Friday, May 09, 2014

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 09, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

RAY C AFUNGUKA KUHUSU KUNUSURIKA KIFO KWA GONJWA HATARI LA DENGUE...!!!

http://jambotz8.blogspot.com/
Staa wa muziki wa Kizazi Kipya Bongo, Rehema Chalamila ‘Ray C’.
MUNGU mkubwa! Staa wa muziki wa Kizazi Kipya Bongo, Rehema Chalamila ‘Ray C’, amesimulia jinsi alivyochungulia kifo baada ya kutikiswa na ugonjwa hatari na tishio ulioibuka hivi karibuni wa Homa ya DengueAkifunguka mbele ya gazeti hili juzi baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini Mwananyamala, Dar alikokuwa amelazwa, Ray C au Kiuno Bila Mfupa alisema kwamba kwenye maisha yake hajawahi kushikwa na ugonjwa wenye mateso makali, tena ya muda mfupi kama ilivyokuwa juzikati alipopata ugonjwa huo.

http://jambotz8.blogspot.com/Alisema kwamba dakika chache tu baada ya kuamka kitandani alikuwa akijisikia kichwa kikiuma kama kinataka kuchomoka ambapo bila kuremba aliwasha gari lake na kukimbilia Hospitali ya Mwananyamala.Staa huyo wa Ngoma ya Na Wewe Milele alisema alipofika kwa kudra za muumba alilazwa tayari kwa kutundikwa dripu. “Huwezi kuamini baada ya madaktari kunipima na kugundua nina Ugonjwa wa Dengue, walinishangaa sana hata namna nilipofika pale na kwamba sikutumia dawa yoyote ya kutuliza maumivu kwa sababu maumivu yake huwa ni lazima utatafuta tu dawa ya kukufanya upoze maumivu. 
“Madaktari wengine wakatishika zaidi maana walisema kama ukimeza vidonge vya ‘Diclopa’ unaweza kupoteza maisha mara moja. 
“Katika magonjwa ya ajabu na yanayostahili kutafutiwa kinga mara moja basi huu ni ugonjwa wa kwanza ambao serikali inatakiwa iwe macho sana maana haufai hata kidogo.
“Tena unatisha sana na wasipoangalia utapoteza maisha ya Watanzania kibao kama hawatautafutia kinga au kuwapa Watanzania elimu ya kutosha.“Mateso niliyoyapata kwa siku mbili nilizolazwa Mwananyamala ni elimu tosha kabisa na kwamba ningekuwa na uwezo wa kuzunguka au kupata nafasi ya kuongea na wakuu wa nchi basi mara moja ningewaomba wafanye jitihada za haraka kuhakikisha wanapata chanjo kwa ajili ya kuudhibiti mfumko wa gonjwa hilo.
“Dengue unaambukizwa na mbu tena wa mchana na dawa yake ni panadol tu!” alimalizia Ray 
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAREKANI 'INAIFUNGIA MLANGO' SYRIA

Viongozi wa upinzani wa serikali ya Syria wapo Washington Marekani kwa mashauriano
Marekani imeiwekea vikwazo benki moja ya Urusi inayofanya biashara na Syria kama sehemu ya jitihada za kuzidisha shinikizo za kiuchumi dhidi ya serikali ya Syria.
Hatua hiyo ilitangazwa wakati viongozi wa upinzani walioitembelea Washington wameanza kukutana na maafisa wakuu wa utawala.

Hii ni mara ya kwanza Marekani imeiwekea vikwazo benki ya Urussi inayofanya biashara na Syria.
Maafisa wa hazina ya Marekani wanasema hatua hii inanuiwa kuifungia milango Syria isiweze kuendelea kupenya mfumo wa kifedha wa dunia.
Vikwazo zaidi pia vimewekewa viwanda kadhaa vya kusafisha mafuta pamoja na maafisa sita wa ngazi ya juu katia serikali ya Syria.
Hayo yalitangazwa mda mfupi tu kabla ya kiongozi wa upinzani wa serikali ya Syria Ahmad Jarba alipokutana na waziri wa mambo ya nje wa wa Marekani John Kerry.
Ahmad Jarba yuko katika ziara ya kwanza rasmi huko Marekani ambako anatarajiwa pia kukutana na rais wa Marekani Barack Obama. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo BBC

