Thursday, October 03, 2013

MASHINE ZA TRA ZAZUA BALAA.... MBEYA WAGOMA KUZINUNUA, VURUGU ZAZUKA

9161303_orig_67cda.jpg

Mabomu ya machozi yalipigwa ili kuzuia wafanyabiashara wasilete vurugu

7024725_orig_b85b7.jpg

Maduka yakiwa yamefungwa

2503579_orig_f146a.jpg

Wafanyabiashara hao walichoma matairi ili kuwazuia polisi wasiweze kuwafikia

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI OKTOBA 03, 2013

DSC 0011 c3260
DSC 0012 8e34e

LIGI YA MABINGWA WA ULAYA

ulaya_88499.jpg
CSKA Moskva 3 - 2 Viktoria Plzeň
Shakhtar Donetsk 1 - 1 Manchester United
Bayer Leverkusen 2 - 1 Real Sociedad
Juventus 2 - 2 Galatasaray
Real Madrid 4 - 0 København
PSG 3 - 0 Benfica
Anderlecht 0 - 3 Olympiakos Piraeus
Manchester City 1 - 3 Bayern München

KAULI YA CHADEMA KUHUSU KUFUNGIWA KWA MAGAZETI.

chadema-logo-i2 6aded
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO Idara ya Habari ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), tangu ilivyopokea kwa masikitiko na mshituko mkubwa taarifa za Serikali ya CCM, kufungia magazeti ya Mwananchi na Mtanzania, imeendelea kufuatilia kwa ukaribu hatua zinazochukuliwa na kauli mbalimbali zinazotolewa na pande zote mbili, serikali na wadau wa uhuru wa habari na vyombo vya habari. 
Ni wazi bila shaka yoyote kuwa kwa mara nyingine tena, serikali hii, imeendelea kutumia sheria mbaya, kutumia madaraka vibaya kufanya uamuzi mbaya, kila inapokosa hoja na uwezo wa kukabiliana na sauti mbadala au maoni kinzani.
Suala hili limekuwa dhahiri zaidi baada ya Serikali kuamua hata kuanza kuingilia uhuru wa habari na maoni kwenye mitandao ya kompyuta (on line) na pia kutishia kulifungia Gazeti la Rai, linalotolewa na Kampuni ya New Habari (2006) Limited, kwa sababu limeanza kuchapiswa kila siku.
Wakati wamiliki wa gazeti hilo wametoa ushahidi unaotokana na nyaraka za serikali hiyo hiyo iliyotoa idhini kwa chombo hicho kuchapishwa kila siku, Serikali yenyewe kwa upande wake imetoa utetezi wa ajabu juu ya tishio lake hilo ikijitetea kuwa kibali hicho kilitolewa kwa Kampuni ya Habari Corporation iliyouza hisa zake kwa Kampuni ya New Habari (2006) Limited.
Katika hili serikali inajichanganya. Hii ni dalili ya wazi kwamba uamuzi wake huo ni mwendelezo wa maamuzi ya kibabe, yasiyofanywa kwa masilahi ya Watanzania, ndiyo maana yanaanza kuipatia tabu jinsi ya kujibu na kujenga hoja za kutetea uovu wake.
CHADEMA, inapinga na itaendelea kupinga kwa kauli na vitendo, hatua hii ya serikali yenye lengo ovu dhidi ya umma wa Watanzania.

Wednesday, October 02, 2013

ZITTO KABWE AMJIBU NAY WA MITEGO...!!!

Rita Paulsen aka Madam Rita wa Bongo Star Search na Walter Chilambo tayari wameshazijibu Salamu za Nay wa Mitego na jana ilikuwa zamu ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe

Kwake mbunge huyo, Nay ni msanii wa pili wa Hip Hop anayemkubali zaidi Tanzania baada ya Roma na kwamba anakiheshimu kile alichokisema kwenye wimbo huo kwakuwa ni kazi ya sanaa.

Tazama tweets hizi.


