Wednesday, April 10, 2013

Irene Uwoya afunguka kuhusu skendo yake na Diamond.......!!!

Baada ya habari nyingi sana kuhusu Irene Uwoya kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Diamond platnumz kutawala vyombo vya habari na kwenye mitandao hapo juzi, hatimaye bongomovies.com tuliamua kumtafuta kwa simu mwanadada Irene Uwoya ili tuweze kumuuliza juu ya tuhuma hizi za yeye kuingilia penzi lwa mwanadada Penny kwa kijana wa “mbongofleva” diamond platnumz.

Baada ya majaribio mengi ya kupiga simu yake ambayo ilikuwa haipatikani muda wote wa mchana baadaye kwenye mida ya saa kumi na mbili hivi jioni tuliweza kumpata hewani na Jibu lake lilikuwa moja tuu kuwa “achana nazo” na sisi tukaona kweli tuachane nazo ila tukufukishie wewe msomaji wetu mpendwa “response” hiyo ili mwenyewe uamue na kutafakari. Hilo ndo jibu alilotupa mwanadada mrembo wa bongo movies Irene Uwoya kuhusu tuhuma za yeye kutoka kimapenzi na msanii Diamond.
Source:Bongo Movies

SHILOLE ANASA KWENYE PENZI LA MZUNGU...!!

SIKU chache baada ya kuripotiwa akijiachia kimalavidavi na ‘lejendari’ wa Bongo Fleva, Aboubakar Katwila, staa wa muziki na filamu za Kibongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amenaswa hotelini na bwana Mzungu aliyetajwa kwa jina moja la George, kamera za Risasi Mchanganyiko ni noma.

Kwa mujibu wa shushushu wetu, tukio hilo lilijiri hivi karibuni katika hoteli moja maarufu jijini hapa ambapo Shilole alikuwa kwenye ziara ya shoo yake.


Ilidaiwa kuwa mara tu baada ya kumaliza ziara ya shoo, Shilole hakuondoka jijini hapa na badala yake alionekana sehemu tofauti akijivinjari na jamaa huyo ambaye uchunguzi wetu ulibaini kuwa ni bosi wa klabu moja maarufu ya usiku Kanda ya Ziwa. 


Kabla ya kuondoka katika jiji hili la sangara na sato, Alhamisi iliyopita na ndege ya jioni, Shilole alinaswa kimalavidavi na Mtasha huyo Jumatano katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere wa Gold Crest kulipokuwa na maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Syria.


Shilole alishuhudiwa akifanyiwa ‘shopping’ ya kufuru na bwana huyo ambapo gazeti hili lilinasa mpango mzima ambapo lilipotaka kujua kama ni wapenzi, Mtasha huyo alijibu kwa kifupi sana: “No comment” (sina la kusema).


Kwa upande wake Shilole alipobanwa mbavu alifunguka: “Nisingependa kuongelea jambo hilo kwani sasa najipanga kimuziki zaidi, shopping ni mambo ya kawaida sana kwa hiyo ni vyema tukaongelea muziki wangu kwani shoo yangu ya Pasaka ilijaa mashabiki wa kufa mtu so nakubalika sana Mwanza na siku moja nitaweka makazi hapa.”

ANGALIA YALIYOJIRI KATIKA SHEREHE ZA KUAPISHWA KWA RAIS UHURU KENYATTA .



SHAA AAHIDI KUVUA NGUO ZOTE HADHARANI ENDAPO VIDEO YAKE ITAFIKISHA VIEWS 100,000


Kwa  waliokuwa  na  hamu  ya  kumuona  huyu  naye  akiwa  nusu  uchi  na  kivazi  cha  kuogelea  tuu, huu  sasa  ni  wakati  wao.....

Coca Cola  pop Star  maarufu  kwa  jina  la  Shaa  amedai kuwa  yupo  tayari  kuvua  nguo  zake  hadharani  na  kuyaanika  maungo yake  nyeti  na  kubakiza  kichupi  cha  kuogelea  tu  endapo  video  yake  mpya  ya  Lava Lava itafikisha  views  100,000  katika  mtandao  wa  youtube 
Popout
“Lava Lava Video imefikisha views 44,000+ leo.Endapo  itafikisha 100,000 basi  ntavua  nguo  zote  na kuogelea coco beach mchana kweupe lets do,”Alitweet  Shaa  katika  mtandao  wa  kijamii wa Twitta  na  kuongeza

“Niliitupia kiutani tu nikidhani in one day kupata views elfu50 ni ngumu…sasa naona watu wameniamkia! Kwa spidi hii…mmmh…noma,”

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE APRIL 10, 2013

DSC 0014 88cc4

DSC 0011 7fee3

DSC 0008 4c17f

BUNGE KITANZINI LEO

Mchakato wa marekebisho ya kanuni za Bunge umeibua mjadala mkali baina ya wabunge, huku wengi wao wakieleza kuwa hatua hiyo ina lengo la kulifanya Bunge kukosa meno ya kuisimamia Serikali.

