Thursday, January 02, 2014

MSIMAMO WA LIGI KUU YA UINGEREZA ULIVYO SASA MARA BAADA YA MECHI ZA JANA

 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

LOWASAA ATANGAZA KUANZA RASMI SAFARI YA NDOTO ZAKE...!!!

lowassa 9c1c5
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa ametangaza kuanza rasmi kwa safari aliyoiita ya matumaini ya ndoto zake, ambayo amesema itatimiza ndoto za Watanzania za kupata elimu bure, maji safi na maendeleo ya uhakika.
Akizungumza katika ibada ya shukrani na kuupokea mwaka mpya, katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT),Usharika ya Monduli Mjini, Lowassa bila ya kutaja safari hiyo ni ipi, aliwashukuru watu wote kutoka maeneo mbalimbali nchini, ambao walimsindikiza katika ibada hiyo.
Lowassa alisema anaamini watu hao waliofika, wana uhakika wa ushindi katika safari hiyo kwa kumtegemea Mungu.
"Nimefarijika sana leo kuwaona hapa marafiki zangu wengi. Ninapowatazama hadi machozi yananitoka na kwa uwezo wa Mungu tutashinda kwani nyote mnajua nia na ndoto yangu,'' alisema Lowassa na kupokelewa na sauti za shangwe kanisani.
 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

HII NDIO HISTORIA NZITO NA FUPI YA MAREHEMU DK. MGIMWA...!!!

 Historia fupi ya Waziri wa Fedha wa Tanzania, Dr. William Mgimwa aliyefariki dunia nchini Afrika Kusini alipokuwa amelazwa kwa matibabu.
Kuzaliwa: Januari 20, 1950 Kalenga Iringa.
Elimu:
1961 -1965 Shule ya Msingi Wasa
1966 - 1967 Shule ya Msingi Tosa
1968 - 1969 Tosamaganga Sekondari

1970-1971 Seminari ya Mafinga
1975 - 1984 Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) - Postgraduate in Finance
1989 - 1991 IDM Mzumbe (MBA - Finance)

Ajira
1981 - 2000 - NBC Ltd (Mhasibu, Mhadhiri, Mkurugenzi, Mkurugenzi Mkuu)
2000 - 2010 - Chuo cha Benki Kuu ya Tanzania Mwanza (Mkuu wa Chuo)
2010 - 2013 - Mbunge, Kalenga (CCM)

Waziri wa Fedha,Dkt. William Mgimwa (pichani) alifariki Dunia Januari 1, 2014 katika Hospitali ya Mediclinic Kloff,alikokuwa amelazwa kwa matibabu.

Wednesday, January 01, 2014

KHERI YA MWAKA MPYA 2014...!!!

Jambo Tz Blog inapenda kuwatakia Watu wote husani wadau wa blog hii popote pale walipo HERI YA MWAKA MPYA 2014. Nakutakia furaha, Baraka, Mafanikio, Afya tele, Amani na Upendo. Kwa namna ya kipekee kabisa. Pia endelea kuwa nasi mwaka 2014 kwani tumejipanga vilivyo kukuletea habari.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

HAYA NDIO MAGAZETI YA KWANZA KABISA KUTOKA MWAKA 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS .... HERI YA MWAKA MPYA

.
.
.
 Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

AJALI MBAYA IMETOKEA ENEO LA CCM MBEYA USIKU WA MWAKA MPYA NA KUUA MTU MMOJA

 
 Boda boda Mbili zikiwa zimegongana
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 


Tuesday, December 31, 2013

JAMAA APANDA JUU YA MNARA WA SIMU UBUNGO JIJINI DAR LEO NA KUGOMA KUSHUKA MPAKA AONANE NA RAISI KIKWETE

 Askari wa Kikosi cha Zima moto na Uokoaji Wakiwa wamepanda juu ya Mnara wa Simu Uliopo Ubungo Jijini Dar Es Salaam Muda mfupi uliopita kwaajili ya kumuokoa kijana mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Hassan Ambaye alipanda juu ya mnara huo kwa lengo la kufikisha Ujumbe wa kutaka kuonana na Raisi Kikwete ili aweze kumwelezea kwa kile anachodai kuwa jeshi la polisi lilimbambikia kesi na hatimaye kuhukumiwa kifungo cha Miaka 6 kwenda jela.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE DESEMBA 31, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.

