Monday, June 10, 2013

MJUE MSANII WA BONGO MOVIE ALIEANZA KUCHEZA FILAMU ULAYA


Lucy Francis Komba (amezaliwa tar. 24 Oktoba, 1980) ni mwigizaji wa filamu, mwongozaji na mtayarishaji kutoka nchini Tanzania. Huenda akawa anafahamika zaidi kwa kutayarisha filamu ya Yolanda 1-2 na Utata. Lucy pia ni mmoja kati ya waliokuwa waigizaji wa kundi la sanaa la Kaole Sanaa Group.

Maisha ya awali


Lucy Francis Komba alizaliwa mnamo tarehe 24 Oktoba ya mwaka wa 1980, katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Alipata elimu yake ya awali (chekechea) katika shule ya St. Peters Nusery School na msingi alisoma katika shule ya Oysterbay Primary School. Elimu ya sekondari alisoma Moshi katika mkoa wa Kilimanjaro, kwa kidato cha 1 - 4 na 5 - 6 alisoma katika shule ya Kibosho Secondary School.
Kwa elimu ya vyuo, alisoma katika Chuo cha Utumishi wa Serikali na alisomea maswala ya IT (Information Technology) na alipata Diploma katika elimu hiyo.
Sanaa ya awali
Lucy Komba alianza maswala ya sanaa katika kundi la sanaa la Fukuto Arts Professional. Akiwa huko alishiriki katika baadhi ya mifululizo ya vipindi vya televisheni kama vile "Valentine Day" na "Rangi ya Chungwa".
Baada ya hapo akaelekea zake katika kikundi cha Dar Talent, akiwa huko alipata kushiriki katika filamu moja ya vichekesho. Baada ya hapo alilekea zake katika kikundi cha sanaa cha Kaole Sanaa Group, akiwa huko alipata kushiriki katika mifululizo minne ya vipindi vya televisheni (tamthilia).
[hariri]Kazi binafsi

JK kuteta na Wabunge, Mawaziri Dodoma.

Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwasili mjini Dodoma, ambapo pamoja na mambo mengine atakutana na Kamati ya Bunge ya Bajeti ikiwa siku chache kabla ya kuwasilishwa kwa Bajeti Kuu ya Serikali itakayoainisha Mapato na Matumizi yake kwa mwaka wa fedha 2013/14, Juni 13.


Kamati hiyo inayoongozwa na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge imekuwa na vikao karibu kila siku, wakati mwingine vikimalizika usiku ili ikijiweka sawa kabla ya


 Rais Jakaya Kikwete akizungumza na vyombo vya habari siku za hivi karibuni
kuwasilishwa kwa Bajeti Kuu ya Serikali.
Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa Rais Kikwete akiwa mjini Dodoma atakutana na baraza lake la mawaziri na Kamati ya Bajeti ili kupata picha ya mwelekeo wa bajeti, ambayo sehemu kubwa imeelezwa kubanwa na upatikanaji wa fedha za kutosha kwa ajili ya kuziwezesha wizara na taasisi zake kwa shughuli za kawaida na maendeleo.
Hata hivyo, habari zinadai kuwa ugumu uliopo ni namna ya kupata fedha kwa asilimia 100 kwa ajili ya kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo na matumizi ya kawaida kwa wizara na Idara za Serikali.

Chanzo chetu kilieleza kuwa pamoja na 'kukuna kichwa' jinsi ya kupata fedha hizo, hata utekelezaji wa bajeti ya 2011/12 na 2012/13, ulikuwa mgumu kwa kuwa baadhi ya wizara na
taasisi zake zilipata nusu ya bajeti iliyopitishwa au asilimia 30 ya bajeti nzima.

Upatikanaji wa fedha hizo chini ya asilimia unatarajiwa kwa wizara na taasisi zake huku ikielezwa kuwa ni kutokana na kumegwa kwa asilimia za mafungu kulikosababishwa na kuongezeka kwa matumizi ya Serikali zikiwemo dharura.

