Friday, June 05, 2015

SERENA ATINGA FAINALI FRENCH OPEN 2015

Serena William,mchezaji tenis nambari moja duniani akifurahia ushindi.
Serena Williams amefanikiwa kutinga fainali za michuano ya tenis ya French Open. Licha ya kujisikia kuumwa Serena aliweza kupambana vikali na kumbwaga mpinzani wake Timea Bacsinszky kwa seti 4-6 6-3 6-0 na kufuzu kucheza fainali za mwaka huu.

Serena nambari moja duniani kwa wanawake sasa atapambana na Lucie Safarova katika mchezo wa fainali kesho, Jumamosi. Serena amekuwa akiumwa kipindi chote cha michuano hiyo, kiasi kwamba anasema hakutarajia kushinda katika mchezo huo.

Serena anajaribu kushindi taji la tatu la michuano hiyo ya French Open na taji la ishirini la michuano mikubwa. Mapema katika uwanja wa Philippe Chatrier, Safarova wa 13 kwa ubora alimtupa nje MSerbia Ana Ivanovic na kuwa mwanamke wa kwanza wa Czech kufika fainali za michuano hiyo katika uwanja wa Roland Garros katika kipindi cha miaka 34.
Kwa upande wa Wanaume, fainali zitafanyika Jumapili hii. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

Tuesday, June 02, 2015

AL-SHABAAB WADAIWA KUVITEKA VIJIJI KENYA

Alshabaab
Hofu kubwa imetanda Kaskazini mwa nchi ya Kenya,baada ya kuwepo kwa taarifa kwamba kundi la wapiganaji wa Al shabaab Limeviteka vijiji kadhaa katika mpaka wa Kenya na somalia.
Mamia ya wakaazi wameyatoroka makaazi yao kufuatia taarifa za kuwepo kwa wapiganaji wa Alshabaab wapatao thelathini.
Shule nne zinaripotiwa kufungwa.
Naibu kamishna wa kaunti ya Mandera amenukuliwa akisema kwamba wamepokea ripoti za kuwepo kwa wapiganaji hao na watawaandama na kulidhibiti eneo hilo. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

MLIPUKO WA BOMU WAUA WATU 20 NIGERIA

Mlipuko nchini Nigeria
Takriban watu 20 wamefariki kutokana na mlipuko wa bomu katika mji wa kaskazini mashariki wa Maiduguri nchini Nigeria.
Mji huo ulikuwa umeshambuliwa saa za alfajiri siku ya jumanne na washukiwa wa kundi la Boko haram .
Saa chache baadaye ,mlipuaji wa kujitolea muhanga alijilipua katika soko la kuuza ngombe la Gamboru ndani ya mji huo kulingana na walioshuhudia.
Wakati wa kuapishwa kwake rais mpya wa Nigeria Muhammadu Buhari alisema kuwa anayahamisha makao makuu ya kijeshi katika vita dhidi ya wapiganaji hao kutoka mji mkuu wa Abuja hadi Maiduguri. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

Thursday, May 28, 2015

MWANASHERIA KENYA AJITOSA KUMUOA MTOTO WA OBAMA...!!!

Rais Barrack Obama wa Marekani akiwa na mtoto wake Malia. 

Mwanasheria kijana nchini ametuma ombi la kumuoa mtoto wa Rais Barack Obama anayeitwa Malia.
Mwanasheria Felix Kiprono alisema jana kwamba yupo tayari kutoa ng’ombe 50, kondoo 70 na mbuzi 30 ikiwa ni mahari ya kumposa mtoto huyo.
Alisema kuwa analazimika kufanya hivyo ili kutimiza ndoto yake ya muda mrefu ya kumuoa mtoto wa Rais Obama.
“Nimevutiwa kumchumbia Malia tangu mwaka 2008,” alisema Kiprono baada ya kuhojiwa na gazeti la The Nairobian. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

ODAMA: NAOGOPA MSAADA WA MASHARTI...!!!

Odama
Jennifer Kyaka ‘Odama

MWIGIZAJI mwenye mvuto katika filamu za Bongo, Jennifer Kyaka ‘Odama’, amesema anaogopa marafiki wa kiume kwa kuwa huwa na masharti magumu pindi wanapotoa msaada.
“Wasanii wa kiume kwangu sipendi kwa kuwa huwa na masharti kuliko marafiki wa kike ambao husaidia bila masharti ya ajabu,” alisema.
Aliongeza kwamba, marafiki wa kike anakuwa huru kuwaeleza shida na matatizo yake kuliko wa kiume ndiyo maana hiyo ni sababu yake nyingine ya kutopenda marafiki wa kiume kama anavyopenda marafiki wa kike. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

SOMA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MEI 28, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC03017
DSC03018
DSC03019
Nunua gari bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

"NATAKA KUWA MCHEKESHAJI" INSPEKTA HAROON

INSPECTOR.
Haruna Kaena ‘Insepkta Haroun’

