Saturday, February 15, 2014

MBEYA CITY YATOKA SARE NA SIMBA, YANGA YAINYUKA TENA KOMOROZINE

goal 
Mchezo uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu baina ya vilabu vya Simba na Mbeya City uliokuwa unachezwa leo huko jijini Mbeya katika dimba la Sokoine umemalizika.
Matokeo ya mchezo huo ni sare ya bao moja kwa moja, Mbeya City ndio walioanza kuliona lango la Simba katika dakika ya 17 kwa mkwaju wa penati, bao hilo lilidumu mpaka mapumziko wenyeji wakitoka kifua mbele.
simba-mpya-2 
Kipindi cha pili Simba walianza kwa kasi na hatimaye katika dakika ya 50, mshambuliaji hatari wa Simba Mrundi Amiss Tambwe akaifungia timu yake bao la kusawazisha.
Timu hizo ziliendelea kushambuliana lakini mpaka refa anapuliza kipenga cha mwisho matokeo yalibaki moja kwa Mbeya City na moja kwa Simba. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz  

KUTOKA COMORO
DSC_0051 
Mabingwa wa Tanzania bara na wawakilishi wa nchi katika michuano ya kombe la mabingwa wa Afrika Dar Young African imefanikiwa kuvuka kwenda raundi ya pili ya michuano hiyo baada ya kuifunga timu ya Komorozine De Domoni mabao 5-2.
Mabao ya Yanga yamefungwa na Mrisho Ngassa aliyefunga hat trick, huku Hamis Kiiza na Msuva wakifunga bao moja moja.
Yanga sasa watakutana na timu kubwa ya Misri Naciona Al Ahly.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz  

HIKI NDICHO ALICHOANDIKA KALA JEREMIAH KUHUSU AJALI ALIYOPATA SIKU YA VALENTINE

kala-ajali  
Leo Kala Jeremiah kupitia ukurasa wake wa Instagram amepost picha inayoonyesha ajali aliyoipata wakati akitokea kwenye show yake iliyokuwa ikifanyika Club East 24 ambayo alikua akifanya show pamoja The B Band ya Banana Zoro.
kala 
Hiki ndicho alichokipost Kala Jeremiah kupitia ukurasa wake wa Instagram.
Screenshot_2014-02-15-14-35-32 
Chini ya Post ya picha ya gari yake Kala aliandika maneno haya>> nIMEPATA AJALI USIKU HUU NIKIWA NATOKEA CLUB EAST 24 AMBAKO NILIKUWA NAFANYA SHOW NA B BAND WAKATI NARUDI NYUMBANI GHAFLA KUNA MTU WA PIKIPIKI AKAWA ANATAKA KUINGIA NIKAJARIBU KUMKWEPA GARI ILIKUA MWENDO KASI KIDOGO IKAYUMBA KWENDA KULIA NIKAIRUDISHA IKARUDI ZAIDI KUSHOTO NIKAIRUDISHA TENA KULIA IKAWA INATAKA KWENDA MTARONI NIKAIRUDISHA TENA KUSHOTO AMBAKO ILIGEUKA ILIKUKUA INATOKA NA KUINGIA MTARONI AMBAKO ILIKITA NA KUVUNJA MLANGO WA UPANDE WANGU.SIJAAMINI KAMA NIMETOKA BILA HATA JERAHA MGUUNI WALA MAUMIVU ZAIDI YA YALE UA KICHWANI KIDOGO NILIYOJIGONGEA KWENYE MLANGO KWA JUU.AHSANTE SANA MUNGU UMENIOKOA.ASANTE SANA MUNGU WANGU.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz  

AL-SHABAAB WAPATA SILAHA ZA SERIKALI...!!!

Ripoti ya umoja wa mataifa imeonya kuwa silaha zilizokuwa zikipelekwa kwa vikosi vya serikali ya Somali zimeingia katika mikono ya kundi la Al-shabaab kutokana na ukiukwaji wa utaratibu katika serikali.
Uchunguzi huo uliofanywa na wataalam walio huru umesema kuwa silaha za kudungua ndege,mabomu na risasi zilizotoka nchini Uganda na Djibout haziwezi kuwajibikiwa.
Ripoti hiyo sasa inataka taifa la Somali kuwekewa vikwazo vya silaha ambavyo viliondolewa mwaka uliopita.
Wataalam hao wamesema kuwa wana ushahidi kwamba mshauri mkuu wa rais nchini Somali amekuwa akihusika na mpango wa kuwapelekea silaha wapiganaji wa Alshabaab. 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI FEBRUARI 15, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS



.. 

