Sunday, June 01, 2014

GHANA YATANGAZA KIKOSI CHAKE KITAKACHOSHIRIKI KOMBE LA DUNIA, GYAN KUONGOZA KIKOSI

414047_heroa 
KOCHA mkuu wa timu ya taifa ya Ghana, Kwesi Appiah ametaja kikosi chake cha mwisho cha wachezaji 23 kwa ajili ya fainali za kombe la dunia zinazoanza kushika kasi mwezi huu nchini Brazil.  
Kikosi hicho cha Appiah kinajumuisha wachezaji 16 wanaokwenda kucheza fainali hizo kwa mara ya kwanza, huku nahodha Asamoah Gyan na Sulley Muntari wakiwa wakongwe wanaokwenda kucheza fainali zao za tatu mfululizo, wakati Jonathan Mensah, Michael Essien, Kwadwo Asamoah, Andre Ayew na Kevin-Prince Boateng wanakwenda kucheza fainali hizo kwa mara ya pili.  
Kocha huyo mwenye miaka 53 amewaacha majeruhi Jerry Akaminko, Jeffrey Schlupp na David Accam katika kikosi hicho kinachoelekea Miami kuweka kambi ya maandalizi ya mwisho ambapo kitacheza mechi ya kirafiki juni 9 dhidi ya Korea kusini Akaminko alipata majeruhi jana jumamosi katika kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Uholanzi kwenye mechi ya kirafiki na atafanyiwa upasuaji utakaomfanya akae nje ya uwanja kwa miezi mitatu. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

GHANA YATANGAZA KIKOSI CHAKE KITAKACHOSHIRIKI KOMBE LA DUNIA, GYAN KUONGOZA KIKOSI


414047_heroa 
KOCHA mkuu wa timu ya taifa ya Ghana, Kwesi Appiah ametaja kikosi chake cha mwisho cha wachezaji 23 kwa ajili ya fainali za kombe la dunia zinazoanza kushika kasi mwezi huu nchini Brazil.  
Kikosi hicho cha Appiah kinajumuisha wachezaji 16 wanaokwenda kucheza fainali hizo kwa mara ya kwanza, huku nahodha Asamoah Gyan na Sulley Muntari wakiwa wakongwe wanaokwenda kucheza fainali zao za tatu mfululizo, wakati Jonathan Mensah, Michael Essien, Kwadwo Asamoah, Andre Ayew na Kevin-Prince Boateng wanakwenda kucheza fainali hizo kwa mara ya pili.  
Kocha huyo mwenye miaka 53 amewaacha majeruhi Jerry Akaminko, Jeffrey Schlupp na David Accam katika kikosi hicho kinachoelekea Miami kuweka kambi ya maandalizi ya mwisho ambapo kitacheza mechi ya kirafiki juni 9 dhidi ya Korea kusini Akaminko alipata majeruhi jana jumamosi katika kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Uholanzi kwenye mechi ya kirafiki na atafanyiwa upasuaji utakaomfanya akae nje ya uwanja kwa miezi mitatu. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

TAIFA STARS YALAZIMISHA SARE YA 2 - 2 NA ZIMBABWE KATIKA MECHI YA MARUDIANO

DSC_457511 
Timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imefanikiwa kuvuka hatua ya kwanza ya michuano ya kuwania kucheza michuano ya kombe la mataifa huru ya Afrika linalotarajiwa kufanyika mwakani.
Stars leo ilikuwa inacheza Zimbwabwe kwenye mchezo wa marudiano baada ya kuwafunga Zimbwabwe 1- 0 uwanja wa taifa wiki moja iliyopita, kwenye mchezo huo Stars imefanikiwa kufuzu baada ya kulazimisha sare ya 2-2.
Zimbwabwe walianza kufunga dakika ya 24, kabla ya Stars kusawazisha dakika kadhaa baadae kupitia Nadir Haroub ‘Cannavaro’ dakika ya 28. 
Muda mchache baadae  Thomas Ulimwengu aliongezea Tanzania bao la pili dakika ya 46, kabla ya dakika 10 baadae Zimbwabwe kusawazisha na kufanya matokeo 2-2.
Mpaka refa anapuliza kipenga cha mwisho matokeo yalibaki 2-2, na sasa Tanzania wanaingia hatua ya pili ambapo watacheza na Msumbiji. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

