Friday, July 25, 2014

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JULAI 25, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


1_ba461.jpg
2_a3788.jpg
3_25f32.jpg 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TIBA, KINGA YA UKIMWI VYANUKIA

Watafiti wakitoa sampuli za damu kutoka kwa sokwe mtu katika utafiti wa Ukimwi huko Gabon. Picha ya Mtandao 

Watafiti katika Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba cha Temple, Marekani wamegundua dawa ya kuangamiza Virusi Vya Ukimwi (VVU) ambayo ni ya uhakika zaidi ukilinganisha na zilizowahi kupatikana katika tafiti za awali duniani.
Dawa yao inaweza kutumika kwa tiba ya wanaoishi na VVU na kinga kwa wale ambao bado hawajaambukizwa.
Mmoja wa watafiti hao, Dk Kamel Khalili aliwaambia waandishi wa habari juzi mjini Philadelphia, Marekani kuwa tofauti na utafiti mwingine, wao wamegundua namna ya kukiondoa kirusi kilichoingia kwenye kinasaba (DNA) ndani ya CD4 na kukitoa nje na hatimaye kukiua.
Alisema dawa hiyo inafanya kazi hiyo bila kuathiri seli za mwili wa binadamu.
Dk Khalili alisema ugunduzi wao ni wa hali ya juu zaidi kwa sababu teknolojia ya kutengeneza dawa hiyo ni tofauti na nyingine zilizokwisha kugunduliwa ambazo hazina uwezo wa kupenya ndani ya seli za binadamu, bali kuathiri tu VVU vilivyopo nje yake, ndani ya mfumo wa damu.
“Dawa yetu inakivuta kirusi nje ya seli (CD4) bila kuiathiri seli yenyewe na kukiua. Hivyo dawa hii itatumika kwa muda fulani na kuua virusi vyote mwilini na hakuna haja ya kuitumia wakati wote kama ilivyo dawa ya kufubaza VVU (ARV).” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MABAKI YA NDEGE ALGERIA YAONEKANA

Mabaki ya ndege iliyopotea ikiwa na watu 116 njiani kutoka Burkanafaso kwenda Algers yamepatikana nchini Mali. Maafisa wa Jeshi wa Burkina faso wamesema ndege hiyo iliyokuwa chini ya shirika la ndege la Algeria imeanguka karibia kilomita 50 kutoka mpaka wa Burkanafaso.
Waongoza ndege walipoteza mawasilino na ndege hiyo muda mfupi baada ya kupata taarifa kutoka kwa Rubani kuwa alikuwa kwenye eneo lenye hali mbaya ya hewa. Utafutaji wa ndege hiyo umeanzia katika eneo la Gao mpaka Tessalit. 
Kumekuwepo na hali mbaya ya hewa kwa zaidi ya saa 24. Waziri wa mambo ya nje wa ufaransa, Laurent Fabius amesema inaonekana ndege ilihamishwa mwelekeo kwa sababu ya hali mbaya ya hewa.
 "Walikuwa wameelekezwa kubadili njia ya kawaida kutoka na mabadiliko ya hali ya hewa. Ndege ilikuwa ikipaa juu ya eneo la Malian. Pamoja na juhudi kubwa , mapaka sasa hakuna dalili za kupatika na kwa ndege hiyo. Pengine ndege imeangua" Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Sunday, June 29, 2014

HOTUBU YA WAZIRI MKUU MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA YA KUAHIRISHA BUNGE

PG4A9702
UTANGULIZI

a)    Masuala ya Jumla

Mheshimiwa Spika,
1.    Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwenye wingi wa Rehema kwa kutupatia uzima na afya hadi kufikia siku ya leo. Tumekuwepo hapa kwa takriban miezi miwili ambapo tumeweza kupokea na kujadili Taarifa za Mapitio ya Utekelezaji wa Kazi za Serikali kwa mwaka 2013/2014 na Mwelekeo kwa mwaka 2014/2015 kwa Wizara mbalimbali na hatimaye kupitisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2014/2015.


2.    Napenda kutumia nafasi hii ya awali kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wote kwa kazi nzuri ya kutukuka ambayo wameifanya kwa nidhamu na ufanisi mkubwa, hususan wakati wa Mjadala wa Bajeti ya Serikali na Mafungu ya Wizara za Kisekta. Kipekee niwashukuru Wajumbe wa Kamati ya Bajeti chini ya Uongozi mahiri wa Mheshimiwa Mtemi Andrew John Chenge, Mbunge wa Jimbo la Bariadi Magharibi kwa kazi yao nzuri ya kuchambua Bajeti ya Serikali na Sheria zinazoambatana na masuala ya Bajeti. Changamoto zilikuwa nyingi,   lakini   kwa   pamoja   tumekubaliana   na   kuafikiana. Kazi kubwa iliyoko mbele yetu ni kwenda kushirikiana na Wananchi katika utekelezaji wa Bajeti hii ili kuwaletea maendeleo.

