Monday, June 03, 2013

MAPYA YAIBUKA KUHUSU KIFO CHA MANGWEA....ALIYELALA NAE ASIMULIA ALIYOYAONA WAKATI NGWEA AKIKATA ROHO..!!

HUKU mwili wake ukitarajiwa kuwasili Bongo kesho, kifo chake Albert Mangweha ‘Ngwea’ kilichotokea katika hali ya utata Mei 28, 2013 nchini Afrika Kusini, kimeibua mambo mapya, Ijumaa Wikienda lina mzigo wote.

MAMA MANGWEA NAYE AZIDIWA, AKIMBIZWA HOSPITALI YA MKOA
Habari kutoka msibani Moro jana zilisema mama mzazi wa marehemu Mangwea, Denisia Mangwea naye alizidiwa na kukimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu zaidi.
Kwa mujibu wa baadhi ya waombolezaji msibani hapo, mama huyo alipata mshtuko wa moyo kufuatia kifo cha mwanaye ambapo taarifa za kifo hicho zilimshtua tangu Jumanne mpaka alipozidiwa jana. 

HABARI KUTOKA SAUZI SASA
Habari kutoka kwenye Jiji la Johannesburg ambako Ngwea alifia, mtiririko wa maelezo ya wenyeji wa Mangwea na Mgaza Pembe ‘M 2 The P’ nayo yanaibua mapya ambayo awali yalikuwa hayajulikani.
MAELEZO YA SAUTI ZA WENYEJI
Wakizungumza hewani kupitia redio moja ya jijini Dar, wenyeji wao wawili waliojitambulisha kwa jina moja moja la Godfrey na Godluck ambao walikuwa na Mangwea na M 2 The P, kila mmoja alisema lake huku maelezo yao yakionesha dalili ya kutofautiana au kuzua maswali masikioni mwa watu.

BINTI AANIKA MAKALIO MBELE YA WABUNGE KATIKA SHINDALO LA MISS TABORA


Mmoja wa washabiki wa muziki wa kizazi kipya ambaye alivaa vazi lililoacha  matako  nje....

Shabiki huyo  alipanda jukwaani kumkumbatia  msanii  maarufu nchini , Ommy Dimpoz  wakati alipokuwa akitoa burudani katika mashindano ya Redds Miss Tabora.

Tukio hilo la aibu lilitokea  mbele ya  wabunge....
Mbunge wa Jimbo la Sengerema  Bw.William Ngereja akiwa na Diwani wa kata ya Kitete manispaa ya Tabora Bw.Daniel Mhina ambaye alikuwa MC katika onesho hilo lililofanyika katika ukumbi wa Frankman Hotel mjini Tabora.

Sophia Simba, Anne Kilango nusura wazichape walipokutana gafla benki

Kushoto Mh. Sophia Simba na kulia ni Mh. Anna Kilango
UHASAMA wa kisiasa kati ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na watoto, Sophia Simba na Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango, umevuka mipaka na sasa ni uadui wa wazi wazi. Hali hiyo ilidhihirika wiki iliyopita mjini Dodoma, wakati wawili hao walipokutana katika Benki ya CRDB iliyopo bungeni na badala ya kusalimiana, waliishia kutofautiana.
Shuhuda wa tukio hilo, aliiambia MTANZANIA, kuwa tukio hilo lilitokea saa 6 mchana, baada ya Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, kuahirisha Bunge kutokana na vurugu zilizosababishwa na wabunge wa upinzani, wakati wa mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.


Shuhuda huyo alisema kuwa, kabla ya tukio hilo, Anne Kilango pamoja na wabunge wengine wa CCM, walikuwa ndani ya benki hiyo wakibadilishana mawazo.

Wakati wakiendelea kuzungumza, Sophia Simba aliingia ndani na kuanza kuwasalimia kila mmoja kama ilivyo kawaida.
 

MWANA FA NA JIDE KWA MARA NYINGINE WATAFANYA SHOW ZAO SIKU MOJA

Ikiwa ni siku chache baada ya wasanii kuahirisha show zao kufuatia kuondokewa mpendwa wetu Albert Mangwea, miongoni mwa show kubwa zilizoahirishwa ni ya Lady Jay Dee (Miaka 13 ya Lady JayDee) na ya Mwana FA (The Finest) zilizokuwa zifanyike siku moja (May 31),show hizi zinaweza kufanyika tena siku moja kwa kuwa wasanii hao wametaja tarehe inayofanana.