UNALIKUMBUKA kundi la Gangwe Mobb, hapo lazima utamtaja Haruna Kaena ‘Insepkta Haroun’ na Luten Kalama, wawili hao baada ya kutengana kila mmoja akawa anafanya kazi binafsi lakini sasa Inspekta Haroun ameibuka na kudai kwamba anataka kuwa mwigizaji wa vichekesho.
Inspekta Haroun aliyetamba na wimbo wa ‘Mtoto wa Geti Kali’ aliendelea kueleza kwamba fani anazozipenda ni muziki na kuigiza vichekesho.
“Mimi msanii hivyo natakiwa niwe mbunifu, nisibweteke na kazi, fani moja na kwa sasa napenda kuwa mwigizaji wa vichekesho kwa kuwa napenda kazi hiyo na ninaiweza,” alijinadi.
Msanii huyo aliwahi kushirikishwa katika vipengele vya uigizaji katika kipindi cha vichekesho kilichokuwa kikirushwa na televisheni ya Clouds. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

WABUNGE WAMKAANGA MAGUFULI

Waziri wa Ujenzi, Dk John Pombe Magufuli 

Waziri wa Ujenzi, Dk John Pombe Magufuli amekuwa hapati wakati mgumu anapowasilisha bajeti ya wizara hiyo, lakini hali ilikuwa tofauti jana wakati wabunge walipoungana kueleza hofu yao katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa barabara kutokana na madeni ya makandarasi.
Wabunge hao walidiriki kueleza kuwa kuna ufisadi katika ununuzi wa kivuko cha Bagamoyo na wengine kueleza kuwa miradi iliyotajwa kwenye hotuba ya bajeti ilishatekelezwa miaka ya 80 na 90.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kamati ya Miundombinu kuhusu bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2015/2016 iliyosomwa na Makamu Mwenyekiti, Profesa Juma Kapuya, deni linalodaiwa na makandarasi ni kati ya Sh850 bilioni na Sh900 bilioni.
“Kamati haijaridhishwa kabisa na hali hii kwani deni hili sasa ni kubwa kuzidi hata bajeti inayotengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya wizara hii, jambo ambalo linafanya bajeti hii kuonekana ni kiini macho tu,” alisema Profesa Kapuya.
Kambi ya Upinzani
Katika taarifa yake, Kambi ya Upinzani Bungeni (KUB) ilimshutumu Waziri Magufuli kwa kuandika hotuba ndefu ili kuwachanganya wabunge, huku hotuba hizo zikitaja hata miradi ya barabara zilizojengwa miaka ya 80 na 90.

Friday, May 22, 2015

UCHAGUZI FIFA, WAWILI WAJITOA


Nembo ya shirikisho la soka Duniani FIFA
Wagombea wawili kati ya wanne waliojitokeza kuwania nafasi ya urais wa shirikisho la vyama vya soka Duniani FIFA wamejitoka katika kinyang'ang'anyiro hicho.

Nyota wa zamani wa soka huko Ureno , Luis Figo ambaye ni mmoja wa waliojitoa kuwania nafasi hiyo,amelalamikia mfumo wa uendeshaji wa uchaguzi huo na kuiita kuwa ni wakinafiki.

Amesisitiza kuwa kwa mtazamo wake anaona kuwa taratibu zilizowekwa zililenga kumnufaisha mgombea mmoja tu na si kuelta usawa wa wote waliojitokeza kuwania nafasi hiyo,ambapo inaonekana kuwa ni mpango uliowekwa kumpatia nafasi ya ushindi Rais wa sasa Sepp Blatter ambaye anawania nafasi hiyo kwa kipindi cha tano.

Hata hivyo Rais wa chama cha soka huko Uholanzi , Michael van Praag , akijitoa. Huku wapinzani waliosalia ni Bw Blatter ambaye ni Jordan Prince Ali Al Hussein ambaye ni mwanachama wa kamati ya utendaji ya FIFA.

Mgombea mwingine aliyejitoa pia ni Rais wa chama cha soka cha Uholanzi Michael van Praag na hivyo kuwaacha Blatter na mtu anayedaiwa kuwa mpinzani wake wa karibu Prince Ali Al Hussein ambaye ni mjumbe wa kamati ya utendaji ya FIFA. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Wednesday, May 20, 2015

MICHUANO YA COSAFA YAANZA AFRIKA KUSINI

Michuano ya COSAFA,nchini Afrika Kusini Michuano ya kumi na tano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu kusini mwa Afrika,COSAFA imezikutanisha timu za ukanda huo nchini Afrika Kusini. Michuano hiyo ilianza kutimua vumbi Jumapili mei 17 na itakamilika mei 30 .

Timu 12 kati ya 14 kutoka nchi wanachama wa COSAFA tayari zipo nchini Afrika Kusini kuchuana katika mashindano hayo.

Angola na Comoro ambazo ni wanachama wa COSAFA hazikuweza kushiriki mwaka huu. Nafasi zao zimechukuliwa na Ghana iliyofikia fainali za michuano ya Caf ya mwaka huu na Tanzania kutoka ukanda wa Afrika mashariki na kati ikiwa mwanachama wa CECAFA.

