Monday, August 12, 2013

MASIKINI WASTARA ALA IDD MAKABURINI...!!!

STAA wa filamu za Kibongo, Wastara Juma, yeye ameamua kula Sikukuu ya Idd El Fitr kwa staili ya tofauti na watu wengine ambapo alikula kaburini kwa mumewe, marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’.
Ishu hiyo ilijiri Ijumaa iliyopita siku ya sikukuu hiyo ambapo Wastara alitundika picha zake zikiwa zinamuonesha akiwa ameshika tama na nyingine akiwa analifanyia usafi kaburi la marehemu Sajuki lililopo katika Makaburi ya Kisutu jijini Dar.
 
Wastara alikiri kuwa aliitendea haki Sikukuu ya Idd kwani alipata nafasi ya kuzuru kaburi la mumewe na kujisikia faraja japo kimwili hayupo naye lakini kiroho wako pamoja.
“Sikukuu yangu nimeitendea haki sana kwa kwenda kuzuru kaburi la mume wangu, alhamdullilah nimefarijika sana, kimwili siko naye ila atabaki kuwa fikrani mwangu milele,” aliandika Wastara.
 
Mashabiki wake na wadau mbalimbali walimpa pole huku wengine wakimpongeza kwa hatua hiyo kwani wasanii wengine waliotumia sikukuu hiyo kujiremba, kwenda klabu na kujirusha. Sajuki alifariki dunia Januari 2, mwaka huu na kuacha mtoto mmoja wa kike.

PETE NA CHENI ANAZOVAA DIAMOND ZINA THAMANI YA SHILINGI MILIONI 24...!!!


Akihojiwa juzi kwenye kipindi cha The Trend cha NTV, mtangazaji wa show hiyo Larry Madowo aliuliza thamani ya bling alizokuwa amevaa.
“It’s a bit expensive,” alijibu Diamond huku akizishika bling hizo.

“Kama hii na hii it’s about dola 2000 something au 1,500, hii peke yake dola 2,000.”

Hata hivyo zingine alishindwa kukumbuka bei yake japo kwa kuangalia saa yenye diamond aliyokuwa nayo, pete zingine mbili za dhahabu na almasi na cheni mbili kubwa za dhahabu gharama yake kwa ujumla inaweza kufika dola 15,000 ukijumlisha na hizo zingine alizotaja gharama yake.

“Zina rates tofauti lakini ni gharama kidogo,” alisema staa huyo.

“Zina ishara? Maanake wengine wanaweza kusema ni Illuminati ama nini,” aliuliza Larry.

“Sidhani mimi navaa tu hii diamond ni jina langu, hii crown as mtu anayelead, kuna diamond nyingi hapa, hii ina alama flani kama ya batman as am flying,” alijibu Diamond.

Aidha Diamond alimtaja Usher Raymond kama msanii anayemtazama na kufuata nyayo zake zaidi.

“I don’t know men, namuona kama anajua sana anachokifanya, tangia nilipokuwa nikimfuatilia mpaka leo. Unajua wanamuziki wengi akitoka mwanamuziki flani yeye anapotea, Usher Raymond yupo. Ukiangalia vitu vyangu mimi namuiba sana. MSIKILIZE HAPO CHINI

