Saturday, June 01, 2013

SERIKALI YAOMBELEZA KIFO CHA MANGWEA

untitled25 a7fc8
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO
SALAAM ZA RAMBIRAMBI KUTOKANA NA KIFO CHA
BW. ALBERT MANGWEA, (Man Ngwair)
1/06/2013.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, imepokea kwa mshituko na masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha msanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongo fleva) Albert Mangwea, aliyefariki huko Afrika Kusini katika hospitali ya St. Hellen akiwa katika shughuli za muziki, Jumanne tarehe 28 Mei, 2013.Kifo cha Albert Mangwea ni pigo kubwa kwa fani ya muziki hapa nchini, na pia kimataifa. Na kutokana na umahiri wake katika fani hiyo ya muziki wa kizazi kipya hususan aina yake ya uimbaji ya "Free Style" alikonga mioyo ya wapenzi wake hasa vijana ndani na nje ya nchi.
Albert Mangwea atakumbukwa na wasanii na wapenzi wa muziki kwa kipaji na juhudi zake za kukuza muziki hapa nchini.
Serikali inawapa pole ndugu na jamaa wote na kuwaomba wawe na uvumilivu na subira katika kipindi cha msiba.
Wito wa Serikali kwa wasanii na wananchi kwa ujumla ni kuendelea kumuenzi kwa yale yote mazuri aliyoyafanya wakati wa uhai wake.
"Mwenyenzi Mungu ailaze roho ya Albert Mangwea mahala pema peponi."
Imetolewa na Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara

ALICHOKISEMA DIAMOND KUPITIA MTANDAO WAKE WA INSTAGRAM KUHUSU MAREHEMU ALBERT MANGWAIR

Hali ya huzuni ikiwa imetanda juu ya nyuso za mamilioni ya
watanzania baada ya msiba mzito
uliotufikia Ghafla kwenye Tasnia ya Muziki wa Kizazi Kipya......
Tumesikia Producers,wanamuziki mbalimbali na watu mbalimbali
wakifunguka na kuongea lolote
juu ya marehemu Albert Mangweha....
Kupitia Mtandao wake wa Instagram bado
Mwanamuziki Diamond Platnumz
akiwa kwenye hali ya kutokuamini
kilichotokea muda mchache uliopita aliweza kufunguka
juu ya matarajio yake ya kufanya kazi za uhakika
na marehemu Albert Mangweha.......
Muda mchache uliopita alitupia kupitia mtandao wake wa
Instagram Picha hii chini akiwa ameiandikia
maneno haya''Kinachoniuma zaidi ni jinsi tulivyokua
tukijaribu kutengeneza HIT bila Mafanikio... si kwa
nyimbo niliyokushirikisha wala uliyonishirikisha, zote
Hazikufikia Malengo yetu na Kuplan kufanya Ngoma Mpya
 Ukirudi toka South Africa.... bt pia kwa Mipango ya
Mwenyez Mungu Haijawezekana... RIP Brother, i will
 always miss and Respect you....''

Ayo ndio maneno aliyoandika Msanii Diamond Platnumz....
R.I.P ALBERT MANGWEHA....

HILI NDILO TAMKO RASMI LA PUSH MOBILE NA BONGO RECORDS KUHUSU MAUZO YA NYIMBO ZA MANGWEAR KWENYE SIMU

Hili ndilo Tamko Rasmi la Push Mobile na Bongo Records Kuhusu Mauzo ya Nyimbo za Mangwear Kwenye Simu

DAKTARI AKIRI NGWEA KAFA KWA KUNYWESHWA SUMU, ADAI KUWA ALITOKWA NA DAMU NYINGI SANA PUANI WAKATI AKIKATA ROHO..!!

