Tuesday, May 13, 2014

TAZAMA VIDEO YA JAY Z AKIPIGWA NA SHEMEJI YAKE MBELE YA MKEWE BEYONCE

Screen Shot 2014-05-12 at 11.40.31 PM 
Ni video kamili ikionyesha kilichotokea kwenye lifti ambapo rapper Jay Z anaonekana akipigwa na shemeji yake ambae ni Solange kwa muda usiopungua dakika 2 kwa kutumia pochi na mateke na baada ya hapo wakatoka nje ya lift.
Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, haya yalitokea wiki iliyopita kwenye After Party ya Met Gala ndani ya Standard Hotel, NYC na ndani ya video inaonesha Jay Z, Beyonce na Solange wakiingia katika Lifti halafu Solange anaanza kumuwakia Jay z kabla ya kuanza kumvamia wakati huo Beyonce akiwa pembeni tu ametulia na wala haingilii.

Bodyguard aliekuemo katika lifti hiyo alianza kumzuia Solange lakini alifanikiwa kuponyoka kama mara tatu hivi na kuendelea kumpiga Jay Z pia kuna muda Solange alirusha teke na Jay Z akazuia lakini hakurudisha kwa aina yeyote ile, sio kwamba alishindwa kumpiga ili alifanya maamuzi ya kuwa mstaarabu tu. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAREKANI KUTAFUTA MATEKA NIGERIA

Marekani kusaidia kuwasaka wasichana waliotekwa na Boko Haram
Marekani imesema inapeleka vifaa vya uchunguzi nchini Nigeria kusaidia katika juhudi za kuwatafuta wasichana wanaozuiliwa na kundi la Boko Haram.
Wasichana hao walitekwa nyara kutoka shule moja Kusini mwa eneo la Borno mwezi mmoja uliopita.
Msemaji wa Rais Obama Jay Carney amesema kikosi cha maafisa 30 kiko nchini Nigeria tayari kushiriki juhudi hizo.
Amesema msaada huo wa Marekani kutoka wizara za mambo ya nje na ulinzi na pia kutoka idara ya uchunguzi ya FBI. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Hatua hiyo imechukuliwa wakati baadhi ya Jamaa za wasichana waliotekwa nyara wakielezea majonzi baada ya kutazama kanda ya video iliyotolewa na kundi hilo.
Marekani kusaidia kuwasaka wasichana waliotekwa na Boko Haram
Baadhi wameiambia BBC kuwa kanda hiyo imewapa matumaini lakini wameshangaa kuona wasichana hao ambao wengi ni Wakristu wamevalia mavazi ya Kiislam.

Akizungumza kwa uchungu nduguye mmoja wa wasicha waliotekwa ameiambia BBC ni heri kanda hiyo ingeonyesha maiti za wasichana hao kwa kuwa hiyo ingeondoa wasiwasi unaoendelea kukithiri na kuumiza mioyo ya wengi.
Kwenye kanda hiyo ya video kiongozi wa Boko Haram , Abubakar Shekau anasikika akiambia serikali ya Nigeria yuko tayari kubadilishana baadhi ya wasichana hao na wafuasi wake waliofungwa jela.
Hatahivyo wizara ya mambo ya ndani ya Nigeria imetupilia mbali pendekezo hilo.
Seneta Ali Ndume kutoka eneo ambapo wasichana hao walitekwa nyara anaisihi serikali kulegeza msimamo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC

MAGAZETI YA LEO JUMANNE MEI 13, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