Wednesday, May 07, 2014

KIKOSI CHA MAREKANI KUSAIDIA NIGERIA

Rais Barack Obama wa Marekani aliyeamuru msaada wa kijeshi na vifaa kuwatafuta wasichana Nigeria.
Marekani imetangaza kwamba imetuma kikosi cha wataalamu nchini Nigeria kusaidia kuwatafuta wasichana takriban 200 wa shule waliotekwa nyara mwezi uliopita na wapiganaji wa kundi la Boko Haram.
Rais Barack Obama ameshutumu utekaji nyara wa wasichana hao na kusema kuwa mataifa yanapaswa kufanya kazi kwa pamoja ili kulikomesha Boko Haram.
"Tayari tumetuma kundi letu Nigeria. Wamekubali msaada wetu ambao unashirikisha wanajeshi, wadumishaji wa sheria na mashirika mengine ambao wanajaribu kutambua waliko wasichana hawa ili wawape msaada," Rais Obama alisema.
Rais Obama amesema kuwa jamii ya kimataifa inapaswa kutumia utekeji wa kikatili wa wasichana hao kama msingi wa kuungana na kuangamiza Boko Haram.
Nchini Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan amekubali msaada huo kama alivyosema msemaji wake, Daktari Reuben Abati.
"msaada huo kutoka kwa Rais Obama uliwasilishwa na Waziri wa Mashauri ya Kigeni John Kerry kama saa tisa alasiri hivi," Daktari Abati alisema. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo BBC

MAHABUSU ARUSHA WAVUA NGUO KUPINGA UBAGUZI


Ramani ya Tanzania
Mahabusu wa Gereza Kuu la Mkoa wa Arusha, jana walisababisha vurugu katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi mjini humo baada ya kuvua nguo na kugoma kushuka kwenye basi lililowachukua kwenda mahakamani wakipinga kitendo cha watuhumiwa wawili wa dawa za kulevya kuachiwa huru.
Watuhumiwa wanaolalamikiwa ambao mashtaka yao yalibadilishwa mara mbili ili wapewe dhamana ni Dharam Patel na Nivan Patel wanaodaiwa kukamatwa na kete 173 za heroini na misokoto 300 ya bangi, Aprili,2014.
Kwa mujibu wa watu waliokuwa katika eneo la mahakama hayo, mahabusu hao walikuwa wakipaza sauti kupinga madaraja(ubaguzi) miongoni mwa watuhumiwa, wenye uwezo kifedha na wasio nacho, hali ambayo imesababisha wengine kuachiwa na wengine kuendelea kusota magerezani kwa kisingizio cha "upelelezi haujakamilika"
Mahabusu hao walisikika wakipaza sauti kutoka ndani ya basi: "Wenzetu hata mwezi haujaisha wanafutiwa kesi, jamani sisi tumekosa nini? Tunataka haki itendeke kwa wote" walisema.
Kuachiwa kwa watuhumiwa wanaolalamikiwa na mahabusu wenzao kunasemekana kumetokana na hatua ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Arusha kubadilisha hati ya mashitaka na hivyo kuwawezesha kupata dhamana.
Kamanda wa Kikosi cha Polisi cha Kuzuia Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa ameliambia gazeti la Mwananchi kuwa ofisi yake haina taarifa za watuhumiwa hao kupewa dhamana lakini alisema kulikuwa na jaribio la kufanya hivyo.
Bwana Nzowa amesema baada ya kubainika njama hizo, ofisi yake ilipinga, akisema kuwa kosa la watuhumiwa lilikuwa wazi na hivyo kuonyesha hali ya kutoamini kuwa watuhumiwa wanaweza kupata dhamana kwa kosa hilo!
Hata hivyo Ofisi ya Mwendesha Mashitaka, DPP haijaweza kulitolea maelezo suala la mahabusu hao kulalamikia mahabusu wenzao kupendelewa katika utoaji wa haki kwa makosa wanayotuhumiwa.
Chanzo BBC 
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Monday, May 05, 2014