FLAVIANA MATATA AENDELEA KUITOA KIMASOMASO TANZANIA, AFRIKA NA KIMATAIFA

Na Mwandishi Wetu
NYOTA ya mwanamitindo wa kimataifa wa Tanzania, Flaviana Matata amezidi kung’ara baada ya kuingia katika orodha ya wanamitindo saba bora kwa upande kipato.
Kwa mujibu wa gazeti la biashara la kimataifa la Forbes kwa bara la Afrika (Forbes Africa) lililotolewa hivi karibuni, Flaviana ni mrembo pekee aliyeingia katika orodha hiyo kwa wanamitindo wa Afrika Mashariki na kuzidi kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania kimataifa.
Katika orodha hiyo, mwanamitindo Maria Borges wa Angola ndiyo aliibuka namba moja na  wengine sita pamoja na Flaviana wakibaki kutoa ushindani mkubwa kwa mlimbwende huyo wa Angola.
Mbali ya Flaviana, wanamitindo wengine ambao wapo katika orodha hiyo ni Candice Swaenpoel, Katryn Kruger wote wakitokea Afrika Kusini, Ajak Deng, Grace Bol ( Sudan) na Liya Kebede wa Ethiopia,.
Flaviana Matata aliibuka katika jukwaa la kimataifa kama Miss Universe Tanzania mwaka 2007 na aliweka historia kwa kuingia 10 bora na baada ya kumaliza muda wake aliendelea na fani ya  uanamitindo Afrika kusini na baadaye alipata nafasi ya kufanya kazi Marekani na Ulaya katika makampuni makubwa ya uanamitindo ya Next Models International na sasa yuko Wilhelmina Models.
Akizungumza kutoka New York, Flaviana ameeleza kufurahia mafanikio haya hata hivyo ameongeza “Mpango wangu ni kuzidi kumweka Mungu mbele na kuhakikisha kuwa najitahidi kadri ya uwezo wangu na kuiletea sifa familia yangu na nchi yangu”.

MGOSI: NARUDI UPYA MSIMU UJAO LIGI KUU...!!!



Mussa Hassan Mgosi.
 
Na Martha Mboma
 
MSHAMBULIAJI mkongwe hapa Bongo, Mussa Hassan Mgosi, amesema amerudi upya, hivyo mashaibiki wake watarajie mambo mapya katika msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Kiungo huyo amejiunga na Mtibwa Sugar hivi karibuni akitokea JKT Ruvu. Kabla ya hapo alikuwa akiichezea timu ya DC Motema Pembe ya DR Congo ambayo alijiunga nayo akitokea Simba.

Akizungumza na Championi Jumatatu, Mgosi alisema kwa sasa anaendelea na maandalizi ya nguvu, hivyo mashabiki watarajie vitu vipya kutoka kwake.
 
“Nimerudi kivingine katika soka, hivyo mashabiki wangu watarajie mengi mazuri kutoka kwangu, ninaamini nitafanya vizuri.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU AUGUST 12, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.


SHEIKH PONDA NA UAMSHO WAHUSISHWA NA SHAMBULIO LA TINDIKALI, ZANZIBAR


Victims Kirstie Trup and Katie Gee
Gazeti la kila siku la Telegraph la hapa Uingereza linaripoti kuwa baadhi ya viongozi wa dini ya Kiislam visiwani Zanzibar wanaamini kuwa shambulio la tindikali dhidi ya mabinti wawili wa Kiingereza, Kirstie Trup na Katie Gee lilifanywa na wafuasi wa kikundi cha UAMSHO, ambacho kinataka Zanzibar ijitenge na Tanzania Bara na kisha kuanzisha sheria kali za Kiislam.

Huko nyuma kumeshatokea mashambulizi dhidi ya viongozi wa dini ya Kiislam na Kikristo, ikiwa ni pamoja na mashambulio ya tindikali na mauaji.


"Ofkoz, itakuwa kazi ya Uamsho," alinukuliwa Sheikh Fadhil Soraga, aliyeshambuliwa kwa tindikali Novemba mwaka jana, na anaamini wahusika katika tukio hilo dhidi yake walikuwa UAMSHO.



Wiki mbili zilizopita, vipeperushi vya vyenye wito mkali wa uchochezi dhidi ya Wakristo vilisambazwa sehemu mbalimbali huo Zanzibar, tukio linalohusishwa na harakati za UAMSHO.



"Siku 10 tu zilizopita, walikuwa wanasema wanaandaa kitu kikubwa. Tukio hili, ambalo Waislamu wote twapaswa kulilaani, ni kazi ya kundi hilo (UAMSHO)," alisisitiza Sheikh Soraga.

MWANAUME AFIA GESTI AKIFANYA MAPENZI NA MPENZI WAKE JIJINI DAR....!!!

MFANYABIASHARA wa sokoni Kariakoo jijini Dar ambaye pia ni mkazi wa Kigogo Flesh, Hamad Kiponda (46), amefia nyumba ya kulala wageni akiwa na mpenzi wake Latifa Saidi (25). Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi alisema tukio hilo lilitokea juzi saa saba mchana katika nyumba hiyo iitwayo Sansiro iliyoko Kiwalani kwa Gude. 