mg 2
mg 1
13 
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

TAARIFA YA WIZARA YA AFYA KUHUSU UGONJWA WA HOMA YA DENGUE


mg1
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid na Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,Charles Pallangyo.
Utangulizi
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inapenda kutoa taarifa kwa Umma juu ya mwenendo wa ugonjwa wa homa ya dengue yaani “dengue fever” hapa nchini.Ugonjwa huu umethibitishwabaada ya sampuli zilizochukuliwa kutoka kwa watu waliohisiwa kuwa na ugonjwa huu jijini Dar es Salaam kupelekwa kwenye maabara yetu ya Taifa Dar es salaam na kuthibitisha kuwa na virusi vya homa ya dengue mnamo mwishoni mwa mwezi wa Januari 2014. Hadi sasa idadi ya wagonjwa ambao wamethibishwa kuwa na ugonjwa huuni 400 na Vifo 3. Kwa wiki iliyoshia tarehe 9 Mei 2014 ya idadi ya wagonjwa waliogundulika mkoani Dar es salaam ni 60 (42-Kinondoni, 14-Temeke na 4-Ilala) na idadi ya wagonjwa waliopo wodini mpaka sasa ni 13.
Aidha, mlipuko wa ugonjwa huu si mpya hapa nchini kwani uligundulika kwa
mara ya kwanza mnamo Juni 2010 mkoani Dar es Salaam ambapo idadi ya watu 40 walithibitika kuwa na ugonjwa. Pia, kati ya mwezi Mei hadi Julai 2013,wagonjwa 172 walithibitishwa kuugua ugonjwa huu.
Homa ya Dengue
Homa ya dengue ni ugonjwa unaosababishwa na kirusi ambacho kinaenezwa na mbu wa aina ya Aedes.
Dengue in ugonjwa uliosambaa duniani katika nchi za ukanda wa joto. Takribani asilimia 40 ya watu wote duniani wanaishi katika nchi zenye ugonjwa huu. Takwimu za Shirika la Afya Duniani zinathibitisha kuwa takribani matukio milioni 5 ya Dengue yanatolewa taarifa kila mwaka. Watu laki 5 hulazwa hospitali kwa kuathirika na Dengue kali. Homa ya Dengue imeshatokea katika nchi zipatazo 34 barani Afrika.
Hapa Afrika Dengue ni ugonjwa unaojulikana kwa kiwango kidogo sana. Licha ya kwamba milipuko ya kwanza imetokea tangu mwanzoni wa karne ya 19. Matukio ya Ugonjwa huu yameongezeka Afrika tangu miaka ya 1980, matukio mengi yakitokea nchi za ukanda wa Mashariki mwa Afrika ikiwa ni pamoja na Msumbiji, Somalia, Kenya, Komoro, Djibouti na Tanzania. Ikumbukwe kuwa jina “Dengue” linatokana na neno “Dinga” la kiswahili linalolomaanisha ugonjwa unaotakana na pepo yaani Kudinga pepo. Mabaharia wa Kispanish walipokuja kwenye pwani ya Afrika Mashariki walirudi kwao na kuuita “Dengue”.

MCHWA WAVAMIA IKULU...!!!

Mchwa wavamia ikulu ya Paraguay
Mchwa wamevamia makaazi rasmi ya rais wa Paraguay na kutishia udhabiti wa jengo hilo.
Watalamu wa maswala ya ujenzi wameonya kwamba huenda Rais huyo akapoteza makaazi yake iwapo hatua za dharura hazitachukuliwa kuwaangamiza mchwa.
Kwa mujibu wa wanasayasi wa kibiolojia mchwa ni mdudu mwenye bidii sana na kamwe hachoki kutekeleza majukumu yake.
Na ni kutokana na hilo ndipo wahenga katika juhudi za kutoa motisha kwa yeyote yule anayetaka kufanikiwa maishani wakasema ''lazima awe na bidii ya mchwa''.
Msemo huu umedhihirika nchini Paraguay baada ya habari kwamba mchwa wamevamia makaazi rasmi ya Rais Horacio Cartes.
Wataalam wa maswala ya ujenzi wanasema mchwa hao wameharibu sakafu na sehemu zilizojengwa kwa mbao.
Wahandisi hao wameonya kuwa huenda sehemu moja ya jengo hilo likaanguka iwapo hatua za haraka hazitachukuliwa.
Wamependekeza Rais huyo ahamishwe kutoka jengo hilo ili wataalam waweze kupambana na wadudu hao wenye bidii na ukarabati uweze kufanyiwa jengo hilo.
Ni dhahiri kuwa wageni hao waharibifu sasa wanatishia starehe na itifaki ya Rais Horacio Cartes. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC

Friday, May 09, 2014

JAQUELINE WOLPER AFUNGUKA KUHUSU KUBADILI DINI, KUCHANA, USAGAJI

Screen Shot 2014-05-09 at 7.02.35 AM 
Ni longtime mwigizaji Mtanzania Jaqueline Wolper amekua kimya na hajasikika akiyatoa ya moyoni kuhusu yote yaliyompata kwenye miezi iliyopita na kumfanya amiliki sana headlines za magazeti, blogs, website pia facebook na twitter huku wengi wakiwa na hamu ya kusikia akiyaongelea.
Kwenye Exclusive interview na mtangazaji Sporah wa The Sporah show, Jaq amekanusha kwamba yeye ni msagaji japo mara kadhaa ameonekana akivaa kiume na kusisitiza ‘sasa hivi nimepunguza sana kuvaa nguo za kiume, wengi walikua wanahisi lakini sijawahi kufanya vitendo vya usagaji na wala sijawahi kushawishiwa na mtu anaejihusisha na vitendo hivyo, boyfriend wangu hana tatizo na mavazi ya kiume ninayovaa… hatujawahi kupangiana mavazi’
Kwenye jibu jingine alilotoa J anasema ‘sijaolewa na wala sijawahi kuolewa, nilishawahi kubadili dini kweli… ni vitu vinatokea na usimuhukumu mtu bila kumuuliza’
Sporah: Ni kweli kwamba ulikutana na mtu ana uwezo wa kifedha na kulikua kuna vitu unataka akununulie akasema hawezi kukufanyia mpaka ubadilishe dini ili upate hizo mali?
J Wolper: ‘Sio hivyo, dini nilikuja kubadilisha wakati nimeshapata mali, nilibadilisha mwishoni kabisa baada ya huyu mwanaume kuja kwetu akitaka kunioa, alinipa mali na vitu vya thamani kabla ya sisi kukutana, unajua unaweza ukawa unachat na mtu mkapendana lakini hamjawahi kukutana… ni mzuri wa kukushawishi, unajua sio rahisi mtu akiwa mbali aweze kukushawishi mkapendana wakati yeye yuko mbali na wewe uko mbali, namsifia kwa uzuri wake… sio wa umbo wala sura bali ana roho nzuri na alinitreat vizuri mpaka nikaona huyu ni sahihi nikabadilisha dini’
Screen Shot 2014-05-09 at 4.43.46 AM 
Sporah:     Ulifikiria kwamba dini yako sio nzuri au?

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 09, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

RAY C AFUNGUKA KUHUSU KUNUSURIKA KIFO KWA GONJWA HATARI LA DENGUE...!!!

http://jambotz8.blogspot.com/
Staa wa muziki wa Kizazi Kipya Bongo, Rehema Chalamila ‘Ray C’.
MUNGU mkubwa! Staa wa muziki wa Kizazi Kipya Bongo, Rehema Chalamila ‘Ray C’, amesimulia jinsi alivyochungulia kifo baada ya kutikiswa na ugonjwa hatari na tishio ulioibuka hivi karibuni wa Homa ya DengueAkifunguka mbele ya gazeti hili juzi baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini Mwananyamala, Dar alikokuwa amelazwa, Ray C au Kiuno Bila Mfupa alisema kwamba kwenye maisha yake hajawahi kushikwa na ugonjwa wenye mateso makali, tena ya muda mfupi kama ilivyokuwa juzikati alipopata ugonjwa huo.

http://jambotz8.blogspot.com/Alisema kwamba dakika chache tu baada ya kuamka kitandani alikuwa akijisikia kichwa kikiuma kama kinataka kuchomoka ambapo bila kuremba aliwasha gari lake na kukimbilia Hospitali ya Mwananyamala.Staa huyo wa Ngoma ya Na Wewe Milele alisema alipofika kwa kudra za muumba alilazwa tayari kwa kutundikwa dripu. “Huwezi kuamini baada ya madaktari kunipima na kugundua nina Ugonjwa wa Dengue, walinishangaa sana hata namna nilipofika pale na kwamba sikutumia dawa yoyote ya kutuliza maumivu kwa sababu maumivu yake huwa ni lazima utatafuta tu dawa ya kukufanya upoze maumivu. 
“Madaktari wengine wakatishika zaidi maana walisema kama ukimeza vidonge vya ‘Diclopa’ unaweza kupoteza maisha mara moja. 
“Katika magonjwa ya ajabu na yanayostahili kutafutiwa kinga mara moja basi huu ni ugonjwa wa kwanza ambao serikali inatakiwa iwe macho sana maana haufai hata kidogo.
“Tena unatisha sana na wasipoangalia utapoteza maisha ya Watanzania kibao kama hawatautafutia kinga au kuwapa Watanzania elimu ya kutosha.“Mateso niliyoyapata kwa siku mbili nilizolazwa Mwananyamala ni elimu tosha kabisa na kwamba ningekuwa na uwezo wa kuzunguka au kupata nafasi ya kuongea na wakuu wa nchi basi mara moja ningewaomba wafanye jitihada za haraka kuhakikisha wanapata chanjo kwa ajili ya kuudhibiti mfumko wa gonjwa hilo.
“Dengue unaambukizwa na mbu tena wa mchana na dawa yake ni panadol tu!” alimalizia Ray 
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAREKANI 'INAIFUNGIA MLANGO' SYRIA

Viongozi wa upinzani wa serikali ya Syria wapo Washington Marekani kwa mashauriano
Marekani imeiwekea vikwazo benki moja ya Urusi inayofanya biashara na Syria kama sehemu ya jitihada za kuzidisha shinikizo za kiuchumi dhidi ya serikali ya Syria.
Hatua hiyo ilitangazwa wakati viongozi wa upinzani walioitembelea Washington wameanza kukutana na maafisa wakuu wa utawala.

