Thursday, July 04, 2013

FBI WAKAGUA OFISI YA KOVA KWA MBWA...!!!

 
 
Ofisa mmoja wa Usalama wa Marekani (FBI), akiwa na mbwa jana aliingia Makao Makuu ya Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na kufanya ukaguzi.

Tukio hilo lilitokea muda mfupi kabla ya msafara wa magari ya Marekani kupita yakitokea Ikulu kwenda Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere kumlaki Rais Barack Obama.

Polisi ambaye hakutaka kutajwa alisema ofisa huyo aliingia na mbwa hadi maeneo ya mapokezi, lakini muda mfupi walitoka.

“Walikwenda moja kwa moja mapokezi wakafanya ukaguzi, kisha wakatoka nje ya jengo na kama hiyo haitoshi, ofisa huyo akiwa na mbwa alikwenda sehemu ya kuegesha magari yenye kesi na yale ya kawaida na kuanza kufanya ukaguzi, baada ya hapo waliondoka,” alisema polisi huyo na kuongeza:

“Licha ya mimi kutokuwa na cheo pale, lakini hili la kutukagua na mbwa, ni kama wametudhalilisha... sisi ndiyo tunaaminika kwa usalama, leo hii wanatukagua na mbwa. Tena Kituo Kikuu.”

Hata hivyo, usalama kwenye vituo vingi ikiwamo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Juliusu Nyerere, vilikuwa chini ya usimamizi na uangalizi wa makachero wa Marekani.
Na Mwananchi.

HATIMAYE SWANSEA CITY YAKAMILISHA USAJILI WA JONJO SHELVEY

Kiungo Mpya wa timu ya Swansea City ya Uingereza Jonjo Shelvey

Hatimaye klabu ya Swansea City imekamilisha zoezi la Kumsajili kiungo wa zamani wa liverpool Jonjo Shelvey kwa dau la Pauni Milioni 5. Jonjo Shelvey amesajiliwa na timu ya swansea akitokea timu ya liverpool.

Kinda huyo mpya wa Swansea Mwenye umri wa Miaka 21 ameweka saini yake na kukubali kufunga ndoa ya miaka minne baada ya kukubali masharti yake binafsi na kufuzu kwa vipimo vya afya na hatimaye atakuwa kwenye dimba la libert kwa miaka minne.

Safari ya Jonjo katika Soka ilianza pale alipokuwa akiichezea timu ya Charlton kabla hajaamia liverpool kwa dau la Pauni Milioni 1.7 mnamo mwaka 2010.

Baada ya kumaliza kutia saini katika mkataba wake wa miaka minne na timu ya Swansea Jonjo Shelvey aliandika katika Ukurasa wake wa twitter kuwa "napenda kuwashukuru kila mmoja na mashabiki wote wa liverpool kwa msaada wake na pia nitawamiss kweli hakika hii ni daraja la kwanza"

"Nitakumbuka sana Jiji pamoja na klabu.Hallaa kwa kila mmoja hapa, Asante sana. Huu ni muda sasa wakuanza ukurasa mpya katika maisha yangu ya Wales. Asante"

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS JULAI 4, 2013


DSC 0280 ac6c7



DSC 0279 63be0

MGAMBO WAMUUA MKULIMA KWA KUMPIGA FIMBO YA KICHWA MBEYA...!!!

Watu wawili ambao ni askari mgambo, wamekimbilia kusikojulikana bado, wanatafutwa na polisi baada ya kumpiga kwa fimbo kichwani na kumwua mkulima aliyetambulika kwa jina la Gigwa Malegi (55, Msukuma) na mkazi wa kijiji cha Iyonyo.

Taarifa iliyotolewa na Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Barakael Masaki inasema kuwa mauaji hayo yalitokea tarehe Mosi Julai, 2013 majira ya saa moja jioni katika kijiji cha Totowe wilayani Chunya, Mbeya. 


Taarifa hiyo imewataja watuhumiwa kuwa ni Focus Fabian na Charles (jina la pili halijafahamika bado).

Imeelezwa kuwa chanzo cha kupigwa na kuuawa marehemu kinatokana na kukutwa akilisha mifugo (ng'ombe) kaitka eneo oevu kandoni mwa ziwa Rukwa.