Alisema kuwa kutokana na tukio hilo, Latifa alitoa taarifa polisi kwamba mpenzi wake aliishiwa na nguvu ghafla na kuanza kutokwa povu mdomoni wakati wakifanya mapenzi. Minangi alieleza kuwa mtoa taarifa huyo aliomba msaada kwa wahudumu wa gesti hiyo, lakini Kiponda alifariki papo hapo kabla ya kupelekwa hospitali. 
Chanzo cha kifo chake bado hakijafahamika, wakati mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi zaidi huku Latifa akishikiliwa kwa kuhojiwa. 

Wakati huo huo, moto umezuka ghafla katika nyumba ya Matiku Nestori (43) mkazi wa Tuamoyo Kigamboni, yenye vyumba sita na kuteketeza vyumba vinne pamoja na mali zote zilizokuwemo ndani ambazo bado thamani yake haijajulikana. Kwa mujibu wa Kamanda Minangi tukio hilo lilitokea juzi saa nane mchana na chanzo cha moto huo inasadikiwa ni hitilafu ya umeme iliyosababisha moto kuanzia kwenye nguzo.

MAN UNITED WAIBUKA VINARA WA NGAO YA HISANI BAADA YA KUITUNGUA WIGAN KWA MAGOLI 2 KWA O KATIKA DIMBA LA WEMBLEY




 Meneja Mpya Wa Man U David Moyes akiwa ameshika ngao ya Hisani pamoja na Mchezaji wa Man U mara baada ya kukabidhiwa leo katika uwanja wa Wembley baada ya kuitungua Wigan Kwa Magoli 2 kwa 0. Hili ni Kombe la Kwanza kwa Kocha Mpya huyo wa Man United david Moyes




Wachezaji wa Man U wakishangilia Mara baada ya Kuibuka Kinara kwa kuitungua Wigan 2 kwa 0 katika Mchezo wa Kuwania Ngao ya Hisani uliofanyika Katika Dimba la Wembley Uingereza

Sunday, August 11, 2013

SERIKALI YA RWANDA IMEAPA KUTOWAFUKUZA WATANZANIA...!!!

Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Rwanda amesema kamwe hawatawafukuza Watanzania wanaoingia na kutoka nchini Rwanda kwa shughuli mbalimbali kwani tupo ndani ya shirikisho la Afrika Mashariki na hata kihistoria Rwanda haijawahi kuwa na tatizo na Tanzania.

Akizungumzia sakata la wahamiaji haramu wa Kinyarwanda kufukuzwa na serikali ya Tanzania amesema, kila nchi inayo mamlaka ya kufanya vile inafaa lakini ingekuwa vizuri Tanzania ingewasiliana na Rwanda ili kujua wataondokaje na kupokelewa vipi.

Amesisitiza, "Kwa kuwa wenzetu wameamua kufanya hivyo, tupo tayari kuwapokea wananchi wetu" Lakini pia, Waziri huyo amesema waasi wa FDRL ni kikundi cha wauaji wanaojipanga kuangamiza watu fulani nchini Rwanda hivyo wanatakiwa kupingwa kwa nguvu zote badala ya kuwatambua na kuzungumza nao kama kundi halali na lenye nia njema.

Naye Mtanzania Mohammed, amependekeza Rais Kagame na Kikwete wakutane na kufikia suluhu.Pia baadhi ya Wanyarwanda wamelalamikia kutokutendewa haki kwa kutenganishwa na wake,waume, n.k

TAARIFA RASMI YA JESHI LA POLISI KUHUSU KUPIGWA RISASI SHEKHE PONDA

 Advera Senso- SSP-Msemaji wa Jeshi la Polisi.
--
 JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI

JESHI LA POLISI TANZANIA 
DAR ES SALAAM AGOSTI 10, 2013.
 
1.  MNAMO TAREHE 10, AGOSTI ,2013 MAJIRA YA SAA 8 MCHANA, MAENEO YA SHULE YA MSINGI KIWANJA CHA NDEGE MANISPAA YA MOROGORO, KULIFANYIKA KONGAMANO LA BARAZA LA EID LILILOANDALIWA NA UMOJA WA WAHADHILI MKOANI MOROGORO. DAKIKA KUMI KABLA YA KONGAMANO HILO KUMALIZIKA  ALIFIKA SHEKHE PONDA ISSA PONDA AMBAYE ALIZUNGUMZA KWA MUDA MFUPI.
 