KIFO cha msanii wa Hip Hop Bongo, Albert Kenneth Mangwea a.k.a Ngwea kilichotokea Jumanne wiki hii jijini Johannesburg, Afrika Kusini ‘Sauzi’, kinaendelea kuibua mapya ambapo sasa sumu imetajwa kuhusika.
Akizungumza na paparazi wetu juzi kwa njia ya simu moja kwa moja kutokea nchini humo, Mtanzania mmoja (jina tunalo) alisema muda huo yeye alikuwa nje ya Hospitali ya St. Helen Joseph ambako mwili wa marehemu ulikuwa umehifadhiwa kwenye Mochwari ya Hillbrow.

M2 The P akiwa amelazwa Hospitali
Mbongo huyo alisema alifanikiwa kuutazama mwili wa marehemu Ngwea ambapo ulionesha kuwa wakati wa kukata roho damu nyingi zilimtoka kupitia puani na mdomoni kiasi cha kuwashangaza wauguzi.
 

NI SUMU
Alisema muuguzi mmoja aliyekuwa akimtibu mshirika wa marehemu, Mgaza Pembe a.k.a M2 The P aliyenusurika, alimwambia wawili hao walionekana kuingiwa na kitu cha hatari na kibaya sana mwilini jambo lililowashtua hata madaktari wenyewe.


Alisema muuguzi huyo alimweleza kuwa kitu walichokula au kulishwa kiliwadhuru sana ndani ya miili yao na kusababisha mishipa ya damu kwa Mangwea kupasuka hovyo kwa kuwa moyo ulizidiwa na presha ya msukumo wa damu.
Mtanzania huyo alidai kuwa hata kama kweli wawili hao walichanganya vileo kama watu wanavyodai, basi ule mchanganyiko ndiyo uliotengeneza sumu mwilini akisisitiza kuwa hilo halina shaka kwa mujibu wa muuguzi huyo.
“Unajua kuna watu wanapenda kuchanganya pombe kali kwa hiyo kuna wanaodai wawili hao walichanganya ‘unga’, bangi na pombe kali.

HAWA NDO WANAFUNZI BORA KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE

WANAFUNZI WALIOFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA MTIHANI WA CSEE 2012
NECTA'S LOGO

 1. Watahiniwa Kumi (10) bora Kitaifa:
NAFASI
NAMBA
JINA
JINSI
JINA LA SHULE NA MKOA
1
S0189-0063
SAID JUMA IRANDO
M
FEZA BOYS'   S  S  (DAR ES SALAAM)
2
S4459-0028
ALEX  ELIFAS
M
JUDE MOSHONO   S   S  (ARUSHA)
3
S0189-0039
JASPER GEOPHREY KAJIRU
M
FEZA BOYS'   S  S   (DAR ES SALAAM)
4
S2549-0086
MOSES J BOSCO
M
ALPHA SECONDARY    S  S (DAR ES SALAAM)
5
S4213-0074
YOHANA L MAYENGA
M
MARIAN BOYS' S   S  (PWANI)
6
S0239-0072
NGUSE  NGULUMBI
F
ST. FRANCIS GIRLS   S   S  (MBEYA)
7
S4213-0044
JOSHUA Z AZZA
M
MARIAN BOYS'  S    S  (PWANI)
8
S0189-0062
SAID ATWAYA NCHIMBI
M
FEZA BOYS'   S  S   (DAR ES SALAAM)
9
S0867-0134
LUPYANA L KINYAMAGOHA
M
PANDAHILL   S   S  (MBEYA)
10
S0101-0350
PETER SEREKA KICHOGO
M
AZANIA    S   S  (DAR ES SALAAM)

