Wednesday, October 02, 2013

ZITTO KABWE AMJIBU NAY WA MITEGO...!!!

Rita Paulsen aka Madam Rita wa Bongo Star Search na Walter Chilambo tayari wameshazijibu Salamu za Nay wa Mitego na jana ilikuwa zamu ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe

Kwake mbunge huyo, Nay ni msanii wa pili wa Hip Hop anayemkubali zaidi Tanzania baada ya Roma na kwamba anakiheshimu kile alichokisema kwenye wimbo huo kwakuwa ni kazi ya sanaa.

Tazama tweets hizi.


CarolNdosi @CarolNdosi
I wonder if @zittokabwe  ever listens to hip hop..local or international..



@CarolNdosi: I wonder if @zittokabwe ever listens to hip hop..local or international..” I do. Roma is my favourite followed by Ney

VYOMBO VYA USALAMA VIKOMESHE UHALIFU, UMAFIA TANZANIA

Meno-ya-tembo_a1920.jpg
Na Daniel Mbega
UHALIFU nchini Tanzania umekuwepo kwa miaka mingi, lakini katika miaka ya karibuni umeonekana kushika kasi kuliko ilivyowahi kutokea, kiasi cha kutishia amani kwa Watanzania kuhusu usalama wa maisha na mali zao.
Kati ya Januari 2005 hadi Januari 2006 kulikuwepo na matukio ya uhalifu na ujambazi wa kutumia silaha ambapo kiasi cha Shs. 16,782,172,419 kiliporwa katika benki kadhaa za maduka ya kubadilishia fedha nchini.
Takwimu zinaeleza kwamba jumla ya wahalifu 46, wakiwemo raia 12 wa Kenya, walikamatwa katika kipindi hicho wakihusishwa na matukio mbalimbali ya uhalifu.


Baada ya hapo ikafuatia kasheshe kubwa ndani ya Jeshi la Polisi, sekeseke ambalo lilifanya iibuliwe orodha ya maofisa 20 wa jeshi hilo ambao wanashirikiana na majambazi katika wizi huo.
Lakini wakati huo zilikuja taarifa mfululizo zikiwatuhumu askari kadhaa ndani ya jeshi hilo ambao wanadaiwa kujihusisha na vitendo vya uhalifu, huku wakiwa wamechuma mali nyingi ambazo haijulikani namna walivyozipata kulinganisha na mishahara yao.
Kama nilivyotangulia kusema, vitendo vya uhalifu hapa nchini vimekuwepo kwa miaka mingi, na kwa kumbukumbu zangu vitendo hivi vilianza kushika kasi mwanzoni mwa miaka ya 1980.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO OKTOBA 02, 2013

DSC 0004 b425a

DSC 0002 b7cb1

BAADA YA KUYAFUNGIA MAGAZETI YA MWANANCHI NAMTANZANIA, SERIKALI SASA YAINYOOSHEA KIDOLE GAZETI LA RAI.

SERIKALI imeitaka kampuni ya New Habari 2006, kuacha kuchapisha gazeti la Rai kila siku na kampuni ya Mwananchi kuacha kuchapisha gazeti la Mwananchi kwenye mtandao.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari Malelezo, Assah Mwamebene, alitoa onyo hilo ofisini kwake jana na kuongeza kuwa ameziandikia barua kampuni hizo, zijieleze ni kwanini zinafanya hivyo.
Tumeona gazeti la Mwananchi baada ya kufungiwa, limeendelea kuchapishwa kwenye mtandano wa intaneti kinyume na amri iliyotolewa. Vivyo hivyo kwa Rai ambayo ilikuwa ikichapishwa mara moja kwa wiki, imeanza kutoka kila siku, tunawataka warejee ratiba yao,” alisema.
Alisema endapo vyombo hivyo havitatekeleza agizo hilo na kujieleza katika ofisi yao ifikapo kesho, Serikali italazimika kuchukua hatua kali zaidi ikiwa ni pamoja na kuongeza adhabu, ikiwemo kufungia kwa muda usiojulikana na kufutiwa usajili wake.
“Umma ufahamu kuwa Serikali haikukurupuka kufungia magazeti hayo, uamuzi ulifanywa baada ya kufuata taratibu zote za msingi ikiwemo kuwasikiliza wahusika.