2. KONGAMANO HILO LILIFUNGWA  MAJIRA YA SAA 12:05 JIONI AMBAPO WATU WALIANZA KUTAWANYIKA, BAADHI YAO WAKIWA WAMEZINGIRA GARI DOGO ALILOKUWA AMEPANDA SHEKHE PONDA. BAADA YA KUTOKA KATIKA  ENEO HILO, ASKARI WA JESHI LA POLISI WALIZUIA GARI HILO KWA MBELE KWA NIA YA KUTAKA KUMKAMATA SHEKHE PONDA AMBAYE MPAKA SASA ANATUHUMIWA KWA KOSA LA KUTOA MANENO YA UCHOCHEZI SEHEMU MBALIMBALI HAPA NCHINI YENYE MLENGO WA KUSABABISHA UVUNJIVU WA AMANI.
 
3. BAAADA YA ASKARI KUTAKA KUMKAMATA, WAFUASI WAKE WALIZUIA UKAMATAJI HUO KWA KUWARUSHIA  MAWE ASKARI.  KUFUATIA PURUKUSHANI HIYO, ASKARI WALIPIGA RISASI HEWANI KAMA ONYO LA KUWATAWANYA.
 
4. KATIKA VURUGU HIZO, WAFUASI HAO WALIFANIKIWA KUMTOROSHA MTUHUMIWA.  HIVI SASA IMETHIBITIKA KUWA SHEKHE PONDA YUKO KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI AKITIBIWA JERAHA KATIKA BEGA LA MKONO WA KULIA LINALODAIWA ALILIPATA KATIKA PURUKUSHANI HIZO.
 
5. KUFUATIA TUKIO HILO, TIMU INAYOSHIRIKISHA WAJUMBE KUTOKA JUKWAA LA HAKI JINAI IKIONGOZWA NA KAMISHINA WA JESHI LA POLISI  CP ISSAYA MNGULU IMEANZA KUFANYA UCHUNGUZI WA TUKIO HILO.
 
6. AIDHA, JESHI LA POLISI LINATOA  WITO KWA  WANANCHI KUWA WATULIVU WAKATI SUALA HILI LINASHUGHULIKIWA KISHERIA.
 
Imetolewa na:-
Advera Senso- SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

HIVI NDIVYO SHEIKH ISSA PONDA ALIVYOJERUHIWA....!!!



SERIKALI YADAIWA KUMGEUKA DR ULIMBOKA YADAI AMEFICHA USHAHIDI WA KUTEKWA KWAKE


SIKU chache baada ya Mahakama ya Kisutu kumwachia mtu aliyedaiwa kumteka na kumtesa kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Steven Ulimboka, serikali imemshukia daktari huyo na kudai ndiye chanzo cha kukwama kwa dola kukamata watu waliomteka.

Jana Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Serikali (DPP), Eliazer Feleshi, alidai kuwa vyombo vya dola vimeshindwa hadi sasa kuwakamata waliohusika katika shambulio hilo kutokana na Dk. Ulimboka kukwepa kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi.

Feleshi ambaye jana aliambatana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema, katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, alidai lawama zinazosukumwa kwa Jeshi la Polisi kwa madai ya kushindwa kuwakamata waliomtendea unyama daktari huyo hazina msingi, kwa kuwa mhusika mwenyewe hajafika polisi, licha ya kuitwa mara nyingi kutoa maelezo.

Alisema kama Dk. Ulimboka angetoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi kungekuwa na mafanikio makubwa katika kuwasaka na hata kuwatia mbaroni waliohusika katika unyama huo.

“Kila mara mmekuwa mkilaumu polisi wanashindwa kukamata wahalifu lakini tutakamataje kama wenye ushahidi hawataki kutoa ushirikiano?

Kwa mfano mdogo tu ni ‘ishu’ (suala) ya Dk. Ulimboka, hadi leo hajatoa taarifa lakini polisi wanaendelea kusakamwa na kutukanwa tu,” alisema.

