Friday, November 28, 2014

WANAUME 13 WASHTAKIWA KWA UDHALILISHAJI

Genge la Wanaume waliotekeleza vitendo vya udhalilishaji dhidi ya Wasichana 
 
Wanaume kumi na watatu wameshtakiwa kwa kujihusisha na vitendo vya udhalilishaji kwa Watoto mjini Bristol, ikiwemo vitendo vya ubakaji na kuwalazimisha watoto wa kike kujiingiza kwenye vitendo vya biashara ya ngono.
Mahakama ya mjini Bristol ilimsikiliza binti wa miaka 16 aliyebakwa na Wanaume watano raia wa kisomali.
Halikadhalika mdogo wake mwenye umri wa miaka 14 alibakwa na mmoja wa wanaume hao, Msichana huyo alipofika kumtembelea Dada yake.
Uchunguzi uliofanywa na Polisi ulibaini kuwa genge jingine la wanaume wenye asili ya kisomali liliwadhalilisha kijinsia wasichana wengine wanne.
Wasichana hao walilipwa pauni 30,au kupewa dawa za kulevya, vilevi na zawadi kwa ajili ya kushiriki vitendo vya ngono na wanaume wenye umri mkubwa wa jamii ya kisomali.
Miongoni mwa walioshtakiwa ,Watu sita walihukumiwa kifungo,wengine saba walitiwa hatiani siku ya jumatano. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...