Monday, June 17, 2013

VIONGOZI NA WAZAZI WAASWA KUFICHUA UOVU DHIDI YA WATOTO

(Picha na maktaba)
Na Mwandishi Wetu Steven Kanyeph.
Viongozi wa serikali kwa kushilikiana na wazazi wametakiwa kutoa taarifa kwenye vyombo husika wanapoona watoto wanafanyiwa vitendo vya ukatili unyanyasaji wa kijinsia, ukeketaji na kuozeshwa katika umri mdogo.

Hayo yamesemwa na mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa mkoa ambaye ni mkuu wa wilaya ya kishapu bwana; Willson Mkambaku kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya shule ya msingi Bubiki kata ya Bubiki wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.

Bwana Mkambaku amewataka viongozi na wazazi washilikiane kwa pamoja kuhakikisha watoto wanalindwa dhidi ya unyanyasaji, ubakaji .ulawiti , na kuhakikisha kuwa watoto wanaendelezwa kielimu kushiriki katika maamuzi , ikiwa ni pamoja na kukomesha ajira kwa watoto.

Aidha watoto waameitaka jamii kwa kushirikiana na viongozi kupiga vita imani potofu zenye kuleta madhara kwa watoto kama vile ukeketaji ,ndoa za lazima, uasherati , mauaji ya vikongwe ,albino pamoja na madawa ya kulevya.,

Madhimisho ya siku ya mtoto wa afrika hufanyika kila mwaka tarehe 16 mwezi wa 6 lengo ni kukumbuka mauaji ya kikatili ya mamia ya watoto wa shule yaliyofanyika katika kitongoji cha Soweto afrika ya kusini mwaka 1976 baada ya watoto kufanya maandamano ya kupinga ubaguzi wa rangi.

Kauli mbiu ya madhimisho hayo kwa mwaka huu ni KUONDOA MILA ZENYE KULETA MADHARA KWA WATOTO NI JUKUMU LETU SOTE

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...