Mheshimiwa Spika,
3.    Katika kipindi hiki tukiwa hapa Bungeni, yapo matukio ya kusikitisha yaliyotokea ambapo baadhi ya Waheshimiwa Wabunge walipoteza Wapendwa wao. Aidha, yapo matukio ya Kitaifa yaliyosababisha kupoteza maisha ya Ndugu, Jamaa na Marafiki. Napenda kutumia nafasi hii kuwapa pole Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote waliofikwa na misiba na majanga mbalimbali, ikiwa ni pamoja na wote waliopotelewa na Ndugu, Jamaa na Marafiki. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

JAMBO TZ BLOG INAWATAKIA WATU WOTE KHERI YA MFUNGO WA RAMADHANI

http://jambotz8.blogspot.com/

 Jambo Tz Blog inawatakia Watanzania wote kheri ya mfungo mtukufu wa Ramadan.
http://jambotz8.blogspot.com/
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 29, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ANGALIA PICHA ZA KIATU CHA MALKIA ELIZABETH WA UINGEREZA ALICHOVAA KWA MIAKA 50...!!!

kiatu

Hizi ndiz0 Picha za kiatu cha aina moja alichovaa malkia Elizabeth wa Uingereza kwa miaka 50. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

kiatu1
kiatu2
kiatu4
kiatu5 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ADA YA VYUO VYA UALIMU YAPANDA MARADUFU...!!!


Baadhi ya wahitimu wa chuo cha Ualimu.PICHA|MAKTABA
Serikali imepandisha maradufu ada kwa wanafunzi wanaosomea ualimu kwenye vyuo vya ualimu nchini kuanzia muhula ujao wa masomo. Ada hizo kwa wale wa ngazi za cheti na stashahada ambazo zimeongezwa kwa karibu mara mbili au zaidi ya zile zilizokuwa zikilipwa awali. Uamuzi huo ambao huenda ukawaathiri zaidi wanafunzi ambao waliona ualimu kama kimbilio, unaelezwa na baadhi ya wadau wakiwamo walimu, wanafunzi na hata wakufunzi wa baadhi ya vyuo nchini kuwa ni wa ghafla.
Kwa mujibu wa baadhi ya wakufunzi, uamuzi huo umetolewa kupitia waraka wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na unatarajiwa kuanza kutekelezwa muhula wa pili wa masomo utakaoanza Julai 2, mwaka huu.
Kabla ya kupandishwa kwa ada hizo, wanafunzi wanaosomea ualimu kwa ngazi ya cheti walikuwa wakilipa Sh200,000, lakini sasa watalazimika kulipa Sh300,000, ikiwa ni ongezeko la asilimia 50. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

CHINA HAITATUMIA MABAVU DHIDI YA MATAIFA MENGINE

Rais Xi Jinping amesema nchi yake haitawahi kutumia nguvu dhidi ya mataifa mengine Rais Xi Jinping wa Uchina amesema nchi yake daima haitojaribu kulazimisha nchi nyengine kufuata matakwa ya Uchina, hata Uchina itapokuwa na nguvu kubwa zaidi.

Alisema hayo mjini Beijing ambapo aliwapokea viongozi wa India na Myanmar (Burma). Rais Xi alisema tabia ya uonevu na kutumia nguvu za kijeshi haimo katika damu ya watu wa Uchina, na kwamba enzi za mabavu ya mataifa makuu zimekwisha.
Mwandishi wa BBC mjini Beijing anasema hotuba ya Rais Xi ilikusudiwa kuwatuliza majirani wa Uchina pamoja na Marekani, ambao wana wasi-wasi kwa vile bajeti ya jeshi la Uchina inazidi kuongezeka, na kile kinachoonekana kama sera ya Uchina ya kudai ardhi katika mizozo kadha na majirani zake.
Mkutano unaofanywa Beijing unaadhimisha miaka 60 ya makubaliano ya ushirikiano wa salama uliotiwa saini na Uchina, India na Burma - ambayo piya inajulikana kama Myanmar. Na nchini Taiwan shughuli mbili zimefutwa wakati wa ziara ya afisa mwandamizi wa Uchina, baada ya waandamanaji kuurushia rangi msafara wa magari yaliyokuwa yakimsindikiza afisa huyo.
Zhang Zhijun, ambaye amemaliza ziara ya siku nne Jumamosi, hakuumia katika mvurugano huo. Watu wengi wa Taiwan hawapendi Uchina kuonesha madaraka yake juu ya kisiwa hicho kinachojitawala, na ambacho Uchina inakiona kama ni chake. Katika miaka ya karibuni kiongozi wa Taiwan amekuwa akijaribu kuzidisha fungamanisho za kibiashara baina ya nchi mbili hizo.
Siku ya Ijumaa, Bwana Zhang alisema Beijing inaheshimu uamuzi wa watu wa Taiwan kuhusu aina ya maisha yao na mfumo wao wa jamii. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC Swahili

