Saturday, November 16, 2013

RATIBA YA SHUGHULI YA KUAGA MWILI WA DKT. SENGONDO MVUNGI LEO - JUMAMOSI NOVEMBA 16 2013

Mvungi_01_f96b1.jpg
NOVEMBA 15, 2013 – UWANJA WA NDEGE WA MWALIMU JK NYERERE
Saa 12:50 jioni
Kuwasili kwa mwili wa Marehemu – Uwanja wa Ndege wa Mwalimu JKN
KESHO, NOVEMBA 16, 2013 – VIWANJA VYA KARIMJEE
Saa 2:00 – 3:30 asubuhi
Kuwasili kwa Wageni, Wananchi na Waombolezaji
Saa 3:30 asubuhi
Kuwasili Mwili wa Marehemu
Saa 4:00 – 5:45 asubuhi
Ibada ya Misa Takatifu, Viwanja vya Karimjee
Saa 5:45 – 6:55 mchana
Salaam za Rambirambi na Neno la Shukurani
Saa 6:55 – 8:40 Mchana
Kuaga Mwili wa Marehemu
Saa 9:00 Alasiri
Msafara kupeleka mwili wa marehemu Kibamba Msakuzi
KESHO KUTWA, NOVEMBA 17, 2013 – NYUMBANI KWA MAREHEMU - KIBAMBA, MSAKUZI
Saa 2:30 – 4:30 asubuhi
Ibada ya Misa nyumbani kwa marehemu
Saa 5:00 asubuhi
Kuanza safari ya kwenda Chanjale, Kisangara Juu, Mwanga, Kilimanjaro

TATOO NA MUONEKANO MPYA WA RAY..... VYAWACHEFUA WASHABIKI WAKE

 
Huu  ni  muonekano  mpya wa  Vicent  Kigosi ambao ni moja ya maandalizi ya movie  yake  mpya ...
Ni  muonekano  ambao  kwa  kiasi  flani  umewachefua  mashabiki  wake  ambao  dakika  chache  baada  ya  picha  hizo  kuwekwa  walijimwaga  kwa  comment  ambazo hazikumuunga  mkono  kwa  asilimia  zote.



  Je nageukia bongoflava au kuna nini kinakuja?. Aliadika  Ray  kwenye  moja  ya  picha  zake.

Friday, November 15, 2013

MAGAZETI YA LEO IJUMAA NOVEMBA 15, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
..



.

LOWASSA: TULIOHUZUNIKA, TUTASHINDA PAMOJA

lowassapx a10b6
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema waliofurahi na kuhuzunika naye pia watashinda pamoja naye.
Bila kufafanua kauli yake jana, Lowassa aliwaambia wakazi wa Monduli mkoani Arusha kuwa: "Kumbukeni kaulimbiu yangu wakati wa Uchaguzi Mkuu uliopita, tulifurahi pamoja, tulihuzunika pamoja na tutashinda pamoja".
Mbunge huyo wa Monduli alikuwa akizungumza kwenye mkutano wa hadhara mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa wodi mbili za ghorofa za wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Monduli.
Katika hotuba yake fupi, pia alitamba kwamba atayashinda majaribu. Hata hivyo, hakufafanua majaribu hayo... "Kuna vita kubwa, lakini ambacho naweza kusema ni kuwa nayaweza yote kwa yeye anitiaye nguvu."
Kuhusu afya yake ambayo mara kadhaa imeelezwa kuwa siyo imara, kiongozi huyo alisema kwa sasa ni nzuri na imeimarika kupita kipindi kingine chochote.

Thursday, November 14, 2013

MAGAZETI YA LEO NOVEMBA 14, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
.

