa hatari wa ebola.
Pesa hizo zitasaidia Liberia, Sierra Leone na Guinea, ili kuboresha vifaa vya afya ya umma na kushughulikia matatizo ya uchumi yaliyosababishwa na ugonjwa huo.
Rais wa Bank ya Dunia Jim Yong Kim amesema amehuzunishwa sana kwa jinsi Ebola unavyoendelea kuvuruga mfumo wa afya kwa nchi tatu.
Kwa mwaka huu pekee karibu watu mia nane na tisini wamekufa kutokanana Ebola katika nchi za Afrika Magharibi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...