TAMKO LA GAZETI LA MWANANCHI BAADA YA KUFUNGIWA KUCHAPISHA HABARI KWA NJIA YA MTANDAO

Tunasikitika kuwaarifu kuwa kutokana na sababu zisizozuilika, tutashindwa kuendelea kuwaletea habari mpya kupitia tovuti yetu (www.mwananchi.co.tz) na mitandao ya kijamii ya Mwananchi kwa wakati wote ambapo uzalishaji wa gazeti la Mwananchi utakuwa umesitishwa.

Tunasikitika kwa usumbufu wowote utakaosababishwa na hali hii na tunatumaini mtaendelea kuwa nasi wakati wa kipindi 
 hiki kigumu cha mpito. Tunatarajia kurejea rasmi hewani na habari moto moto wiki ijayo, Ijumaa, tarehe 11 October.

Tunawakaribisha muendelee kusoma habari zetu za zamani (archives) kwenye tovuti ya Mwananchi na kurasa zetu za Facebook na Twitter ili mzidi kuhabarika.

Pia tunawakaribisha mtembelee tovuti zetu za www.thecitizen.co.tz na www.mwanaspoti.co.tz ambazo zitaendelea kufanya kazi kwa ufanisi, zikiwaletea habari za uhakika na kuaminika kipindi hiki ambapo Mwananchi imefungiwa.

Ahsanteni,

Wahariri.

WEMA AMWAGA MACHOZI MARA BAADA YA MAGAZETI KUMWANDIKA KUWA AMEHUKUMIWA KUNYONGWA NCHINI CHINA


C.E.O wa kampuni ya Endless Fame Film maarufu kma Wema Sepetu ameonekana kuchukizwa na kitendo cha kuchafuliwa kwa jina lake katika moja ya magazeti ya udaku ya hapa nchini.
Mapema asubuhi ya leo kupitia account yake ya Instagram mwanadada Wema alitupia picha ya gazeti hilo lililo mchafulia jina kwa kumuandika kuwa "Wema Kunyongwa China Awaomba Watanzania Wamuombee".Pia dakika chache zilizopita kupitia account yake hiyohiyo ya Instagram wema amefunguka zaidi kwa kitendo hicho cha kuchafuliwa jina na kuandika hivi ... 

ANGALIA VIDEO YA MCHINA ALIYEOTESHWA PUA KWENYE PAJI LA USO ILI IKIKUA IWEKWE BAADA YA PUA HALISI KUHARIBIKA.


Mchina aoteshwa pua nyingine kwenye paji lake la uso. Mchina huyo ambaye anatumia jina moja tu la Xiaolian, alipata matibabu ya kuunda pua ambayo itakaa badala ya pua yake halisi ambayo iliathirika na kuharibika.
Taratibu zilifanyika katika hospitali iliyoko Fuzhou huko Fujian
Mwanaume huyo mwenye miaka 22 aliharibu pua yake kwenye ajali ya gari Agosti 2012 lakini alishindwa kupata matibabu. 
Matokeo yake  pua yake ikaathirika mpaka wale madaktari wakashindwa kuirekebisha.
Hawakuwa na jinsi nyingine yeyote ila kumuotesha pua nyingine alafu kuiondoa baadae ili iwekwe pale ambapo pua halisi iliharibiwa.

Pua hiyo ilitengenezwa kwa kuweka tissue expander za ngozi kwenye paji la uso la Xiaolian.Ilikatwa kwenye shepu ya pua na ikawa imehimarishwa na cartilage iliyotolewa kwenye mbavu zake. Madaktari hao wa oparesheni wamesema kuwa pua hiyo imekua vizuri na oparesheni ya transplant itafanyika hivi karibuni

Ila mh! Kweli hii nose job! Mchina ana pua nyingine kwenye paji la uso kuireplace pua halisi iliyoharibika kwenye ajali ya gari....!!