Monday, May 18, 2015

NKURUNZIZA AWAFUKUZA KAZI MAWAZIRI WATATU

Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza .

Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza, amewafuta kazi mawaziri watatu, huku maandamano yakiendelea katika mji mkuu kufuatia jaribio la mapinduzi, juma lililopita. 

Mawaziri walioachishwa kazi ni wa Ulinzi, mashauri ya nchi za kigeni na biashara. 

Mapema hii leo, polisi walifyatua risasi hewani katika mji mkuu Bujumbura, kujaribu kuutawanya umati wa vijana uliokuwa ukifanya ghasia.

IS WAUTEKA MJI WA RAMADI


Wapiganaji wa Islamic State

Baada ya mapigano makali kwa siku kadhaa katika mji wa Ramadi nchini Iraq, hatimaye mji huo kwa sasa unashikiliwa na wapiganaji wa kundi la IS.

Makundi ya wanajeshi wa serikali wamekimbia kutoka katika eneo hilo na Islamic State wamejitangazia ushindi dhidi ya mji huo na kwamba wanaushikilia. 

Mapema msemaji wa Gavana wa jimbo hilo amesema kuwa wapiganaji hao wanayashikilia baadhi ya majengo mhimu ya serikali katika jimbo hilo. 

Hata hivyo umoja wa Mataifa umelaani hatua hiyo ya IS, ambapo pia Waziri Mkuu wa Iraq Haider al-Abadi amesema kuwa kwa sasa wanajipanga kwa kushirikiana na majeshi ya Shia ili kukabiliana na wapiganaji hao. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAN CITY YAICHAPA SWANSEA 4-2

Yaya Toure mshambuliaji wa Man City

Matokeo ya Mechi mbili za ligi kuu ya England zilizochezwa hapo jana,Manchester City iliwachabanga Swansea mabao 4-2 .

Ni Wilfried Bony ambaye mnamo dakika ya 90 lililopigilia msumali wa moto kwa Swansea baada ya kufunga bao la nne.

Lakini Yaya Toure yeye alizifumania nyavu mara mbili dakika 21 na 74. , James Milner naye akifunga mnamo dakika ya 36.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Huku katika mechi ya pili Arsenal wakitoa sare ya bao 1-1 dhidi ya Man united,ambapo kwa matokeo hayo sasa Arsenal wanaendelea kujiimarisha katika nafasi ya tatu. Leo West Brom watakipiga na Chelsea katika dimba la The Hawthons.

Sunday, May 17, 2015

'SI IKULU ILIYOWASAFISHA MAWAZIRI' PINDA


Waziri Mkuu Mizengo Pinda. 

Waziri Mkuu Mizengo Pinda amewajibu wabunge waliokosoa kitendo cha mawaziri watano waliotajwa kwenye kashfa za Operesheni Tokomeza na akaunti ya escrow, akisema Ikulu haikuhusika kuwasafisha bali ilitangaza matokeo ya uchunguzi wa tume. 

Mtendaji huyo mkuu wa Serikali pia amesema mawaziri hao bado wanachunguzwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Jeshi la Polisi, kuhusu kuhusishwa kwao na operesheni hiyo iliyotekelezwa kwa kukiuka haki za binadamu, na sakata la escrow lililohusisha uchotwaji wa Sh306 bilioni zilizokuwa Benki Kuu.

Wakichangia hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu wiki iliyopita, baadhi ya wabunge walihoji kitendo cha Ikulu kuwasafisha mawaziri wachache na kuwaacha wengine waliojiuzulu kisiasa kutokana na wizara zao kukumbwa na kashfa na kumtaka Waziri Mkuu atoe majibu wakati akifanya majumuisho ya mjadala.

RAIA WAPYA WAKUTWA NA NYARA ZA SERIKALI...!!!

 Kamanda wa Polisi mkoa wa Katavi.

POLISI mkoani Katavi imewakamata raia wapya watatu waliokuwa wakimbizi kutoka Burundi kwa kujihusisha na biashara haramu ya meno ya tembo.

Watu hao walikamatwa na nyara za Serikali zenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 1.2. Nyara hizo za Serikali ni vipande vitatu vya meno ya tembo vikiwa sawa na jino moja la mnyama huyo vikiwa tayari kusafirishwa kwenda mjini Tabora.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi , Dhahiri Kidavashari amewataja watuhumiwa hao kuwa ni pamoja na Frank Hamis (18) , Steven Jonas (22) na Jackson Erasto ambao karibuni wamepewa uraia wa Tanzania. 

Kidavashari alibainisha kuwa watuhumiwa hao walikutwa juzi saa 3:00 asubuhi katika chumba alichopanga mwanafunzi wa kidato cha Nne katika shule ya sekondari Katumba, Ernest John (19) katika eneo la Mnyasi kijijini Katumba wilayani Mlele. 

“Mwanafunzi huyo ana uhusiano nao wa kindugu hivyo aliwakaribisha kulala chumbani kwake alimokuwa amepanga katika nyumba ambayo ni mali ya Felix Gado iliyopo eneo la Mnyasi kijijini Katumba.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...