Thursday, August 08, 2013

WAPINZANI WACHEZEA KICHAPO KIKALI KIBONDO....!!!

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akizungumza na madiwani wa CCM wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma wiki iliyopita.

Katika hali inayothibitisha ule usemi wa mwanamuziki Chameleon wa Uganda kuwa "fitina yako bahati yangu" wapinzani wamechezea kichapo cha mwaka kwenye Halmashauri ya wilaya ya Kibondo baada ya CCM kushinda kwenye nafasi zote za kuongoza Halmashauri hiyo, ushindi uliowaacha midomi wazi wapinzani waliokuwa wakisubiri kufaidi kwenye ugomvi wa madiwani wa CCM wilayani hapo.

Diwani wa CCM Ndugu  Emily Msanya kuibuka Mwenyekiti wa Halmashauri baada ya kupata kura 14 kati ya 17 zilizopigwa na Makamu Mwenyekiti ni Apronary Mazinda ambaye pia alishinda kwa kura 14 kati ya 17.

Kuchaguliwa kwa madiwani hao na ushindi huo wa CCM kwenye ngome ya upinzani ambapo Mbunge wa jimbo hilo ni Ndg. Mkosamali wa NCCR-Mageuzi ni uthibitisho dhahiri kuwa CCM ina mkakati mkubwa wa kuzidhibiti ngome zote za upinzani nchini kuelekea uchaguzi wa 2014 na 2015.

MUME WA PILI WA WASTARA AIBUKA, ADAI WASTARA NI MKEWE....!!!

Na Issa Mnally
MIEZI nane baada ya kufariki dunia mumewe Juma Kilowoko ‘Sajuki’, ...


 hatimaye mume wa pili wa staa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma aitwaye Ahmed Kushi ameibuka na kudai kwamba anatambua kwamba staa huyo bado ni mkewe na anataka ampatie mwanaye aliyezaa naye.
Kwa muda mrefu kulikuwa na taarifa kuwa Wastara aliachana na mwanaume huyo kwa talaka kabla ya kuolewa na Sajuki lakini kuibuka kwake na madai kuwa bado mwanadada huyo ni mkewe kumezua mshangao mkubwa.

MADAI YA KUSHI
Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni, Kushi alifunguka kwa mara ya kwanza kuwa yeye na Wastara walifunga ndoa ya Kiislamu mwaka 2000 na kujaliwa kupata mtoto mmoja wa kiume aitwaye Fares.

Alisema: “Kisheria bado ni mke wangu kwa kuwa nilikuwa nimempa talaka moja tu wala hazikufika tatu,” alisema Kushi na kudai kwamba ndoa yake na staa huyo ilidumu kwa mwaka mmoja na nusu na kuvunjika kutokana na kutawaliwa na migororo.

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI AGOSTI 08, 2013

DSC 0002 ffed9
DSC 0003 490e8

HII NDIO HOTEL ILIYOKUWA INAUZA NYAMA ZA WATU ILIYOBOMOLEWA NA WANANCHI WENYE HASIRA KALI...!!!

hotel human heads in onitsha
HAPA WANANCHI WAKIIVUNJA HOTELI HIYO
Polisi walifanikiwa kuvikamata vichwa hivyo baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema wanaoishi karibu na hoteli hiyo ambapo mbali na vichwa hivyo viwili lakini pia walikamata bunduki mbili aina ya  AK47,kofia mbili za jeshi pamoja na simu nyingi.

Watu saba wanashikiliwa na jeshi la polisi nchini Nigeria katika hoteli moja iliyopo karibu na soko moja maarufu sana nchini humo linalofahamika kwa jina la Ose-Okwodu katika mji wa Anambra baada ya kukamatwa kwa vichwa viwili vya binadamu vikiwa bado vibichi lakini jina la hoteli hiyo linahifadhiwakutokana na sababu za kiusalama

"MAUAJI YA SOWETO YALIPANGWA NA KUTEKELEZWA NA POLISI" LEMA

Mbunge wa Arusha, Godbless Lema, ameendelea kushikilia madai yake kuwa polisi wanahusika na tukio la bomu lililolipuka katika mkutano wa kampeni ya chama hicho Viwanja vya Soweto Arusha na kusababisha vifo vya watu wanne.