TANZIA: MAMA MZAZI WA MBUNGE ZITTO KABWE AFARIKI DUNIA

http://jambotz8.blogspot.com/ http://jambotz8.blogspot.com/Mama Mzazi wa Zitto enzi za uhai wake.
http://jambotz8.blogspot.com/ 
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGEREZA 12 TANZANIA HAYAFAI KWA MATUMIZI YA BINADAMU...!!!




Mahabusu 


Wakati mamilioni ya fedha za Watanzania yakipotea kila mwaka kutokana na ufisadi na misamaha ya kodi, imebainika kuwa baadhi ya magereza nchini hayafai kutumiwa na wafungwa kutokana na kukosa sifa ukiwemo uchakavu wa majengo.

Ripoti ya utafiti uliofanywa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kwenye magereza na vituo vya polisi 102 katika mikoa 12, inaeleza kuwa magereza 12 hayafai kutumiwa na binadamu.

Hali hiyo inaamanisha kwamba magereza hayo siyo tu ni hatari kwa wafungwa na mahabusu, bali pia kiwa watumishi wa Idara ya Magereza. Ripoti hiyo inaweka bayana kuwa magereza hayo yana hali mbaya kutokana na majengo yake kujengwa miaka mingi iliyopita, huku mengine yakikabiliwa na ukosefu wa mwanga wa kutosha.

Magereza yaliyotajwa kukosa sifa za kutumiwa na binadamu ni Rombo, Nzega, Geita, Ngudu, Kasungamile, Ukerewe, Mugumu, Musoma, Bunda, Ushora, Mang’ola na Bariadi.

“Hali kwenye haya magereza ni kinyume na Kanuni namba 10 ya Umoja wa Mataifa, inayozungumzia namna ya kuwahifadhi wafungwa ambayo inataka sehemu za kulala zikidhi vigezo vya kiafya, hali ya hewa, nafasi ya kutosha, joto na mwanga wa kutosha,” inasema sehemu ya ripoti hiyo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

'JK VUA KOTI LA CCM, VAA LA UARAIS'




Mwenyekiti wa Kongamano la Katiba, Dk Ayub Rioba akizungumza na wajumbe mbalimbali waliohudhuria mdahalo ulioandaliwa na Muungano wa Asasi za Kiraia (Azaki) uliofanyika Dar es Salaaam jana. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa utetezi wa Haki za Binadamu, Onesmo Olengurumwa na Awadhi Ally Saidi aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya kukusanya maoni. Picha na Venance Nestory      

Dar es Salaam/Mwanza. Rais Jakaya Kikwete ameshauriwa kunusuru mchakato wa kupata Katiba Mpya ili usisimame kwa kuvua koti la Uenyekiti wa CCM na kubaki na Urais ili awaeleze wananchi nini cha kufanya kupata Katiba Mpya.
Ushauri huo umetolewa na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na wasomi walioshiriki katika mdahalo wa Katiba uliofanyika jijini Dar es Salaam na Mwanza jana. Walisema kuwa Rais ana wajibu kuunusuru mchakato huo kwa kuwa yeye ndiye aliyeuvuruga kwa hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge Maalumu la Katiba iliyoonekana kuelemea upande wa chama chake CCM.
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa amesema Rais Jakaya Kikwete amekuwa kigeugeu juu ya Muundo wa Serikali za Muungano kama zilizopendekezwa kwenye Rasimu ya Kwanza na ya Pili ya Katiba.
Alisema kuwa Rais Kikwete alionyesha wazi kukubaliana na Muundo wa Serikali tatu, kwani kabla Rasimu ya Pili ya Katiba haijapelekwa kwenye Bunge Malaumu la Katiba ili kujadiliwa, alisaini kuonyesha kuwa amekubaliana na yaliyopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 01, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