May 28 ambayo ndiyo siku aliyofariki Mangwea mwana FA alithibitisha kuahirisha show yake, lakini alipoulizwa siku ambayo anadhani atairudia show hiyo, yeye alifunguka kupitia akaunti yake ya twitter na kuitaja June 14.

 “Sina uhakika,but I'll pick June 14th kama brother tutakuwa tushampumzisha"@umykitwana”, alitweet Mwana FA a.k.a Binamu.
 
 
Kwa upande wake Lady Jay Dee ambae kwa sasa a.k.a yake mpya ‘Anaconda’ inaonekana ku-take over ametumia akaunti yake ya twitter kuiweka wazi tarehe ya show yake alipokua akijibu swali la fan wake ambae atasherehekea siku moja ya kuzaliwa na msanii huyo (June 15).

“@MteiHaikaJ Gud. Chukua hii tar 13 June Mahakamani, tar 14 June miaka 13 ya Jide na tar 15 June Bday ya Jide. Let's celebrate long week end.”Alitweet Lady Jay Dee June 2.

Kwa tweets za wakali hawa wa bongo fleva inaonesha kabisa kuwa show zao zinaweza kufanyika june 14 japo Mwana FA alisema hana uhakika, labda kama atatangaza siku nyingine tena. June 14,tunatarajia kuwa marehemu Ngwair atakuwa amekwisha pumzishwa kwenye nyumba yake ya milele huko Morogoro.
CHANZO : LEOTAINMENT

WABUNGE WAKUTWA KWENYE DANGURO LA UCHI DODOMA

 Watu wanaingia mmoja mmoja, wengine kwa makundi na baadhi wapo nje wakipunga kwanza upepo kabla ya kuingia.

Siku hizi wanawake wanaingia bure au kwa jina jingine ‘ladies free’ jambo linalosababisha ukumbi huu ufurike watu.

Katika ukumbi huu, yapo maeneo mawili. Kuna sehemu ya kawaida ambayo kiingilio chake ni kuanzia Sh5,000 hadi Sh10,000 kutegemeana na matukio au burudani ya siku hiyo.

Pia kuna eneo jingine ambalo ni kwa watu maalumu ama waweza kusema ni ‘VIP’ ambapo wateja wake hutakiwa kulipa Sh20,000.

Ukumbi wa VIP upo juu na ule wa kawaida upo chini. Hata hivyo maeneo yote haya hujaza watu kwa kiasi kikubwa.

Mwandishi wetu alifika katika ukumbi wa VIP saa tano usiku, hata hivyo bado watu ni wachache katika eneo hili ukilinganisha na kule kwa watu wa kawaida.

Ukumbi wa VIP si mkubwa kieneo . Kuna kaunta ya vinywaji, makochi madogo madogo aina ya sofa yenye meza mbele yake, viti vilivyoizunguka kaunta na katikati ya ukumbi huu kuna meza mbili za duara zenye mti wa chuma katikati.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNE 03, 2013

1 a9412
17 20f78
5 173d6

Sunday, June 02, 2013

DIAMOND ATOA SIRI YAKE NA MANGWAIR.

 
DIAMOND.

 https://encrypted-tbn1.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcTcbPsmB8oL0NdNY9ZTMuOtFcF-881836OfLxvYzL9xEVxaoG1Z5Q


WAKATI watu mbalimbali maarufu nchini, hususan wasanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongo Fleva), wakiendelea kutoa historia ya mahusiano yao na aliyekuwa msanii wa Hip Hop nchini Tanzania Albert Mangweair.

wea, msanii maarufu wa muziki nchini Nassib Abdul (Diamond Platnumz) amevunja ukimya na kutoa siri yake na marehemu Mangwea.

Akielezea hisia zake pamoja na mipango mingi aliyokuwa nayo kuhusu kufanya kazi ya muziki na marehemu katika ukurasa wake wa mtandao wa Instagram, Diamond alisema kwamba alijaribu kufanya kazi ya pamoja na msanii huyo lakini kwa bahati mbaya kazi zote zikaharibika.


