Wednesday, August 28, 2013

KODI YA SIMU BADO KIMBEMBE...!!!


                       Waziri wa Fedha, William Mgimwa

Wakati wananchi wakiwa hawajajua majaliwa yao juu maamuzi ya serikali kuhusu kilio chao dhidi ya kodi ya simu ya Sh. 1,000 kwa mwezi iliyopitishwa na Bunge la Bajeti ya mwaka 2013/14, kuna habari kwamba mzigo huo sasa unaweza kuhamishiwa kwenye ununuaji wa vocha.
Hofu hii inajengeka wakati Mkutano wa Bunge wa 11 ambao unatarajiwa kujadili suala la kodi ya simu ukianza mjini Dodoma huku kukiwa na habari kwamba serikali inatafakari uwezekano wa kupandisha ushuru kwenye vocha (excise duty) kwa asilimia 5.5.
Kama maamuzi hayo yatafikiwa ushuru huo utapaa hadi kufikia asilimia 20 kutoka asilimia 14.5 wa sasa.
Mpango huo wa serikali ni moja ya mikakati yake ya kuziba pengo la kiasi cha Sh. bilioni 178.5 kama kodi ya simu itaondolewa kwani ilikuwa imekadiriwa kuwa ingeingiza mapato ya kiwango hicho kwa mwaka wa fedha wa 2013/14.
 
Kama ushuru huo utaongezwa na kukubaliwa na wabunge, basi Tanzania itakuwa na ushuru mkubwa kwenye simu kuliko viwango vinavyotozwa na nchi zingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

ALIYEGEUZWA MTUMWA WA NGONO AANIKA 'UCHAFU' WA KANALI GHADAFI....!!!


Kanali Muammar Gaddafi aliamuru kutekwa kwa wasichana wa shule ambao baadaye walishikiliwa kama watumwa wa ngono kwenye eneo lake, kwa mujibu wa kitabu kuhusiana na dikteta huyo.

Msichana mmoja, aliyetajwa kama Soraya, alitekwa nyara wakati akiwa na umri wa miaka 15 na kushikiliwa kwa miaka mitano katika sehemu ya chini kwenye ngome yake yenye urefu wa maili sita nje kidogo ya mji wa Tripoli.

Anasema alibakwa ovyo-ovyo, kupigwa na kudhalilishwa kwa utaratibu wa takribani kila siku na kushuhudia udhalilishaji unaofanana na huo kwa wasichana na wavulana wengine.

Stori yake na nyingine za wengine ambao wanasema walibakwa na dikteta huyo zinasimuliwa kwenye kitabu cha "Gaddafi's Harem: The Story Of A Young Woman And The Abuses Of Power In Libya" kilichoandikwa na mwandishi wa kimataifa wa Ufaransa Annick Cojean.

Kitabu hicho kimeshauza zaidi ya nakala 100,000 tangu kilipochapishwa nchini Ufaransa mwaka jana na tafsiri ya Kiingereza itakuwa mitaani mwezi ujao.

MADIWANI WALIOTIMULIWA BUKOBA WARUDISHWA


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa imejadili na kutolea maamuzi pamoja na mambo mengine suala la Madiwani wanane waliotangazwa kufukuzwa uanachama na Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera.

Katika maamuzi yake, Kamati Kuu imebatilisha uamuzi uliofanywa na Halmashauri Kuu CCM ya Mkoa wa Kagera Agosti 13, 2013 wa kuwafukuza uanachama Madiwani hao. Hivyo Madiwani hao wanane ni wanachama halali wa CCM.

Kamati Kuu imetoa uamuzi huo, baada ya kubaini kuwa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera haikuzingatia Katiba ya CCM ya 1977 Toleo la 2012 Ibara ya 93 (15). Ibara hiyo inasomeka kuwa moja ya kazi ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa ni:-

“Kumwachisha au kumfukuza uongozi kiongozi yeyote ambaye uteuzi wake wa mwisho unafanywa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Mkoa, isipokuwa kwa suala la kumvua uanachama au uongozi Diwani lisifanyike hadi Kamati Kuu imearifiwa na kutoa maelekezo”.