NDOTO ZA LUIS MONTES KUCHEZA FAINALI ZA KOMBE LA DUNIA ZAZIMA GHAFLA

Clash: Luis Montes came off worse than Segundo Castillo when the pair went for a 50-50 ball
Agony: It left Montes in severe pain as his team-mates urged the club doctor to come to his attention
 Mchezaji mwenzake akimuita daktari wa timu baada ya Montes kupata majeruhi kubwa
Worried: Montes' Mexican team-mates look on as their midfielder is lifted on to a stretcher
 Wasiwasi: Wachezaji wenzake wakimtazama Montes anapobebwa na machela.
NDOTO za Luis Montes kuichezea Mexico katika fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil zimezima ghafla kufuatia kuvunjika mguu jana usiku kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Ecuador.
Nyota huyo mwenye miaka 28 alishuhudia timu yake ikishinda mabao 3-1 na yeye akifunga bao dakika ya 33, lakini dakika mbili baadaye alipata majeruhi mbaya.
Montes alibebwa na machela kutoka nje ya uwanja baada ya kugongana na mchezaji wa Ecuador,  Segundo Castillo, na kumuacha kocha wake Miguel Herrera akikiri wazi kuwa timu umwombee mchezaji huyo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

AMUUA MKEWE KWA WIVU WA MAPENZI...!!!

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi
Watu wanne wamefariki dunia katika matukio tofauti likiwamo la mwanamke mmoja kudaiwa kuuawa na mume wake kutokana na wivu wa mapenzi.
Katika tukio la kwanza, Mkazi wa Kijiji cha Liwalanje, wilayani Mbozi, Christina Hayola (35) amefariki dunia baada ya kukatwa na kitu chenye ncha kali kifuani na miguuni na mtu anayedaiwa kuwa mume wake.
Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya, Ahmed Msangi alisema uchunguzi wa awali umebaini kwamba chanzo cha mauaji ni wivu wa mapenzi na kwamba polisi wanamsaka mhusika.
Katika tukio la pili, Msangi alisema mkazi wa Isanga jijini hapa, Abdi Sanga aliuawa kwa vipigo baada ya kutuhumiwa kuwa wizi katika eneo la Forest.
Alisema marehemu anadaiwa alikuwa na mwenzake ambaye alitoroka baada ya kuiba vitenge vyenye thamani ya Sh70,000.
Katika tukio la tatu na la nne, alisema mwanafunzi wa Shule ya Msingi Ibumila wilayani Mbarali, Fitina Mwandosya alifariki dunia baada ya kudondoka kutoka kwenye trekta dogo aina ya ‘Powertiller’ alilokuwa amepanda akitoka kuvuna mpunga.
Alisema mwanafunzi huyo alipatwa na mkasa huo juzi wakati wanarudi na wenzake waliokwenda kuvuna mpunga wa shule.
Wakati huohuo mwanafunzi mwingine wa kidato cha pili Sekondari ya Makongorosi, wilayani Chunya, Aden Ngombe(17) amefariki dunia juzi baada ya kugongwa na lori aina ya scania alipokuwa akikatisha barabara.
Msangi alisema polisi walimkamata dereva wa lori na kubainika alikuwa amelewa pombe.
Katika matukio mengine watu wanne wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma mbalimbali zikiwamo za kukutwa na bastola kinyume na sheria.
Kamanda wa polisi alisema aliyekamatwa na bastola ni mkazi wa Kijiji cha Itentula, Mbozi aliyekuwa na bastola aina ya Baby. risasi tatu. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Na Mwananchi