2.    Wasichana Kumi (10) bora Kitaifa
NAFASI
NAMBA
JINA
JINA LA SHULE NA MKOA
1
S0239-0072
NGUSE  NGULUMBI
ST. FRANCIS GIRLS   S  S   (MBEYA)
2
S0239-0078
SAMMOTA  CHUNGU
ST. FRANCIS GIRLS   S   S  (MBEYA)
3
S0239-0075
RAHMA  MKWATA
ST. FRANCIS GIRLS   S    S (MBEYA)
4
S0239-0018
DIANA  MGAYA
ST. FRANCIS GIRLS  S  S  (MBEYA)
5
S1060-0066
REBECCA J MWAMBEGELE
ST.MARY'S   S   S (DAR ES SALAAM)
6
S0239-0010
BELDA  THOMAS
ST. FRANCIS GIRLS  S   S  (MBEYA)
7
S0239-0002
AGNES  NTAPARA
ST. FRANCIS GIRLS   S  S  (MBEYA)
8
S0248-0045
JOANGELINE J BAMWENZAKI
MARIAN GIRLS   S  S   (PWANI)
9
S0298-0011
FATMA M MOSHI
FEZA GIRLS' S  S   (DAR ES SALAAM)
10
S0239-0045
JESCA  CHENGULA
ST. FRANCIS GIRLS   S  S  (MBEYA)

  1. Wavulana Kumi (10) bora Kitaifa
NAFASI
NAMBA
JINA
JINA LA SHULE NA MKOA
1
S0189-0063
SAID JUMA IRANDO
FEZA BOYS'   S    S  (DAR ES SALAAM)
2
S4459-0028
ALEX  ELIFAS
JUDE MOSHONO   S  S   (ARUSHA)
3
S0189-0039
JASPER GEOPHREY KAJIRU
FEZA BOYS'S   S   S   (DAR ES SALAAM)
4
S2549-0086
MOSES J BOSCO
ALPHA   S   S    (DAR ES SALAAM)
5
S4213-0074
YOHANA L MAYENGA
MARIAN BOYS'   S  S   (PWANI)
6
S4213-0044
JOSHUA Z AZZA
MARIAN BOYS'   S   S   (PWANI)
7
S0189-0062
SAID ATWAYA NCHIMBI
FEZA BOYS'   S  S  (DAR ES SALAAM)
8
S0867-0134
LUPYANA L KINYAMAGOHA
PANDAHILL   S   S   (MBEYA)
9
S0101-0350
PETER SEREKA KICHOGO
AZANIA     S   S   (DAR ES SALAAM)
10
S0692-0065
NORBERT S KIMARYO
ROSMINI    S   S   (TANGA)

TAARIFA YA MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA (ACSEE) ULIOFANYIKA FEBRUARI 2013 KWA UFUPI.

Taarifa hii imeidhinishwa na Baraza la mitihani la Tanzania katika kikao chake cha 94 kilichofanyika Mei 30.
Idadi ya watahiniwa wa shule waliofanya mtihani: 42,952
Idadi ya watahiniwa wa shule waliofaulu: 40,242 sawa na 93.92%
Mfumo wa kusahihisha mtihani huu ulitumia Fixed Grade Range na Standardization.
Mchanganuo wa madaraja kwa asilimia:
- Division I - 0.76%
- Division II - 12.54%
- Division III - 70.45%
- Division IV - 10.18%
- Division 0 - 6.08%

Shule kumi bora zenye watahiniwa zaidi ya 30.
1. Marian Girls (Pwani
2. Mzumbe (Morogoro)
3. Feza Boys (Dar-es-salaam)
4. Ilboru (Arusha)
5. Kisimiri (Arusha)
6. St. Mary's Mazinde Juu (Tanga)
7. Tabora Girls (Tabora)
8. Igowole (Iringa)
9. Kibaha (Pwani)
10. Kifungilo Girls (Tanga)

Shule kumi za mwisho zenye watahiniwa zaidi ya 30.
1. Pemba Islamic College (Pemba)
2. Mazizini (Unguja)
3. Bariadi (Simiyu)
4. Hamamni (Unguja)
5. Dunga (Unguja)
6. Lumumba (Unguja)
7. Oswald Mang'ombe (Mara)
8. Green Acres (Dar-es-salaam)
9. High View International (Unguja)
10. Mwanakwerekwe "C" (Unguja)

Matokeo ya mtihani wa kidato cha sita (ACSEE) 2012 yanapatikana katika tovuti zifuatazo:

Obama atumiwa barua nyingine yenye sumu hatari aina ya Ricing.