Hii ni mara ya kwanza Marekani imeiwekea vikwazo benki ya Urussi inayofanya biashara na Syria.
Maafisa wa hazina ya Marekani wanasema hatua hii inanuiwa kuifungia milango Syria isiweze kuendelea kupenya mfumo wa kifedha wa dunia.
Vikwazo zaidi pia vimewekewa viwanda kadhaa vya kusafisha mafuta pamoja na maafisa sita wa ngazi ya juu katia serikali ya Syria.
Hayo yalitangazwa mda mfupi tu kabla ya kiongozi wa upinzani wa serikali ya Syria Ahmad Jarba alipokutana na waziri wa mambo ya nje wa wa Marekani John Kerry.
Ahmad Jarba yuko katika ziara ya kwanza rasmi huko Marekani ambako anatarajiwa pia kukutana na rais wa Marekani Barack Obama. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo BBC

Wednesday, May 07, 2014

KIKOSI CHA MAREKANI KUSAIDIA NIGERIA

Rais Barack Obama wa Marekani aliyeamuru msaada wa kijeshi na vifaa kuwatafuta wasichana Nigeria.
Marekani imetangaza kwamba imetuma kikosi cha wataalamu nchini Nigeria kusaidia kuwatafuta wasichana takriban 200 wa shule waliotekwa nyara mwezi uliopita na wapiganaji wa kundi la Boko Haram.
Rais Barack Obama ameshutumu utekaji nyara wa wasichana hao na kusema kuwa mataifa yanapaswa kufanya kazi kwa pamoja ili kulikomesha Boko Haram.
"Tayari tumetuma kundi letu Nigeria. Wamekubali msaada wetu ambao unashirikisha wanajeshi, wadumishaji wa sheria na mashirika mengine ambao wanajaribu kutambua waliko wasichana hawa ili wawape msaada," Rais Obama alisema.
Rais Obama amesema kuwa jamii ya kimataifa inapaswa kutumia utekeji wa kikatili wa wasichana hao kama msingi wa kuungana na kuangamiza Boko Haram.
Nchini Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan amekubali msaada huo kama alivyosema msemaji wake, Daktari Reuben Abati.
"msaada huo kutoka kwa Rais Obama uliwasilishwa na Waziri wa Mashauri ya Kigeni John Kerry kama saa tisa alasiri hivi," Daktari Abati alisema. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo BBC

MAHABUSU ARUSHA WAVUA NGUO KUPINGA UBAGUZI


Ramani ya Tanzania
Mahabusu wa Gereza Kuu la Mkoa wa Arusha, jana walisababisha vurugu katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi mjini humo baada ya kuvua nguo na kugoma kushuka kwenye basi lililowachukua kwenda mahakamani wakipinga kitendo cha watuhumiwa wawili wa dawa za kulevya kuachiwa huru.
Watuhumiwa wanaolalamikiwa ambao mashtaka yao yalibadilishwa mara mbili ili wapewe dhamana ni Dharam Patel na Nivan Patel wanaodaiwa kukamatwa na kete 173 za heroini na misokoto 300 ya bangi, Aprili,2014.
Kwa mujibu wa watu waliokuwa katika eneo la mahakama hayo, mahabusu hao walikuwa wakipaza sauti kupinga madaraja(ubaguzi) miongoni mwa watuhumiwa, wenye uwezo kifedha na wasio nacho, hali ambayo imesababisha wengine kuachiwa na wengine kuendelea kusota magerezani kwa kisingizio cha "upelelezi haujakamilika"
Mahabusu hao walisikika wakipaza sauti kutoka ndani ya basi: "Wenzetu hata mwezi haujaisha wanafutiwa kesi, jamani sisi tumekosa nini? Tunataka haki itendeke kwa wote" walisema.
Kuachiwa kwa watuhumiwa wanaolalamikiwa na mahabusu wenzao kunasemekana kumetokana na hatua ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Arusha kubadilisha hati ya mashitaka na hivyo kuwawezesha kupata dhamana.
Kamanda wa Kikosi cha Polisi cha Kuzuia Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa ameliambia gazeti la Mwananchi kuwa ofisi yake haina taarifa za watuhumiwa hao kupewa dhamana lakini alisema kulikuwa na jaribio la kufanya hivyo.
Bwana Nzowa amesema baada ya kubainika njama hizo, ofisi yake ilipinga, akisema kuwa kosa la watuhumiwa lilikuwa wazi na hivyo kuonyesha hali ya kutoamini kuwa watuhumiwa wanaweza kupata dhamana kwa kosa hilo!
Hata hivyo Ofisi ya Mwendesha Mashitaka, DPP haijaweza kulitolea maelezo suala la mahabusu hao kulalamikia mahabusu wenzao kupendelewa katika utoaji wa haki kwa makosa wanayotuhumiwa.
Chanzo BBC 
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Monday, May 05, 2014