Lema alitoa madai hayo juzi alipohutubia mkutano wahadhara Viwanja vya Shule ya Msingi Ngarenaro.


Alidai Rais Jakaya Kikwete amegoma kuunda tume huru ya kimahakama kuchunguza tukio hilo, ili kunusuru polisi na aibu ya kushiriki uhalifu na mauaji ya raia wasio na hatia.


“Mauaji ya Soweto yalipangwa na kutekelezwa na polisi, RPC (Kamanda wa Polisi) wa Arusha anajua mpango mzima ndiyo maana Rais hataki kuunda tume kama Chadema tulivyomuomba, ili tuwasilishe ushahidi wa video kuonyesha jinsi walivyohusika,” alisema Lema

MTUHUMIWA WA WIZI WA FEDHA KWENYE ATM ANASWA JANA JIJINI DAR



Dar es Salaam. Msako wa wezi wa kwenye Mashine za Kutolea Fedha (ATM), umeanza kuzaa matunda baada ya raia wa Bulgaria kukamatwa akiiba kwenye ATM ya Bank of Africa (BOA), Tawi la Afrikana, Kinondoni, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa za benki, mtuhumiwa huyo ambaye
hakutajwa jina lake alikamatwa baada ya kamera maalumu zilizowekwa kwenye ATM za BOA, kumtambua kuwa ni mwizi sugu wa benki hiyo anayetafutwa.

Mmoja wa wafanyakazi wa benki hiyo ambaye hakupenda kutajwa jina kwa kuwa si msemaji, alisema tukio hilo lilitokea jana saa 12 asubuhi baada ya mtuhumiwa huyo kuwekewa mitambo maalumu ya kumnasa.

Alisema benki hiyo ilipelekewa malalamiko na baadhi ya wateja kwamba wakienda kutoa fedha kwenye ATM wanakuta akaunti zao hazina salio wakati wanaamini zilikuwa na fedha.

Wednesday, August 07, 2013

MFANYABIASHARA MKUBWA WA MADINI JIJINI ARUSHA AUWAWA KWA KUPIGWA RISASI NA WATU WASIOJULIKANA.

Pichani juu askari wakikagua mwili wa  Erasto Msuya, mmoja wa Wafanyabiasha wakubwa wa Madini jijini Arusha aliyejulikana ambaye pia ni mmiliki wa SG HOTEL mkoani humo, baada ya kupigwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi na kufa papo hapo.

 Kwa mujibu wa baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa mfanya biashara huyo alifariki dunia mara baada ya majibishano ya risasi baina ya majambazi hayo na mfanya biashara huyo ambapo alizidiwa  nguvu na kupigwa risasi na kufariki dunia

Habari zinaeleza na kubainisha zaidi kuwa Marehemu alikuwa akitokea KIA kwenda BOMA ambako alikuwa ameitwa na watu (ambao hawakujulikana mara moja) ili wakafanye biashara.Habari zaidi tuvute subra kidoogo, tutazidi kufahamishana kadiri ya taarifa zitakapokuwa zikiingia. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi-Amen.

CHADEMA WATOA TAMKO KALI JUU YA KUNG'ATUKA KWA JOHN TENDWA .....!!!