Thursday, June 26, 2014

UBABE BUNGENI, MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI NUSURA AMPIGE KAFULILA

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema (kushoto) akizuliwa na Mawaziri na Manaibu Waziri kutomfuata Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila baada ya kupandwa na hasira kufuatia mbunge huyo kumtuhumu kwa kumuita mwizi kwenye ukumbi wa Bunge, mjini Dodoma jana. Picha na Edwin Mjwahuzi 
Kwa ufupi
“Profesa Muhongo aliliambia Bunge kuwa Serikali ililipa fedha hizo ili kuondokana na kesi hiyo lakini ninazo nyaraka za Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kuteua kampuni mbili za uwakili kwenda kuiwakilisha katika kesi nchini Uingereza,” alisema Kafulila.


Kama siyo kuzuiwa na mawaziri, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema jana angezua tafrani bungeni kutokana na kitendo chake cha kutaka kumpiga Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila. 

Sakata hilo lilitokea jana asubuhi baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azzan Zungu kuahirisha kikao cha Bunge hadi jioni, ikiwa ni muda mfupi baada ya Werema na Kafulila kurushiana maneno bungeni. Jaji Werema alichukia baada ya Kafulila kumwita mwizi, akijibu mapigo baada ya mbunge huyo kuitwa tumbili na mwanasheria huyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS JUNI 26, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MSEKWA ATOBOA SIRI YA CCM KUNG'ANG'ANIA SERKALI MBILI...!!!


Spika mstaafu wa Bunge, Pius Msekwa akikusanya baadhi ya vitabu alivyoviandika  alipokuwa akifanya mahojiano na wahariri wa gazeti hili nyumbani kwake jijini Dar es Salaam. 

Makamu Mwenyekiti mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Pius Msekwa ametoboa siri ya chama hicho kung’ang’ania Muungano serikali mbili akisema hiyo ndiyo sera yake pekee iliyopitishwa na wanachama wake wote kwa kura ya maoni.
Msekwa alieleza hayo katika mahojiano maalumu na wahariri wa gazeti hili yaliyofanyika nyumbani kwake Oysterbay, Dar es Salaam.
Msekwa ambaye katika habari iliyochapishwa na gazeti hili jana alieleza kuwa binafsi, hana tatizo na suala la idadi ya Serikali katika Muungano, alisema kamwe hawezi kukishauri chama chake kukubaliana na mapendekezo ya Rasimu ya Katiba iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya muundo wa serikali tatu.
“Siwezi kuishauri CCM kukubali serikali tatu. Hili la Serikali mbili ni sera ya CCM, siyo tu sera ya kawaida, bali hii ni sera pekee iliyopitishwa na wanachama wote kwa kura ya maoni,” alisema Msekwa ambaye pia ni Spika mstaafu wa Bunge.
Alisema tofauti na sera hiyo ya serikali mbili, sera nyingine za chama hicho huanzia katika ngazi ya Kamati Kuu, kujadiliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) na kupitishwa na Mkutano Mkuu wa Taifa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WALIOVUNJA 'MOCHWARI' WAPATA DHAMANA

