Thursday, January 07, 2016

MTOTO WA KARUME ASHAURI SHEIN KUKAA PEMBENI

Mwanasheria wa kujitegemea nchini, Fatma ofisinakizungumzaini Dar es Salaam jana. Picha na Florence Majani

Dar es Salaam: Mwanasheria wa kujitegemea nchini, Fatma Karume amemshauri Rais wa Zanzibar, Ali Mohamed Shein kuachia madaraka.

“Dk Shein lazima aondoke kwa sababu kuendelea kubaki madarakani ni kuwanyang’anya Wazanzibari haki yao ya msingi,” alisema Fatma ambaye ni mtoto wa aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Fatma alisema kuwa mzozo wa Zanzibar umesababishwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salum Jecha kutangaza kufutwa matokeo yote ya Uchaguzi Mkuu visiwani humo wakati hana mamlaka kisheria kufanya hivyo.

JANUZAJ KUREJEA MAN U

Manchester United imemwita nyumbani Adnan Januzaj kutoka Borussia Dortmund ambako amekuwa kwa mkopo wa msimu mmoja.

United wamemtaka mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji arejee Old Trafford kwa sababu ya kukosa kuchezeshwa Ujerumani.

Januzaj, mwenye umri wa miaka 20, amecheza mechi 12 pekee katika klabu hiyo ya Bundesliga, sana akiingia kama nguvu mpya.

Tuesday, January 05, 2016

PROF. JAY KUHAMISHIA STUDIO YAKE MIKUMI

MSANII na Mbunge wa Jimbo la Mikumi, Joseph Haule ‘Profesa Jay’, amesema ana mpango wa kuihamishia studio ya Mwanalizombe kwenye jimbo lake ili aweze kutekeleza ahadi ya kuinua sanaa. Profesa Jay alisema kuwa moja ya ahadi alizowaahidi

wakazi wa Mikumi kwenye kampeni zake ni kuibua vipaji vipya ndiyo maana ameamua kuihamishia studio hiyo huko ili aweze kutekeleza ahadi hiyo.

“Mikumi kuna vipaji vingi vya muziki lakini hakuna aliyeweza kuviibua kwa miaka mingi, ila mimi nikiwa kama Mbunge wao nitatekeleza ahadi hii kwa kuihamishia studio yangu Mikumi ili wasanii chipukizi waweze kufanya kazi zao,” alisema Profesa Jay.

Mwanalizombe ni studio inayomilikiwa na msanii huyo ipo maeneo ya Mbezi Luis, jijini Dar es salaam na imeshatoa nyimbo kali kama Makamanda wimbo wa Sugu, Tatu Chafu na Kipi Sijasikia chini ya mtayarishaji Villy.

BENITEZ ATUPWA NJE REAL MADRID, ZIDANE ACHUKUA NAFASI

Uongozi wa klabu ya Real Madrid umemtimua kocha wake Rafael Benitez ambaye ana Miezi 7 tu katika Mkataba wake wa Miaka Mitatu.

Sasa nafasi yake imechukuliwa na mchezaji mkongwe mfaransa Zinedine Zidane ambaye awali alikuwa Kocha wa Kikosi B cha Real Madrid .

Hii inatokana na matokeo mabaya kwa timu hiyo, ambapo ilitoka Sare 2-2 na Valencia, katika Mechi ya La Liga, Sare ambayo imewaacha Vigogo hao nafasi ya 3 wakiwa nyuma ya Atletico Madrid kwa pointi 4.

Tangu atue Madrid, Benitez amekuwa si kipenzi cha Mashabiki wa Klabu hiyo, baada ya kufungwa bao 4-0 kwenye mechi ya El Clasico Mwezi Novemba na Mahasimu wao Barcelona, pia kutupwa nje ya michuano ya Copa del Rey.

Tuesday, December 29, 2015

ARSENAL YAPAA KILELENI


Wachezaji wa timu ya Arsenal

Washika bunduki wa London, Arsenal wamekaa kileleni mwa ligi ya England kwa pointi 39 baada ya kuichapa Bournemouth kwa mabao 2-0.

Arsenal walipata mabao yao kupita kwa beki Gabriel Paulista aliyefunga bao la kwanza Dakika ya 27 ya mchezo kisha kiungo wa Kijeruman Mesut Ozil, akahitimisha kazi kwa bao la pili alilolifunga katika dakika ya 63.

Nao Mashetani Wekundu wa Man United wakaenda sare ya 0-0 na mabingwa watetezi Chelsea, Everton wakicheza katika dimba lao la Goodson Park wakalala kwa kipigo cha mabao 4-3 dhidi ya Stoke city.

Matokeo mengine ni: Crystal Palace 0 – 0 Swansea Norwich 2 – 0 Aston Villa Watford 1 – 2 Tottenham West Brom 1 – 0 Newcastle West Ham 2 – 1 Southampton

Monday, December 28, 2015

MLINZI WA OSAMA BIN LADEN AFARIKI DUNIA


Al Bahri


Taarifa kutoka Yemen zinasema aliyekuwa mlinzi wa Osama Bin Laden, amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Vyanzo vya habari vya kitabibu vimesema kwamba Nasser al Bahri ambaye pia alikuwa akijulikana kama Abu Jandal alifariki siku ya Jumamosi, katika Hospitali iliyoko kwenye mji wa Mukalla kusini mwa Yemen.