John Tendwa alipaswa kuwa ameondoka kwenye Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, tangu mwaka 2008, alipofikisha umri wa kustaafu kwa mujibu wa sheria. Aliendelea kufanya kazi zake hata baada ya muda wa mkataba wake alioongezewa kuwa umefikia mwisho, hivyo alikuwa anakalia ofisi hiyo ya umma, kinyume cha sheria.Ametumia muda huo wa miezi kadhaa, aliokuwa anakalia ofisi ya umma kinyume cha sheria, kuropoka na kuharibu demokrasia, kwa manufaa ya mamlaka iliyomteua na CCM. Kutokana na mwenendo (maneno na matendo) wake mbovu, CHADEMA ilitangaza kutokumpatia ushirikiano wowote, yeye kama Tendwa. Ikamtangaza kuwa adui wa demokrasia nchini.
 Kwa muda wote huo, CHADEMA ilikuwa ikitoa ushirikiano kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa. Badala ya kuifuta CHADEMA na kufanikisha dhamira ovu ya kuharibu amani ya nchi, ameondoka yeye.
Kuondoka kwa Tendwa hakuzuii kutekelezwa kwa mapendekezo ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, iliyomkuta na hatia ya kuvunja Sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Sensa, hivyo akasababisha kutokea kwa mauaji ya Mwandishi wa Habari, Daudi Mwangosi, Nyololo, Iringa.

MADAM RITA ATAJA SABABU ZILIZOMFANYA AIHAMISHIE BONGO STAR SEARCH TBC1

 
Epiq Bongo Star Search ya mwaka 2013 haitaoneshwa tena kupitia ITV. Mwaka huu shindano hilo la kusaka vipaji vya kuimba litakuwa likioneshwa kupitia TBC1. 

Kupitia Facebook, Rita Paulsen aka Madam Rita ambaye ni mwanzilishi na jaji mkuu wa shindano hilo ametoa sababu mbili za kuhamisha matangazo hayo kutoka ITV hadi TBC1.


“Baada ya kusoma maoni yenu, ningependa kufafanua sababu mbili za kurusha Epiq Bongo Star Search 2013 kupitia kituo cha Televisheni cha TBC1. 


Kwanza kabisa ni sababu za kibiashara ndio zimepelekea kipindi cha EBSS kurushwa kupitia TBC1 na sababu ya pili ni kwamba baada ya kwenda kidigitali, TBC1 sasa inapatikana kwenye ving’amuzi karibia vyote vikiwemo Star Times, DSTV na Zuku.”

PETER WA P-SQUARE AOMBA KUMUOA MSICHANA KWA KUMZAWADIA RANGER ROVER SPOT MPYAAAA...!!!

Peter Okoye Finally Propose To His Baby Mama Lola Omotayo With A range Rover Sport
P-Square's Peter Okoye has finally put a ring on it. He proposed to the mother of his two children, Lola Omotayo today with a brand new Range Rover...and Lola said yes! The two have been dating for over seven years and have two children together. Continue to see the engagement ring and the SUV. Sometimes the wait is worth it.
Peter Okoye Finally Propose To His Baby Mama Lola Omotayo With A range Rover Sport Ediapark


Peter Okoye Finally Propose To His Baby Mama Lola Omotayo With A range Rover Sport Ediapark

WEMA, KAJALA... WATINGA GEREZANI, WAMLIZA PAPII KOCHA....!!!

Kajala Masanja na Wema Isaac Sepetu.
MASTAA wawili wanaotamba katika filamu za Kibongo, Kajala Masanja na Wema Isaac Sepetu hivi karibuni walifunga safari hadi Gereza la Ukonga jijini Dar kwa ajili ya kumuona Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ anayetumikia kifungo cha maisha gerezani humo.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, mara baada ya mastaa hao kufika na kuonana na Papii Kocha ambaye anatumikia kifungo cha maisha sambamba na baba yake Nguza Viking ‘Babu Seya’ inadaiwa kuwa Papii aliangua kilio cha nguvu.
“Nimewaona Kajala na Wema Gerezani Ukonga,wameenda kumuona Papii Kocha. Sasa nimeamini kuwa Kajala amejifunza mengi kutokana na kuwekwa mahabusu kipindi kile,” kilisema chanzo chetu kwa sharti la kutotajwa jina lake gazetini.
 Johnson Nguza ‘Papii Kocha’.
 