Miongoni mwa mambo yaliyozua mvutano katika kikao cha awali cha wabunge wote ni suala la muda wa wabunge kuchangia bungeni na jinsi wanavyotakiwa kupangwa kulingana na idadi yao kwa kila chama.

Bunge linakusudia kuwasilisha azimio la kutaka kubadili kanuni ambazo zilitarajiwa kuwasilishwa na Naibu Spika jana bungeni, lakini kutokana na baadhi ya mapendekezo kupingwa, hatua hiyo iliahirishwa hadi leo.


Mabadiliko hayo ni muhimu kabla ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kuwasilishwa leo, kwani baadhi yake yanalenga kuwezesha mfumo mpya wa Bunge wa kuanza na Bajeti za wizara na baadaye kumalizia na Bajeti Kuu ya Serikali.

HOTUBA YA RAIS WA KENYA MARA BAADA YA KUAPISHWA HII HAPA


PRESIDENT UHURU KENYATA

SPEECH BY H.E. HON. UHURU KENYATTA, C.G.H., PRESIDENT AND COMMANDER-IN-CHIEF OF THE DEFENCE FORCES OF THE REPUBLIC OF KENYA DURING HIS INAUGURATION AND SWEARING-IN CEREMONY ON TUESDAY, 9TH APRIL 2013 AT THE MOI INTERNATIONAL SPORTS COMPLEX, NAIROBI.

o Your Excellency Hon.Mwai Kibaki, C.G.H., M.P.;
o Your Excellency Daniel arap Moi;
o Your Excellencies, Visiting Heads of State & Government;
o Chief Justice Willy Mutunga;
o All our Invited Guests;
o Fellow Kenyans,


Let me begin by thanking all Heads of State present and the representatives of Heads of State for choosing to be here as a symbol of your continued support and goodwill towards Kenyans.
I particularly note, with gratitude, the large presence of our brothers and sisters from across the continent. This is a clear indication of your commitment to the Pan-African agenda. You have bestowed a great honor on me and our country by being here. On behalf of the Kenyan people I welcome all of you to Kenya. Karibuni Sana!Let me also acknowledge with gratitude and respect the distinguished service of my predecessors. President Mwai Kibaki, a true statesman and a great leader who over the past 10 years has laid a firm foundation for the future prosperity of our country. Asante sana Mzee. Shukrani nyingi sana.

YANGA WAKATAA RASMI MECHI ZAO KUONYESHWA BURE NA SUPER SPORT


Siku moja baada ya shirikisho la soka nchini TFF kubadilisha ratiba ya baadhi ya mechi za ligi kuu ya Tanzania bara ili kuweza kufanikisha mpango wa kuonyesha mechi hizo kupitia kituo cha Supersport, klabu ya Yanga kupitia makamu wake mwenyekiti Clement Sanga imesema haikubaliani na mpango huo kwasababu haujafuata utaratibu na pia utaziingizia hasara kubwa klabu zinazohusika na mpango huo.

Akizungumza na mtandao huu Sanga alisema kwamba mpango huo wa kuonyesha mechi za ligi kuu bure kwenye Supersport haupo katika kuzinufaisha vilabu bali wahusika wengine wa mpango huo.

Tuesday, April 09, 2013

SKENDO YA ASKOFU PENGO KUUZA MADAWA YA KULEVYA YAITIKISA KANISA KATOLIKI............!!!

 

SKENDO kwamba Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kadinali Pengo, anafanya biashara ya madawa ya kulevya, ilitikisa kisha ikapoa, ila sasa Uwazi lipo kwenye nafasi nzuri ya kupasua jipu.


Januari mwaka jana, Pengo ndiye alikuwa wa kwanza kutamka hadharani kuwa anaambiwa anauza ‘unga’, kipindi hichohicho, Uwazi lilizungumza na Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya, Godfrey Nzowa ambaye alisema wanafanya kazi kisayansi.
“Kama jina la Pengo tunalo kwamba anauza madawa ya kulevya au hatuna, siwezi kutamka kwa sasa, hatutaki kupindisha ushahidi au kuvuruga upelelezi wetu,” alisema Nzowa.
Hata hivyo, hivi karibuni, Uwazi lilifanikiwa kuzungumza na mmoja wa vigogo wa jeshi la polisi nchini, aliyeomba hifadhi ya jina lake gazetini, akasema kuwa suala la Pengo lina utata ila siyo zito.
“Labda mimi nipasue jipu kwamba jina la Pengo halionekani katika orodha ya viongozi wa dini wanaochunguzwa kutokana na kashfa ya madawa ya kulevya,” alisema kigogo huyo.
Aliongeza: “Hata kwenye ule mkanda uliokwenda bungeni, ukionesha wafanyabiashara wa madawa ya kulevya, Pengo haonekani. Tulishangaa sana aliposema anaambiwa anauza madawa ya kulevya.”...