MAAJABU YA MWAKA: MUME AUZA KABURI LA MKEWE...!!!


Hii ndiyo kali ya kufungia mwaka katika zote zilizotokea mwaka 2013! Mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Abrahaman, mkazi wa Kimara-Kilungule, Dar, anadaiwa kuuza kiwanja ambacho ndani yake kuna kaburi marehemu mkewe, Aisha Abdul aliyefariki Julai 21, 2004.

MALALAMIKO MEZANI
Wakizungumza na Uwazi kwa nyakati tofauti, watoto wa marehemu ambao wanapingana na tukio hilo la baba yao kuuza eneo hilo ambalo ni mali ya marehemu mama yao, walidai kuwa wamefedheshwa na kitendo hicho.
 “Kiukweli alichokifanya baba siyo sawa. Haiwezekani auze eneo ambalo lipo kaburi la mama yetu. Mbaya zaidi hadi sisi watoto wa kutuzaa yeye mwenyewe anatutishia maisha.

RAIS KIKWETE AMWAPISHA IGP MPYA PAMOJA NA NAIBU WAKE

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha Inspekta Generali wa Polisi (IGP) mpya Afande Ernest Mangu katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam jioni hii
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpatia nyenzo za kazi baada ya kumuapisha Naibu  Inspekta Generali wa Polisi (IGP) mpya Afande Abdulrahman Kaniki katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam jioni hii

Monday, December 30, 2013

BONGO MOVIE KAMA KAWADA YAO SAFARI HII WAMFANYIA WASTARA, MWEEEEEEE...!!!

DUA maalum ya kumbukumbu na kumuombea aliyekuwa msanii wa filamu Bongo, Marehemu Juma Issa Kilowoko ‘Sajuki’ imezua minong’ono mingi kufuatia wasanii wengi wanaounda Kundi la Bongo Movie kudaiwa kumfanyia mbaya mkewe, Wastara Juma kwa kutohudhuria. Dua hiyo ya ilifanyika Jumamosi iliyopita nyumbani kwa marehemu Tabata-Bima, Dar na kumalizikia kaburini kwake Kisutu. Katika tukio hilo, wadau mbalimbali wa filamu na burudani, walionekana kushangazwa na kitendo cha wasanii wengi wa Bongo Movie kutokuwepo licha ya marehemu Sajuki kushirikiana nao kwa karibu enzi za uhai wake. Aidha, wengine walifika mbali kwa kuhoji kulikoni wafanye hivyo, maswali ambayo yalimuongezea uchungu mkubwa Wastara aliyekuwa akibubujikwa machozi mara kwa mara. Kwa upande wake, Wastara alisema anamshukuru Mungu kwa kufanikisha shughuli hiyo na kuwaombea kwa Mungu wote waliojitokeza kumuunga mkono kwenye dua hiyo. “Nawashukuru wote waliojitokeza, wamenifariji sana,” alisema Wastara kwa simanzi.
Wasanii wa filamu waliohudhuria dua hiyo, ni pamoja na Denis Sweya ‘Dino’, Ahmed Olotu ‘Mzee Chilo’, Flora Mvungi, Hamis Ramadhan ‘H. Baba’ na Suleiman Bin Sinan ‘Bond’.  
Mwenyekiti wa Bongo Movie, Vincent Kigosi ‘Ray’ alipotafutwa, simu iliita bila kupokelewa.
Sajuki alifariki dunia Januari 2, 2012 na katika kutimiza mwaka mmoja kaburini misa nyingine itafanyika nyumbani kwa wazazi wake mkoani Songea Januari 2, 2014.
Na GPL
Tafadhari Like page yetu ya facebook kwa ku-click Jambo Tz

WABUNGE 15 KUKATWA MISHAHARA KWA KOSA LA KUCHUKUA POSHO ZA SAFARI BILA KUSAFIRI...!!!

