Saturday, August 24, 2013

KUWA WAKWANZA KUSIKILIZA NA KUDOWNLOAD WIMBO WA MSANII MPYA WA HIP HOP CHATTA RYMES KUTOKA SHY TOWN

Ujio mpya katika mziki wa kizazi kipya katika miondoko ya hiphop.. Anaitwa ISSA ALLY  a.k.a CHATTA RYMES  ni kijana mdogo mwenye uwezo wa kushangaza katika mziki Anakuja na wimbo wake mpya  aliofanya na KING DIZZO unaitwa SEMA NAO ameufanyia katika Studio  za SHY TOWN REC pande za SHINYANGA Tz


Kwa muonekano ni mdogo lakini kiuandishi ni hatari sana na anaplan ndefu ya kuhakikisha mziki unaweza kumlipa na kumfanya aendeshe maisha yake kupitia mziki na hatimae kuitangaza Tanzania kimataifa zaidi.


SUPORT YAKO NDIO ANAYOIHITAJI 



                   ARTIST: Chatta Rymes Ft King Dizzo

                   TRACK:Sema nao

                   STUDIO:Shy Town Recs

                   PRODUCER:Hance Q

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI AUGUST 24, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

CHANZO CHA MAUAJI YA BILIONEA ERASTO MSUYA HIKI HAPA


 Mbunge wa Simanjiro Ole Sendeka alipo wasili Msibani.



Mc wa Shughuli ya Mazishi alikua ni JB.



Friday, August 23, 2013

MADAM RITA: "NAY WA MITEGO HANA PESA ZA KUNILIPA HATA NIKIMFUNGULIA KESI"


                                        Madam Rita

 Mratibu wa shindano la Epic Bongo Star Search(EBSS) Rita Paulsen (Madam Rita ) ameshangazwa na taarifa zilizoenea katika vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo mitandao ya kijamii ,kuhusiana na yeye kutaka kumfungulia mashtaka msanii Nay Wa Mitego ambaye anadaiwa kumchafua (defamation) katika wimbo wake mpya unaotamba sasa (Salamu Zao). Amesema hana mpango
wa kumfungulia mashitaka kwa kuwa hatakuwa na pesa za kumlipa kwa maana itakuwa kesi ya kumchafua na inaweza kumgharimu pesa nyingi.
.
Madam Rita ameyasema hayo wakati akifanya mahojiano katika kipindi cha burudani cha The Strengo Saturday kinachorushwa na Radio Victoria fm kupitia 90.6 kilichopo Musoma, Mara. Ambapo mtangazaji wa kipindi hicho Patrick Derrick Mwankale alitaka kujua sababu kubwa ya EBSS kuhamishiwa katika kituo cha televisheni cha TBC1 ikitokea ITV na vipi kuhusiana na habari zilizopo za yeye (Madam Rita) kutaka kumfungulia Nay Wa Mitego kesi ya kumchafua .

JK AAPISHA MAKATIBU WAKUU NA NAIBU MAKATIBU WAKUU IKULU DAR ES SALAAM LEO

 Rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu Kiongozi Mhe Ombeni Sefue wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa ofisi ya Sekretariate ya Baraza la Mawaziri ambako watumishi wake wawili wameteuliwa kuwa manaibu Makatibu wakuu, ambao ni Injinia Angelina Madete (kulia kwa Rais) na Mhe. Consolata Mgimba (kushoto kwa Rais) mara baada ya kuapishwa Makatibu wakuu na Manaibu Katibu wakuu Ikulu jijini Dar es salaam leo.
 Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilal na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue katika picha ya pamoja na Makatibu wakuu na manaibu Katibu wakuu wapya mara baada ya kuapishwa Makatibu wakuu na Manaibu Katibu wakuu Ikulu jijini Dar es salaam leo.
 Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilal na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue katika picha ya pamoja na Makatibu wakuu wapya mara baada ya kuapishwa Makatibu wakuu hao na Manaibu Katibu wakuu Ikulu jijini Dar es salaam leo.

HIKI NDICHO KILICHOMPONZA LULU MPAKA FILAMU YAKE YA FOOLISH AGE KUPIGWA STOP





Bodi ya ukaguzi wa filamu na michezo ya kuigiza nchini imeipiga stop filamu ya Foolish age ya msanii wa kike mwenye mvuto Bongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ baada ya kukuta picha zilizo nje ya maadili ya Kitanzania katika filamu hiyo, filamu hiyo ambayo ilipanga kuzinduliwa mwezi huu tarehe 30 katika ukumbi wa Mlimani City inahitaji marekebisho.

Kikwazo kilichoikumba filamu hiyo ni nguo fupi zilizotumika katika waigizaji walioshiriki katika filamu hiyo ambayo inatabiriwa kufanya vizuri katika soko la filamu Bongo kama itafanikiwa kuzinduliwa na kuingia sokoni, juhudi zinafanyika kuhakikisha kuwa marekebisho yanafanyika ili kwenda na ratiba kama ilivyopangwa.