CarolNdosi @CarolNdosi
I wonder if @zittokabwe  ever listens to hip hop..local or international..



@CarolNdosi: I wonder if @zittokabwe ever listens to hip hop..local or international..” I do. Roma is my favourite followed by Ney

VYOMBO VYA USALAMA VIKOMESHE UHALIFU, UMAFIA TANZANIA

Meno-ya-tembo_a1920.jpg
Na Daniel Mbega
UHALIFU nchini Tanzania umekuwepo kwa miaka mingi, lakini katika miaka ya karibuni umeonekana kushika kasi kuliko ilivyowahi kutokea, kiasi cha kutishia amani kwa Watanzania kuhusu usalama wa maisha na mali zao.
Kati ya Januari 2005 hadi Januari 2006 kulikuwepo na matukio ya uhalifu na ujambazi wa kutumia silaha ambapo kiasi cha Shs. 16,782,172,419 kiliporwa katika benki kadhaa za maduka ya kubadilishia fedha nchini.
Takwimu zinaeleza kwamba jumla ya wahalifu 46, wakiwemo raia 12 wa Kenya, walikamatwa katika kipindi hicho wakihusishwa na matukio mbalimbali ya uhalifu.


Baada ya hapo ikafuatia kasheshe kubwa ndani ya Jeshi la Polisi, sekeseke ambalo lilifanya iibuliwe orodha ya maofisa 20 wa jeshi hilo ambao wanashirikiana na majambazi katika wizi huo.
Lakini wakati huo zilikuja taarifa mfululizo zikiwatuhumu askari kadhaa ndani ya jeshi hilo ambao wanadaiwa kujihusisha na vitendo vya uhalifu, huku wakiwa wamechuma mali nyingi ambazo haijulikani namna walivyozipata kulinganisha na mishahara yao.
Kama nilivyotangulia kusema, vitendo vya uhalifu hapa nchini vimekuwepo kwa miaka mingi, na kwa kumbukumbu zangu vitendo hivi vilianza kushika kasi mwanzoni mwa miaka ya 1980.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO OKTOBA 02, 2013

DSC 0004 b425a

DSC 0002 b7cb1

BAADA YA KUYAFUNGIA MAGAZETI YA MWANANCHI NAMTANZANIA, SERIKALI SASA YAINYOOSHEA KIDOLE GAZETI LA RAI.

SERIKALI imeitaka kampuni ya New Habari 2006, kuacha kuchapisha gazeti la Rai kila siku na kampuni ya Mwananchi kuacha kuchapisha gazeti la Mwananchi kwenye mtandao.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari Malelezo, Assah Mwamebene, alitoa onyo hilo ofisini kwake jana na kuongeza kuwa ameziandikia barua kampuni hizo, zijieleze ni kwanini zinafanya hivyo.
Tumeona gazeti la Mwananchi baada ya kufungiwa, limeendelea kuchapishwa kwenye mtandano wa intaneti kinyume na amri iliyotolewa. Vivyo hivyo kwa Rai ambayo ilikuwa ikichapishwa mara moja kwa wiki, imeanza kutoka kila siku, tunawataka warejee ratiba yao,” alisema.
Alisema endapo vyombo hivyo havitatekeleza agizo hilo na kujieleza katika ofisi yao ifikapo kesho, Serikali italazimika kuchukua hatua kali zaidi ikiwa ni pamoja na kuongeza adhabu, ikiwemo kufungia kwa muda usiojulikana na kufutiwa usajili wake.
“Umma ufahamu kuwa Serikali haikukurupuka kufungia magazeti hayo, uamuzi ulifanywa baada ya kufuata taratibu zote za msingi ikiwemo kuwasikiliza wahusika.