ObamaRicin
Shirika la upelelezi la Marekani FBI limesema kuwa barua yenye sumu hatari aina ya ricin imetumwa kwa rais Barack Obama kutoka Spokane katika jimbo la Washington, siku ambayo barua ya sumu kama hiyo ilipotumwa kwa Jaji wa mahakama kuu na kwa posta.

Mtu mmoja alikamatwa wiki iliyopita huko Spokane kuhusiana na barua hiyo iliyotumwa kwa jaji na ambayo ilizuiliwa tarehe 14 mwezi huu.
FBI imesema barua iliyokuwa imetumwa kwa rais Obama iligunduliwa tarehe 22 na kuongeza kuwa barua nyingine kama hiyo ilikuwa imetumwa kwenye kituo cha ndege za kijeshi kilicho karibu.
Taarifa ya FBI na ya huduma za posta imesema kuwa barua zote 4 ziliwekewa stampu tarehe 13 Mei huko Spokane.
Tatu kati ya barua hizo zimethibitishwa kuwa na sumu ya ricin na nyingine moja bado inachunguzwa.-DW.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JUNI 1, 2013


11 9ad30


1 5874c

Friday, May 31, 2013

DIAMOND AMPIGIA MAGOTI JOKATE NA KUMUOMBA MSAMAHA

MKALI wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, ameibuka na kuelezea kuhusu uhusiano wake na mpenzi wake zilipendwa, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ ambaye ni mwigizaji na modo moto wa kuotea mbali Tanzania.


Nasibu Abdul ‘Diamond’ akiwa na Jokate Mwegelo ‘Kidoti’.

Akizungumza kwa uhakika kabisa, Diamond alisema inampasa amuombe radhi Jokate kwa sababu katika uhusiano wao, Jokate hakuwahi kumkosea ila yeye ndiye tatizo na chanzo cha kuachana kwao.
Diamond alisema hayo kwenye mahojiano na Mtangazaji Zamaradi Mketema katika Runinga ya Clouds kwenye Kipindi cha Take One, kilichorushwa juzi Jumanne usiku kituoni hapo.

DIAMOND ANAFAFANUA
“Inanipasa nimuombe radhi Jokate. Ni kweli nilimtenda vibaya wakati wa mapenzi yetu. Hakukosea sana maana hakuwahi kufanya jambo lolote kinyume. Sijui niseme nini lakini nataka kueleza wazi kuwa mimi ndiyo sababu ya kuachana kwetu na ilitokea tu.


Diamond na Jokate wakicheza.

“Naamini hilo jambo lilimuuma sana, maana nakumbuka wakati ule, baada ya mimi kurudi kwa Wema (Sepetu), watu walimwandama sana kwa maneno na alionekana msaliti lakini ukweli ni kwamba nilimpenda sana lakini ndiyo hivyo, siwezi kufafanua zaidi.
“Kutoka moyoni mwangu, namuomba msamaha Jokate, kama hatanisamehe nitaendelea kumuomba mpaka naingia kaburini. Sina raha kabisa kutokana na jambo hilo. Lazima niwe mkweli.”

JACQUELINE WOLPER
Diamond alikwenda mbali zaidi na kuwazungumzia baadhi ya wasichana aliowahi kutoka nao kimapenzi akiwemo mwigizaji Jacqueline  Wolper ambaye alisema ni mwanamke aliyempenda sana, ndiyo maana alimtungia wimbo wa Mawazo.

PENNY SASA
Kwa upande wa mpenzi aliye naye sasa, Mtangazaji wa Runinga ya DTV, Penieli Mungilwa ‘Penny’ alisema ni mwanamke mtulivu na sahihi kwake kwa sababu anatambua majukumu yake kwake, pia anamheshimu.

“Huyu kwa kweli ana karibu sifa zote alizonazo Wema ila uzuri wa Penny ananiheshimu sana. Hafanyi mambo yake hadharani. Unajua wakati nikiwa na Wema hata kama akifanya mambo yake siku mbili au tatu baadaye nayaona kwenye magazeti, tofauti na Penny ambaye kwangu mimi naona ananiheshimu, hata kama anafanya mambo yake ni kwa siri.”