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz


YANGA KUSHUKA DIMBANI NA COMORO LEO



WAWAKILISHI wa Tanzania kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Yanga leo inatarajiwa kushuka dimbani ikiwa ughaibuni kwa kuumana na Komorozine ya Comoro katika pambano la marudiano la michuano hiyo.
Mechi hiyo inatarajiwa kuchezwa kwenye uwanja wa Sheikh Said Mohamed International uliopo mji wa Mitsamihuli na Yanga ina kazi nyepesi ya kukamilisha ushindi mnono iliyopata katika mechi yao ya nyumbani ilipoisasambua Komorozine mabao 7-0.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Comoro zilizoripotiwa na mtandao wa klabu hiyo ni kwamba mara baada ya juzi jioni kufanya mazoezi mepesi katika uwanja mdogo wa hotel ya Retaj, Yanga ilijifua tena jana  asubuhi majira ya saa 5 ausbuhi katika Uwanja wa Sheikh Said kwa ajili ya kuuzoea tayari kwa ajili ya mchezo wa leo.
Kocha mkuu wa Young Africans Hans Van der Pluijm amesema anashukuru kikosi chake kipo vizuri kuelekea mchezo huo na hakuna mchezaji majeruhi hata mmoja hivyo anapata fursa ya kuchagua amtumie nani katika mchezo huo.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

Friday, February 14, 2014

MAGAZETI YA LEO SIKU YA WAPENDANAO FEBRUARI 14, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARDNEWS

.

.  
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

HISTORIA FUPI YA SIKU YA WAPENDANAO AU VALENTINE'S DAY

http://jambotz8.blogspot.com/

Sikukuu ya wapendanao inasherekewa kila ifikapo tarehe 14 mwezi wa pili kila mwaka.
Watu wengi wanaosherekea siku hii kwa Nchi za Afrika Mashariki ni vijana walio kati ya miaka 18 hadi 35.
Historia ya sikukuu hii inaanzia miaka mingi jijini, Roma, Italia ikiwa inahusishwa na mtakatifu Valentine au Valentinus aliyekuwa akiishi jijini humo katika karne hiyo. Wakati wa maisha ya mtakatifu Valentine Roma ilikuwa ikitawaliwa na Kaisari, Claudius II, ambaye alipata hisia wakati huo kuwa askari mkakamavu na bora zaidi ni yule asiyekuwa na mke wala familia. 
http://jambotz8.blogspot.com/
Claudius alilifanyia kazi wazo lake na aliamua kupiga marufuku ndoa zote kwa askari wa nchi hiyo, jambo ambalo halikukubaliwa na mtakatifu, Valentinus. Hivyo Valentinus alichukua jukumu la kukaidi amri ile na kuendelea kuwafungisha ndoa kwa siri maaskari waliokuwa wakitaka kufungishwa ndoa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz
 
Haikuchukua muda mrefu, taarifa zilimfikia mfalme, Claudius na alipopata habari hizo aliamuru kukamatwa na kufungwa gerezani na kisha Valentinus aliuawa kwa amri ya Kaisari. Kuna taarifa zinadai kuwa kabla ya kuuawa kwa Valentine wakati huo akiwa amefungwa, mtakatifu Valentine aliandika barua ya salamu kwa binti aliyekuwa amekwenda  kumsalimia gerezani. Na mwisho wa barua kulisomeka maneno yaliyoandikwa ‘From your Valentine’.
Tangu hapo Valentine akawa anakumbukwa kama mtetezi wa wapendanao na siku hii ikawa inaadhimishwa duniani kote.
Baada ya kufariki kwa mtakatifu huyo ndipo wananchi wengi duniani wakaamua kuadhimisha siku hii kama sherehe ya kumkumbuka Mtakatifu Valentinus
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

Thursday, February 13, 2014

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS FEBRUARI 13, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS



Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

TOYOTA YATOA AGIZO LA KUREJESHA MAGARI KIWANDANI...!!!

prius22_b3ff7.jpg
Kampuni ya kutengeza magari ya Toyota nchini Japan, imeagiza kurejeshwa kwa magari milioni 1.9 aina ya Prius katika kiwanda cha magari hayo nchini Japan.
Hii ni kutokana na hitilafu ya kimitambo ambayo inaweza kusababisha gari hilo kukwama.
Gari la Prius ni moja ya magari yenye muundo unaonyesha ubunifu wa hali ya juu wa kampuni ya Toyota.
Gari hilo linaweza kutumia petroli na betri huku likitoa kiwango kidogo sana cha moshi kuliko magari ya kaiwada.
Sasa kampuni hiyo imetambua hitilafu ya programu ya gari hilo ambayo inaweza kusababisha vifaa vya elektroniki vya gari hilo kukwama.
Magari mengi yenye hitilafu hiyo yako nchini Japan na Amerika ya Kaskazini na Toyota inasema kuwa haijapokea taarifa zozote za ajali au majeraha kutokana na hitilafu hiyo. CHANZO BBC
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

KAULI YA ZITTO KABWE KUHUSU MADAI YA WAFANYABIASHARA NA TRA...!!!

Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia Chadema Zitto Kabwe muda mfupi uliopita kupitia kwenye ukurasa wake wa Facebook ametoa yake ya moyoni kwa hili seke seke linaloendelea nchini juu Wafanyabiashara na Mamlaka ya Mapato Tanzania[TRA]kuhusu mashine za kutolea risiti za EFD.
Zitto alianza kwa kuandika>>’EFD zilianza kutumiwa mwaka 2010 kwa jumla ya wafanyabiashara 16,000 waliosajiliwa kwenye Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT). Mwaka wa fedha 2009/2010, kabla ya EFD, makusanyo ya kodi ya VAT yalikuwa tshs 791 bilioni’
‘Mwaka 2011/2012 makusanyo yaliongezeka kwa asilimia 40 mpaka tshs 1,086 bilioni. Mwaka 2012/2013 makusanyo yakaongezeka kwa asilimia 63 mpaka kufikia tshs 1,770 bilioni. Makusanyo haya ni kwa Wafanyabiashara 16,000′
‘Iwapo awamu ya pili ya EFD itatekelezwa bila vikwazo jumla ya Wafanyabiashara 200,000 watafikiwa ikiwemo ni pamoja na vituo vya mafuta (Petrol Stations), Mahoteli na Migahawa nk. Mamlaka ya Mapato inatarajia kukusanya zaidi ya tshs 3,500 bilioni kutoka VAT peke yake iwapo EFD zitatumika’
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

GHASIA ZAONGEZEKA JAMHURI YA AFRIKA YA KATI

dede_d2268.jpg

Takriban wanajeshi 1,600 wa Ufaransa na 6,000 wa Umoja wa Afrika wamo nchini humo kujaribu kulinda raia wakati ghasia zenye maafa zikiendelea kati ya Wakristo na Waislam.
Waziri wa ulinzi wa Ufaransa anasema lazima tahadhari zichukuliwe ili Jamhuri ya Afrika ya Kati isigawanyike. Onyo hilo limetolewa huku makundi ya kutetea haki za binadamu yakionya kuwa mauaji ya kikabila yanaendelea katika taifa hilo lililokumbwa na mgogoro wa kisiasa.
Waziri huyo Jean Yves Le Drian alifanya mazungumzo mjini Bangui na maafisa wa ngazi ya juu ya jeshi la Ufaransa pamoja na kaimu rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati Catherine Samba- Panza aliyeungana naye wakati wa ziara yake kusini magharibi mwa nchi.
Hii ni mara ya tatu kwa waziri Le Drian katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, tangu Ufaransa ilipozindua operesheni ya kijeshi mwishoni mwa mwaka jana. Onyo lake limetolewa huku makundi mawili ya kutetea haki za binadamu Amnesty International na Human Rights Watch yakionya juu ya mauaji ya kikabila katika baadhi ya maeneo ya nchi yanayolenga waislam walio wachache.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Wednesday, February 05, 2014

MTIBWA SUGAR KUWAKARIBISHA SIMBA UWANJA WA JAMHURI LEO MOROGORO

Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaingia raundi ya 16 leo (Februari 5 mwaka huu) kwa mechi tano huku Mtibwa Sugar ikiikaribisha Simba kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Kiingilio katika mechi hiyo ambayo itakuwa ya kwanza kuchezwa kwenye uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 10,000 tangu uanze mzunguko wa pili wa VPL kitakuwa sh. 5,000. Jonisia Rukyaa kutoka Bukoba ndiye atakayechezesha mechi hiyo.
Mechi nyingine za ligi hiyo ni Tanzania Prisons vs Coastal Union (Sokoine, Mbeya), Mgambo Shooting vs Ruvu Shooting (Mkwakwani, Tanga), Rhino Rangers vs Oljoro JKT (Ali Hassan Mwinyi, Tabora) na JKT Ruvu vs Ashanti United (Chamazi, Dar es Salaam).
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...