LUIS SUAREZ KAFNYA YAKE TENA

Screen Shot 2014-05-05 at 3.48.52 PM 
Wiki mbili baada ya kutangazwa kuwa mchezaji bora wa ligi kuu ya England kupitia chama cha wanasoka wanaocheza EPL mshambuliaji wa kimataifa wa Uruguay Luis Suarez ambae ni miongoni mwa mastaa wa soka waliowahi kumiliki headlines kwa kipindi kirefu, amechaguliwa tena kuwa mwanasoka bora wa England na chama cha waandishi wa habari za michezo Uingereza.
Suarez mwenye umri wa miaka 27 aliwashinda kwa kura nyingi wachezaji wengine akiwemo nahodha wa Liverpool na England Steven Gerrard.
article-2620532-1D69BE9B00000578-539_306x423 
Magoli 30 aliyofunga msimu huu kwenye EPL yameiweka Liverpool kwenye nafasi ya kutwaa ubingwa wa Premier League baada ya miaka 24.  Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Hii ndio listi ya washindi wa tuzo hiyo tangu mwaka 1990 mpaka leo
1989–90     John Barnes          
1990–91     Gordon Strachan
1991–92     Gary Lineker
1992–93     Chris Waddle
1993–94     Alan Shearer
1994–95     Jurgen Klinsmann
1995–96     Eric Cantona
1996–97     Gianfranco Zola
1997–98     Dennis Bergkamp
1998–99     David Ginola
1999–00     Roy Keane
2000–01     Teddy Sheringham
2001–02     Robert Pires
2002–03     Thierry Henry
2003–04     Thierry Henry
2004–05     Frank Lampard
2005–06     Thierry Henry
2006–07     Cristiano Ronaldo
2007–08     Cristiano Ronaldo
2008–09     Steven Gerrard
2009–10     Wayne Rooney
2010–11     Scott Parker
2011–12     Robin van Persie
2012–13     Gareth Bale

MAGAZETI YA LEO JUMATATU MEI 05, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAPIGANO MAKALI YAANZA TENA SUDAN KUSINI

Wanajeshi wa Sudan Kusini
Mapigano makali yamekuwa yakiendelea katika mji wa Bentiu nchini Sudan Kusini ambapo vikosi vya serikali vinajaribu kuurejesha mji huo uliotekwa na waasi.
Mwandishi wa Habari wa BBC aliyeandamana na kikosi cha Umoja wa Mataifa nje ya mji huo anasema amesikia milio ya bunduki na silaha nzito nzito ambapo pia ameona kikosi cha majeshi ya serikali kikijipanga.
Hata hivyo amesema bado haijajulikana ni kundi gani kwa sasa linaloshikilia mji huo wa wenye utajiri wa mafuta.
Kwa upande serikali nchini Sudan kusini inasema majeshi yake yameudhibiti mji wa huo na ngome ya waasi ya Nasir.
Baadhi ya wakimbizi wa Sudan Kusini waliokimbia makazi yao hivi karibuni kutokana na vita
Mjumbe wa Umoja wa mataifa mjini humo anasema mji huo umedhibitiwa upya na kikosi cha serikali katika operesheni kubwa iliyoanza hapo jana Jumapili.
Shambulio hilo linajiri siku mbili baada ya rais Salva Kiir kumwambia Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani John Kerry, kwamba yupo tayari kufanya mazungumzo ya amani ya moja kwa moja na kiongozi wa waasi, Riek Machar. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo BBC

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...