Wednesday, November 06, 2013

LULU AFUNGUKA KUHUSU YEYE KUCHUMBIWA...!!!

 
Muigizaji wa filamu nchini Elizabeth Michael aka Lulu amekanusha fununu zilizoandikwa kwenye gazeti la udaku liitwalo ‘Filamu’ kwamba amechumbiwa na muda mchache ataolewa.
 
Akizunguza jana  kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, muigizaji huyo wa Foolish Age, alisema hajachumbiwa na mtu yeyote ila ni magazeti ya udaku tu ndio yamekuwa yakiandika kile yanachojisikia.
 
“Mimi sijachumbiwa na hakuna mtu yeyote aliyenichumbia na kama itatokea siku nikachumbiwa kila mtu atajua, na ni mimi mwenyewe ndiye nitakaesema,” alisema mrembo huyo.
  “Lakini sasa sijajua wao wamepata hiyo habari kutoka kwenye chanzo gani, by the way kwaajili kumekuwa na habari kila kukicha kila mtu anayejisikia kuandika anaandika ,anaamka anaandika, anaamka anandika. 

 "Kwa hiyo leo wameandika nimechumbiwa, kesho wataandika nimeolewa, kwa hiyo inategemea na mood ambayo wao waliamka nayo, kwamba ‘leo Lulu tumchumbie, tumuozeshe, tumuachishe’, I don’t know.
 
“Kuchumbiwa, kuolewa,kuwa mke ni vitu ambavyo tumeumbiwa binadamu, vipo kama ukiwa mpango wa mwenyezi Mungu nitachumbiwa na nitaolewa.” Lulu

ANGALIA PICHA ZA JUX KING OF PAMBA KWA WASANII WA BONGO

http://distilleryimage8.ak.instagram.com/d08bd338f3c411e289bf22000a1fa4a9_7.jpg

http://distilleryimage2.ak.instagram.com/ddfe26f6ef9611e2a63622000a9e28ec_7.jpg


http://distilleryimage11.ak.instagram.com/cbffd894453311e3984822000a1f9707_7.jpg 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

UJUMBE MZITO WA LULU KWA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

MSANII wa filamu nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’, ameliomba Bunge kurekebisha sheria za Magereza katika vikao vyao vinavyoendelea mjini Dodoma.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam juzi, Lulu alisema kutokana na kukaa huko kwa mwaka mmoja, ameona mambo mengi ambayo yanatakiwa kufanyiwa marekebisho.
“Unaweza ukamkuta mfungwa ana miaka zaidi ya 20 lakini hajawahi kufikishwa mahakamani wala kuulizwa chochote kutokana na kitu ambacho kimempeleka hapo, kiukweli hata kama ana makosa haiwezekani kumkalisha miaka yote hiyo pasipo kusikilizwa,” alisema.
Alisema yeye amekaa huko kwa muda mfupi lakini amepata shida sana kuyazoea mazingira hayo, kwani huwezi kuishi kama nyumbani, hivyo ni vizuri ukiwekwa utaratibu mtu anasomewa kesi yake kwa muda gani.
Lulu alilazimika kukaa gerezani kwa muda huo kwa tuhuma za mauaji ya aliyekuwa nguli wa filamu nchini, Steven Kanumba, aliyefariki dunia nyumbani kwake Sinza Vatican Aprili 7, mwaka jana

MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 06, 2013

.
.
.

MAELEZO BINAFSI YA MH. ESTER BULAYA KUHUSU WAHARIFU WA DAWA ZA KULEVYA.....!!!


 bulaya
Haya ni maelezo binafsi ya Mheshimiwa Ester Amos Bulaya bungeni Dodoma November 4 2013 kuitaka serikali kufanya mabadiliko ya sheria ya dawa za kulevya na kuanzisha mahakama maalum ya kushughulikia wahalifu wa dawa za kulevya.
Kwa mujibu wa Kanuni ya 28(8) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la mwaka 2013, napenda kutoa maelezo binafsi ya juu ya tatizo sugu la uagizaji, uuzaji na usafirishaji wa dawa za kulevya linaloongezeka kwa kasi kubwa nchini, lengo likiwa ni kuitaka serikali ifanye mabadiliko/marekebisho ya sheria ya Dawa za kulevya na kuanzisha Mahakama Maalum kushughulikia wahalifu wanaojihusisha na usafirishaji na biashara ya dawa za kulevya.
chinese
Mheshimiwa Spika,
Nimeona ni wakati muafaka kutoa maelezo haya, ili Bunge lako tukufu na Serikali ipate fursa ya kuona uzito wa tatizo hili kutokana na ukweli kwamba katika miaka ya karibuni tatizo la dawa za kulevya katika nchi yetu limeongezeka kwa kasi ya ajabu hali inayopelekea athari kubwa za kiuchumi, kijamii na kiafya. Na mbaya zaidi kundi kubwa linaloathirika ni kundi la vijana, ambao ndio nguvu kazi ya Taifa letu.

