Thursday, June 20, 2013
Wednesday, June 19, 2013
LUNDENGA AMTIMUA MREMBO JUKWAANI BAADA YA KUTINGA NA KIVAZI CHA NUSU UCHI...!!!

MWENYEKITI
wa Kamati ya Mashindano ya Miss Tanzania, Hashimu Lundenga Jumamosi
iliyopita alimtimua mshiriki wa shindano la Redd’s Miss Morogoro 2013, Saphina Chumba (20) jukwaani wakati shindano hilo lilipokuwa likiendelea.
Tukio
hilo lilitokea Jumamosi iliyopita katika Ukumbi wa Hoteli ya Kitalii
ya Nashera mjini hapa wakati mrembo huyo alipokuwa akiwania kuvaa taji
la mkoa huo.
Kisa cha mrembo huyo aliyevalia namba 5 kutimuliwa ni kukiuka maadili na kanuni za mashindano hayo kwa
kuvaa nusu utupu mbele ya mgeni rasmi ambaye alikuwa Mbunge wa Kilosa,
Mustapha Mkulo na mbele ya Kamati nzima ya Miss Tanzania.
Baada
ya kuona jinsi alivyovaa, Lundenga na kamati yake walikubaliana
kumtimua mshiriki huyo kwa kumwita Jaji Mkuu wa shindano, Alex Niktasi
na kumtaka amuondoe haraka.
Mbali
na Chumba, pia jaji alimtimu mrembo mwingine aliyevalia namba 8, Neema
Joel (20) kutokana na kushiriki shindano hilo mara mbili mwaka huu,
inadaiwa mara ya kwanza alishiriki mkoani Arusha.
Lundenga
alipohojiwa na waandishi wa habari alisema kamati yake inataka kuendeleza
nidhamu tangu ngazi ya chini, hivyo hawawezi kuruhusu utovu wa nidhamu.
CCM YAOMBWA IRUHUSU WATU KUJITANGAZA URAIS.
VUGUVUGU
la Uchaguzi Mkuu wa 2015 linazidi kupamba moto ambapo juzi aliyekuwa
Waziri Mkuu, Frederick Sumaye, ameomba CCM itoe ruhusa mapema kwa
wanaowania urais kuanza kutangaza nia lakini bila kukampeni.
Sumaye
ambaye alipata kugombea urais mwaka 2005, alionya kuwa kama CCM
haitaruhusu wagombea kutangaza nia leo, yanayofanyika chini chini ni
mabaya zaidi.
Akizungumza katika kipindi cha dakika 45 juzi, Sumaye mbali na kuitaka CCM kuruhusu wanachama wake kuan
za
kutangaza nia ya kugombea mapema, pia alielezea athari za muundo wa
Serikali tatu uliopendekezwa na Rasimu ya Katiba mpya na mfumo mpya wa
kusoma Bajeti ya Serikali bungeni.
Urais 2015
MDADA ACHEZEA KICHAPO KWA KUFANYA UKAHABA JIRANI NA MSIKITI...!!!

Richard Bukos na Issa Mnally
KHAAA!
Operesheni Fichua Maovu ‘OFM’ iliyo chini ya Global Publishes, ipo
mzigoni na hivi karibuni imenasa tukio la aina yake ambapo mke wa mtu
amechezea kichapo ‘hevi’ akidaiwa kufanya ukahaba jirani na msikiti,
Risasi Mchanganyiko lina kisa kamili.

WENZAKE WATOKA NDUKI
Baada
ya wenzake kufanikiwa kutoka nduki mithili ya mwanariadha Usai Bolt wa
Jamaika, mwanamke huyo alishuhudiwa akila bakora kisha akapelekwa katika
Kituo cha Polisi Kijitonyama, Dar akaunganishwa na wengine waliokamatwa
usiku huo.
Ilielezwa kuwa wanawake hao wamekuwa wakiuza miili kwa wanaume karibu na msikiti huo na pembezoni mwa baa hiyo.
Ilisemekana
kuwa kumekuwa na kawaida ya wanawake hao kusimama maeneo ya nyumba hiyo
ya ibada na kufanya biashara hiyo huku wakichafua mazingira kwa kutupa
ovyo kondomu na kujisaidia maeneo hayo.