"Kinacho niumiza ni jinsi tulivyo jaribu kutengeneza HIT bila mafanikio yaani siyo nilizo mshirikisha hata zile alizo nishirikisha na tuka amua kuplan kutengeneza nyingine akirudi kutoka Afrika Kusini, lakini haikuwezekana yani mungu alimpenda zaidi":alisema Platnumz.


Kila binadamu huwa na jambo lake muhimu ama siri ya mafanikio baina yake na mtu mwingine ambayo pengine si rahisi kuizungumzia hadharani ama wakati wowote, lakini inapotokea mmoja kati yao akifariki dunia anayebaki duniani hujikuta akitoa siri hiyo.


Hatua ya Binadamu kuamua kutoa siri yake na mwenzake wakati wa msiba wa mmoja wao inaweza ikawa na tafsiri nyingi lakini ukweli nikwamba huzuni na machungu ya kuondokewa na mtu muhimu kwake aliyekuwa akitarajia kufanya naye jambo flani muhimu ndiyo husababisha mtu huyo kutoa siri.R.I.P Mgwea.

DEREVA MWANAMKE WA BASI LA NDENJELA COACH AWA KIVUTIO KWA ABIRIA

DEREVA NUSURA MAGULUKO 28 AKIMWOMBA MUNGU KABLA YA KUANZA SAFARI
SASA HAPA YUPO KAZINI
BAADHI YA ABIRIA WAKIFURAHIA MWENDO MZURI WA DEREVA NUSURA MGULUKO

ABIRIA WAKIPATIWA HUDUMA YA VITAFUNWA NDANI YA BASI HILO LA NDENJELA

MISS SHINYANGA CENTRE APIGWA NA KUNYANG'ANYWA PESA NA MUANDAAJI WA SHINDANO HILO BAADA YA KUKATAA KUONDOKA NAE....!!!

 



Na Mwandishi wetu Steve Kanyeph
Mashindano ya kumtafuta mrembo Shinyanga yaani Miss Shinyanga Centre yamemalizika huku yakiingiwa dosari baada ya mshindi wa taji hilo SCOLASTIKA SITTA{19} kutoa malalamiko kuwa amedhalilishwa kwa kupigwa na kunywanganywa pesa kiasi cha shilingi laki 3 alizopewa ikiwa ni zawadi
mrembo huyo amesema tukio hilo limefanywa na muuandaaji wa mashindano ya miss Shinyanga ASELA MAGAKA baada ya mrembo huyo kukataa kuondoka kwenda Kahama usiku wa manane.

“Alitaka tuondoke baada ya kushuka jukwaani na twende Kahama kwaajiri ya kambi ya miss Shinynga usiku huo huo mimi nikakataa kwa sababu ilikuwa ni usiku sana na baada ya hapo akapanick akanipiga makofi na kuninyang'anya pesa zote shilingi laki 3”.Alisema mrembo huyo.




Mrembo huyo amesema kitendo hicho ni cha udhalilishaji na kimemkatisha tamaa ya kuendelea kushiriki mashindano kwa ngazi ya mkoa na amekwenda kutoa taarifa polisi na taratibu za kisheria zinaendelea.
Scolastica anatoa ushauri kwa waandaaji wa mashindano ya urembo kutowadhalilisha washiriki na kwamba warembo wanatakiwa kuwa imara na jasiri katika kudai haki zao na kupinga vitendo vya udhalilishaji kwani mashindano ya urembo yanakabiliwa na changamoto nyingi.

WANYARWANDA WANASWA WAKIJIUZA JIJINI DAR


POLISI Mkoa wa Ilala, jijini Dar es Salaam imeendesha oparesheni maalum ya kuwanasa machangudoa wanaofanya biashara hiyo haramu katika eneo lao na kufanikiwa kuwaweka ‘mtu kati’ makahaba kibao, wakiwemo raia wa Rwanda na Burundi...Kamatakamata hiyo ilichukua nafasi usiku mnene wa Alhamisi ya Mei 23, mwaka huu kwenye danguro kubwa la makahaba lililopo Kariakoo, jijini Dar ambalo machangu hao hutegea mingo zao kwa ajili ya kuwanasa wateja.


