KOCHA msaidizi wa Azam FC, Denis Kitambi,
amewatupia lawama washambuliaji wake kwa kushindwa kufuata maelekezo ya walimu,
kiasi cha kuyumbisha mwenendo wa timu hiyo katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu
Tanzania Bara.
Kitambi aliyasema hayo baada ya kumalizika kwa
mchezo wao na Simba na timu hizo kutoka sare ya 0-0, katika mechi ya ligi
iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kitambi alisema, sare
hiyo imefifisha mbio zao katika kuwania taji la Ligi Kuu linaloshikiliwa na
Yanga.
“Washambuliaji wetu wana kiwango kizuri, lakini
hakuna faida ya kuonyesha uwezo bora ikiwa unashindwa kuipatia timu yao mabao. Tangaza
biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo
Tz. tu-follow instagram @jambotz.