Tuesday, August 27, 2013

HII NDILO JENEZA LENYE KIYOYOZI NDANI, WACHA LILE LA MSUYA LINALOFUNGULIWA KWA RIMOTI

Hili ni sanduku ya aliyekua Mfalme wa Roma(self-appointed Roma king),Florin Cioaba aliyefariki wiki moja iliyopita kwa mshtuko wa moyo huko Uturuki. Sanduku lake lilikua na Kiyoyozi kama lionekanavyo pichani.
Hivi karibuni watanzania tulishangazwa pale tulipoona sanduku la Billionea wa Arusha ambalo lilikua likifunguliwa kwa 'Remote Control'. Nadhani sanduku hili pia litawashangaza wengi.


MAGAZETI YA LEO JUMANNE AGOSTI 27, 2013

DSC 0048 a976f
DSC 0049 e302d
DSC 0050 81f49
DSC 0051 86967

EAC KUJITOSA MZOZO WA TANZANIA, RWANDA

sezi_cbe2f.jpg
Wakati Tanzania ikisema kuwa iko tayari kukaa meza moja na jirani yake Rwanda kumaliza hali ya uhasama iliyoanza kujitokeza katika siku za hivi karibuni, Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk Richard Sezibera amesema jitihada za kidipolomasia zinafanyika kutatua tofauti hizo za kimawazo.

Bila kutaja taasisi wala wanaohusika katika jitihada hizo za kidiplomasia, Dk Sezibera aliwaambia waandishi wa habari jijini Arusha jana kuwa jitihada hizo zinafanyika kimya kimya bila kushirikisha vyombo vya habari "Migongano na tofauti za kimtazamo miongoni mwa viongozi wakuu wa nchi wanachama wa EAC ni jambo lisilo la afya kwa Jumuiya na linastahili kushughulikiwa kidiplomasia," alisema Dk Sezibera.


Akizungumza kwa tahadhari kubwa kukwepa kuingia kwa undani kuhusu suala hilo, Katibu Mkuu huyo alisema inafaa kila linalowezekana lifanyike kutatua mgongano wowote unaotokea kati ya viongozi wakuu.
Mjini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe naye alisema katika mahojiano kuwa iwapo Rwanda itaomba kukutana na Tanzania kwa ajili ya kumaliza mzozo huo Serikali itakuwa tayari kutoa ushirikiano.

TAARIFA KAMILI KUHUSU BOMU KATIKA KANISA LA KKKT DAR ES SALAAM


POLISI Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, imebaini kuwa chombo kilichodhaniwa kuwa bomu katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kijitonyama hakikuwa bomu, bali ni kifaa cha Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) cha kuchunguza anga.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleman Kova alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari, baada ya kufanya uchunguzi kwa kushirikiana TMA.
"Baada ya kupata taarifa, polisi walifika eneo la tukio na kukuta kifaa kilicho katika umbo la kasha kikining'inia kwenye transfoma karibu na Kanisa kikiwa kinawaka taa.

“Katika kasha hilo kulikuwa na maandishi ya kalamu ya wino yaliyosomeka TMA na Airport," alisema Kamanda Kova.
Alisema baada ya uchunguzi wa awali, polisi walibaini kuwa kifaa hicho si bomu na kuondoka nacho kwa uchunguzi zaidi. Mtabiri Mwandimizi wa hali ya hewa kutoka TMA, Augustino Kanemba, alisema kifaa hicho kinaitwa Radio Sound na hutumiwa na Mamlaka hiyo kufanya utafiti wa hali ya anga za juu.

DADA YAKE FREEMAN MBOWE AIKIMBIA CHADEMA NA KUJIUNGA CCM, ADAI CHADEMA HAINA JIPYA



DADA wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Grace Mbowe, amejiunga na Chama Cha Mapinduzi ( CCM) akitokea Chadema, kwa kile alichodai haoni jambo jipya katika chama hicho.

Grace amesema amehama kutokana na kuwepo propaganda zisizotekelezeka. Hata hivyo, amesisitiza kwamba kuwepo kwake katika Chadema, siyo kwa sababu ya familia.

Alikabidhi kadi hiyo jana kwenye ofisi za CCM Wilaya ya Hai. Alisema itikadi za kisiasa, zisihusishe masuala ya kifamilia, kwani upendo wao uko pale pale.

Alisema kilichomfanya kujiunga na chama hicho ni utashi wake. Alidai CHADEMA wanafanya propaganda za 



kuwadanganya wananchi.