Katika hali iliyowashangaza polisi, midume iliyokutwa na makahaba hao ilitimua mbio ili kujiokoa na mtego huo wa polisi uliodhamiria kusafisha eneo la Kariakoo kwa ukahaba uliopitiliza.

Baadhi ya wanaume wakati wakitimua mbio walisikika wakisema kuwa wakukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya dola ni wanawake hao kwa vile wanavaa kimitego huku wakijua binadamu anapitiwa na shetani wakati wowote.


“Sisi kosa letu nini? Wakamateni haohao machangudoa, watavaaje kimitego mbele yetu sisi wanaume? Shetani naye atakuwa wapi wakati huo?” alisikika akisema mmoja wa wanaume hao huku akichanganya miguu kupita kawaida.
Awali kabla ya zoezi la kuwanasa makahaba hao halijaanza, afande mmoja alipowauliza wanachofanya hapo, kahaba mmoja aliuliza: Una maswali mengi kwani we ni polisi?

Mei 24, mwaka huu, makahaba hao walipandishwa kwenye Mahakama ya Jiji na kusomewa mashitaka yao na mwendesha mashitaka, John Kijumbe mbele ya Hakimu Timoth Lyoni.

Waliosomewa mashitaka ni Natasha Bahati, 30 (Mrundi), Asma Athuman, 23 (Mrundi), Niyonkuru  Evelinde, 29 (Mnyarwanda), Zaimana Hawa, 20 (Mrundi) na Wabongo 35.
Wote walikana mashitaka lakini walipelekwa Gereza la Segerea, jijini Dar baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.

WAZIRI MKUU ACHARUKA KASI NDOGO YA UJENZI WA BARABARA RUKWA

20120913_164754
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 *Afanya ziara ya kushtukiza kwenye kambi ya wajenzi wa Kichina
*Aahidi kumtuma Waziri Magufuli kufuatilia, ataka mkandarasi aongeze kasi, awe makini
*Amtaka RC Rukwa aunde timu ya kumpatia ripoti kila mwezi
 WAZIRI MKUU Mizengo Pinda jana jioni (Jumamosi, Juni Mosi, 2013) alilazimika kufanya ziara ya ghafla kwenye kambi ya wajenzi wa barabara ya Kanazi-Kizi-Kibaoni ili kupata maelezo ni kwa nini kazi hiyo inasusua na haionyeshi kuendelea.
Waziri Mkuu ambaye alikuwa akitoka Namanyere, wilayani Nkasi, mkoani Rukwa ambako alikuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo Kitaifa yanafanyika mkoani Rukwaalilazimika kusimama kwenye kambi hiyo ya wajenzi iliyopo Paramawe, wilayani Nkasi.

Wasemavyo wasanii kuhusiana na kifo cha Ngwea

Kutokana na kifo cha msanii Albert Mangwea ambaye amefariki nchini Afrika ya Kusini ambako alikwenda kufanya maonyesho, wasanii mbalimbali  wamezungumzia kifo chake.
Ni dhahiri, Albert Mangwea alikuwa katika kuutangaza muziki wa Tanzania nje ya nchi na ndiyo uhai wake ulikopotea, Mwandishi wetu Kalunde Jamal aliongea na baadhi ya wasanii wenzake na maongezi yakawa kama ifuatavyo:
Joseph Haule a.k.a Profesa Jay
Anasema katika hili hakuna jinsi kwa kuwa kila binadamu atayaonja mauti.
“Inaniuma sana lakini sina cha kufanya kwa kuwa ni kazi ya Mungu na kazi yake haina makosa, kinachotakiwa ni kumuombea apumzike kwa amani  huko aendako.         
Selamani Msindi ‘Afande Sele’
Anasema anamtambua Ngwea siyo kama msanii bali ni mdogo wake wa karibu na ameshindwa kujizuia kutoa machozi kuhusiana na kifo hicho.
Anaongeza kuwa katika kuonyesha ni kwa jinsi gani kijana huyo alikuwa na mapenzi na watu kwani kwao ni Morogoro lakini alijulikana ni kijana wa Dodoma almaarufu East Zoo.
Ngwea kapambana na muziki ukiwa hauna mbele wala nyuma kapambana kuhakikisha unakuwa bora lakini kwa sasa ndiyo unatambulika baada ya kufanya jitihada za kila aina kuufanya uwe ulivyo.”
“Sidhani kama atanitoka kichwani kwangu, naona kama ametutoroka kwa kuwa hatuhitaji aondoke muda huu lakini hakuna jinsi tutakutana naye siku ya mwisho na nitamweleza machungu yangu na kwa jinsi gani kifo chake kimeniumiza,” anasema.
Snura Mushi ‘Snura’
Anasema anasikitika sana hasa kwa wao ambao ndiyo kwanza wameingia kwenye muziki na walitaka kujifunza mengi kutoka kwa wasanii wanaofanya vizuri kama Mangwea, lakini kwa bahati mbaya au nzuri Mungu amechukua kiumbe chake hakuna cha kufanya kupinga hilo kwani haliwezekani.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 2, 2013