RAILA ODINGA ASUSIA ZOEZI LA KUPISHWA KWA RAIS WA KENYA NA KUKIMBILIA AFRIKA KUSINI


 Wako kwenye mbuga za wanyama Afrika Kusini wanakula bata ....ni Raila Odinga na wenzake wawili akiwemo Kalonzo Musyoka.
Taarifa kuhusu kina Odinga na wagombea wenza kwenda Afrika Kusini zimetokea @FORA_2013 page ya Organisation inayomsupport Odinga aliekua mgombea Urais kwenye Uchaguzi wa Kenya ambao Uhuru Kenyatta ndio katangazwa mshindi na anaapishwa leo.

Inadaiwa Raila Odinga na wagombea wenza wameamua kukwepa kuwepo kwenye kuapishwa kwa Rais Uhuru Kenyatta na kuamua kwenda Afrika Kusini .

HILI NDILO POZI LA LULU LA MITEGO KATIKA SIKU YA KUMUENZI KANUMBA


 Hii ndo picha ya kimitego imewekwa kwenye instagram na Lulu kwenye siku ya kumuenzi marehemu Kanumba  ikiwa  ni  masaa  machache  tu  baada  ya  kutoka  katika  kaburi  la  marehemu Kanumba.....

HII PICHA YA UHURU KENYATTA ENZI ZA UTOTO AKIWA NA BABA YAKE MZEE JOMO.

.Mzee Jomo Kenyatta akiwa na mwanae Uhuru Kenyatta enzi hizo akiwa mdogo ambapo leo ndio ameapishwa kuwa Rais wa Kenya. (imetoka Nation Media Kenya)

MAMA KANUMBA AMSAMEHE LULU YALIYOTOKEA AMWACHIA MUNGU


Mama wa marehemu Kanumba Flora Mtegoa amesema amemsamehe msanii Elizabeth Michael 'Lulu' kutoka moyoni .Ingawa bado kesi iko mahakamani, kwa upande wake yeye hana tatizo naye na yaliyotokea anamuachia mungu

Akizungumza katika makaburi ya Kinondoni mara baada ya kumuombea marehemu na kuweka mashada ya maua alisema kuwa yeye ni mkristo safi hivyo hawezi kuendelea kukaa na kinyongo ingawa kila anapomuona msanii huyo humkumbuka mwanaye

Alisema kuwa Kanumba alikuwa zaidi ya mtoto kwake, mume, rafiki, kaka  alimfanya kuwa mtu wa karibu sana kwake na alimfanya kuwa karibu kwake na kumzoea kwa kila kitu hali ambayo imemfanya kuwa mpweke mpaka leo

SOMA WABUNGE TZ WALIVYOKULA MSOTO JESHINI


Kutoka kushoto: Halima Mdee, Ester Bulaya na Neema Hamid.
WABUNGE katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao walihudhuria mafunzo ya kijeshi katika kambi tofauti za Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), walipata msoto wa nguvu.

Tofauti na ilivyokuwa ikidhaniwa kwamba wabunge hao wangepewa mafunzo kwa kubembelezwa kutokana na nafasi zao, walikutana na msoto wa nguvu mwanzo hadi mwisho.

HILI NDIO JUMBA LA MILIONI 500 ZA KENYA SERIKALI ALILOMZAWADIWA RAIS MWAI KIBAKI.

..
Wakati Rais mpya wa Kenya Uhuru Kenyatta akitarajiwa kuapishwa leo kuiongoza nchi hiyo, nimeipata ripoti ya kituo cha TV cha NTV inayoonyesha jumba lililojengwa na Serikali ya Kenya kwa ajili ya kumzawadia Rais Kibaki anaestaafu.
Ripoti ya NTV imeamplfy kwamba kuna uwezekano Rais huyo akaja kuishi kwenye nyumba hii iliyopo Mweiga Nyeri nchini humo japo pia kuna taarifa nyingine zinaamplfy kwamba Rais huyo hapendelei maisha ya kijijini, zaidi anapenda mjini.
Mwai Kibaki mwenye umri wa miaka 81, anamiliki nyumba tatu za kifahari kwenye jiji la Nairobi na ana nyumba moja nyumbani kwao alikowahi kuwa mbunge.
..Na Millard Ayo

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...