Alirudi nchini humo mwishoni mwa mwaka 2008, baada ya kuachiliwa kutoka katika kizuizi alichowekewa na Marekani huko Guantanamo.

Al Bahri alijulikana kuhusika na mashambulizi yaliyofanywa na mtandao wa kigaidi katika miaka ya 90, katika nchi za Afghanistan, Somalia na Bosnia.

Thursday, December 17, 2015

MAGUFULI "ELIMU BURE ITAPATIKANA"

Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amewahakikishia Watanzania kwamba elimu ya bure itapatikana kama alivyoahidi.

Akijibu swali la fedha zitapatikana wapi za kutimiza ahadi yake ya elimu ya bure, Magufuli amesema, mwezi huu wa Desemba pekee, Tanzania inatarajiwa kukusanya kiasi cha dola bilioni 1, ambazo hazijawahi kukusanywa.

Amesema kuanzia mwezi huu fedha za kusomesha wanafunzi bure zitaanza kutengwa kuanzia mwezi huu. Kwa mujibu wa Dkt Magufuli, Serikali imefikia uamuzi wa kutenga dola milioni 65.5, ambazo zitapelekwa moja kwa moja katika shule zenye uhitaji na kwamba fedha zitakapotumwa, nakala ya barua itapelekwa kwa mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya pamoja na mkurugenzi wake.

Rais Magufuli ameonya yeyote atakayetumia fedha hizo vinginevyo kwamba atachukuliwa hatua kali. Amesema fedha hizo zitasaidia katika ununuzi wa vitu kama vile chaki, maandalizi ya mitihani na vitu vingine vya muhimu shuleni.

Thursday, December 10, 2015

MH. MAGUFULI ATANGAZA BARAZA LA MAWAZIRI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akitangaza baraza lake la mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Desemba 10, 2015. Kulia kwake ni Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na kushoto ni Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa.

BARAZA LA MAWAZIRI

Wizara ya Ofisi ya Rais,Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora.
Mawaziri - George Simbachawene  na Angella Kairuki
Naibu Waziri - Sumeilam Jafo. Naibu.

Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Raisi, Muungano na Mazingira
Waziri - January Makamba
Naibu Waziri – Luhaga Jerrson Mpina

Thursday, November 26, 2015

DJIBOUTI, ZANZIBAR HEROES HALI TETE

Kikosi cha Zanzibar Heroes

Michuano ya CECAFA CHALENJI CUP 2015 imeendelea jana Jumatano kwa michezo minne ya hatua ya makundi. Harambe stars ya kenya ilitoka sare ya bao 1-1 na Burundi, wenyeji Ethiopia wameifunga somalia bao 2-0, Malawi imeifunga Djibout bao bao 3-0.

Sudani kusini ikitoshana nguvu na ndugu zao Sudan baada ya kutoka bila ya kufungana.
Michuano hiyo itaendelea tena kesho ijumaa kwa michezo kadhaa, Rwanda wataikabili somalia, Vibonde Zanzibar Heroes watakuwa viwanjani dhidi ya Kenya.

Sudan kusini watawakabili Malawi na Djibout itachuana na SudanMichuano hiyo itaendelea tena kesho ijumaa kwa michezo kadhaa, Rwanda wataikabili somalia, Vibonde Zanzibar Heroes watakuwa viwanjani dhidi ya Kenya.

Sudan kusini watawakabili Malawi na Djibout itachuana na Sudan. Michuano hiyo itaendelea tena kesho ijumaa kwa michezo kadhaa, Rwanda wataikabili somalia, Vibonde Zanzibar Heroes watakuwa viwanjani dhidi ya Kenya.

Sudan kusini watawakabili Malawi na Djibout itachuana na Sudan.

Wednesday, November 25, 2015

BARAZA LA MAWAZIRI LABADILISHWA...!!!


Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta

Rais wa Kenya amefanya mabadiliko katika Baraza lake la Mawaziri, na kuwaacha wote wizara zao zilizotajwa katika ufisadi. 

Rais Uhuru Kenyatta amechukua hatua hiyo siku moja tu baada ya kutangaza ufisadi kuwa tishio kwa usalama wa kitaifa.

Rais ameahidi kufanya mabadiliko zaidi katika afisi yake hivi karibuni. Katika hotuba ilioonyeshwa kwa njia ya Televisheni, Rais Uhuru Kenyatta ameongeza idadi ya wizara kutoka kumi na tisa hadi ishirini na kuongeza idara mpya chini ya wizara mbalimbali katika kile alichosema ni kusaidia mawaziri kutekeleza majukumu yao bora zaidi .

KILIMANJARO STARS YACHINJA MTU CECAFA...!!!