4 aaa9f
1 802eb
2 2b5a3

Saturday, June 01, 2013

SERIKALI YAOMBELEZA KIFO CHA MANGWEA

untitled25 a7fc8
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO
SALAAM ZA RAMBIRAMBI KUTOKANA NA KIFO CHA
BW. ALBERT MANGWEA, (Man Ngwair)
1/06/2013.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, imepokea kwa mshituko na masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha msanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongo fleva) Albert Mangwea, aliyefariki huko Afrika Kusini katika hospitali ya St. Hellen akiwa katika shughuli za muziki, Jumanne tarehe 28 Mei, 2013.Kifo cha Albert Mangwea ni pigo kubwa kwa fani ya muziki hapa nchini, na pia kimataifa. Na kutokana na umahiri wake katika fani hiyo ya muziki wa kizazi kipya hususan aina yake ya uimbaji ya "Free Style" alikonga mioyo ya wapenzi wake hasa vijana ndani na nje ya nchi.
Albert Mangwea atakumbukwa na wasanii na wapenzi wa muziki kwa kipaji na juhudi zake za kukuza muziki hapa nchini.
Serikali inawapa pole ndugu na jamaa wote na kuwaomba wawe na uvumilivu na subira katika kipindi cha msiba.
Wito wa Serikali kwa wasanii na wananchi kwa ujumla ni kuendelea kumuenzi kwa yale yote mazuri aliyoyafanya wakati wa uhai wake.
"Mwenyenzi Mungu ailaze roho ya Albert Mangwea mahala pema peponi."
Imetolewa na Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara

ALICHOKISEMA DIAMOND KUPITIA MTANDAO WAKE WA INSTAGRAM KUHUSU MAREHEMU ALBERT MANGWAIR

Hali ya huzuni ikiwa imetanda juu ya nyuso za mamilioni ya
watanzania baada ya msiba mzito
uliotufikia Ghafla kwenye Tasnia ya Muziki wa Kizazi Kipya......
Tumesikia Producers,wanamuziki mbalimbali na watu mbalimbali
wakifunguka na kuongea lolote
juu ya marehemu Albert Mangweha....
Kupitia Mtandao wake wa Instagram bado
Mwanamuziki Diamond Platnumz
akiwa kwenye hali ya kutokuamini
kilichotokea muda mchache uliopita aliweza kufunguka
juu ya matarajio yake ya kufanya kazi za uhakika
na marehemu Albert Mangweha.......
Muda mchache uliopita alitupia kupitia mtandao wake wa
Instagram Picha hii chini akiwa ameiandikia
maneno haya''Kinachoniuma zaidi ni jinsi tulivyokua
tukijaribu kutengeneza HIT bila Mafanikio... si kwa
nyimbo niliyokushirikisha wala uliyonishirikisha, zote
Hazikufikia Malengo yetu na Kuplan kufanya Ngoma Mpya
 Ukirudi toka South Africa.... bt pia kwa Mipango ya
Mwenyez Mungu Haijawezekana... RIP Brother, i will
 always miss and Respect you....''

Ayo ndio maneno aliyoandika Msanii Diamond Platnumz....
R.I.P ALBERT MANGWEHA....

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...