BREAKING NEWZZZZZZZZZZZ...!!! NECTA YATANGAZA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA (ACSEE 2013)


Matokeo ya kidato cha 6 yametangazwa. Ufaulu umeongezeka mara dufu zaidi ya wanafunzi 90% wamefaulu. Shule zilizoongoza ni
    1. Marian Girls
    2. Mzumbe

f Matokeo ya kidato cha sita (ACSEE) 2013 - Link 1

f Matokeo ya kidato cha sita (ACSEE) 2013 - Link 2

TANGAZO MUHIMU KWA UMMA KUTOKA BENKI KUU YA TANZANIA

 
 Benki Kuu inapenda kuutahadharisha umma kuwa katika siku za karibuni kumekuwepo
na mtandao wa matapeli unaotumia TOVUTI ifuatayo www.jakayafoundation.wapka.mobi/index.html

Mtandao huo unajidai kuwa ni Taasisi ya Fedha ijulikanayo kwa jina la Jakaya foundation ambayoinamilikiwa na Benki Kuu chini ya utawala wa bodi kuu ya mikopo inayotolewa na serikali kupitia sekretariat ya Utumishi wa umma ofisi ya Rais. 


Matapeli hao wanaeleza kwamba Taasisi hiyo inatoa mikopo ndani ya masaa 24 kwa Mtanzania yeyotemwenye umri kuanzia miaka 18 endapo atajiunga kwa kulip a ada ya shilingi 37,000/=.BENKI KUU INAUARIFU UMMA KUWA HAIITAMBUI NA WALA HAIHUSIANI KWA NAMNA YOYOTE ILE NA TAASISI INAYOELEZWA KWENYE TOVUTI HIYO.


Kwa taarifa hii, Benki Kuu inatoa tahadhari kwa Wananchi kutojihusisha na Taasisi hiyo ya kitapeli kwa ajili ya kupata huduma za mikopo kama ambavyo inadai.
 

IMETOLEWA NA
IDARA YA UHUSIANO NA ITIFAKI
BENKI KUU
YA TANZANIA
DAR ES SALAAM.
29/5/2013

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MAY 31, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS HAYA HAPA

14 b3187

1 1c845

HAWA NDIO WADADA WALIO FUNGA NDOA YA JINSIA MOJA

Mashoga hao wakifungishwa ndoa kwenye ofisi ya msajili nchini Uingereza.
Wanawake wawili raia wa Pakistan wameweka historia kama Waislamu wa kwanza wa jinsia moja kufunga ndoa nchini Uingereza.

Rehana Kausar, miaka 34, na Sobia Kamar, miaka 29,wameweka historia pale walipofunga pingu za maisha katika sherehe iliyofanyika kwenye ofisi ya msajili, kisha haraka wakaomba hifadhi ya kisiasa baada ya kuwa wamefunga ndoa, wakidai kwamba maisha yao yatakuwa hatarini kama wakirejea kwenye nchi yao ya asili.
Wakishuhudiwa na wasimamizi wao na marafiki wawili, wanandoa hao walivalia mavazi meupe asilia ya ndoa pale walipofunga ndoa mjini Leeds, West Yorkshire.
Wawili hao, kutoka mikoa ya Lahore na Mirpur ya Pakistan, walisema walipokea vitisho vya kuuawa kutoka kwa wapinzani nchini Pakistan - ambako mahusiano ya jinsia moja ni kinyume cha sheria na kuchukuliwa ni kusaliti Uislamu.
Na tangu habari za ndoa yao mapema mwezi huu kuzagaa, wanandoa hao walidai kupokea vitisho vya kuuawa hata kutoka nchini Uingereza 
Kabla ya zoezi hilo, hata msajili aliwashauri wawili hao kufikiria kwa makini kuhusu uamuzi wao wa kufunga ndoa sababu ya mtazamo wa baadhi ya Waislamu kuhusu mahusiano ya jinsia moja.