LIST MPYA YA MATAJIRI 50 AFRIKA, WATANZANIA WAKO WANNE

dangote
Mtandao wa Forbes maarufu kwa kutoa taarifa kama hizi, umetoa list mpya ya matajiri 50 kutoka Africa na kuhusisha vyanzo vya pesa zao, umri wao pamoja na kiasi cha pesa wanachomiliki.
List imeongozwa na Mnigeria Aliko Dangote (kwenye picha hapo juu) na mtanzania wa kwanza ameonekana kwenye namba 27 akiwa na utajiri wa dola bilioni moja. Cheki list yote hapa.
Watanzania hawa wanne ni Rostam Aziz kwenye namba 27, Reginald Mengi namba 34, Bakhresa namba 38 na Mohammed Dewji namba 38.

1
2
3
4
5

MZEE MIAKA 80 AJIUA KISA WIVU WA MAPENZI, MKEWE ADAIWA KUTEMBEA NA MWANAYE WA MIAKA 12


Mke wa marehemu, Asha Ali (50) anayetuhumiwa kutembea na mwanaye wa miaka 12.

Stori: Gladness Mallya na Chande Abdallah
AMA kweli duniani kuna mambo! Mzee Juma Kondo (80) mkazi wa Mkuranga mkoani Pwani amejiua kwa kunywa dawa ya macho hivi karibuni kutokana na wivu wa kimapenzi, Risasi Mchanganyiko limefukunyua.


Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichopo jirani na familia hiyo, mzee Juma na mkewe, Asha Ali (50) walikuwa na mgogoro wa muda mrefu uliotokana na mambo ya mapenzi.
Mzee huyo alikuwa akimtuhumu mkewe kutembea na mtoto wao wa mwisho ambaye ana umri wa miaka 12 (jina kapuni).
“Mpaka marehemu anachukua uamuzi wa kujiua, mgogoro mkubwa kati yao ulikuwa ni kumlalamikia mkewe kutembea na mtoto wao huyo anayesoma darasa la tano,” kimesema chanzo hicho.

Waandishi wetu walizungumza na mke wa marehemu, Asha ambaye alikiri mumewe kujiua kutokana na wivu huo wa mapenzi.
“Ndani ya ndoa yetu tulikuwa na mgogoro na mume wangu alikuwa akinituhumu kutembea na mwanangu kitu ambacho hakikuwa cha kweli, binafsi siwezi kulala na mwanangu kwa sababu mimi siyo kuku.

Mtoto wa mwisho wa marehemu mwenye umri wa miaka 12 anayesoma darasa la tano anayetuhumiwa kutembea na mama'ke.

MAELEZO MAPYA ALIYOYATOA MOHAMED MORSI JINSI ALIVYOPINDULIWA EGYPT.

Morsi 1 
Rais Mohamed Morsi aliepinduliwa madarakani nchini Misri July 2013 amesema alitekwa nyara na wanajeshi ambao ndio walimtoa kwenye madaraka ambapo kikundi cha wanasheria waliojitolea ambao hawako kwenye upande wa Morsi, wametangaza hii baada ya kukutana na Morsi gerezani.

Rais huyu aliepinduliwa anataka kulishtaki jeshi na anasema hakutakua na utulivu Misri mpaka hawa watu waliompindua watolewe na wale waliohusika na umwagaji damu za Wamisri  watakapowajibishwa.
morsi gerezani

FUTURE YOUNG TAIFA STARS YAICHAPA TAIFA STARS 1-0 ANGALIA ILIVYOKUWA


Mshambulia wa Taifa Stars, Mrisho Ngasa (kulia) akichuana na mchezaji wa Future Young Taifa Stars, Kabanda katika mchezo kirafiki uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam. (Picha na Francis Dande)
Kiungo wa Taifa Stars, Athuma Idd "Chuji" akichuana na mchezaji wa Future Young Taifa Stars,Paul Nonga.

ALIYEMUUA GWIJI LA SHERIA YA KATIBA DAKTA MVUNGI AKAMATWA DAR

kova1 e15c3
Kamanda wa Kanda Maalum Dsm, Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi (ACP) Suleiman Kova.