MWANAMKE ALIYEBADILI DINI NA KUPEWA ADHABU YA KIFO APATA UTETEZI

Bi.Meriam Ibrahim na mumewe
Afisa mmoja mwandamizi katika wizara ya maswala ya kigeni nchini Sudan amesema kuwa mwanamke aliyepewa hukumu ya kifo kwa kubadili dini yake ya kiislamu, Meriam Ibrahim atawachiliwa huru katika kipindi cha siku chache zijazo.
Abdullahi Alzareg ambaye ni katibu katika wizara hiyo amesema kuwa Sudan inatilia maanani uhuru wa kuabudu na kwamba serikali itamtetea mwananmke huyo.
Kumekuwa na shutma za kimataifa kuhusu hukumu aliyopewa mwanamke huyo.
Meriam Ibrahim anazuiliwa katika jela moja ambapo alijifungua mtoto wa kike juma hili.
Ameolewa na mkristo na pia amehukumiwa kuchapwa viboko mia moja kwa kuzini kwa sababu mwanamke wa kiislamu kuolewa na mkristo ni haramu kulingana na sheria za Sudan. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Na BBC

Friday, May 30, 2014

WAMILIKI WA MAGARI WATAKIWA KURUDISHA MAGARI YAO KIWANDANI, SOMA HAPA UJUE NI GARI ZA AINA GANI

Kampuni kubwa ya kutengeza magari nchini Marekani imeagiza magari milioni 1.4 yarejeshwe kutokana na hitilafu ya usukani.
Takriban magari milioni 1.1 yaliyoundwa kwa mtindo wa kispoti yaliyokuwa yameuzwa Marekani Kaskazini yametakiwa kurejeshwa kwani huenda yana hitilafu kwenye usukani.
Vilevile magari mengine 200,000 yenye muundo wa Taurus yaliyoundwa kati ya mwaka wa 2010 na 2014 huenda yakakumbwa na tatizo ya kushika kutu kwa haraka.
Matukio kama hayo yaliyofanyika majuzi huenda yakaifanya kampuni hiyo kuvunja rekodi ya kutaka magari mengi zaidi yarejeshwe katika kipindi cha mwaka mmoja.
Urejesho huo umetokea wakati sakata ya usalama inawakumba wapinzani wakuu wa kampuni ya hiyo , General Motors (GM). GM ililaumiwa kwa kutotoa ilani za kiusalama kwamba baadhi ya magari yake hata baada ya kubaini kuwa magari hayo yanazima ghafla.
Dosari hiyo imehusishwa na vifo 13, ingawa wasanifu wa Marekani wanaamini kuwa idadi hiyo itaongezeka.
Pindi tangazo hilo lilipofanywa, kampuni za kutengeneza magari hayo pamoja na wasanifu wa Marekani wameongeza juhudi za kurejesha magari ambayo yanapatikana kuwa na dosari. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 30, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MMILIKI WAMANCHESTER UNITED, MALCOM GLAZER AFARIKI NA KUIACHA TIMU KWA WATOTO WAKE


Mmiliki wa Manchester United, Malcom Glazer amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 85, na kuacha umiliki wa klabu hiyo kwa watoto wake sita.
Familia ya bilionea huyo iliinunua Man United kwa gharama ya Euro 790 milioni Mei, 2005 licha ya pingamizi kali kutoka kwa mashabiki wa klabu hiyo. Hata hivyo, chini ya umiliki wake uliosababisha deni kubwa kwa klabu hiyo ‘’the Red Devils’’ walishinda taji la Ligi Kuu mara tano na Ligi ya Mabingwa 2008.
Watoto wa Mmarekani huyo waliozaliwa Marekani Byan, Joel, na Avram wote wamejumuishwa katika bodi ya klabu hiyo, huku Joel na Avram wakiwa wenyekiti wenza.
Kifo cha Glazer hakitarajiwi kuathiri umiliki wa Man United, kwani familia hiyo bado inamiliki asilimia 90 za hisa za klabu hiyo.
Asilimia 10 inayosalia inamilikiwa na wenye hisa katika soko la hisa la NY stock Exchange. Glazer alikuwa pia mmiliki wa Tampa Bay Buccaneers, iliyobadili sura ya kandanda ya Marekani kwa kushinda taji la Super Bowl. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Bilionea huyo ambaye hakuwahi kukanyaga uwanjani Old Trafford kutokana na hofu ya kuwaudhi mashabiki wa timu hiyo ambao walikuwa wanamsuta kwa kupanga njama ya kuinunua klabu hiyo kwa kutumia madeni.