Hivi sasa baada ya urasimishaji wa filamu mamlaka na taasisi zinazohusika na masuala ya filamu zimekuwa makini na kuhakikisha kuwa filamu zinazoingia sokoni na zile zinazozinduliwa kukaguliwa kabla ya kufanyika kwa matukio hayo kama ilivyokuwa awali, kama filamu hiyo ya Foolish age itashindwa vigezo vya madaraja yanayotolewa na Bodi hiyo haitaonyeshwa.

Lulu ndio mwigizaji bora wa kike kwa mwaka 2013 kupitia tamasha la filamu la kimataifa la ZIFF katika kipengere cha tuzo za Bongo movie kilichopewa jina la Zuku Bongo movie Awards zilizotolewa katika ukumbi wa Ngome Kongwe.

TFF: YANGA WAMEONGEZA ADHABU YA MRISHO NGASSA

 
Mrisho Ngassa.
Na Khatimu Naheka
IMEFAHAMIKA kuwa Klabu ya Yanga, ndiyo iliyochangia ukubwa wa adhabu aliyopewa kiungo wake mshambuliaji Mrisho Ngassa, Championi Ijumaa limebaini.
Taarifa hiyo inakuja wakati ambao Ngassa amefungiwa kucheza mechi sita za mashindano pamoja na kuilipa Simba jumla ya shilingi milioni 45, sababu kubwa ikiwa ni kusaini mikataba miwili, ule wa Yanga na ule wa Simba.

Boniface Wambura ambaye ni Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ameliambia Championi Ijumaa kuwa, adhabu ya kufungiwa michezo sita kwa Ngassa imewekwa maalum, kutokana na Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji kutaka mchezaji huyo apate uchungu wa makosa aliyoyafanya na siyo kutegemea kulipiwa na klabu.
Wambura alisema adhabu hiyo imetokana na kasumba ya klabu mbalimbali ambazo zimekuwa zikiamua kulipa faini wanazokatwa wachezaji wao kwa makosa mbalimbali, maamuzi ambayo yanasababisha wachezaji kurudia makosa hayo.

SHAHIDI KESI YA WEMA AGEUKA ‘BUBU’ GHAFLA

KESI inayomkabili staa wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu ya kudaiwa kumtukana matusi ya nguoni na kumpiga vibao meneja wa hoteli, Goodluck Kayumbu ilizua kituko baada ya shahidi kugeuka ‘bubu’ ghafla.
 
Kituko hicho kilijiri Agosti 20, mwaka huu katika Mahakama ya Mwanzo Kawe jijini Dar ambako kesi hiyo inaunguruma.
Mmoja wa makarani wa mahakama hiyo aliyeomba hifadhi ya jina lake, alisema kitu kilichoonekana kituko ni pale shahidi wa mwisho aliposhindwa kutoa ushahidi baada ya sauti kukauka ghafla.
 “Mlalamikaji alifika hapa na mashahidi wake watatu, Boniface Mati, Taito Osa na Melao  ambapo wawili walitoa ushahidi lakini Taito alishindwa kutoa ushahidi wake kwani sauti ilikata ghafla na ndipo hakimu Bernice akamuamuru anyamaze na kupanga tarehe nyingine ya kuwasikiliza mashahidi hao,” alisema karani huyo.


Mlalamikaji wa kesi hiyo, alipoombwa na paparazi wetu azungumzie ‘ ishu’ ya shahidi wake kushindwa kuzungumza alisema amekubaliana na uamuzi wa mahakama  na anasubiri tarehe ya kurudi mahakamani ambayo ni Septemba 30, mwaka huu.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA AGOSTI 23, 2013

DSC 0244 1381a
DSC 0245 1e04d

MUNGU ALINIAMURU NIJIUZULU, ASEMA PAPA BENEDICT XVI

pope_37848.jpg
Rome, Italia. Miezi sita baada ya kujiuzulu, Papa Benedict XVI, amefungua mdomo na kueleza sababu za kufikia uamuzi huo wa kushangaza.
Jana, vyombo vya habari vilimkariri Papa Mstaafu Benedict akimweleza mgeni wake kuwa aliitwa na Mungu kwa miujiza.
P.T

Kiongozi huyo ambaye alishangaza watu kwa uamuzi huo wa Februari 8, mwaka huu, hata hivyo alisema sauti ya Mungu imejibu kupitia kwa mfuasi wake, Papa Francis.
Papa Benedict alitangaza uamuzi wa kujiuzulu Februari 11, maelezo yake yalielekeza katika afya yake.
Alisema nguvu zake zilikuwa zimepungua kiasi cha kutokuweza kumudu majukumu yake ipasavyo.