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AANZA KUTEKELEZA AHADI ZAKE KWA VITENDO

1
Na Gladness Muushi wa Fullshangwe-Meru
Chama cha mapinduzi Wilaya ya Meru kimefanikiwa kutoa   Kiasi cha
Shilingi Milioni sita  pamoja na ahadi ya Milioni nane ikiwa ni ahadi
ya Katibu mkuu wa chama hicho Abdulrahman  Kinana aliyotoa mwaka jana
kwa ajili ya maendeleo ya vijana na wanawake wa Wilaya hiyo ingawaje
inatawaliwa na wapinzani
 Akikabidhi fedha hizo  mapema jana  katika uzinduzi  wa mashina ya
wakereketwa wa ccm   mjumbe wa kamati ya siasa mkoa wa arusha John
Pallangyo alisema kuwa fedha hizo ni moja ya ahadi zilizotolewa na
katibu mkuu wa ccm taifa Abdulrhaman Kinana mara alipofanya ziara ya
kujitambulisha mwaka  jana
Alisema kuwa mara baada ya katibu huyo kufanya ziara wilayani humo
aliamua kuwaunga mkono  vijana wa bodaboda  na wanawake wajasiramali
wa wilaya hiyo mkono ili waweze kujiendeleza kiuchumi ili waweze
kujikwamua katika hali ngumu ya kimaisha.
Aliongeza kuwa kwa kuwa ajira ni sehemu ya ilani ya chama cha
mapinduzi wameamua kutekeleza ahadi hiyo ili kuhakikisha kuwa vikundi
hivyo vinajiendeleza na kuachana na hali ya kuwa tegemezi  kwa kuwa
kupitia fedha hizo wataweza kujipatia mitaji ya kujienedeleza.
“Katika kutekeleza ilani ya chama chetu cha mapinduzi ni lazima
kuhakikiasha kuwa ajira inakuwepo hasa kwa vijana hivyo naombeni fedha
hizi mzitumie kwa uangalifu ili ziweze kuwasaidia kujiajiri wenyewe na
pia zitawasaidia kuachana na makundi ya upotoshaji”alisema Pallangyo

Kwa upande wake katibu wa chama hicho wilaya ya meru Langaeli Akyoo
alitoa wito kwa vijana wote na wanawake wa uwt wilayani humo kutumia
vizuri mitaji waliyopewa na chama hicho na kuhakikisha kuwa fedha hizo
zinawabadilishia hali zao za maisha pamoja na familia zao.
Aidha akyoo akielezea kuhusiana na uzinduzi wa mashina ya wakereketwa
alisema kuwa ni mkakati wa wa chama hicho wa kuhamasisha wananchi wote
katika harakati zake za kurudisha jimbo lililoko chadema na
kulirudisha mikononi mwao
Hata hivyo katika uzinduzi huo  mashina   yaliyozinduliwa ni pamoja na
kilala,usa madukani,sabato,imbaseny madukani,mji mpya,njia ng’ombe
,kimandafu pamoja na Arudeco.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNI 10, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


1 8a11b

2 bd675

Sunday, June 09, 2013

AKAMATWA KWA KUIBA STULI YA MWENGE WA UHURU...!!!

 

JIJI la Arusha limeendelea kujijengea sifa ya kuwa moja ya maeneo yenye vituko, kufuatia kijana mmoja mkazi wa eneo la Phillips, kata ya Sekei jijini humo, Hamad Rashid (32) kukamatwa leo akiiba kiti (stuli) kinachotumika kuwekea mwenge wa Uhuru wakati mwenge ukiwa katika mbio zake mkoani Arusha.
Tukio la kuiba na kisha kukamatwa limetokea jana saa 11 jioni katika eneo la Sanawari Mataa eneo lililopangwa kwaajili ya mkesha wa mwenge huo baada ya kukamilisha mbio zake na kazi ya kuweka mawe ya msingi na uzinduzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Kamanda wa polisi mkoa wa  Arusha Liberatus Sabas ameithibitishia Nkoromo Blog kutokea tukio hilo na kwamba mtuhumiwa huyo alikamatwa na polisi waliokuwa wakiulinda mwenge pamoja na kiti hicho.

SALAMA JABIR ATAMANI KUOLEWA NA A.Y.....!!!

  

Mtangazaji mahili wa show za TV/Radio aliyeisimamisha wima show mpya na kali inayorushwa kupitia channel 5 ‘Mkasi’ namzungumzia Salama Jabir ametupia ‘neno’ kupitia kipindi hicho kuwa huenda siku moja akaolewa na AY!