TAMKO LA GAZETI LA MWANANCHI BAADA YA KUFUNGIWA KUCHAPISHA HABARI KWA NJIA YA MTANDAO

Tunasikitika kuwaarifu kuwa kutokana na sababu zisizozuilika, tutashindwa kuendelea kuwaletea habari mpya kupitia tovuti yetu (www.mwananchi.co.tz) na mitandao ya kijamii ya Mwananchi kwa wakati wote ambapo uzalishaji wa gazeti la Mwananchi utakuwa umesitishwa.

Tunasikitika kwa usumbufu wowote utakaosababishwa na hali hii na tunatumaini mtaendelea kuwa nasi wakati wa kipindi 
 hiki kigumu cha mpito. Tunatarajia kurejea rasmi hewani na habari moto moto wiki ijayo, Ijumaa, tarehe 11 October.

Tunawakaribisha muendelee kusoma habari zetu za zamani (archives) kwenye tovuti ya Mwananchi na kurasa zetu za Facebook na Twitter ili mzidi kuhabarika.

Pia tunawakaribisha mtembelee tovuti zetu za www.thecitizen.co.tz na www.mwanaspoti.co.tz ambazo zitaendelea kufanya kazi kwa ufanisi, zikiwaletea habari za uhakika na kuaminika kipindi hiki ambapo Mwananchi imefungiwa.

Ahsanteni,

Wahariri.

WEMA AMWAGA MACHOZI MARA BAADA YA MAGAZETI KUMWANDIKA KUWA AMEHUKUMIWA KUNYONGWA NCHINI CHINA


C.E.O wa kampuni ya Endless Fame Film maarufu kma Wema Sepetu ameonekana kuchukizwa na kitendo cha kuchafuliwa kwa jina lake katika moja ya magazeti ya udaku ya hapa nchini.
Mapema asubuhi ya leo kupitia account yake ya Instagram mwanadada Wema alitupia picha ya gazeti hilo lililo mchafulia jina kwa kumuandika kuwa "Wema Kunyongwa China Awaomba Watanzania Wamuombee".Pia dakika chache zilizopita kupitia account yake hiyohiyo ya Instagram wema amefunguka zaidi kwa kitendo hicho cha kuchafuliwa jina na kuandika hivi ... 

ANGALIA VIDEO YA MCHINA ALIYEOTESHWA PUA KWENYE PAJI LA USO ILI IKIKUA IWEKWE BAADA YA PUA HALISI KUHARIBIKA.


Mchina aoteshwa pua nyingine kwenye paji lake la uso. Mchina huyo ambaye anatumia jina moja tu la Xiaolian, alipata matibabu ya kuunda pua ambayo itakaa badala ya pua yake halisi ambayo iliathirika na kuharibika.
Taratibu zilifanyika katika hospitali iliyoko Fuzhou huko Fujian
Mwanaume huyo mwenye miaka 22 aliharibu pua yake kwenye ajali ya gari Agosti 2012 lakini alishindwa kupata matibabu. 
Matokeo yake  pua yake ikaathirika mpaka wale madaktari wakashindwa kuirekebisha.
Hawakuwa na jinsi nyingine yeyote ila kumuotesha pua nyingine alafu kuiondoa baadae ili iwekwe pale ambapo pua halisi iliharibiwa.

Pua hiyo ilitengenezwa kwa kuweka tissue expander za ngozi kwenye paji la uso la Xiaolian.Ilikatwa kwenye shepu ya pua na ikawa imehimarishwa na cartilage iliyotolewa kwenye mbavu zake. Madaktari hao wa oparesheni wamesema kuwa pua hiyo imekua vizuri na oparesheni ya transplant itafanyika hivi karibuni

Ila mh! Kweli hii nose job! Mchina ana pua nyingine kwenye paji la uso kuireplace pua halisi iliyoharibika kwenye ajali ya gari....!!