Hata hivyo, wakati Feleshi akitoa kauli hiyo, Dk. Ulimboka katika andiko lake alilolitoa mara tu baada ya kurejea nchini kutoka Afrika Kusini alikopelekwa kwa ajili ya matibabu, alimtaja mtu anayeaminika kuwa mfanyakazi wa Idara ya Usalama wa Taifa, Ramadhani Ighondu, kuwa ndiye aliyemteka na kumtesa.

Ulimboka akimtumia Wakili Nyaronyo Kicheere alisema Ighondu na wenzake ni mhusika mkuu katika unyama aliofanyiwa, kauli ambayo imekanushwa mara kadhaa na serikali.

Mapema wiki hii, raia wa Kenya, Joshua Mulundi, aliyekuwa akikabiliwa na tuhuma za kumteka na kumtesa Dk. Ulimboka aliachiwa na Mahakama ya Kisutu baada ya DPP Feleshi kumfutia shitaka. Hata hivyo Mulundi alikamatwa tena na sasa amefunguliwa mashitaka ya kutoa maelezo ya uongo kwa polisi.

KUTOKA KWENYE MTANDAO WA DAILYMAIL UINGEREZA:SHEIK PONDA AHUSISHWA NA KESI YA MABINTI WA UINGEREZA WALIOMWAGIWA TINDIKALI

Sheikh Ponda Issa who is suspected of inciting the attack on Kirstie Trup and Katie Gee was shot by police in Tanzania's capital last night

Sheikh Ponda Issa who is suspected of inciting the attack on Kirstie Trup and Katie Gee was shot by police in Tanzania's capital last night 


A radical Muslim preacher wanted in connection with an acid attack on two British teenagers in Zanzibar has been shot by police, it was reported.

Sheikh Issa Ponda Issa was hit in the shoulder with a tear gas canister as he tried to escape from officers after being cornered near Tanzania's capital Dar es Salaam, The Sunday Mirror said.

JAPAN KUJENGA KIWANDA CHA PIKIPIKI TANZANIA

070 6d3e9 
Serikali ya Japan imesema ina mpango kabambe wa kukuza uchumi wa Tanzania, ikiwa ni pamoja na kampuni kubwa duniani za Honda na Panasonic kujenga viwanda vitakavyokuwa matawi yake hapa nchini. (HM)

Uamuzi na msimamo wa Japan umetangazwa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda wa nchi hiyo, Toshimistu Motegi alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Jakaya Kikwete, Ikulu.

Taarifa ya Ikulu iliyosambazwa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, ilimnukuu Motegi akisema: "Kwa kuanzia kampuni mbili za Honda na Panasonic zimekubali kujenga viwanda nchini, kimoja kwa ajili ya kutengeneza pikipiki za Honda na kingine kwa ajili ya kutengeneza vifaa vya umeme."

Akaweka msisitizo: "Huu ni mwanzo tu Mheshimiwa Rais (Kikwete) kwa sababu kama nilivyosema kuwa tunataka Tanzania kuwa nchi ya mfano ya uwekezaji wa Japan katika eneo hili la dunia, na namna hiyo kwa pamoja tutakuwa tumeshirikiana katika kuongeza ajira kwa wananchi wa Tanzania."

WAINGEREZA WALIOMWAGIWA TINDIKALI WAITESA SERIKALI

071 c44b8

Siku tano baada ya raia wawili wa Uingereza kumwagiwa tindikali visiwani Zanzibar, Serikali kupitia vyombo vyake vya uchunguzi imeibuka na kueleza kuwa bila wananchi kutoa taarifa za ushahidi wa uhalifu wa aina mbalimbali, ni vigumu kuwabaini wahusika. (HM)

Kauli hiyo ilitolewa kwa pamoja jana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema, Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele na Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP) Eliezer Feleshi, katika mkutano wao na waandishi wa habari, uliolenga kueleza mikakati ya kupambana na matumizi yasiyo sahihi ya tindikali nchini.

Katika ufafanuzi wao walisema, "Kutoa taarifa ya uhalifu wa jambo lolote siyo hiari, ni jukumu la kisheria na kikatiba," huku Feleshi akitolea mfano jinsi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk Steven Ulimboka alivyoshindwa kutoa ushahidi wa tukio lililomkuta la kutekwa, kupigwa na kisha kutupwa katika Msitu wa Mabwepande, hivyo kufanya uchunguzi kuwa mgumu.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...