Kama uliiangalia show ya Mkasi jumatatu ama marudio yake leo (jumamosi) ambapo crew nzima ya kipindi cha mkasi chini ya C.E.O na Producer wa show Ambwene Yesaya ‘AY’ walikuwa wakieleza changamoto na mambo mbalimbali waliyokutana nayo wakati wanaanza kufanya kipindi hicho, mwishoni Salama ambae alikuwa akimuelezea AY kuwa ni msanii ambae anajivunia kufanya nae kazi kutokana na jinsi alivyomchapakazi na mtu wa kuaminika alimaliza kwa kusema “huenda ipo siku moja tutaona..!”.

Wote tunajua Salama  alivyo mtu wa utani sana, kitu kinachoongeza burudani ya ziada katika show zake, alitamka hivyo na kumgeukia AY akimuuliza, na AY mwenyewe akajikuta anacheka na kukubali.
Pengine ulikuwa ni utani tu, lakini hakuna aijuae kesho ukizingatia wote wako single!

"MNAOWANIA URAIS MSIKUBALI KUPOKEA PESA ZA HUYU MFANYABIASHARA FISADI AMBAYE NI KINARA WA MADAWA YA KULEVYA".... REGINALD MENGI


Mwenyekiti wa makampuni ya IPP Reginald Mengi ametoa ya moyoni kwa wote wenye mpango wa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania miaka miwili ijayo.

Bwana Mengi ameyatoa maombi yake ya moyoni na kuyaweka hadharani kupitia akaunti yake ya twitter June 7, na hiki ndicho alichokiandika.

“Nawaombea Mungu wanaotaka Urais wasipokee mshiko wa mfanyabiashara fisadi mkubwa ambaye pia ni kinara wa madawa ya kulevya.”

Swali ni mfanyabiashara gani, hilo linaweza kuwa ni jiwe gizani kama yupo kweli aliyetajwa litakuwa limemfikia. 
Na  kama  kuna  msomaji  wetu  anayemjua, ANARUHUSIWA  KUMTAJA  kwenye  COMMENTS  hapo  chini

WASHINDI WA TUZO ZA MUZIKI ZA KILI ( KILIMANJARO ) 2013


KALA JEREMIAH, OMMY DIMPOZ  WATISHA KWA KUZOA TUZO TATU 

* CHALZ BABA,  , OMMY DIMPOZ  WAZOA TUZO MBILI MBILI

NEY WA MITEGO ABEBA TUZO NDANI YA SIKU YAKE YA KUZALIWA

*OMMY DIMPOZ AMSHUKURU ZITTO KABWE KWA KUFANIKISHA UTENGENEZAJI WA VIDEO YAKE YA BAADAE

* ZEMBELA ATISHA KWA USHEHERESHAJI

* SALEHE ABDALLAH YAZIPU NA KILIMANJARO BAND WABEBA TUZO ZA HESHIMA
* LADY JAY DEE ABEBA TUZO YA MSANII BORA WA KIKE


MBUNGE WA MTWARA MJINI AKAMATWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUCHOCHEA VURUGU ZA MTWARA

Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limemkamata mbunge wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnain Murji likimtuhumu kuchochea vurugu za kupinga mradi wa bomba la gesi kutoka mkoani humo kwenda jijini Dar es Salaam.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Msemaji wa Jeshi la polisi nchini, Advera Senso zinaeleza kuwa Murji alikamatwa jana jioni nyumbani kwake maeneo ya Shangani mjini Mtwara.

Kukamatwa kwa mbunge huyo kunakuja ikiwa zimepita siku tano tangu viongozi wanne wa vyama vya upinzani mkoani Mtwara, kufikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mtwara, Juni 4, mwaka huu wakikabiliwa na mashtaka matatu ikiwamo kula njama, kufanya uchochezi na kuamsha hisia mbaya kwa wakazi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Washtakiwa hao ni Katani Ahmed Katani (33) na Saidi Kulaga (45) wa CUF, Hassan Uledi (35) wa NCCR Mageuzi na Hamza Licheta (51) wa TLP, wote wakazi wa Mtwara.

Taarifa zaidi zilieleza kuwa baada ya polisi kumkamata mbunge huyo, walifanya upekuzi katika nyumba yake kwa saa kadhaa na baada ya kujiridhisha walikwenda kupekua na ofisi yake.