Baada ya kupata taarifa hizo Risasi Mchanganyiko liliwatafuta mastaa hao ili kutaka kujua undani wa safari yao hiyo.
Gazeti hili liliwapigia simu na kuzungumza na Kajala baada ya namba ya Wema kutokuwa hewani.
“Kweli mimi na Wema tulienda gerezani kumuona Papii ilikuwa ni safari ya majonzi sana, Papii aliangua kilio sana alipotuona,” alisema kwa kifupi Kajala na kukataa kusema kilichojiri zaidi.

SELLY AMUOMBA MSAMAHA MPENZI WAKE KWA KUFANYA MAPENZI NA NANDO NDANI YA BIG BROTHER


Hatimaye mshiriki wa Ghana katika reality show ya Big Brother ‘The Chase’ Selorm Galley maarufu kama Selly aliyetoka wiki moja iliyopita, amemuomba msamaha boy friend wake (wa Ghana) kwa yale aliyoyafanya mbele ya Camera za nyumba ya Big Brother.

Kupitia kipindi cha live ‘Celebrity Show’ cha ETV ya Ghana Selly ambaye pia ni muigizaji alianza kwa kumshukuru mpenzi wake Praye Tietia, na kutokana na kwamba kuna uwezekano yaliyomkwaza mpenzi wake ni mengi, Selly alimuomba msamaha kwa yale yote yaliyojiri mjengoni (ikiwemo kufanya mapenzi na Nando) alipokuwa anaiwakilisha nchi yake kuzifukuzia $300,000.

Selly mwenye miak 25 alisema “I am very thankful for the opportunity given me. I want to thank my boyfriend, Praye Tietia and also use this opportunity to say I am very sorry (for all that happened)”, na akasisitiza “I am very sorry”.

Selly amekuwa akiandamwa na maneno mengi toka camera za Big Brother zimnase akifanya mapenzi na aliyekuwa mwandani wake katika The chase Nando, kitendo kilichowaudhi zaidi mashabiki wa nchini kwake Ghana ambao wamekuwa wakimuandama kupitia mitandao ya kijamii.

POLISI AMWANDIKIA BARUA NZITO MAKAMU WA RAIS...!!!

Na Bryceson Mathias

ASKARI Polisi (pichani) mwenye namba D5788D Koplo Patrice Masiko wa Upelelezi Wilaya ya Dodoma, amemwandikia Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akipinga kufukuzwa kwa aibu Juni 24, 2011.

Katika barua yake ya Agosti 2, mwaka huu, Masiko anamuomba Makamu wa Rais Dk. Bilal, amsaidie kumhimiza Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Said Mwema, ampe Majibu ya rufaa ya Mashitaka ya Kijeshi yaliyosikilizwa tangu Novemba 30, 2010 hadi Juni 24, 2011.

Katika barua hiyo kwa Dk. Bilal, Masiko anasema, anamuombi amsaidie kumhimiza IGP ampatie majibu ya rufaa ya Mashitaka na Hukumu ya Kijeshi dhidi yake, yaliyosikilizwa na ZM Majunja na SSP-OCD Mpwapwa toka Novemba 30, 2010 hadi Juni 24, 2011.

“Julai 19, nilimwandikia IGP rufaa ya kupinga mwenendo mzima wa Mashitaka na Hukumu iliyotolewa lakini sikupata majibu. Agosti 16, 2011 nilimwandikia tena kukumbushia, lakini sijapata majibu.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO AGOSTI 07, 2013

DSC 0001 31969
DSC 0002 5a1a2

MOTO MKUBWA WAZUKA UWANJA WA NDEGE WA JOMO KENYATTA...!!!

K1 03646

K3 1a99f
NAIROBI, Kenya Aug 7 – Operations were grounded at Kenya's main airport, JKIA on Wednesday following a major fire that broke out at dawn, authorities said, adding flights were being diverted to other airports."There is a serious fire at JKIA, but we are doing everything possible to avert a crisis," Interior and Coordination of National Government Principal Secretary Mutea Iringo said.
K2 c552c
His office also posted on twitter "A serious fire at JKIA kindly take caution."
Fire fighters were battling the inferno.
Witnesses said they had seen a huge smoke billowing from the international arrivals and departure areas, but there were no immediate reports of casualties.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...