Kamanda Masaki ametoa wito kwa jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi badala yake amewasihi watatue matatizo yao kwa mazungumzo na kwa kufuata sheria.

Ametoa wito kwa watuhumiwa kujisalimisha mikononi mwa askari mara moja ama yeyote mwenye taarifa za watuhumiwa, azitoe mara moja katika mamlaka husika ili hatua za kisheria zichukuliwe.

RAIS WA MISRI ATIMULIWA NA JESHI LA NCHI HIYO


jeshi nchini Misri limemuondoa madarakani Rais aliyechaguliwa kwa njia ya kidemokrasia nchini humo Mohamed Morsi na imemteuwa kiongozi wa muda wa nchi baada ya maandamano makubwa yanayoipinga serikali.

Akihutubia kwa njia ya televisheni jumatano jioni, mkuu wa jeshi, Abdul Fatah Khalil Al-Sisi alisema katiba ya Misri imesitishwa kwa muda na mkuu wa mahakama ya katiba ameteuliwa kuwa kiongozi wa muda nchini humo. 


Sisi alitangaza kwamba jeshi linaangalia watu wa Misri kufuatana na maandamano makubwa ya upinzani yakidai kuwa Rais Mohamed Morsi ajiuzulu.

Kufuatia hotuba ya kwenye televisheni Bwana Morsi alitoa taarifa kupitia akaunti yake ya Twitter, akiita hatua ya jeshi ni “mapinduzi kamili”. Aliwasihi wa-misri wote kukataa hatua ya jeshi lakini pia aliwataka kuwa na amani.

Kiongozi mpya wa muda nchini Misri, Adli Mansour ana umri wa miaka 68 ni mkuu wa sheria katika mahakama ya juu ya katiba. Ataapishwa alhamisi.

Kama sehemu ya mwongozo mpya unaoungwa mkono na jeshi kwa nchi, sisi aliutaka uchaguzi wa urais na wabunge, jopo kutathmini katiba na kamati ya mashauriano kitaifa. Alisema mwongozo ulikubaliwa na makundi kadhaa ya kisiasa.

Wednesday, July 03, 2013

MJUKUU WA MANDELA AFIKISHWA MAHAKAMANI....!!!

Jamaa za familia ya aliyekuwa rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, wamewasilisha kesi ya uhalifu dhidi ya mjukuu wa Mandela,Mandla Mandela.
Msemaji wa polisi, Mzukisi Fatyela aliambia BBC kuwa maafisa wa usalama watachunguza tuhuma dhidi ya Mandla za kufukua makaburi kinyume na sheria
Mwendesha mashtaka wa umma, kisha ataamua ikiwa amshtaki Mandla au la.
Inahusisha maiti za watoto watatu wa Mandela ambao inaaminika walifukuliwa na Mandla kutoka makaburi ya familia miaka miwili iliyopita.
Katika kesi nyingine, jamaa kumi na sita wa familia ya Mandela, wanataka kurejesha miili hiyo katika kijiji cha Qunu, ambako Mandela, ambaye anaumwa sana hospitalini anataka kuzikwa akifa.
Kesi hiyo inayosikilizwa katika mahakama kuu ya Mthatha, katika mkoa wa Mashariki iliakhirishwa hapo jana kuanza kusikilizwa leo.
Wiki jana, mahakama ilitoa amri ya muda kwa maiti za watatu hao kuhamishwa kutoka nyumbani kwa Mandla katika kijiji cha Mvezo hadi Qunu, umbali wa kilomiya 22.
Lakini Mandla Mandela, ambaye alitawazwa kama kiongozi wa kijamii na babu yake, sasa anapinga vikali amri hiyo.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO JULAI 3, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC 0015 775bb


DSC 0012 90b4b

SIFA ZA GARI YA OBAMA INAWEZA KWENDA 97KM TU KWA SAA AT MAXIMUM ..... YA JK IPO JUU KWA SPEED

 
Walioona msafara wa obama wataona namna msafara ulipita kwa speed ya kawaida sana tofauti na ile speed tuliyozoea anapopita JK, our president normally huwa ana cruise at an average of 120kmh.