ANGALIA PICHA ZA RAIS ROBERT MUGABE WA ZIMBABWE ALIPOKULA KIAPO JANA

 Rais wa Zimbabwe Robert Gabriel Mugabe akila kiapo cha kuongoza nchi hiyo kwa miaka mitano ijayo katika sherehe zilizofana sana katika Uwanja wa Taifa wa Michezo wa Harare Agosti 22, 2013
  Rais wa Zimbabwe Robert Gabriel Mugabe akivishwa shada na medali baada ya kula kiapo cha kuongoza nchi hiyo kwa miaka mitano ijayo katika sherehe zilizofana sana katika Uwanja wa Taifa wa Michezo wa Harare Agosti 22, 2013

MKENYA AKIRI KUUA NA KULA MOYO NA UBONGO WA MAREHEMU, MAREKANI


Alexander Kinyua (kushoto) na mwanamume aliyekuwa akiishi naye nyumba moja Kujoe Bonsafo Agyei-Kodie. Picha/MAKTABA



Mwanafunzi kutoka Kenya aliyekuwa akiishi Marekani amekiri kwamba alimuua mwanamume waliyekuwa wakiishi nyumba moja na kula moyo wake na ubongo wake.

MWANAFUNZI kutoka Kenya aliyekuwa akiishi Marekani amekiri kwamba alimuua mwanamume waliyekuwa wakiishi nyumba moja na kula moyo wake na ubongo wake.
Alexander Kinyua, 22, alikiri mashtaka ya mauaji ya Kujoe Bonsafo Agyei-Kodie, 37, katika jimbo la Maryland mwaka jana lakini Jaji akasema hafai kulaumiwa aliposhtakiwa Jumatatu wiki hii.

Thursday, August 22, 2013

HATIMAYE MWANAMUZIKI MKONGWE WA DANS MUHIDIN GURUMO AKUBALI YAISHE NA SASA ASTAAFU RASMI MUZIKI



Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi wa bendi ya Msondo Ngoma, Mzee Muhidin Gurumo, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uamuzi wake wa kustaafu rasmi kazi ya muziki aliyoifanya kwa muda wa miaka 53 sasa. Gurumo alitoa kauli hiyo leo katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam. Picha na Magreth Kinabo.


************************************


Na Jennifer Chamila, Maelezo.


MWANAMUZIKI mkongwe wa bendi ya Msondo Ngoma Mzee Muhidin Gurumo amestaafu rasimi kazi ya muzika alioifanya kwa muda wa miaka 53.




Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Mzee  Gurumo mwenye umri wa miaka 73 amesema ameamua kustaafu kazi hiyo kwa hiari yake mwenyewe kutokana na umri wake kuwa mkubwa.




“Muziki kwangu umekuwa kama asili yangu na kazi yangu lakini nimeamua kustaafu kutokana na umri wangu na nitabaki kuwa mshauri tu kwa mwanamuziki yeyote atakayetaka ushauri wangu,”alisema  Mzee Gurumo.

MAAFISA WA JESHI LA POLISI WAVULIWA MADARAKA NA KUSIMAMISHWA KAZI

pic 2
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt.Emmanuel Nchimbi akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu hatua  ya kuwavua madaraka Maafisa wanne wa Jeshi la polisi nchini na kumsimamisha kazi mmoja kutokana na kukiuka maadili na taratibu za Jeshi la Polisi.
……………………………………………………………….
Na Lydia Churi, MAELEZO

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewavua madaraka Maafisa wanne wa Jeshi la Polisi nchini na kumsimamisha kazi mmoja ambaye atafunguliwa mashtaka ya kijeshi kutokana na kukiuka maadili na taratibu za jeshi hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo, Waziri Nchimbi amesema hatua hiyo ni katika kuendeleza vita ya kuhakikisha kuwa jeshi la polisi linakuwa na nidhamu, linatekeleza wajibu wake wa kutenda haki na kuwalinda raia na mali zao.
Alisema amewachukulia hatua Maafisa hao baada ya kuridhia maoni ya kamati aliyoiunda kufanya uchunguzi wa matukio yaliyolalamikiwa dhidi ya askari polisi katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Morogoro na Kigoma kati ya Desemba 2012 na Mei, 2013.

FILAMU YA “FOOLISH AGE” YAIKUTANISHA LULU NA BODI YA FILAMU...!!!



 Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Bi. Joyce Fissoo akiwaonyesha wajumbe pamoja na wahusika wa Kampuni ya Proin Promotions baadhi ya maeneo muhimu ya kufanyiwa marekebisho wakati walipowasilisha filamu yao ya “Foolish Age” katika Bodi ya Filamu kwa ajili ya ukaguzi.
 Msanii wa filamu Elizabeth Michael (Lulu) akieleza jambo mbele ya Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Bi. Joyce Fissoo wakati kampuni yake ya Proin Promotions ikiwasilisha filamu yake ya “Foolish Age” kwa ajili ya ukaguzi.
 Msanii wa filamu Elizabeth Michael (Lulu) akiweka sahihi yake kuashiria amekubaliana na taratibu zote alizoelekezwa na Bodi ya Filamu wakati wa ukaguzi wa filamu yake ya “Foolish Age”.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...