Saturday, May 03, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MEI 03, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

POLISI NIGERIA WAOMBA PICHA ZA WANAFUNZI


Waandamanaji nchini Nigeria wakidai wasichana waliotekwa katika mji wa Chibok, Borno warejeshwe
Polisi nchini Nigeria wamewataka wazazi wa wanafunzi wasichana zaidi ya 200 waliotekwa kuwasilisha picha za mabinti hao.
Wasichana hao walichukuliwa na watu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Kiislam kutoka shuleni kwao katika jimbo la Borno zaidi ya wiki mbili zilizopita.
Polisi wa jimbo la Borno wameiambia BBC kuwa serikali inataka kuthibitisha bayana ni nani ambaye ametoweka kwa sababu vitabu vya kumbukumbu vya shule vilichomwa moto katika shambulio hilo.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

WATU 30 WAFA KWA MOTO VITANI UKRAINE


Majeshi ya Ukraine pamoja na vifaru kuelekea kwenye mapambano
Polisi wa Ukraine wanasema kuwa zaidi watu 30 wameuawa katika moto ulioanza baada ya makabiliano kati ya vikosi vya wanamgambo wanaounga mkono Urusi na wafuasi wa serikali katika mji wa kusini magharibi wa Odessa.
Haijulikani ni nini kilichosababisha moto huo katika jengo la chama cha wafanyikazi ,huku ripoti zikiarifu kwamba pande zote mbili zilikuwa zikitumia mabomu ya petroli.
"Waziri wa mpito wa Mambo ya Ndani nchini Ukraine Arsen Avakov amesema kuwa harakati za serikali kudhibiti mji wa mashariki wa Sloviansk uliopo mashriki mwa Ukraine zinaendelea na kwamba vikosi vyake vimeliteka jengo la Televisheni karibu na Kromartosk.Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Friday, May 02, 2014

JK: MISHAHARA ITAPANDA NA KUPUNGUZWA KODI


Rais Jakaya Kikwete akiangua kicheko wakati walimu (juu), walipokuwa wakipita kwa maandamano, huku wakiimba ‘Shemeji mshahara bado’ wakati wa sherehe za Siku ya Wafanyakazi (Mei Mosi) zilizofanyika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam jana. Walimu walimwita shemeji kwa kuwa mkewe, Salma ni mwalimu kitaaluma. Picha na Silvan Kiwale. 
Dar/mikoani. Rais Jakaya Kikwete ametoa ahadi mbili za kuwafurahisha wafanyakazi. Kwanza ametangaza nia ya kuongeza mishahara yao na pili, kupunguza kodi inayokatwa kwenye mishahara hiyo mambo ambayo ameahidi kutekelezwa katika Bajeti ya mwaka 2014/2015 inayotarajiwa kuwasilishwa bungeni hivi karibuni.
Akizungumza kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi (Mei Mosi), yaliyofanyika kitaifa Dar es Salaam jana, Rais Kikwete alisema anatambua kuwa wafanyakazi wana hamu ya kujua Serikali itasema nini kuhusu masilahi yao.
Alisema malalamiko ya wafanyakazi wengi ni kutaka kuona kima cha chini cha mshahara kinaongezwa huku kodi kwenye mishahara (Paye), ikipungua.
“Mimi na wenzangu serikalini hatuna upungufu wa dhamira ya kufanya hivyo, tumethibitisha miaka iliyopita na tutaendelea kuwa hivyo,” alisema. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Huku akishangiliwa na wafanyakazi waliofurika katika Uwanja wa Uhuru, Rais Kikwete alisema: “Najua kuwa nyongeza tuliyotoa mwaka jana si kubwa kama wafanyakazi walivyotaka iwe... hata mimi nisingependa iwe hivyo.”

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...