Ile speed ikanifanya nitafute habari zaidi, niliyoyaona yamenishangaza, kumbe
Maximum speed ya limo ya obama ni 60mph tu, sawasawa na kilimita kama 97 kwa saa. hii gari haina ujanja wa kwenda hata 100km kwa saa, hata boda boda inaweza kwenda speed kuliko hii gari

  1. ina uzito unaokadiria kukaribia tani 9
  2. matumizi ya mafuta ni 8mpg, kwa lugha ingine inahitahi lita 35.31 ili kutembea kilomita 100, hii ni sawa na lita 1 kwa kila kilomita 2.8
  3. vioo vyote havifunguki isipokua pale kwa dereva kwa mbele. gari iko 100% sealed
  4. Vioo vya dirishani vina thickness ya inchi 5 wakati milango ni nchi 8.
  5. kutokana na unene wa madirisha na milango, obama hawezi kusikia chochote kinachoendelea nnje, spika zimewekwa ili kunasa sauti za nje
  6. gari ina night vision kamera zinazomuwezesha dereva kuendesha usiku bila hata kuwasha taa

OBAMA AAHIDI KUJA TENA NA KUPITA MITAANI ILI WATU WAMUONE...!!!

Kana kwamba alisikia kilio cha wakazi wa Dar es Salaam waliokuwa na shauku ya kumwona lakini ikashindikana, Rais Barack Obama wa Marekani amewaomba radhi kwa hali hiyo.
Akizungumza juzi wakati wa dhifa iliyoandaliwa kwa ajili yake na ujumbe wake na Rais Jakaya Kikwete katika Ikulu ya Dar es Salaam, Obama alisema akirudi nchini siku zijazo, atapita mitaani akiwa katika gari la wazi.


"Niliona wananchi walivyojitokeza kwa wingi kutupokea barabarani, nilifarijika sana lakini hawakuweza kutuona vizuri kwani tulikuwa ndani ya gari maalumu-The Beast.

"Miaka ya sitini Rais John Kennedy alipokuja hapa, alipita na gari la wazi mitaani wananchi wakamwona, naomba radhi nikija tena nitaonekana," alisema Obama.

Watu wengi waliozungumza na vyombo vya habari walionesha dhahiri kiu ya kutaka kumwona Rais huyo wa kwanza mweusi wa Marekani, lakini wakaishia kuona gari lake ambalo hata hivyo, lilipita kwa kasi barabarani kwenda Ikulu na kurudi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

WATUHUMIWA WA MAUAJI YA DAUD MWANGOSI WAACHIWA HURU NA MAHAKAMA...!!!

MAHAKAMA ya Wilaya ya Mufindi imetupilia mbali mashtaka yaliyokuwa yakiwakabili Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Hamad Yusuph na wenzake 42.

Kiongozi huyo pamoja na wenzake walikuwa wakikabiliwa na makosa matatu likiwemo la kufanya mkutano bila kibali pamoja na kuharibu mali ambazo ni kofia za pikipiki (helmenti) 2 za polisi katika tukio lililosababisha kuuawa aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Channel Ten Daudi Mangosi katika kijiji cha Nyololo wailayani Mufindi.

Kutokana na tuhuma hizo Chadema iliweka pingamizi za kutaka kesi hiyo ifutwe kwa kuwa ilifunguliwa kinyume cha sheria.

Wakili wa Chadema Lugaziya akisaidiana na mwanasheria wa Chadema Luka Sinkala Mwenda waliweka pingamizi kuwa aliyetoa amri ya kusitisha mkutano na kusababisha kifo cha mwandishi wa habari huyo ni kamanda wa Polisi Michael Kamuhanda ambapo aliingilia kazi ya OCD wa Mufindi kwa kuwa hakupaswa kutoa amri hiyo, kwamba wakati amri ya kusitisha mkutano ilitolewa wakati hakukukuwa na vurugu na polisi walipiga mabomu wakati watu wanatawanyika.

Pingamizi zingine ni kwamba aliyetoa amri ya kutawanya mkutano hakuwa na cheo chochote.Wakati Chadema ikizuiliwa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika jimbo la Bububu Zanzibar walikuwa na mkutano wa kampeni za uchaguzi..

STOKE CITY YAKAMILISHA DILI YA KUMSAJILI MARC MUNIESA KUTOKA BARCELONA

 
Marc Muniesa, Beki wa timu ya Barcelona aliyesaini mkataba wa kuichezea Stoke City Msimu ujao

Aliyekuwa beki wa Timu ya Barcelona ya Uhispania Marc Muniesa kijana wa Miaka 29 amekamilisha Usajili wake wa kuicheza timu yake mpya ya Stoke City ya Uingereza.