NGUO YA NDANI YAMVUKA
Wakati
mwanamke huyo akicharazwa bakora, nguo ya ndani ilimvuka huku akipiga
kelele kuwa hatarudia kufanya hivyo na kama akirudia basi akatwe kichwa.
BAADA YA KUZUSHIWA KIFO, HIKI NDICHO ALICHOSEMA MSANII SAIDA KAROLI
HOFU YATANDA MKOANI SHINYANGA JUU YA MAUAJI YA WATOTO
( Picha na maktaba )
Na Steve Kanyeph
Wakazi wa manispaa ya Shinyanga wamegubikwa na hali ya hofu na wasiwasi kufuatia matukio ya mara kwa mara ya kuuawa kwa watoto wa kike wanaofanyiwa ukatili na unyanyasaji na kisha kuuawa ama kutelekezwa wakiwa hawajitambui.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi hao walisema vitendo vya unyanyasaji kwa watoto wa kike wenye umri wa kuanzia miaka tisa hadi kumi na nne katika manispaa ya Shinyanga kwa zaidi za miezi minne sasa vimekithiri hali ambayo inatishia amani kwa wakazi hao.
Akizungumza na Jambo Tz jana mkazi wa eneo la Ngokolo katika Manispaa ya Shinyanga bi Dafrossa Pius ambaye ni mjasiliamali, siku moja baada za tukio la kuuawa kikatili kwa binti mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kumi na mbili hadi kumi na tatu, kisha mwili wake kufungwa kama mzigo kwenye boksi na kutupwa kwenye ghuba la takataka katika eneo hilo la ngokolo mitumbani,alisema ni ukatili usiovumilika hata kidogo “ukatili kama huu kwa watoto wa kike wasio na hatia haupaswi kuvumiliwa wala kufumbiwa macho``
Tuesday, June 18, 2013
SIRI NZITO YA KIFO CHA MWANAMUZIKI LANGA
Na Mwandishi Wetu
MWILI
wa mwanamuziki Langa Kileo jana (Jumatatu) ulipumzishwa kwenye nyumba
ya milele katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar lakini nyuma ya kifo
chake kuna siri ambayo rafiki yake wa karibu (jina linahifadhiwa) mkazi
wa Mikocheni A jijini Dar ameamua kuiweka hadharani.
Akizungumza
na Uwazi juzi, rafiki huyo wa marehemu alisema, siku chache kabla ya
kifo chake alimfuata na kumwambia kuwa Israel mtoa roho anamtembelea
usiku na anahisi siku si nyingi atamfuata mshikaji wake aliyetangulia
mbele ya haki, Albert Mangweha ‘Ngwea’.
“Hii
ni siri ambayo hata ndugu zake hawaijui lakini mshikaji alijua anakufa.
Alijitahidi kukikwepa kifo lakini alishindwa. Siku chache kabla hajafa,
usiku alikuja kwangu na kuniambia kule kwao kwenye geto lake analoishi
ambalo liko ghorofani, anaona mauzauza na anahisi kifo kinamuita.
“Nilishangazwa
sana na maneno yale. Akazidi kuniambia eti kwa jinsi mambo
yanavyokwenda hawezi kuendelea kulala kwao na kuanzia siku ile angelala
na mshikaji wetu mwingine pale Geza, Mikocheni A.
“Kweli
siku hiyo alilala pale akiwa na hofu kubwa na asubuhi baadhi ya watu
wakawa wanamshangaa akiwa ‘amezima’ nje ya lile geto la mshikaji wake.
Alivyoondoka sikumuona tena mpaka nilipokuja kuambiwa yuko hoi kwa
malaria na kesho yake nikasikia hatunaye, nimeumia sana,” alisema mtoa
habari huyo.
Alipoulizwa juu ya
uhusiano wa kifo cha Langa na matumizi ya madawa ya kulevya, rafiki huyo
alisema: “Inaweza ikawa ngumu kwa ndugu wa marehemu kuhusisha kifo
chake na madawa ya kulevya lakini mimi namjua Langa nje ndani, ukweli ni
kwamba jamaa alikuwa akiendelea kula ‘mambo’.
“Alikuwa
anakuja maskani tunakula mambo yetu na hata wakati anafanya kazi kwenye
ile Kampuni ya Barrick hapa Dar, ilikuwa kabla hajaenda anapita kwanza
huku uswahilini kisha ndiyo anaenda. Kwa maana hiyo malaria ndiyo
iliyomuua lakini hata madawa yamechangia.”
Langa
alifariki dunia Juni 13, mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili
jijini Dar. Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi. Amini!
SORCE: Globalpublishers
JESHI LA POLISI LINAWASHIKILIA WABUNGE 4 WA CHADEMA KWA KUSABABISHA VURUGU ARUSHA