KENYA - BILA USALAMA SOMALIA, HATUTOKI

President-Uhuru-Kenyatta3_9e43d.jpg
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametangaza kuwa majeshi ya Kenya yataendelea kukaa Somalia hadi usalama utakapoimarishwa katika nchi hiyo iliyokumbwa na vita vya miaka mingi.
Rais Kenyatta amesema kuwa nchi yake haitashurutishwa na magaidi walioteka jengo la maduka la Westgate kwa siku 4.
Rais Kenyatta alihutubia umati uliokusanyika kwa maombi ya pamoja ya dini mbali mbali, kwa ajili ya watu 67 waliouawa katika shambulio la Westgate.
Shambulio hilo ndio baya zaidi kuwahi kutokea nchini Kneya tangu majeshi yake yaingie nchini Somalia mwaka wa 2011.
''Hawa wauaji waliokuja kutenda ukatili wao ulio na woga hapa nchini kwetu, walikuwa wanadai kuwa wanafanya hivyo kwasababu majeshi ya Kenya yapo nchini Somalia. Nataka niwaeleze bayana kuwa, majeshi yetu yatakaa huko hadi kuwepo amani katika nchi hiyo.''

PAPA JOHN PAUL KUTANGAZWA MTAKATIFU APRILI MWAKANI

zzzzzzzzzzzzpope_25f2f.jpg
Papa John Paul II na John XXIII wanatarajiwa kutangazwa watakatifu Aprili 27 mwakani, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkuu wa sasa wa kanisa Katoliki, Papa Francis.
Taarifa ya uamuzi huo imetolewa leo kwenye mkutano wa makadinali unaoendelea mjini Vatican, ikiwa ni hatua mihimu ya kuthibitisha tangazo lake la Julai mwaka huu kwamba atawapa heshima viongozi hao wawili wa juu wa Kanisa waliopita katika karne ya 20.
Katika taarifa iliyonakiliwa kutoka kwenye gazeti la mtandaoni la Daily Mail, alisema wakuu hao wa Kanisa Katoliki duniani ambao kwa sasa ni marehemu waliweza kutumia karama zao kwa uamunifu na kuonyesha matendo makuu.
Wachambuzi wa masuala ya Kanisa hilo alieleza kwamba inaonekana umuzi huo ni wa makusudi ikiwa ni hatua ya kujaribu kuliunganisha kanisa hilo ambalo lina mkanganyiko kwa sasa.
Kila mmoja ana watu wanaomuunga mkono na wanaompinga, ambapo kwa sasa Francis anaonekana kuungwa mkono na wote wa pande zote mbili hivyo kuwa kichocheo cha kuunganisha na kufuta makovu yaliyolikumba Kanisa hilo kwa miaka ya hivi karibuni.

Tuesday, October 01, 2013

WAKAZI DODOMA WAANDAMANA KUPINGA BOMOABOMOA YA CDA




 Maelfu ya Wananchi wa Kata ya kikuyu kusini wakiandamana katika mitaa ya mji wa Dodoma kwa ajili ya kupinga kubomolewa na mamraka ya ustawishaji makao makuu  [CDA] wanaotarajia kubomoa nyumba, mapagale na misingi ya wakazi hao.

  Maelfu ya Wananchi wa Kata ya kikuyu kusini wakiandamana katika mitaa ya mji wa Dodoma kwa ajili ya kupinga kubomolewa na mamraka ya ustawishaji makao makuu  [CDA] wanaotarajia kubomoa nyumba, mapagale na misingi ya wakazi hao.

JAMAA APEWA ADHABU YA KUOSHA GARI LA ZIMA MOTO MARA BAADA YA KUWADANGANYA KWA KUWAPIGIA SIMU

Mmoja wa wakazi wa Rugelele kata Rujewa wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya  DUKA MKWILA[20]ni miongoni mwa wananchi waliopiga simu za uongo katika kikosi cha zimamoto mkoa wa mbeya akiwa amepewa adahabu ya kuosha gari la zimomoto
Hata hivyo DUKA alikiri kutenda kosa na kuomba msamaha kwa jeshi hilo ambapo aliachiwa huru na kisha kurejea kwao huku akijutia kosa alilolifanya na kuahidi kutorudia tena.