Thursday, May 30, 2013

Wema Afunguka na Kusema: "Sikuwahi kumsaliti Diamond na tulikuwa tunapendana sana"

 
Miss Tanzania mwaka 2006 na muigizaji wa filamu Wema Sepetu amefunguka kupitia jarida jipya la Mzuka kuwa katika uhusiano wake wote na Diamond hakuwahi kumsaliti.

Wema ambaye yupo kwenye cover la jarida hilo linalotolewa na  Bongo5,amefunguka kwa kusema kuwa yeye na Diamond walikuwa wakipendana sana.


“Maisha yangu yote tangia nimeanza mapenzi na Naseeb naweza kusema kuwa sikuwahi kuwa unfaithful. I used to be very faithful to him na tulikuwa tunapendana sana. With Naseeb nilikuwa nimesharidhika na maisha ambayo niko nayo,” amefunguka Wema.

Wema amefunguka pia kuhusu jinsi Diamond alivyomcheat na Jokate kwa kusema, “nadhani pia inacost mwanaume akishajua kwamba anakutawala in one way or another so labda ni shetani au ni ibilisi alimuingilia baada ya kutaka kuanza kushoot video ya Mawazo ndo rumors zilianza, nikawa siamini kwanza.”

Katika jarida hilo ambalo linauzwa kwa shilingi 1,500 tu, Wema amesimulia mengi tangia alipokutana na Diamond, jinsi alivyoumizwa na kitendo chake cha kumrekodi na kusambaza sauti kwenye radio, mapenzi yake na Kanumba, utajiri wake, jinsi anavyowapenda mbwa wake na mambo mengine exclusive.

HII NDIO RIPOTI YA KUTEKWA, KUUMIZWA KIBANDA



TAARIFA YA UCHUGUZI JUU YA KUTEKWA NA KUUMIZWA KWA ABSALOM KIBANDA IMEWASILISHWA NYUMBANI HOTEL - TANGA MEI 30, 2013


UTANGULIZI: 

Usiku wa Jumanne ya Machi 5 kuamkia Machi 6, 2013, Mhariri Mtendaji wa New Habari (2006) Ltd, ambaye pia Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda alivamiwa na kujeruhiwa vibaya akiwa nje ya lango la kuingilia nyumbani kwake Mbezi Juu, Dar es Salaam.Tukio hilo liliishtua na kutikisa taifa kwa kiwango kikubwa si tu katika tasnia ya habari nchini, bali pia jamii kwa ujumla hasa baada ya aina ya utekaji, utesaji na usiri uliotumika katika kufanikisha uhalifu huu kufanana kwa karibu na tukio lilomkuta Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madkatari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka lililotokea karibu miezi tisa kabla ya tukio la Kibanda yaani, usiku wa Juni 26, 2012.Ukiacha matukio hayo, miezi sita kabla ya Kibanda kutekwa na kuteswa Mwandishi Daudi Mwangosi, aliuawa akiwa mikononi mwa vyombo vya dola Septemba 2, 2012 huko Nyololo, Iringa akiwa kazini.Tukio la Kibanda limekuwa na sura ya mwendelezo wa mauaji au utesaji wa wanahabari, hasa ikitiliwa maanani kuwa Mwandishi Issa Ngumba (45) wa Radio Kwizera aliyekuwa anafanyia kazi zake katika Wilaya ya Kakonko, Kigoma, Januari mwaka huu, alipigwa risasi na kuuawa katika mazingira ya kutatanisha.Kama hiyo haitoshi, tukio la kutekwa na kudhuriwa kwa Kibanda limetokea mwezi mmoja tu baada ya Mwandishi wa Gazeti la Tanzania Daima, Shaaban Matutu kupigwa risasi na polisi akiwa nyumbani kwake Dar es Salaam kwa maelezo kuwa kimakosa polisi walidhani Matutu ni jambazi.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...