Jeshi
la polisi mkoani Arusha linawashikilia viongozi wanne wa CHADEMA na
watu wengine huku likiendelea kuwatafuta wabunge wawili na watu wengine.
Jeshi
la Polisi limesema limewatua nguvuni watu hao kwa makosa ya kuhutubia
mkutano haramu wakati wa kuwaaga marehemu waliopoteza maisha kwenye
mlipuko wa bomu uliotokea katika eneo la Soweto jijini humo mwishoni mwa
wiki. Makosa mengine ni wanayotuhumiwa kwayo ni kufunga barabara na kuwashambulia askari polisi.
Amesema wataendelea kubaki korokoroni hadi uchunguzi utakapokamilika.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas amewataja Wabunge wanaoshikiliwa ni pamoja na Tundu Lissu na Mustapha Akunai.
Wanaotafutwa
ni pamoja na Mwenyekiti CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe na Mbunge wa
Arusha Mjini, Godbless Lema ambao waliponyoka mikono ya polisi.
MBOWE ADAI ANA USHAHIDI WA ALIYERUSHA BOMU, ARUSHA
MWENYEKITI
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe
amefichua siri kuhusu tukio la mlipuko wa bomu lililotokea jusi katika
viwanja vya Soweto, jijini Arusha.Katika kauli yake jana, Mbowe ameibua tuhuma nzito dhidi ya Jeshi la Polisi, ambapo alidai kuwa askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) ndiye aliyerusha bomu hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa,baada ya kutembelea majeruhi katika Hospitali ya Selian, Mbowe alisema chama chake kina ushahidi wa kutosha juu ya askari huyo kurusha bomu.
Mbowe ambaye pia ni kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni,alisema wamefanikiwa kupata ushahidi wa kutosha juu ya tukio hilo baya linalochafua taswira ya nchi.
VIDEO YA MSHIRIKI WA TANZANIA ( FEZA KESSY ) AKIMUOGESHA MSHIRIKI WA ZIMBABWE ( HAKEEM) NDANI YA JUMBA LA BIG BROTHER

Video hizi hutolewa na big borther wenyewe kwa jamii kama sehemu ya shindano hilo....
Wahiriki wote wa big brother wanajua
ya kwamba jumba hilo limezingirwa na kamera kila kona.Kwa hiyo, kama
mtu ataamua kufanya ufuska au kukaa uchi basi ajue kamera
zitamrekodi na
kumwanika hadharani....
Masharti hayo hujuzwa mapema kabla ya kuanza kwa shindano hilo...
Hakeem
Huyu ni mshiriki toka zimbabwe aliyepata bahati ya kuoga na dada yetu Feza ndani ya bafu moja
Feza
Huyu ni mshiriki toka Tanzania....Yuko ndani ya afu moja akioga na mshiriki wa Zimbabwe.....
Dakika chache baada ya kila mmoja kuoga kivyake,Hakeem anaamua kumuomba Feza amsugue mgongoni....
<< VIDEO IKO HAPA >>
CCM YASHINDA KATA 16 KATI YA 22 UCHAGUZI MDOGO WA MADIWANI,CHALAANI CHADEMA KUJITAFUTIA UMAARUFU MISIBANI
Itakumbukwa
tarehe 16/06/2013 ilikuwa ni siku ya uchaguzi mdogo wa madiwani kwa
baadhi ya kata nchini. Uchaguzi huo umefanyika kwenye kata ishirini na
mbili (22) kati ya kata ishirini na sita (26) zilizotangazwa kufanya
uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi wazi.
Matokeo tuliyoyapata toka kwenye maeneo yaliyofanya uchaguzi yanaonyesha kuwa kati ya kata 22 zilizofanya uchaguzi CCM tumeshinda kata 16 sawa na asilimia 72.72% na wenzetu wamechukua kata 6 zilizobaki sawa na asilimia 27.28%.
Tunawashukuru sana kote walikoonyesha imani yao kubwa kwa Chama chetu kwa kutupa dhamana ya kuendelea kuwatumikia. CCM inawaahidi utumishi uliotukuka.
Hata wale 27.28% walioamua kuwajaribu wenzetu, tunawatakia kila lakheri, kwani wametumia haki yao ya kidemokrasia kuchagua wanaodhani watawasaidia kufikia malengo yao ya kimaendeleo. Uchaguzi kwenye kata hizi zote umeisha sasa tuwatumikie wananchi.
Bw Nape Moses Nnauye
Matokeo tuliyoyapata toka kwenye maeneo yaliyofanya uchaguzi yanaonyesha kuwa kati ya kata 22 zilizofanya uchaguzi CCM tumeshinda kata 16 sawa na asilimia 72.72% na wenzetu wamechukua kata 6 zilizobaki sawa na asilimia 27.28%.
Tunawashukuru sana kote walikoonyesha imani yao kubwa kwa Chama chetu kwa kutupa dhamana ya kuendelea kuwatumikia. CCM inawaahidi utumishi uliotukuka.
Hata wale 27.28% walioamua kuwajaribu wenzetu, tunawatakia kila lakheri, kwani wametumia haki yao ya kidemokrasia kuchagua wanaodhani watawasaidia kufikia malengo yao ya kimaendeleo. Uchaguzi kwenye kata hizi zote umeisha sasa tuwatumikie wananchi.
Kata nne za jiji la Arusha hazikufanya uchaguzi baada ya kuahirishwa
kufuatia tukio la kusikitisha la kulipuka kwa bomu kwenye mkutano wa
kampeni wa Chadema mjini Arusha tarehe 15/06/2013.
CCM tunalaani tukio hilo la mlipuko wa bomu na matukio yanayofanana na hayo katika nchi yetu.
CCM tunalaani tukio hilo la mlipuko wa bomu na matukio yanayofanana na hayo katika nchi yetu.
MTUHUMIWA WA MAUAJI YA PADRI MUSHI AZIDI KUSOTA RUMANDE