Katibu wa Bunge  Dk. Thomas Kashililah akiwa ofisini kwake jana wakati wa mahojiano na mwandishi wa gazeti hili. Picha na Kelvin Matandiko  
********
Ofisi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limewaanika wabunge 15, waliobainika kuchukua posho za safari bila kusafiri huku wengine wakikatisha safari zao.
Akizungumza katika mahojiano maalumu jana na mwandishi wa habari hii, Katibu wa Bunge Dk Thomas Kashililah, alisema tayari fedha hizo zimesharejeshwa kwa kukatwa kwenye mishahara yao.
Dk Kashililah alisema baadhi ya wabunge waliomba wasikatwe fedha hizo kwenye mishahara yao, badala yake wazirejeshe wao wenyewe.
Hata hivyo, Katibu huyo wa Bunge alisema wabunge hao walishindwa kusafiri kutokana na sababu mbalimbali, zikiwamo kuwa na ugeni wa viongozi wa chama na matatizo ya kifamilia.
Tafadhari Like page yetu ya facebook kwa ku-click Jambo Tz

MAALIM SEIF: "WAZANZIBAR WANATAKA MAMLAKA KAMILI"

maalim1 1e311
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amesema Wazanzibar wanaisubiri kwa hamu Rasimu ya Katiba ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ili kuona kama imezingatia masilahi na matakwa yao katika kupata mamlaka kamili ya Zanzibar.
Msimamo huo ameutoa kwenye mkutano wa hadhara wa CUF uliofanyika Kinyasini, Mkoa wa Kalazini Unguja na kuhudhuriwa na wajumbe wa Kamati ya Maridhiano inayoongozwa na Mwenyekiti wake, Mzee Hassan Nassor Moyo.
Aidha, katika mkutano huo, kwa mara ya kwanza Waziri wa zamani wa SMZ na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Mansoor Yussuf Himid alihutubia tangu avuliwe uanachama wa CCM kutokana na madai ya kwenda kinyume na sera, maadili na nidhamu ya chama hicho.
Katika maelezo yake, Maalim Seif alisema wanachodai Wazanzibar
ni mamlaka kamili ni kuifanya Zanzibar ijitegemee kiuchumi, kujipangia na kujiamulia mambo yake ya ndani na nje bila ya kutegemea upande wowote.
Alisema Zanzibar ilikuwa taifa huru lililoungana na Tanganyika kwa ridhaa na siyo mateka wa Tanganyika, hivyo wanayo sababu ya kujitegemea.
Tafadhari Like page yetu ya facebook kwa ku-click Jambo Tz

JAJI MKUU AWA MCHUNGAJI WA KANISA LA ANGLIKANA ZANZIBAR


Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino Ramadhani ametawazwa kuwa Mchungaji wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Zanzibar na kusema ameshangazwa na mashambulizi ya tindikali dhidi ya viongozi wa dini Visiwani humo.
Akizungumza na waaandishi wa habari mara baada ya kutawazwa ndani ya Kanisa la Anglikana la Minara Miwili Mjini Unguja, Jaji Ramadhan amesema vitendo vya hujuma vinavyofanywa dhidi ya viongozi wa dini na Serikali ni kinyume na utamaduni wa Zanzibar.

Alisema Wakristo na Waislamu Zanzibar kwa miaka mingi wamekuwa wakiishi kama ndugu bila ya kubaguana kwa sababu za itikadi ya dini licha ya Waislamu kuwa asilimia 95.

Hata hivyo, alikumbusha kuwa wakristo wana mchango katika harakati za ukombozi wa Zanzibar, ambapo idadi kubwa ya waumini wake walianzisha Chama cha African Association mwaka 1935, ambapo rais wake wa kwanza alikuwa hayati, Mzee Augustino Ramadhan na baadaye akafuata hayati Mzee Abeid Amani Karume.
Tafadhari Like page yetu ya facebook kwa ku-click Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU DESEMBA 30, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.


Tafadhari Like page yetu ya facebook kwa ku-click Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...