“Amekamatwa kwenye saa 11:00 jioni, hata hati ya kukamatwa kwake imeeleza kuwa anatuhumiwa kuchochea vurugu za kupinga gesi inayopatikana mkoani Mtwara kwenda Dar es Salaam,” alisema Katibu wa Mbunge huyo, Meckland Millanzi.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 9, 2013

2 b911e

3 21fb8

Saturday, June 08, 2013

WENGI WANACHANGANYA MAMBO, ILA HUU NDIO UHUSIKA WA BIG BROTHER NA FREEMASON

WATU WANASEMA MANENO UUMBA, INAWEZA KUA KWELI AU SI KWELI. JIONI HII WAKATI NIKIZUNGUKA ZUNGUKA NIMEKUTANA NA PICHA HAPO JUU IKIICHAMBUA LOGO MPYA YA BIG BROTHE. KAMA UNAVYOONA HAPO JUU KATIKA PICHA UTAONA KUA LOGO HIYO INAHUSISHWA NA MAMBO YA FREEMASON. UKIANZA NA HILO JICHO PAMOJA NA VITU VINGINE.

 SO KAZI KWAKO KUCHAMBUA PUMBA ZIPI NA MCHELE UPI.

HII NDO NYUMBA YA MASANJA MKANDAMIZAJI ALIYO JENGA KIJIJINI KWAO

Aliyekuwa na Ngwair "M 2 The P" Aongea na Kusema Haya...!!!

 'M 2 the P' ambaye awali naye aliripotiwa kuwa amefariki kabla ya taarifa hizo kukanushwa, alisema jana kuwa hadi sasa hajui nini kiliwatokea.
Msanii huyo alisema kwamba hakumbuki kilichotokea hadi wakazidiwa na kukimbizwa hospitali wakiwa hawajitambui.

Alisema pia bado anajisikia anaumwa hadi sasa licha ya kuruhusiwa kutoka katika hospitali ya St. Hellen Joseph ya Afrika Kusini alikokuwa amelazwa.
chanzo:Nipashe
Msanii 'M 2 the P' ambaye alikuwa na marehemu Albert Mangweha nchini Afrika Kusini wakati rapa huyo anafariki na yeye pia kuzidiwa hadi kulazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi, alihudhuria mazishi mjini Morogoro juzi.

MAGARI MATANO YALIYOWAHI KUTUMIWA NA HAYATI BABA WA TAIFA ENZI ZA UHAI WAKE

Leo tupo katika utalii wa ndani kwa kutazama baadhi ya  magari aliyotumia Baba wa Taifa na Rais wa kwanza wa Tanzania Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wakati wa harakati za Uhuru na baada ya Uhuru mpaka alipofariki Oktoba 14,1999. Maelezo ya makala haya ni kwa mujibu wa nyaraka zilizopo Makumbusho ya Taifa, Dar es Salaam hasa kuhusiana na magari na miaka ya magari yalipotumika. Fuatana nasi.
1.AUSTIN MORRIS A-40

AUSTIN MORRIS A-40

 Gari aina ya  Austin Morris A-40 lilitengenezwa nchini Uingereza kati ya mwaka 1940 – 1950. Ni gari la kwanza kutumiwa na Baba wa Taifa na Rais wa kwanza Tanzania hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JUNI 8, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
.
.

SHOW YA SNURA YAACHA WANAUME MIDOMO WAZI, KWELI MAJANGA


 

Naamini kwapicha hizi uwezi kosa show yake jumapili hii NEW MAISHA CLUB atazindua video yake ya majanga kuwa mjanja kuwa wa kwanza kuiona, atasindikizwa na WEMA SEPETU atakata utepe wa video ya majanga,MIRROR,SAMIR,ALI NIPISHE,TIMBULO,BAUCHA,MENINAH, na MADEE kiingilio 10,000 tu hii show sio yakukosa kabisa.
 

MWIGIZAJI WA KIKE WA BOLLYWOOD “JIAH KHAN” AJIUA IKSA MAPENZI


Muigizaji maurufu ambae ni mmoja kati ya wanadada warembo nchini India anaejulikana kama “Jiah Khan” amekutwa amekufa juzi kwa kujiua baada ya kujua Boyfriend wake ana mwanamke mwingine….