Na Damas Makangale, Moblog
Siku moja baada ya nguli ya sheria za katiba nchini, Dakta Sengodo Mvungi kuaga dunia nchini Afrika Kusini, Jeshi la Polis Kanda Maalum Ds, linamshikilia mtuhumiwa mmoja John Ikondia Mayunga (56) kwa kosa la kushiriki kikamilifu kwenye mauaji ya mwanasheria huyo na mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Kanda Maalum Dsm, Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi (ACP) Suleiman Kova amesema mtuhumiwa huyo ni mkazi wa kiwalani walipata taarifa kwa raia wema kwamba alishiriki kikamilifu kwenye tukio hilo lilosababisha kifo cha Dakta Sengodo Elibariki Mvungi.

"mnamo tarehe 12/11/2013 Polisi walipata taarifa kutoka kwa raia mwema kwamba kuna mtu ambaye amehusika na tukio la mauaji ya Dakta Mvungi na kwamba kipindi hicho mnamo saa 12 jioni mtuhumiwa alikuwa maeneo ya mtaa wa Twiga Jangwani akiwa anaangalia Televisheni," amesema Kamishina Kova. Marehemu Dakta. Sengodo Mvungi.

CCM YATOA POLE MSIBA WA DR.SENGONDO MVUNGI


 KINANA_MKUTANO_WA_SHIRIKISHO_LA_CCM_VYUO_VIKUU_MORO_PIX_NO_2_529d1.jpg
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Abdulrahaman Kinana amesikitishwa na taarifa ya kifo Cha Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Dr Sengondo Mvungi kilichotokea Jana katika Hospitali ya Millpark nchini Afrika ya Kusini.

Kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi, Katibu Mkuu anawapa pole wanafamilia, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba na Uongozi wa Chama Cha NCCR-Mageuzi. Hakika Taifa limepoteza Mtaalamu wa Sheria, Kiongozi Mzalendo na hodari katika kipindi ambacho mawazo yake yanahitajika kwa kiasi kikubwa kuliendeleza Taifa hili.
Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi.

Imetolewa na:
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA
ITIKADI NA UENEZI
13/11/2013
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha mjumbe wa tume ya mabadiliko ya katiba Dr Sedondo Mvungi ambacho kimetokea katika hospitali ya Millpark nchini Afrika kusini.

Uongozi wa UVCCM Taifa unatoa pole kwa familia na ndugu wa marehemu, pia UVCCM inatoa pole kwa uongozi wa NCCR- Mageuzi na kwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Warioba pamoja na Vijana nchini kote ambao wamenufaika na Utaalamu na mafunzo. 
Kama vijana tulihitaji sana mchango wa mawazo, hekima na utaalamu kutoka kwake, hakika tumepoteza kiongozi shupavu, muadilifu na mzalendo ambae ni mfano wa kuigwa kwa Vijana wa Taifa hili.

Wednesday, November 13, 2013

SNURA WA MAJANGA ALETA SHIDA, KWELI HII NI BALAA DUNIANI....!!!


 Ilikuwa kwenye show ya kichwaji cha GRAND MALT maeneo ya karumeshida ilianza pale mkali wa viuno mwanadada snura alivyopanda jukwaaani hali ilikuwa si shwali kabisa pale wauza mitumba waliaamua kupiga shangwe za hatari na kutaka mpaka kumshika snura kwa balaa alilolifanya. show ilivyoisha alitumia lisali moja na nusu kutoka kaatika uwanja huo kila mtu alitamani kumshika kila mtu alitaka kupiga nae picha. angalia video hapo chini hali ilivyokuwa.

MAINDA: NIMETOA MIMBA YA RAY

Stori:  Jelard Lucas
HILI ndiyo Risasi bwana! Sikia, kama ulikuwa hujui ni kwamba msanii mkongwe katika filamu za Kibongo, Ruth Suka ‘Mainda’ ameibuka na kueleza mengi ikiwemo kutoa mimba ya mpenzi wake wa siku nyingi, Vincent Kigosi, tulia hapohapo.

Mbali na uhusiano wao huo uliokuwa ukifanywa siri, Mainda ameeleza kwa machungu jinsi Ray alivyomtesa kwa kumchanganya na wasanii wenzake, Blandina Chagula ‘Johari’ na Chuchu Hans ambaye ni mke wa mtu.

