Tuesday, May 03, 2016

KOCHA WA AZAM ALAUM WACHEZAJI WAKE

KOCHA msaidizi wa Azam FC, Denis Kitambi, amewatupia lawama washambuliaji wake kwa kushindwa kufuata maelekezo ya walimu, kiasi cha kuyumbisha mwenendo wa timu hiyo katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Kitambi aliyasema hayo baada ya kumalizika kwa mchezo wao na Simba na timu hizo kutoka sare ya 0-0, katika mechi ya ligi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kitambi alisema, sare hiyo imefifisha mbio zao katika kuwania taji la Ligi Kuu linaloshikiliwa na Yanga.

“Washambuliaji wetu wana kiwango kizuri, lakini hakuna faida ya kuonyesha uwezo bora ikiwa unashindwa kuipatia timu yao mabao. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

LEICESTER CITY MABINGWA WAPYA EPL

Klabu ya soka ya Leicester City wameshinda taji la ligi kuu England katika historia inayovutia kwenye ligi hiyo. Suluhu ya 2-2 waliyoipata Tottenham dhidi ya Chelsea siku ya jumatatu usiku ilisababisha mafanikio hayo makubwa kuwahi kutokea kwa upande wa Claudio Ranieri.

Leicester walianza kampeni zao za ubingwa huku wakipewa nafasi moja tu kati ya 5000 kushinda taji la ligi na pia wakitoka katika janga la kutaka kushuka daraja. Lakini wamepoteza michezo mitatu tu katika kile kinachotafsiriwa kama hadithi za kale na ushindi wa kipekee katika timu hiyo. 

Wapinzani wao wa karibu Spurs, Arsenal,Manchester City, Manchester United na washindi wa ligi msimu uliopita Chelsea wameshindwa kuwazuia mbweha katika msimu mzima wa ligi.

Sunday, May 01, 2016

MWILI WA MAMA LUCY KIBAKI WAWASILI NCHINI KENYA

 Mama Lucy Kibakienzi za uhai wake.
Mwili wa mke wa aliyekuwa rais wa Kenya Mwai kibaki , mama Lucy Kibaki umewasili leo alfajiri mjini Nairobi ukitokea London Uingereza na kutumbukiza taifa zima katika kipindi cha maombolezi.

Mabaki ya bi Kibaki yalilakiwa katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta na rais Uhuru Kenyatta Naibu wake William Ruto na viongozi na wakenya wa haiba mbalimbali mwendo wa saa kumi na moja. Ndege iliyoileta familia ya rais Kibaki ilitua saa kumi na moja na dakika tatu na kupewa hadhi ya kitaifa.

AL SHABAB WAUA WANAJESHI 30 WA SOMALIA

Wanamgambo wa Al Shabab.
Wapiganaji wa Kiislamu wa Somalia, Al Shabab wanasema wamewauwa wanajeshi wa serikali zaidi ya 30. Al Shabab, wanadai kutekeleza mauaji hayo walipoteka tena kijiji cha Runorgood, Kaskazini-Mashariki mwa mji mkuu wa Somali Mogadishu.

Wenyeji wa kijiji hicho wamethibitisha, kwamba kijiji chao kinadhibitiwa tena na wanamgambo wa Al Shabab.
Wanamgambo wa Al Shabab.
Wapiganaji hao walikuwa wametimuliwa kutoka kijiji hicho hapo jana. Kwengineko nchini Somalia, watu kama watatu waliuwawa, kwenye shambulio la bomu, katika soko la mifugo huko Qoryoolay, inavoelekea shambulizi hilo lililengwa maafisa wa kukusanya kodi wa serikali.

SIMBA, AZAM ZATOKA SARE YA BILA KUFUNGANA

SIMBA SC imelazimisha sare ya bila kufungana na Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Matokeo hayo yatapokewa kwa furaha na mahasimu, Yanga ambao sasa wanaongoza Ligi Kuu kwa wastani wa pointi sita kuelekea mechi nne za mwisho. Kwa sare hiyo ya 0-0, Azam FC inafikisha pointi 59, wakati Simba sasa inakuwa na pointi 58, nyuma ya mabingwa watetezi, Yanga wenye pointi 65 baada ya timu zote kucheza mechi 26.

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Mathew Akrama wa Mwanza, aliyesaidiwa na washika vibendera Abdallah Mrisho wa Pwani na Omar Kambangwa wa Dar es Salaam hakukuwa na mashambulizi ya kusisimua na timu zote zilionekana kucheza kwa tahadari kupita kiasi, hivyo kuufanya mchezo upooze. 

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...