Marc Muniesa alikuwa ni moja wa memba wa kikosi cha Hispania chini ya Miaka 21 kilichoshinda Katika ligi ya Ubingwa wa ulaya chini ya Miaka 21.

Marc Muniesa, alisema " anafurahi kujiunga na timu ya Stoke City na atajitahidi kadri ya uwezo wake katika kuhakikisha timu yake hiyo mpya ya Stoke anailetea Ushindi"

Aliongezea kwa kusema Hakuwa na uamuzi mgumu katika kuamua kujiunga na timu hiyo ya Uingereza ya Stoke City na nimekuja uingereza jana kwaajili ya kukutana na watu wa klabu hii ya Stoke City na kuangalia Uwanja wa Mazoezi na kuona unavutia

MACHANGUDOA WALALAMIKIA UJUO WA OBAMA WASEMA AFADHALI UJIO WA BUSH:

Rais Barack Obama wa Marekani

Polisi wa Kimarekani waliokuwa mwiba mkali kwa ulinzi wa Obama

Machangudoa wakiwinda wazungu maeneo ya Oysterbay Karibu na Ubalozi wa Merikani

Machangudoa wakiwa kazini

Na Livingstone Mkoi

Katika hali ilisiyokuwa ya kawaida wakina dada maarufu wanaojihusisha na biashara ya kuuza miili yao maarufu kwa majina ya machangudoa wameulalamikia ujio wa Rais Barack Obama kwa kile kilichodaiwa haukuwa na faida yoyote kwa kukosa dili za pesa.

Wakiongea Xdeejayz kwenye baadhi ya sehemu wanazopatikana wakina dada hao walisema kuwa” Tumesikitishwa sana na ujio wa Obama kwani tulikuwa tumejipanga kupiga hela ndefu sana lakini patutu kwani watu wake tuliokuwa tumewategemea kuwanasa walikuwa busy na usalama pia kukaa kipindi kifupi kumechangia sisi kukosa mapato" Walisema wakina dada hao waliokutwa maeneo ya Coco Beack

Aidha machungudoa hao waliongeza kusema kuwa kipindi cha Bush ambae alikaa nchini karibu wiki moja walinufaika sana ambapo wengi wao walijenga majumba kwa pesa za ziara ya Busha kwani walifanikiwa kuwanasa watu wake na kufanya nao biashara kwa bei nzuri.

Tuesday, July 02, 2013

ANGALIA RAIS OBAMA AKIONYESHA UWEZO WAKE WA KUPIGA DANADANA....!!!

 
Rais Kikwete akimwangalia Obama wakati akipiga mpira danadana. 
 
OBAMA akionyesha uwezo wa kumiliki mpira kwa kupiga kichwa bila kutua chini wakati alipotembelea mit
ambo ya kuvua umeme Ubungo jijini Dar es salaam muda mfupi kabla ya kuondoka nchini.
 
 
 
Hapa akipiga danadana huku akishuhudiwa na Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete

ANGALIA PICHA ZA GEORGE BUSH ALIPOKUTANA NA RAIS OBAMA TANZANIA KABLA HAJAONDOKA

  
Rais Obama pamoja na Bush walikutana leo Asubuhi katika Ubalozi wa Marekani uliopo jijini Dar es Salaam na kufanya tendo la kutoa heshima zao kwa Walipoteza Maisha pamoja na wale wote walioathirika katika shambulio la Ugaidi katika Ubalozi wao hapa nchini mwaka 1998.




RAIS BARACK OBAMA WA MAREKANI AMALIZA ZIARA YAKE YA SIKU MBILI HAPA NCHINI


 
Rais Barack Obama wa Marekani ameondoka nchini mchana huu kurudi nchini Marekani,baada ya kumaliza  ziara yake ya siku mbili hapa nchini iliyoanza jana.Rais Obama na mwenyezi wake Rais Jakaka Kikwete,leo walifanya ziara ya kutembelea mitambo ya kuzalisha umeme ya Symbion
iliopo Ubungo jijini Dar es Salaam na kuzindua rasmi mradi huo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...