Risasi Mchanganyiko lilipata wasaa wa kufanya naye mahojiano ‘exculusive’ kwa saa moja na dakika tano, wikiendi iliyopita, makao makuu ya gazeti hili, Mwenge – Bamaga, jijini Dar.

Hata hivyo, alisema uhusiano wao kwa sasa umevunjika rasmi huku akibainisha jinsi alivyonyooshewa vidole na watu wakiamini kwamba aliambukizwa Ukimwi na aliyekuwa mpenzi wake kabla ya Ray, marehemu Said Maulid Banda  ‘Maxi’.
Soma mwenyewe mahojiano yalivyokuwa mstari kwa mstari, neno kwa neno:

Risasi: Baada ya kifo cha Maxi, Ray alijitokeza na kukutongoza au siyo?
Mainda: Hapana, nakumbuka ilikuwa Siku ya Valentine’s Day mwaka 2004...sikumbuki kama tulitongozana ama vipi lakini ilitokea tukajikuta kwenye uhusiano.

SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA KIFO CHA DK MVUNGI KUTOKA CHADEMA

 

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe ametuma salaam za rambirambi ya kifo cha Dkt. Edmund Sengondo Mvungi, akitoa pole kwa familia, uongozi na wanachama wa NCCR-Mageuzi, Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya na wananchi wote walioguswa na msiba huo. Akitoa kauli hiyo kwa niaba ya CHADEMA na wanachama wa chama hicho, Mwenyekiti Mbowe amesema kuwa amepokea kwa masikitiko na mshituko mkubwa taarifa za kifo cha Dkt. Mvungi, akimwelezea kuwa alikuwa mwanasiasa mwenye msimamo ambaye hakuwahi kutetereka kusimama na chama chake tangu alipojiunga nacho na kuanza kushiriki siasa za mageuzi nchini. “Kwa niaba ya CHADEMA na wanachama wetu nchi nzima, napenda kutoa salaam za pole sana kwa familia ya marehemu, mjane na watoto. Natoa pole kwa Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia na wanachama wa chama hicho, pia tunatoa pole kwa Jaji Mstaafu Joseph Warioba na makamishna wote wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwakifo cha Dkt. Mvungi. Tunaomba Mwenyezi Mungu awatie nguvu sana wakati huu wa majaribu na majonzi makubwa. “Dkt. Mvungi alikuwa mwanasiasa mwenye misimamo ambaye hakuwahi kukihama chama chake tangu alipoanza siasa za mageuzi nchini. Ni kati ya wasomi wachache waliokuwa na ujasiri na kuthubutu kujiunga na vyama vya upinzani tangu mapema. "Mvungi pia alikuwa mmoja wa wanasiasa wa mwanzo kabisa kupigania nchi yetu iwe na Katiba Mpya, ili hatimaye siasa zetu, hususan demokrasia ya vyama vingi nchini iendeshwe kwa misingi iliyo imara,” amesema Mwenyekiti Mbowe na kuongeza; “Mwenyezi Mungu alimjalia marehemu akaweza kushiriki kutimiza ndoto hiyo baada ya kuteuliwa kuwa mmoja wa makamishna wa Tume ya Mpya, kazi ambayo ameifanya hadi siku alipokutwa na tukio lililosababisha mauti yake.” Mwenyekiti Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Hai, amesisitiza kuwa kwa namna ambavyo Dkt. Mvungi alikuwa mstari wa mbele katika suala hilo, Tume ya Katiba Mpya inao wajibu wa kuthamini mchango wake katika hatua iliyofikia sasa ya mchakato huo nyeti hadi utakapofika mwisho. “Wakati tukimwombea marehemu kwa Mungu, alazwe mahali pema peponi, ni matumaini yetu kuwa serikali kupitia vyombo vyake itahakikisha kuwa wale wote waliohusika katika tukio la lililosababisha kukatisha uhai wa Dkt. Mvungi wanapatikana na kuchukuliwa hatua zote zinazostahili kisheria,” amesema Mwenyekiti Mbowe.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 13, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...