LUIS SUAREZ KAFNYA YAKE TENA

Screen Shot 2014-05-05 at 3.48.52 PM 
Wiki mbili baada ya kutangazwa kuwa mchezaji bora wa ligi kuu ya England kupitia chama cha wanasoka wanaocheza EPL mshambuliaji wa kimataifa wa Uruguay Luis Suarez ambae ni miongoni mwa mastaa wa soka waliowahi kumiliki headlines kwa kipindi kirefu, amechaguliwa tena kuwa mwanasoka bora wa England na chama cha waandishi wa habari za michezo Uingereza.
Suarez mwenye umri wa miaka 27 aliwashinda kwa kura nyingi wachezaji wengine akiwemo nahodha wa Liverpool na England Steven Gerrard.
article-2620532-1D69BE9B00000578-539_306x423 
Magoli 30 aliyofunga msimu huu kwenye EPL yameiweka Liverpool kwenye nafasi ya kutwaa ubingwa wa Premier League baada ya miaka 24.  Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Hii ndio listi ya washindi wa tuzo hiyo tangu mwaka 1990 mpaka leo
1989–90     John Barnes          
1990–91     Gordon Strachan
1991–92     Gary Lineker
1992–93     Chris Waddle
1993–94     Alan Shearer
1994–95     Jurgen Klinsmann
1995–96     Eric Cantona
1996–97     Gianfranco Zola
1997–98     Dennis Bergkamp
1998–99     David Ginola
1999–00     Roy Keane
2000–01     Teddy Sheringham
2001–02     Robert Pires
2002–03     Thierry Henry
2003–04     Thierry Henry
2004–05     Frank Lampard
2005–06     Thierry Henry
2006–07     Cristiano Ronaldo
2007–08     Cristiano Ronaldo
2008–09     Steven Gerrard
2009–10     Wayne Rooney
2010–11     Scott Parker
2011–12     Robin van Persie
2012–13     Gareth Bale

MAGAZETI YA LEO JUMATATU MEI 05, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAPIGANO MAKALI YAANZA TENA SUDAN KUSINI

Wanajeshi wa Sudan Kusini
Mapigano makali yamekuwa yakiendelea katika mji wa Bentiu nchini Sudan Kusini ambapo vikosi vya serikali vinajaribu kuurejesha mji huo uliotekwa na waasi.
Mwandishi wa Habari wa BBC aliyeandamana na kikosi cha Umoja wa Mataifa nje ya mji huo anasema amesikia milio ya bunduki na silaha nzito nzito ambapo pia ameona kikosi cha majeshi ya serikali kikijipanga.
Hata hivyo amesema bado haijajulikana ni kundi gani kwa sasa linaloshikilia mji huo wa wenye utajiri wa mafuta.
Kwa upande serikali nchini Sudan kusini inasema majeshi yake yameudhibiti mji wa huo na ngome ya waasi ya Nasir.
Baadhi ya wakimbizi wa Sudan Kusini waliokimbia makazi yao hivi karibuni kutokana na vita
Mjumbe wa Umoja wa mataifa mjini humo anasema mji huo umedhibitiwa upya na kikosi cha serikali katika operesheni kubwa iliyoanza hapo jana Jumapili.
Shambulio hilo linajiri siku mbili baada ya rais Salva Kiir kumwambia Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani John Kerry, kwamba yupo tayari kufanya mazungumzo ya amani ya moja kwa moja na kiongozi wa waasi, Riek Machar. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo BBC