HILI NDILO JUMBA LA KIFAHARI LENYE UWANJA WA NDEGE HAPO HAPO NYUMBANI

article-2486741-1923386700000578-170_634x475Nyumba hii ipo huko Las Vegas Marekani na ina heka 40 na indoor car parking kubwa sana kuingiza magari zaidi ya kumi kwa wakati mmoja na upande wa mwingine ina zoo humohumo ndani, jet inayopark kwenye airport yako binafsi hapo mjengoni haina haja ya kwenda kwenye public airport na ukitaka kumiliki hii nyumba inabidi zikutoke $ 48 millioni.
article-2486741-1923389000000578-571_634x475
Vyumba vya kulala vipo vingi kiasi kwamba wakati mwingine inabidi kuwasiliana kwa simu chumba hadi chumba kwasababu ya umbali wa kufikia vyumba vingine pia kuna ofisi binafsi kiasi kwamba unaweza usiende sehemu yoyote kazi zako zote zikafanyika ndani ya hizi heka 40.
Upande wa michezo kuna uwanja wa kucheza golf, basketball, swimming pool kubwa likiunganishwa na water falls na pia kuna eneo kubwa sana la wazi na humo ndani kumewekwa nakshi na material ya gharama kuanzia dinning, jikoni hadi vyumbani.

article-2486741-1923388400000578-459_634x475

RAIS KIKWETE KULIHUTUBIA BUNGE KESHO....!!!

jk_d71ab.jpg
Rais Jakaya Kikwete, kesho anatarajiwa kulihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Habari zilizopatikana Mjini Dodoma jana na kuthibitishwa na uongozi wa Bunge pamoja na Ikulu, Dar es Salaam zinasema atahutubia mchana.
Kutokana na ujio huo, Serikali imewaelekeza Mawaziri na Manaibu Waziri kutotoka nje ya Dodoma hadi hapo Rais atakapokuwa amehutubia Bunge. 
Kadhalika safari zote za Kamati za Bunge ambazo zilikuwa katika mchakato wa kutekelezwa zimeahirishwa hadi baada ya kesho, ili kutoa fursa kwa wabunge wote kuwapo wakati wa hotuba hiyo.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema jana kuwa hata yeye amesikia taarifa kuwa Rais atazungumza bungeni lakini hajui atazungumza kitu gani... "Hata mimi nimesikia kuwa atazungumza lakini sijui atazungumza jambo gani kwa kuwa siyo miongoni mwa watu wanaomwandalia hotuba," alisema Balozi Sefue.
Kadhalika, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu alithibitisha kuwa Rais Kikwete atalihutubia Bunge, Alhamisi... "Nathibitisha ni kweli, ila kwa taarifa nyingine watafuteni watendaji wa Bunge, kama Katibu wa Bunge nadhani wana taarifa zaidi."

M23 'WAMALIZA UASI' BAADA YA KIPIGO

130913125600_m23_congo_304x171_afp_nocredit_ab833.jpg
Waasi wa M23 katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wametangaza kumaliza uasi wao ndani ya nchi hiyo muda mfupi baada ya kupigwa katika ngome yao ya mwisho na majeshi ya serikali ya Congo yakishirikiana na kikosi maalum cha Umoja wa Mataifa kilichopewa uwezo wa kupigana na waasi hao.
Katika taarifa walioitoa waasi hao wamesema badala ya kufanya uasi sasa wataendesha harakati zao kutumia njia ya kisiasa.
Muda mfupi uliopita Kiongozi wa waasi hao Bertrand Bisimwa ametangaza kuwaamuru mkuu wa wapiganaji wa M23 na makamanda wa vikosi vyote muhimu wa kundi hilo kuwaandaa wapiganaji wao kusalimisha silaha, kutawanyika kuondoka katika eneo la mapigano na kukubaliana na matakwa yatakayowekwa na serikali ya Congo
Awali Msemaji wa Serikali ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo Lambert Mende aliambia BBC kuwa majeshi ya nchi yameishambulia ngome ya mwisho ya waasi na wamekimbia na wengine huenda wakawa wamejisalimisha.
Majeshi ya serikali ya Kongo yakishirikana na kikosi maalum cha Umoja wa Mataifa kilichopewa uwezo wa kupambana na waasi hao walianza mapambano dhidi ya M23 Octoba mwaka huu na kufanikiwa kuwaondoa katika eneo la Bunagana kwenye mpaka wa Uganda ambayo ni ngome yao muhimu.