Wachezaji wa Kilimanjaro Stars

Michuanao ya Cecafa Chalenji Cup Imeendelea tena jana kwa michezo miwili katika hatua ya makundi. Zanzibar ilifungwa bao 4-0 na Uganda ikiwa ni Mechi ya Kundi B.

Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) imeichapa Rwanda bao 2-1 katika mchezo uliopigwa mjini Awassa na kupaa kileleni mwa Kundi A wakiwa na Pointi 6 kwa Mechi 2 na kujihakikishia kucheza hatua ya Robo Fainali.

Mabao ya Kilimanjaro stars yalifungwa na Said Ndemla pamoja na Simon Msuva huku bao la Rwanda likifungwa na mchezaji Tisiyege.

Michuano hiyo itaendelea tena leo jumatano kwa mechi kadhaa ambapo Kenya itachuana na Burundi.

Somalia itaivaa Ethiopia, Malawi itaikabili Djibouti na Sudan kusini watachuana na ndugu zao Sudan.

BARCELONA YAIZIMA AS ROMA


Mchezaji wa As Roma

Barcelona wakiwa nyumbani walichomoza na ushindi wa mabao 6-1 dhidi ya As Roma.

Buyen Munich wakiichapa Olympiakos bao 4-0, Maccabi Tel Aviv wakila hio kwa Chelsea kwa kichapo cha mabao 4-0. 

BATE Borislov wakifungana bao 1-1 na Buyer Liverkusen , FC Porto wakilala bao 2-0 dhidi ya Dynamo Kiev, Zenit St P wakiichapa Valencia bao 2 – 0 na Lyon wakilala mbele ya KAA Gent bao 2-1.

ANDY MURRY TAYARI KWA DAVIS CUP


Kikosi cha Timu ya Tennis ya Uingereza

Timu ya Taifa ya Uingereza ya Tenis, imewasili nchini Ubegiji kwa mchezo wa fainali ya Davis Cup utakaopigwa ijumaa nchini humo. 

Timu hiyo inaongozwa na Andy Murray imewasili chini ya uangalizi wa ulinzi mkubwa kufuatia tishio la matukio ya kigaidi ambayo yameonekana kutishia amani nchini ubelgiji.

Timu hiyo inayojulikana pia kama Great britain ilipaswa kufika nchini humo tangu Jumapili lakini ikaahirisha kutokana na masuala ya kiusalama zaidi.

 Kikosi cha Uingereza kinawakilishwa na Andy Murray, Jamie, Kyle Edmund, Dominic Inglot na James Ward ambao tayari wapo nchini Ubelgiji.

Tuesday, November 10, 2015

MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA MUHIMBILI, ABADILISHA USIMAMIZI WA HOSPITALI

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dr. John Pombe Magufuli akiongea na mgonjwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipofanya ziara ya kushitukiza hospitalini hapo.

Rais wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli leo amefanya ziara nyingine ya kushtukiza, wakati huu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kufanyia mabadiliko usimamizi wa hospitali hiyo.

Kiongozi huyo mpya amesikitishwa na kuhuzunishwa na hali ya huduma kwa wagonjwa hususan wanaolala chini, kwa mujibu wa taarifa kutoka ikulu. 

“Pia amekasirishwa na hali ya kutokujali wala kushughulikia vifaa vya kufanyia kazi ambapo amekuta mashine muhimu za uchunguzi wa magonjwa kama vile MRI na CT-SCAN zikiwa hazifanyi kazi kwa muda wa miezi miwili sasa, ilihali mashine kama hizo katika Hospitali za binafsi zinafanya kazi na wagonjwa wanaelekezwa kwenda kutafuta huduma huko,” katibu wake mkuu Ombeni Sefue amesema.

Sunday, November 01, 2015

MATOKEO YA DARASA LA SABA 2015 YATANGAZWA, UFAULU JUU


Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), Dkt Charles Msonde


Wahitimu 518, 034 kati ya 763, 602 waliofanya mitihani ya kuhitimu darasa la saba iliyofanyika nchini kote kuanzia Septemba 2 hadi Septemba 10, mwaka huu wamefaulu mitihani yao, Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limesema leo.


 Akitangaza matokeo hayo jijini Dar es Salaam leo, Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Dkt Charles Msonde amesema idadi ya watahiniwa waliofaulu ni sawa na asilimia 67.84, asilimia 10.85 zaidi ya ufaulu wa mwaka 2014 ambapo waliofaulu walikuwa asilimia 56.99. 

Dkt Msonde amesema, ufaulu katika masomo yote umeongezeka kwa asilimia kati ya 4.61 hadi 17.22 ikilinganishwa na mwaka 2014 huku watahiniwa wakifaulu zaidi somo la Kiswahili (asilimia 77.20) na kufaulu kwa kiwango cha chini katika somo la Kiingereza (asilimia 48.56.

Amesema kati ya watahiniwa wote waliofaulu 264, 130 ni wasichana ambao ni sawa na asilimia 64.60 ya wasichana wote 408, 900 waliotahiniwa huku wavulana wakiwa 253, 904 sawa na asilimia 71.58 ya wavulana 354, 706 waliotahiniwa.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...