Watu sita kati ya 12 wanaotuhumiwa kwa uchochezi na kuvunja chumba cha kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya Kaigara wilayani hapa, jana wamepata dhamana baada ya kutimiza masharti ya mahakama.
Mwendesha mashtaka wa polisi, Cleophace Waane Maatu aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni pamoja na Georgina Angelo, Triphory Joseph, Georgia Triphory, Shafii Abdul, Venanti Benard na Shamim Yusuph.
Aliiambia mahakama kuwa mnamo Juni 16, mwaka huu watuhumiwa hao walifanya uchochezi na kuvunja chumba cha maiti cha kituo hicho na baadaye kutoa mwili wa binti aliyedaiwa kufariki na kunyofolewa viungo vya mwili.
Maatu alisema mtuhumiwa wa kwanza ni shangazi wa marehemu, Georgina Angelo aliyekuwa ametoroka na kukamatwa na polisi kwa kuhusika na uchochezi kwenye mazishi ya binti huyo katika Kijiji cha Bukono wilayani hapa.
Alisema Triphory Joseph na mkewe Georgia ambao ni wazazi wa binti aliyefariki akifanya kazi za ndani mkoani Arusha na Georgina Angelo wanatuhumiwa kwa uchochezi wa kuvunja mochwari ya kituo hicho.
Alisema katika vurugu hizo, pia siku hiyo saa 11:00 jioni walivamia shamba la Valentina Maxmilian na kukatakata migomba pamoja na mazao mengineyo kisha kuchoma nyumba mbili, vitu vyote vikiwa na thamani ya Sh20 milioni.
Watuhumiwa wengine sita hawakutimiza masharti ya dhamana na kesi hiyo itatajwa tena Julai 10, mwaka huu.
Kesi hiyo imevuta hisia za wengi kufuatia kifo cha binti huyo kuzua sintofahamu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MLIPUKO WAUA WATU 21 NA KUJERUHI 50 NIGERIA



Moto ukiteketea kulikolipuka bomu nje ya kituo cha biashara Abuja, Nigeria.

Kumetokea shambulizi la bomu mbele ya soko lenye shughuli nyingi katika mji mkuu wa Nigeria Abuja na kuwauwa zaidi ya watu 21.

Taswira ya majonzi na kilio ilitanda katika mji wa Abuja, mamia ya watu waliokuwa wakinunua bidhaa katika soko hilo wakijikuta wakivuja damu kutokana na majeraha ya mlipuko huo na wengine kuishia mauti.

Bomu hilo lililipuka mbele ya kituo kikubwa cha biashara, kinachotembelewa na watu wengi.

Walioshuhudia walisema sehemu za miili ya wanadamu zilitapakaa kila mahali sakafuni.

Magari yalichomeka kabisa na vioo katika madirisha ya nyumba zilizokuwa karibu kuvunjika vyote. Watu waliokuwa na hofu walielekea kwenye mahospitali yaliyo karibu ambapo walishuhudia magari ya wagonjwa yakisongamana kila mahali yakiwaleta wagonjwa na miili ya waliokufa.

John Tobi Wojioa aliwasili mahali hapo muda mfupi baadaye akimtafuta jamaa wake. Alitaja alichoona kama mafuriko ya damu:

"Kulikuwepo magari ya wagonjwa wa shirika la FRCS (federal Road Safery Corps) na ya mashirika mengine yaliyokuwa yakiingia na kuondoka yakibeba miili ya waathirika. Kwenye barabara alama za damu za nyayo za wanadamu zilionekana kila mahali," alisema Bwana Wojioa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, June 21, 2014

MARCIO MAXIMO KUTUA BONGO JUMANNE

417570_heroaMaandalizi ya msimu wa ligi kuu ya Tanzania yameanza kupamba moto huku vilabu vikijaribu kujiimarisha tayari kwa mapambano, kwa upande wa klabu ya Yanga wameanza kwa kuimarisha benchi la ufundi kwa kumuajiri kocha Marcio Maximo.
Kocha huyo mbrazil anayeheshimika zaidi nchini, Marcio Maximo atatua Jangwani ndani ya siku nne kuanzia leo Jumamosi. Bosi huyo ambaye anasifika zaidi kwa msisitizo wake katika nidhamu za wachezaji atatua Jumanne ikiwa ni mapema kabla ya uchaguzi wa Simba utakaofanyika Juni 29 Jijini Dar es Salaam. Mwanaspoti linajua kwamba Maximo yuko jijini Brasilia akifanya kazi ya uchambuzi wa mechi za Kombe la Dunia kwenye televisheni ya Taifa ya Mexico na mkataba wake unamalizika Jumatatu.
Yanga imethibitisha kwamba Maximo ameshaanza maandalizi ya safari hiyo tangu juzi ambapo katika hilo pia amewajulisha baadhi ya maofisa wa Ubalozi wa nchi hiyo nchini kuwa atakuwa Tanzania mapema wiki hii kumalizia maongezi yake na mabosi wa Yanga.
Yanga wamemleta Maximo mapema kufanya maandalizi ya uhakika katika kikosi cha timu hiyo ikiwa ni kuwawahi wapinzani wao wa jadi Simba ambao bado wapo katika mchakato wa uchaguzi.
“Ilikuwa kuna baadhi ya viongozi waende Brazil kumalizia mazungumzo na kusainishana mkataba  lakini hilo limebadilishwa. Maximo ndiyo atakuja Dar es Salaam kuepuka gharama,”alisisitiza mmoja wa viongozi wa Yanga.
Source: Mwanaspoti

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...