Tuesday, November 05, 2013

NEY WA MITEGO AMPA KICHAPO BABA 'AKE...!KISA KUMUONEA MAMA' AKE...!

Nay wa Mitego ni moja kati ya wasanii wenye tungo zenye utata sana tangu anaanza kufanya muziki ambapo alikuwa akisikika kwenye baadhi ya ngoma akimchana hata baba yake mzazi kwa kushindwa kuwa responsible kwake. Hit maker wa ‘Muziki Gani’ ambae anakiri kuwa zamani alikuwa mkorofi sana na kwamba sasa hivi amebaki kuongea tu kwenye muziki, amewahi kufunguka kuwa alimpa kichapo baba yake wa kambo/baba yake wa kufikia ambae alikuwa akimtunza kwa muda huo.
Kisa cha kumpa kichapo mzee wa watu.. ni kwa sababu alikuwa anampiga sana mama yake Nay wa Mitego kitu ambacho kilikua kinamuumiza sana yeye, na mwisho wa siku akachukua uamuzi wa kumpiga akimtetea mama yake.
  Tukio hilo lilimsukuma Nay wa Mitego kuandika mashairi ya wimbo unaohusu wanawake akiwaambia wanaume wenye tabia kama za baba yake wa kufikia kwamba ‘Mwanamke hapigwi, anatulizwa na mapenzi.’
  “Ule wimbo ulikuwa ni dedication kwa mama yangu mzazi, mama yangu mzazi alikuwa anaishi na baba yangu wa kufikia, yule baba yangu alikuwa mkorofi sana, alikuwa anampiga sana mama bila sababu, kiasi kwamba alisababisha mimi na mama tusielewane kwa sababu mimi nilikua sipendi vile alivyokuwa anamfanyia mama, mi nakumbuka kwa bahati mbaya nilishawahi kumpiga yule mzee and then mama yangu akachukua hatua ambayo mimi sikuitegemea kwa sababu mimi nilikuwa namtetea mama.
  “Mi nikajifunza kwamba mwanamke hatakiwi kupigwa hata siku moja, na ndo maana nikaimba, so ilikuwa dedication kwa mama yangu na wanawake wote Afrika.” Alisema Nay wa Mitego.

MAGAZETI YA LEO NOVEMBA 05, 2013

DSC 0015 383d6
DSC 0016 21d82

SULEIMAN ANAHITAJI MSAADA WETU AENDE INDIA KUTIBIWA

Wapendwa, Siku ya Leo haikuwa nyepesi kwangu na hata kwa mtoto Suleiman na familia yake, baada ya kupokea ujumbe rasmi kutoka kwa madakatri bingwa wa upasuaji wa Hospitali ya CCBRT kuwa Upasuaji huo HAUTAWEZEKANA kufanyika CCBRT kama tulivyojipa moyo mara ya kwanza.

LAKINI, wamekubali kutusaidia kupata hospitali nzuri nchini India kwa ajili ya kumsafirisha kijana Suleiman. Nguvu zenu zinahitajika sana kipindi hiki kigumu kwa familia hii. Tayari msamaria mwema ametoa tiketi moja ya kumsindikiza Suleiman India. Wapendwa, tushikamane, tunaweza. Hatua zinazofuata:
Kwanza kupata hospitali India.
Kufanya malipo
Kupata barua ya referral na kutafuta passport na visa ya Suleiman na msindikizaji Safari

CCBRT wataturudishia milioni 3 tulizolipa kama gharama za matibabu na tukijumlisha na pesa alizo nazo Imelda tuitakuwa tumebakiwa na shilingi milioni 6.2. Safari ni ndefu lakini msichoke.
Asanteni sana. Mola atuongoze. Amen

PAPII KOCHA, BABU SEYA KAZI IMEKWISHA.

Na Mwandishi Wetu

 MABERE Nyaucho Marando, wakili wa mwanamuziki maarufu nchini, Nguza Viking ‘Babu Seya’ na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ amesema amemaliza kazi ya kuwatetea wafungwa hao waliohukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kukutwa na hatia ya kuwanajisi watoto 12 waliokuwa wakisoma Shule ya Msingi Mashujaa, Sinza jijini Dar es Salaam..........
Babu Seya (wa pili kulia) na Papii Kocha (wa pili kushoto) wakiwa mahakamani kusikiliza rufaa yao.

 Akizungumza na gazeti hili juzi, Marando alisema kazi aliyokusudia kuifanya ameimaliza, sasa anasubiri majaji waliosikiliza alichokisema ili watoe uamuzi wa mwisho lakini pia anamtegemea Mungu.