Mama yake na Khan amesema kua alirudi na kukuta mwili wa mtoto wake akiwa ameshakufa huku Police wakiwa bado wanachunguza chanzo cha kifo cha mrembo huyo ila baadhi ya majirani walizungumza na Mtandao wa BBC na kusema kua wanachujua mwanadada Khan alikua na mkwaruzano na BF wake…..

Jiah Khan amefariki wakiwa na Miaka 25 na alijipatia umaarufu mkubwa Inchin india baada ya kuigiza na mkongwe wa tasnia ya movie anaijulikana kama Amitah Bachchan na pia aliweza kuigiza na Aamir Khan na Akshay Kumar kwa wale mnaofatilia Bollywood Movies hakika mnawatambua hawa.

mwili wa Jiah Khan ulipelekwa Hospital kwa uchunguzi zaidi…..


Khan alizaliwa New York na akakulia London kabla ya kwenda Mumbai India na kujiingiza kwenye mambo ya sanaa ya uigizaji wa filamu…

Filamu yake ya Mwisho kuigiza inaitwa Housefull ambayo ilitoka mwaka 2010..

TAZAMA VIDEO YA MAZISHI YAKE HAPA

Popout

SPIKA wa Bunge, Anne Makinda amekiri kuwepo kwa vitendo ngono UDOM.

SPIKA wa Bunge, Anne Makinda amekiri kuwepo kwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na rushwa ya ngono kwa wanafunzi wa kike katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na hivyo kukataa mwongozo wa mbunge akisema hali iko hivyo.


Makinda alitoa kauli hiyo jana mjini hapa wakati Bunge likiwachagua wawakilishi wake katika mabaraza ya vyuo na SADC-PF, ambapo Naibu Waziri wa Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu aliuliza swali hilo la uwepo wa vitendo vya rushwa ya ngono.


Mwalimu alimuuliza mmoja wa wagombea, Murtaza Mangungu (CCM) kuwa UDOM imekithiri kwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kwa wanafunzi wa kike kuombwa rushwa ya ngono na baadhi ya wahadhiri wasio waadilifu.

Naibu waziri huyo alitaka kujua, Mangungu ataondoshaje kero hiyo kwa wanafunzi wa kike chuoni hapo, endapo atachaguliwa kuwa mjumbe wa baraza.

Katika majibu yake, Mangungu alisema kuwa atashirikiana na wenzake kuhakikisha wanaondosha kero hiyo kwa wanafunzi wanaofanyiwa vitendo hivyo.

HOUSE GIRL AJINYONGA KISA PENZI LA CHRISTOPHER...!!






Mfanyakazi wa ndani aliyejiua kisa mapenzi aitwaye Devotha Sanga leo ameagwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam. 
Marehemu Devotha alijinyonga Juni 4 mwaka huu akiwa nyumbani kwa bosi wake eneo la Kitunda jijini Dar kwa wivu wa mapenzi. 
Devotha alikuwa katika penzi na kijana mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Christopher anayedaiwa kuwa na wapenzi wengi kiasi cha kusababisha marehemu kuchukua uamuzi huo. 
Baada ya kuagwa mwili wa Devotha umesafirishwa kuelekea Njombe kwa mazishi.

Friday, June 07, 2013

NGONO ZAANZA KUTAWALA JUMBA LA BIG BROTHER.....VIDEO YA BOLT NA BETTY YANASWA WAKIFANYA MAPENZI LIVE


Mpaka sasa tayari tumeshuhudia couple 4 za housemates katika Big Brother ‘The chase’ , lakini couple ya mu Ethiopia Betty na mu Sierra Leon Bolt ndio ilikuwa ya kwanza kufahamika katika wiki ya kwanza toka mchezo uanze (May 26).


bolt & betty


Couple ya Bolt na Betty ndio ilikuwa ya kwanza pia ku’kiss kama uthibitisho wa ‘love at first sight’. Baada ya hapo maisha ya mjengoni yaliendelea vizuri huku mapenzi ya ‘love birds’ hawa yakizidi kukua kila kukicha japo waliamua kupeleka mambo taratibu.


Lakini wiki hii inaonekana kiu ya toka (May 26) iliwakaba ‘love birds’ hawa na kuamua kuikata kwa kufanya kile wanachofanya wapenzi wanapokuwa faragha (watu wazima naamini mnanielewa) yes , they did it! Bolt iliifunga nut ya Betty usiku wa manane wakati washiriki wenzao wakiwa wamelala!!