VIWANGO VYA NAULI KUTOKA UBUNGO HADI MIKOA MINGINE

MAGAZETI YA LEO JUMANNE OKTOBA 1, 2013

DSC 0051 4272d
DSC 0052 dc9bc

MKENYA ALIYEDAIWA KUMTEKA DK. ULIMBOKWA ATOZWA FAINI 1,000/-

fain_269e9.jpg
Mkenya Joshua Mulundi aliachiwa huru baada ya kulipa faini ya Sh1,000 kwa kupatikana na hatia ya kuidanganya polisi kuwa alihusika kumteka na kumjeruhi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilimhukumu kifungo cha miezi sita jela au kulipa faini hiyo. Mulundi alilipiwa faini hiyo na Mwandishi wa Habari wa Redio Times, Chipangula Nandule.
Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu Mkazi, Aloyce Katemana baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Tumaini Kweka kusoma maelezo ya awali na mshtakiwa huyo kukiri alitoa taarifa ya uongo kwa polisi kuhusu tukio hilo.
Kabla ya hukumu hiyo, Mulundi aliomba Mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa hilo lilikuwa kosa lake la kwanza. Pia alijitetea kuwa Juni 27, 2012 akiwa Arusha alitekwa na kupelekwa Dar es Salaam ambako alikuwa hana mwenyeji wala hakuwahi kufika.
Alisema kutokana na kutekwa huko alichanginyikiwa hivyo kukubali chochote alichoambiwa afanye kwa kuwa aliyemteka alikuwa na silaha na alimwelekeza mambo ya kuzungumza.
"Mheshimiwa kwa ajili ya vitisho hivyo, nilikwenda Kawe katika Kanisa la Ufufuo na Uzima lililoko kwenye eneo la Tanganyika Packers, mbele ya Mchungaji Joseph Malwa Kiliba na kuungama kuwa ni miongoni mwa watu waliomtesa Dk Ulimboka katika Msitu wa Pande," alisema Mulundi na kuongeza:
"Siwalaumu Serikali, upande wa mashtaka wala polisi kwa kitendo cha kuniweka gerezani kwa muda mrefu, najilaumu mimi mwenyewe."
Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, Kweka aliiambia Mahakama kuwa hana kumbukumbu za uhalifu za mshtakiwa lakini aliomba apewe adhabu kali kutokana na mazingira ya tukio hilo.
Akitoa hukumu, Hakimu Katema alisema alifikia uamuzi huo kwa kuzingatia maombi ya mshtakiwa ya kupunguziwa adhabu.

VIJANA WANAVYOSAJILIWA KUPIGANIA AL SHABAAB

alshabaab-soldiers-in-training_495033_e5a43.png
Uchunguzi wa BBC umefichua ambavyo vijana husajiliwa kujiunga na kundi la kigaidi la Al Shabaab katika pwani ya Kenya.
Al Shabaab limekiri kufanya shambulizi la kigaidi dhidi ya jengo la Westgate ambapo zaidi ya watu sitini waliuawa na mamia kujeruhiwa.
Uchunguzi wa BBC, unatizama ambavyo vijana wanafunzwa itikadi kali za dini katika kuwaandaa, kujiunga na kundi la Al Shabaab.
Vikao vya kuwasajili Vijana hao huanza na viongozi wa dini kutoa hotuba kwa vijana waisilamu wengi ambao wamesilimu.
Uchunguzi huo umebaini kuwa vijana hao ambao wanakuwa wamejitolea kupigania kile wanachosema ni dini, hupelekwa katika maeneo ya vijijini katika fuo za bahari kama sehemu ya kwanza ya safari yao kwenda Somalia.
Mmoja wa wahubiri hao kwa jina Makaburi, ametetea shambulizi lililofanywa dhidi ya Jumba la Westgate na kuwaua watu zaidi ya sitini akisema kwamba ilikuwa hatua sahihi.
Kulingana naye, ilikuwa sawa kwa sababu majeshi ya kigeni yanapigana nchini Somalia.
Jeshi la Kenya lilipeleka wanajeshi wake nchini Somalia,miaka miwili iliopita kupambana na kundi la Al Shabaab.
Wakati huohuo, maombi yanafanyika katika sehemu mbali mbali mjini Naiobi kuwaombea waathiriwa wa shambulizi hilo

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...