Zanzibar.
Mahakama Kuu ya Zanzibar, imekataa kumwachia kwa dhamana, mshtakiwa
Omar Mussa Makame, anayekabiliwa na shtaka la kumuua Padri Evarist Mushi
wa Kanisa Katoliki.Hatua hiyo ilifanywa
jana na Jaji Mkuza Issac Sepetu, baada ya upande wa utetezi katika kesi
hiyo ,kuiomba mahakama imwachie kwa dhamana mshtakiwa hadi hadi hapo
upande wa mashtaka, utakapokamilisha upelelezi.Alisema mahakama itaendelea na kesi isiyokuwa na dhamana na ambayo upelelezi wake unaweza kuchukua hadi miezi tisa.
Jaji huyo alisema mahakama haifanyi kazi zake kwa kuzingatia taarifa za watu au magazeti yaliyoko nje yake.“Mahakama
hii haichukui vielelezo vya barua za nje ya chombo hiki. Mtu anayeweza
kusema kila kitu ni mkurugenzi wa mashtaka, yeye ndiye mwenye dhamana ya
kuondoa kesi mahakamani,” alisema Jaji Sepetu.
Baada
ya msimamo huo, wakili Abdallah Juma anayemtetea mshtakiwa, aliiomba
mahakama iuamuru upande wa mashtaka ,kuharakisha upelelezi wa kesi hiyo.
Alisema ni vyema upande huo ukatoa muda maalum wa kukamilisha upelelezi huo.
Jaji aliipanga kesi hiyo kutajwa tena Julai 2 mwaka huu.
Omar ambaye ni mkazi wa Mwanakwerekwe, Mjini Magharibi, anadaiwa kumuua kwa kumpiga risasi Padri Mushi Februari 17 mwaka huu.
Mwananchi
BANANA ZORRO KURUDI KWENYE GAME KWA KISHINDO
Msanii
na mmiliki wa Band ya B-band Banana Zorro amefunguka kuwa kimya kingi
siku zote kina mshindo na kueleza kuwa alikuwa kimya kwa sababu alikuwa
busy na kazi za Band lakini kwa sasa anatarajia kudodosha ngoma nyingine
siku za karibuni kwa wale fans wake kaeni mkao wa kura. Banana
amefunguka hayo leo alipokuwa katika Show ya Kikaangoni Live
inayofanyika kila siku ya Ijumaa kupitia Accounts za Facebook za Eatv na
East Africa Radio ambapo mashabiki wake wanapata nafasi ya kuuliza
maswali na yeye kuwajibu.
Moja ya shabiki aliuliza akitaka kujiunga katika B-band afanyaje na jibu lilikuwa anapaswa kufanya mazoezi ya kutosha na akiwa teyari awasiliane na meneja wake Allan Lucky na mambo yatakuwa poa.
Akizungumzia moja ya fanikio aliyopata katika Muziki ni pamoja na kumiliki Band yake mwenyewe ambayo ni B-band ambayo inaendelea kukuwa kila siku na kufanya vizuri pia.
Moja ya shabiki aliuliza akitaka kujiunga katika B-band afanyaje na jibu lilikuwa anapaswa kufanya mazoezi ya kutosha na akiwa teyari awasiliane na meneja wake Allan Lucky na mambo yatakuwa poa.
Akizungumzia moja ya fanikio aliyopata katika Muziki ni pamoja na kumiliki Band yake mwenyewe ambayo ni B-band ambayo inaendelea kukuwa kila siku na kufanya vizuri pia.
Subscribe to:
Comments (Atom)





.jpg)