HUKUMU YA WANAJESHI WABAKAJI DRC LEO

Wanajeshi wa serikali ya DRC
Hukumu inatarajiwa kutolewa baadaye leo kwenye kesi inayowahusu wanajeshi 39 wanaotuhumiwa kuendesha ubakaji na uhalifu wa kivita nchini Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo.
Wanajeshi hao wanatuhumiwa kusababisha machafuko yanayoendelea kwenye mji mdogo wa Minova ulio mashariki mwa nchi hiyo mwaka 2012.
Waasi wa M23 ambao wanadaiwa nao kujihusisha na vitendo vya ubakaji
Wakati wa machafuko hayo maelfu ya wajeshi wa serikali walikuwa wakirudi nyuma baada ya kupoteza mji wa Goma kwa waasi wa M23 .
Ripoti ya Umoja wa Mataifa inasema kuwa wanajeshi hao waliwabaka karibu wanawake na wasichana 135.
Matukio ya ubakaji yameenea katika eneo la mashariki mwa Congo na yanaidiwa kufanywa na askari wa pande zote mbili waasi na wale serikali. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Sunday, May 04, 2014

DIAMOND AIBUKA KIDEDEA KWA KUNYAKUA TUZO SABA (7) ZA KTMA 2014

Msanii wa kizazi kipya, Nasib Abdul a.k.a Diamond Platinumz leo May 3, 2014 amedhihirisha kuwa yeye ni msanii mkali kwa kuchukua tuzo saba katika Tuzo za Kilimanjaro 2014 (KTMA).
Diamond amejinyakulia tuzo:
Msanii Bora wa Kiume,
Video Bora ya Mwaka.
Mtumbuizaji bora wa Muziki wa Kiume.
Wimbo Bora wa Afro Pop.
Wimbo Bora wa Mwaka.
Mtunzi Bora wa mwaka Kizazi Kipya.
Wimbo Bora wa Kushirikisha/Kushirikiana.
Hakika Diamond ameonyesha ukali wake, na kuonyesha kuwa yeye ni bora zaidi na anapendwa na watu.  Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

TAZAMA PICHA 40 ZA MATUKIO YALIYOJILI KWENYE TUZO ZA KTMA 2014 USIKU WA KUAMKIA LEO, DIAMOND AVUNJA REKODI

Wanamuziki Ommy Dimpoz na Vanessa Mdee wakifanya vitu vyao stejini. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

BOMU LAUA WATU WATATU MOMBASA

Moja kati ya milipuko iliyowahi kutokea Mombasa
Watu watatu wanaripotiwa kuuawa katika mlipuko uliotokea katika mji wa Mombasa nchini Kenya.
Kwa mujibu wa taarifa bomu la mkono lilitupwa kwenye basi katika kituo cha mabasi cha Mwembe Tayari ambao hupendwa kutembelewa na watalii na kusababisha vifo hivyo na wengine kujeruhiwa.
Mlipuko mwingine umetokea katika mtaa wa kifahari wa Nyali.
Kamishna mkuu wa polisi Mombasa, Nelson Marwa, amesema watu 6 wamejeruhiwa na kuwa watu waliotekeleza shambulizi hilo walitoroka kwa Pikipiki.
Kenya imekuwa ikikumbwa na matukio ya mashambulio yanayodaiwa kutekelezwa na kundi la kiislamu la Alshabaab la nchini Somalia.
Aidha nchi hiyo imekuwa katika tahadhari tangu mwezi Septemba mwaka jana ambapo wanamgambo wa Alshabaab walivamia kituo cha biashara cha Westgate kilichopo mji mkuu wa Nairobi na kuua watu wapatao 67.
Al Shabaab ni kundi ambalo lina uhusiano na kundi la kigaidi la Al Qaeda ambalo limeapa kulipiza kisasi kufuatia Kenya kutuma majeshi yake nchini Somalia mwaka 2011ambayo yameungana na yale ya Umoja wa Afrika AMISOM. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo BBC

WATU 2000 WAFUKIWA KWA UDONGO AFGHANISTAN


Juhudi za uokoji zinaendelea siku ya pili Kaskazini mashariki mwa Afghanistan ambapo watu wapatao elfu mbili wanasadikiwa kufa kutokana na maporomoko ya ardhi katika maeneo ya vijiji kwenye mkoa wa Badakhshan.
Vijiji hivyo vimefunikwa na udongo wenye ukubwa wa karibu mita kumi kwenda juu baada ya sehem ya mlima mmoja kuporomoja kutokana na mvua kubwa zinazonyesha. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MEI 04, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...