 “Mimi kazi nimemaliza sasa nawasubiri hao wakubwa (majaji) ili wapime nilichowaambia kwa mujibu wa sheria na kisha watoe uamuzi, lakini pia namtegemea Mungu,” alisema Marando.

SERIKALI YAIRUDISHA DARAJA SIFURI


Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imebatilisha uamuzi wake wa kubadili mfumo wa upangaji wa madaraja ya ufaulu kwa mitihani ya kidato cha nne kama ilivyotolewa awali kwa kurudisha daraja sifuri.

Kutokana na uamuzi huo, sasa daraja la tano lililotangazwa wiki iliyopita kuchukua nafasi ya daraja sifuri sasa limefutwa.

Uamuzi huo umetolewa siku nne baada ya wizara hiyo kupitia kwa Katibu Mkuu wake, Profesa Sifuni Mchome, kutangaza kuwa serikali imeamua kubadilisha mfumo wa kupanga alama na madaraja ya ufaulu.

Uamuzi wa kushusha alama za ufaulu ulipokewa kwa hisia tofauti na wadau wa elimu nchini ambao walikosoa mfumo huo kwa kueleza kuwa unaipeleka kaburini sekta ya elimu ya Tanzania.

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo akizungumza na NIPASHE jana kwa njia ya simu kutoka Dodoma, alisema baada ya kutafakari serikali imeamua kuondoa daraja la tano kama ilivyokuwa imetangaza awali na kurejesha daraja sifuri.

“Kwanza niwaombe radhi Watanzania kwa mkanganyiko huo uliojitokeza ambao ni jambo moja tu limewachanganya, lakini walio wengi wanapongeza mfumo huu wa madaraja, tulichokuja kuharibu ni ‘statement’ ya neno division five,” alisema.

Monday, November 04, 2013

GLOBAL EDUCATION LINK YAZINDUA MIKOPO KWA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU NJE YA NCHI

Mkurugenzi wa Elimu ya juu, Wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi, Profesa Sylvia Temu ambaye alikuwa mgeni rasmi aliyemwakilisha Waziri wa Elimu na mafunzo ya Ufundi akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi wa mpango wa utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wanaosoma vyuo vya nje ya nchi uliofanyika jana katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Kaimu Katibu mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania, Profesa Magishi Nkwabi Mgasa akiwapongeza kampuni ya Global Education Link kwa kushirikiana na Benki ya Afrika (BOA) kwa kuweza kubuni njia itakayowawezesha wanafunzi wengi waliokuwa wanapenda kwenye kusoma nje ya nchi ila wanakosa pesa. Vile vile aliwaomba wanafunzi kuacha kukurupukia vyuo vya nje bila kutambua kama vinatambulika Tanzania ama lah ili kuwaepushia usumbufu.  Uzinduzi huo ulifanyika jana katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

RAIS KIKWETE NAYE ANAFUATILIWA NA MAREKANI?

kikwete_2e5c8.jpg
NA MWANDISHI WETU
HATUA ya Marekani kudaiwa kufuatilia mawasiliano ya viongozi wa nchi washirika wake wa karibu, sasa ni wazi imeiacha Tanzania katika wingu la shaka, kama viongozi wake nao wanafuatiliwa kwa namna ile ile inayoelezwa na viongozi wa Ulaya. Shaka hiyo inatokana na urafiki wa muda mrefu uliopo kati ya Tanzania na Marekani, ambapo kwa nyakati tofauti, marais watatu wa taifa hilo kubwa duniani wamepata kuzuru nchini.
Kauli tofauti zilizotolewa ndani ya wiki hii na majasusi wa mataifa makubwa duniani, ikiwemo Marekani na Uingereza, wakati wakizungumzia madai ya Marekani kufuatilia mawasiliano ya Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel, kwamba nchi zote duniani zinachunguzana, ndiyo ambayo baadhi ya wafuatiliaji wa mambo wanadai kuwa Tanzania bila shaka haiwezi kukwepa kufuatiliwa.


Mbali na hiyo, kauli ambayo imepata kutolewa na mfanyakazi wa zamani wa shirika la NSA, Edward Snowden, kwamba ujasusi huo wa Marekani haufanywi dhidi ya watuhumiwa wa ujasusi na wakazi wa nchi zenye ugomvi na Marekani tu, bali hata marafiki na waitifaki wa karibu kabisa na nchi hiyo, ndiyo ambayo inajenga mazingira ya Tanzania nayo kuwemo kwenye orodha hiyo ya kufuatiliwa.
Marais watatu wa Marekani, kwa nyakati tofauti wamepata kuzuru nchini. Maraisi hao ni pamoja na Bill Clinton, George W. Bush na Barack Obama, ambaye alitembelea nchini mwezi Julai, mwaka huu.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...