KENYA - BILA USALAMA SOMALIA, HATUTOKI

President-Uhuru-Kenyatta3_9e43d.jpg
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametangaza kuwa majeshi ya Kenya yataendelea kukaa Somalia hadi usalama utakapoimarishwa katika nchi hiyo iliyokumbwa na vita vya miaka mingi.
Rais Kenyatta amesema kuwa nchi yake haitashurutishwa na magaidi walioteka jengo la maduka la Westgate kwa siku 4.
Rais Kenyatta alihutubia umati uliokusanyika kwa maombi ya pamoja ya dini mbali mbali, kwa ajili ya watu 67 waliouawa katika shambulio la Westgate.
Shambulio hilo ndio baya zaidi kuwahi kutokea nchini Kneya tangu majeshi yake yaingie nchini Somalia mwaka wa 2011.
''Hawa wauaji waliokuja kutenda ukatili wao ulio na woga hapa nchini kwetu, walikuwa wanadai kuwa wanafanya hivyo kwasababu majeshi ya Kenya yapo nchini Somalia. Nataka niwaeleze bayana kuwa, majeshi yetu yatakaa huko hadi kuwepo amani katika nchi hiyo.''

PAPA JOHN PAUL KUTANGAZWA MTAKATIFU APRILI MWAKANI

zzzzzzzzzzzzpope_25f2f.jpg
Papa John Paul II na John XXIII wanatarajiwa kutangazwa watakatifu Aprili 27 mwakani, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkuu wa sasa wa kanisa Katoliki, Papa Francis.
Taarifa ya uamuzi huo imetolewa leo kwenye mkutano wa makadinali unaoendelea mjini Vatican, ikiwa ni hatua mihimu ya kuthibitisha tangazo lake la Julai mwaka huu kwamba atawapa heshima viongozi hao wawili wa juu wa Kanisa waliopita katika karne ya 20.
Katika taarifa iliyonakiliwa kutoka kwenye gazeti la mtandaoni la Daily Mail, alisema wakuu hao wa Kanisa Katoliki duniani ambao kwa sasa ni marehemu waliweza kutumia karama zao kwa uamunifu na kuonyesha matendo makuu.
Wachambuzi wa masuala ya Kanisa hilo alieleza kwamba inaonekana umuzi huo ni wa makusudi ikiwa ni hatua ya kujaribu kuliunganisha kanisa hilo ambalo lina mkanganyiko kwa sasa.
Kila mmoja ana watu wanaomuunga mkono na wanaompinga, ambapo kwa sasa Francis anaonekana kuungwa mkono na wote wa pande zote mbili hivyo kuwa kichocheo cha kuunganisha na kufuta makovu yaliyolikumba Kanisa hilo kwa miaka ya hivi karibuni.

Tuesday, October 01, 2013

WAKAZI DODOMA WAANDAMANA KUPINGA BOMOABOMOA YA CDA




 Maelfu ya Wananchi wa Kata ya kikuyu kusini wakiandamana katika mitaa ya mji wa Dodoma kwa ajili ya kupinga kubomolewa na mamraka ya ustawishaji makao makuu  [CDA] wanaotarajia kubomoa nyumba, mapagale na misingi ya wakazi hao.

  Maelfu ya Wananchi wa Kata ya kikuyu kusini wakiandamana katika mitaa ya mji wa Dodoma kwa ajili ya kupinga kubomolewa na mamraka ya ustawishaji makao makuu  [CDA] wanaotarajia kubomoa nyumba, mapagale na misingi ya wakazi hao.

JAMAA APEWA ADHABU YA KUOSHA GARI LA ZIMA MOTO MARA BAADA YA KUWADANGANYA KWA KUWAPIGIA SIMU

Mmoja wa wakazi wa Rugelele kata Rujewa wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya  DUKA MKWILA[20]ni miongoni mwa wananchi waliopiga simu za uongo katika kikosi cha zimamoto mkoa wa mbeya akiwa amepewa adahabu ya kuosha gari la zimomoto
Hata hivyo DUKA alikiri kutenda kosa na kuomba msamaha kwa jeshi hilo ambapo aliachiwa huru na kisha kurejea kwao huku akijutia kosa alilolifanya na kuahidi kutorudia tena.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...