Ikiwa ni sehemu ya kujaribu kuyaokoa mapenzi yao, wiki hii baada ya Betty kutwaa ukuu wa Diamond House (HOH) aliweza kupata mamlaka ya kumuokoa mshiriki yeyote anayekuwa ameingia kikaangoni. 
Hivyo aliitumia nafasi hiyo kuliokoa penzi lake kwa kumuokoa Bolt ambaye alikuwa amependekezwa kuingia kikaangoni, na kumchagua Feza Kessy wa Tanzania aingie kikaangoni badala ya kipenzi chake.


video  mbili  za  uchafu wao...


video
video

TANGAZO KWA WAKAZI WA MBEYA

Nafasi za Kazi na Mafunzo

SIFA:


>>> Elimu ya kidato cha nne au zaidi.
>>> Taaluma ya uandishi wa habari ni added advantage.
>>> Uwezo, ufahamu, utundu, uzoefu, na ujuzi katika matumizi ya "Mitandao ya Kijamii" ndio kigezo kikuu.
>>> Umri miaka 18 na kuendelea.
>>> Uchapakazi, kujituma, creativity na ubunifu katika masuala ya mitandao ya kijamii ni vigezo muhimu.
>>> Awe mkazi wa Mbeya Mjini.


NAFASI ZILIZOPO NI NNE KAMA VIGEZO VITAKIDHIWA.

FIKISHA MAOMBI YA KAZI OFISI YA JIGAMBE (MbeyaCity.com) ILIYOPO KATIKA YA SAE NA ILOMBA OPPOSITE/MKABALA NA MASHOKO BAR.

The Boss lady Huddah Monroe na Prezzo Mapenzi Tele, Diva Aamua Kuweka Picha ya Nusu Uchi Kupoteza Soo

Prezzo akiwa na huddah jana muda mchache baada ya lady boss kutua katika  ardhi ya kenya.. ahahahahahah  prezzo kajiachiajeee!!!
Baada ya huddah kuweka picha yake akiwa na prezzo na kuzua gumzo ndani ya mtandao huo wa twirraa, dada yetu akaamua kuweka picha yake ya.....(sijaielewa sijui AVI na hii ahahahha samahani lakini) ili kupotezea soo hilo..
ahahahahah Sasa bado hatuelewi  kama ile LOVE AT THE FIRST SIGHT IMEISHIA WAPI maana presidente anaongea kwa vitendo tu!! #okeee

Source: Zeddylious blog

HUYU NDO MBUNGE ALIYEHUKUMIWA KWENDA JELA MIEZI KUMI, HILI NDO KOSA ALILOFANYA

 

MBUNGE wa Mbarali, Modestus Kilufi (CCM) amehukumiwa kifungo cha miezi 10 baada ya kupatikana na hatia ya kutishia kuua, Mbunge huyo (51) alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Oktoba 10 akidaiwa kutishia kumuua Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ruiwa, Mbarali, Jordan Masweve.


Kabla ya kusoma hukumu hiyo leo Mbunge aliomba Mahakama impunguzie adhabu, kwani ana watoto watano kati yao wawili wanasoma Chuo Kikuu na wananchi wanamtegemea kuwasilisha matatizo yao bungeni.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya, Michael Mteite, alisema ameridhika na ushahidi wa upande wa mashitaka ukiongozwa na mawakili wa Serikali, Epimack Mabrouk na Griffin Mwakapeje, pia mawakili wa upande wa mashitaka walimwomba Hakimu Mteite kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa, ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.

"Kutokana na maelezo hayo na ushahidi ulioletwa mahakamani, ninakuhukumu kifungo cha miezi 10" alisema Hakimu Mteite.

Mbunge akihojiwa katika chumba cha mahakama alisema unajuwa siku hizi haki inatendeka pale tu iwapo mwanaCCM ametiwa hatiani, lakini kama ni mpinzani ametiwa hatiani utasikia ooh kaonewa au hii ni hukumu kutoka ikulu, hata hivyo alisema atakata rufaa katika hukumu hiyo

SAKATA LA DADA MTANZANIA KUNYONGWA WIZARA YA MAMBO YA NCHI ZA NJE YASEMA..