Alisema itikadi za chama, haziwezi kuingilia masuala ya kifamilia, hivyo kwake siyo ajabu kuondoka CHADEMA, kwani kila mtu ana utashi wake wa kisiasa.

MAN U, CHELSEA HAKUNA MBABE



Beiki wa Chelsea, Ashley Cole (kushoto) akikwaana na Wyne Rooney wa Manchester United.
Mshambuliaji wa Manchester United, Wyne Rooney (kushoto)  akijaribu kupiga shuti langoni mwa Chelsea.
Mourihno na Moyes wakisalimiana kabla ya mechi hiyo.

MANCHESTER UNITED VS CHELSEA 0-0 FULL HIGHLIGHTS

Monday, August 26, 2013

WANAUME WAWILI WAAMUA KUOA MWANAMKE MMOJA ILI KUEPUSHA UGOMVI WA KUMGOMBEA


Wanaume wawili nchini Kenya wameibuka na mbinu isiyo ya kawaida ya kupata suluhu ya kupigania mwanamke ambaye wote wanampenda Wamesaini mkataba wakikubaliana kuishi nae kwa zamu.


Silvester Mwendwa ni mmoja wa wanaume hao anayeanza kwa kueleza kwa nini binafsi anamuhusudu mwanamke huyo.

Mmoja ya wa wanaume hao alisema haoni ubaya wowote kwa yeye na
mwenzake kumuoa mwanamke mmoja.

Amehoji sheria ya sasa inayoruhusu wanaume kuoa wanawake wengi na wakati huo huo kuharamisha mpango kama huo kwa kina mama.

Sylvester Mwendwa anasema wazazi wake wamekubali na mpango wake na wakotayari kumtolea mahari

MBWA AZIKWA NA MAELFU YA WATU......! APEWA HESHIMA ZOTE


dog hero

 
Unacho kiona katika picha hapo chini ni mazishi shujaa ambayo yalitolewa kwa mbwa. Jina la mbwa alikuwa akiitwa Zanjeer na yeye kuokoa maelfu ya maisha ya watu wakati wa milipuko Mumbai Serial Machi 1993. Yeye alikua na  kilo zaidi ya 3329 ya RDX kulipuka, detonatorer 600, mabomu 249 mkononi na raundi ya 6406 ya risasi kuishika kusudi watu wasilipuke.
Kusema kwaheri kwa Zanjeer baada ya yeye kupita, alizikwa kwa heshima kamili.

ANGALIA VIDEO YA MWANAFUNZI ALIYESHITAKIWA KWA KUIBA SADAKA....!!!


 
Tembelea http://jambotz8.blogspot.com/ kila siku.

MSICHANA AMEJIKUTA AKIZOMEWA NA KUCHAPWA VIBOKO BAADA YA KUVAA NGUO FUPI...!!!


Msichana mmoja ambaye jina lake halikujulika amejikukuta katika wakati mgumu baada ya kuzomewa na   kuchapwa viboko na kundi la watu katika eneo la soko la nmc jiji arusha kwa madai ya kuvaa nguo fupi hali iliyowalazimu wasamariawema kuingilia kati  na kutumia nguvu kubwa ili  kumwokoa na kumsitili kwa kumfunika na nguo zingine.

 Mwandishi wetu Halfani Lihundi  kutoka arusha alikuwapo katika sakata hilo na ametuma taarifa hii iliyosema,  watu walio shuhudia tukio hilo wamesema wamechukizwa na aina ya nguo alizizovaa msichana huyo ambazo haziendani na maadili ya Kitanzania, ndiyo maana wameamua kumwadabisha ili kukomesha tabia hiyo. Tembelea http://jambotz8.blogspot.com/ kila siku.

Kwa upande wao wanawake waliyo msitili msichana huyo kwa kumpa nguo za heshima na kumhifadhi katika Gareji ya jirani kabla ya kumkimbiza kwa gari aina ya Toyota Hiace wamesema hawaridhishwi na tabia hiyo inayowazalilisha wanawake na kuwataka wasichana kuavaa nguo za kujisitili ili kujenga heshima katika jamii.
Source ITV

AHUBIRI ZAIDI YA MASAA MATATU BILA WAUMINI...!!!

Mhubiri wa injili akitoa neno pembeni ni viti kwa ajili ya waumini japo hakuna aliyejitokeza.
...Akizidi kumwaga injili.
 ...Akielezea umuhimu wa kumtukuza bwana.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...