Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya CFAO Motors Roddy Sharp (kulia) akiongozana na  Waziri wa Nchi Mh. Anne Ruth Herkes wa Wizara ya Uchumi na Teknolojia ya Ujerumani (kushoto) baada ya kuupokea Ujumbe kutoka nchini Ujerumani kunakotengenezwa magari aina ya Volks Wagon walipofika kushuhudia uzinduzi wa showroom mpya ya Kampuni ya Alliance Autos wauzaji wa magari ya Volkswagon. Kushoto ni Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Mh. Klaus Peter Brandes aliyeambata na ugeni huo.
  Waziri wa Nchi Mh. Anne Ruth Herkes wa Wizara ya Uchumi na Teknolojia ya Ujerumani akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika hafla ya uzinduzi wa Showroom mpya ya magari ya Volkswagon ya  Kampuni ya Alliance Autos iliyopo Pugu/Nyerere road jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Msaidizi wa Mkurugenzi wa CFAO Motors Mama Maria Petro akipokea wageni waalikwa.
Mgeni rasmi Waziri wa Uchukuzi Mh. Dkt Harrison Mwakyembe akizungumza na wageni waalikwa pamoja na ujumbe wa wafanya biashara kutoka Ujerumani walioongozwa Balozi wa Ujerumani nchini Klaus –Peter Brandes katika hafla ya kuzindua Showroom ya magari ya kampuni ya Alliance Autos inayouza magari aina ya Volkswagon ambapo pamoja na mambo mengine amepongeza hatua hiyo na kusema serikali iko bega kwa bega na wafanya biashara wabunifu na pia kuuhakikishia ujumbe kutoka Ujerumani kuwa serikali imeweka mazingira bora ya kuwekeza hivyo wasisite kujitokeza.