Dada anaetuhumiwa kukamatwa na madawa ya kulevya.

Akizungumza na Gazeti la Mwananchi jana Mkuu wa Kitengo cha Habari cha Wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa, Mkubwa Ali, alikiri kukamatwa kwa watu hao (majina yanahifadhiwa) ambao mmoja ni mkazi wa Ilala na mwingine wa Magomeni jijini Dar es Salaam. “Taarifa tulizonazo zilizo rasmi kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Misri kwa sasa ni kukamatwa kwa Watanzania wawili waliokuwa wakisafirisha heroin kuelekea Bara la Asia na walikamatwa nchini Misri wiki mbili zilizopita.”

“Tumewasiliana na balozi wetu nchini Misri amesema hana taarifa za kuhukumiwa kunyongwa kwa watuhumiwa hao, isipokuwa wameshasomewa shtaka lao la awali. Wapo rumande kwa sasa kwani kesi hiyo imetajwa mara moja tu. Balozi amekiri kushikiliwa kwa watuhumiwa hao wakiwa na dawa zinazoaminiwa ni za kulevya,” alisema.

Alisema watuhumiwa wote wanashikiliwa polisi na wanatarajia kufikishwa mahakamani wakati wowote.

Video inayomwonyesha mmoja akikaguliwa na maofisa wa polisi wa nchini Misri na kukutwa na dawa hizo, ilisambaa siku nne zilizopita katika mitandao mbalimbali ya kijamii.,

TFF KUTOA TAMKO KOMBE LA KAGAME

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema linafanyia kazi hoja ya klabu za Yanga na Simba kutaka kujitoa kwenye michunao ya Kombe la Kagame zikihofia usalama wa Sudan Kusini.
Akizunguza kwa njia ya simu jana jioni, Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema baada
ya kuibuka hofu hiyo, wanafanyia kazi jambo
hilo kabla ya kutoa tamko rasmi.
“Tunalifahamu vizuri jambo hilo. Tutakaa na kujadili kwa kina kabla ya kutoa tamko rasmi,” alisema Angetile.
Kauli ya Angetile imekuja siku moja tangu Simba na Yanga zitamke kujitoa kwenye michuano hiyo kama itafanyika Darfur zikhofia hali ya usalama.
Juzi, kwa nyakati tofauti viongozi wa Simba na Yanga, walisema wao wametafakari kwa kina tahadhari ya Serikali kupitia kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, hivyo hawakwenda Darfur.
Viongozi hao walitamka wazi kuliacha jambo hilo mikononi mwa TFF kuamua nini kifanyike baada ya tahadhari ya serikali kuona nini kifanyike.

HUYU NDIYE DADA WA KIZUNGU ANAYEDAIWA KUWA NDIO SHEMEJI WETU KWA NGWEA

Mzungu anayedaiwa kuwa alikuwa demu wa Ngwea aitwaye Misheily akilia kwa uchungu wakati wa kuaga.
Na Gladness Mallya
MAJONZI na vilio vilitawala juzi katika zoezi la kuuaga mwili wa marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’ kwenye Viwanja vya Leaders lakini mmoja wa waliotia fora katika kuangua kilio alikuwa dada mmoja mzungu anayedaiwa kuwa alikuwa demu wa Ngwea aitwaye Misheily.Mzungu huyo alionekana akilia kwa uchungu huku akitoa maneno yaliyoashiria kuwa ameumia sana kuondokewa na ‘mtu’ wake huyo ambaye huenda walikuwa na malengo mazuri ya baadaye.

...akiwa na simanzi nzito.
Aidha, kilio alichokuwa akiporomosha binti huyo kiliwafanya watu waliokuwa karibu naye kumsikitikia na kuzidishiwa majonzi kwani ilifika wakati akaishiwa nguvu.
...Akitolewa eneo hilo kwa kusaidiwa na mtu wake wa karibu.
Paparazi wetu alijaribu kumfuata na kumuomba kuzungumzia juu ya kifo cha Ngwea lakini alikataa na kusema asingeweza kufanya hivyo kufuatia majonzi aliyokuwanayo huku akionekana kutoamini kama jamaa yake huyo ametutoka .
 
na global publisher

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 7, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
.
.
.
.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...