AUSTRALIA YAWA TIMU YA KWANZA KUWASILI BRAZIL NA REKODI YAKE YA MABAO 31-0

Australia-National-Football-Team-3 Timu ya soka ya Taifa ya Australia, maarufu kama ‘ Soccerrose’ ndiyo timu inayoshikilia rekodi ya kufunga magoli mengi katika mchezo mmoja duniani. Australia waliichapa, American Samoa magoli 31-0, April 11, 2001 katika mchezo wa kimataifa unaotambuli wa na FIFA…Soccerrose, walitua nchini, Brazil siku ya juzi  tayari kwa michuano ya kombe la dunia inayotaraji kuanza kutimua vumbi, juni 12.  Australia ipo katika kundi la pili sambamba na mabingwa watetezi, Hispania, makamu bingwa wa fainali zilizopita, Uholanzi, na Chile.

Kikosi cha kocha, Ange Postecoglou kimeshawahi kucheza michuano hiyo mara tatu na mafanikio yao makubwa ni kufika hatua ya 16 bora, mwaka 2006… Kwa mara ya kwanza, Australia, ilifuzu kwa fainali za mwaka 1974 zilizofanyika nchini Ujerumani na kuondoka patupu. 

Walipata suluhu-tasa dhidi ya Chile, kisha wakapoteza kwa waliokuwa wenyeji wa michuano, Ujerumani Mashariki, na Ujerumani Magharibi na kuondoshwa mashindanoni pasipo kufunga goli lotote. 
Ikiwategemea zaidi wachezaji wake wazoefu kama Tim Cahiil, na nahodha wa kikosi hicho, Michael Jadinak ambaye anakipiga katika kikosi cha Crystal Palece ya England ,kikosi hicho kimekuwa timu ya kwanza kuwasili, Brazil. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

RAIS BANDA "NITAHESHIMU MAAMUZI YA MAHAKAMA KUU"

Rais Joyce Banda wa Malawi akipungia wafuasi wake waliokusanyika huko Lilongwe wakati wa uzinduzi wa kampeni yake. Machi 29, 2014.
Rais Joyce Banda wa Malawi akipungia wafuasi wake waliokusanyika huko Lilongwe wakati wa uzinduzi wa kampeni yake.
Mahakama kuu inapanga Ijumaa kutoa maamuzi kama iwapo matokeo ya uchaguzi yatangazwe hadharani au kura zihesabiwe tena. Matokeo ya awali yamemuweka Bi. Banda nyuma ya mpinzani wake Peter Mutharika.
Bi.Banda anasema uchaguzi ulijaa ubadhirifu, ikiwemo pamoja na wizi wa kura na watu kupiga kura zaidi ya mara moja.
Ameliambia shirika la habari la reuters kwamba atakubali maamuzi ya mahakama kuu, akifahamu fika kuwa amejaribu kutetea haki za wamalawi kwa kuhakikisha kuwa kiongozi anachaguliwa kwa haki na utaratibu wa heshima. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Bi.Banda ameamuru uchaguzi mpya uitishwe katika kipindi cha siku 90 na kusema hatakuwa mgombea. Lakini mahakama kuu imebatilisha maamuzi yake pale chama kikuu cha upinzani kilipowasilisha malalamiko.
CHANZO:VOA

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...