Sunday, November 02, 2014

MCHUNGAJI AKAMATWA NA DAWA ZA KULEVYA ZA BIL. 2 ZA KITANZNIA...!!!

dawaaa
Jeshi la Polisi kitengo cha Kupambana na Dawa za kulevya limekamata kilo 40 za dawa za kulevya aina ya heroine zenye thamani ya shilingi bilioni 2.
Tukio hilo lilitokea juzi eneo la Tegeta nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam ambapo Polisi walifaniikiwa kuwanasa watu wawili wakiwa na dawa hizo ndani ya nyumba inayomilikiwa na mchungaji ambaye wakati huo alikua katika kanisa lake lililopo eneo la Sinza.
Kamanda wa kikosi cha kupambana na dawa za Kulevya Godfrey Nzowa alilithibitishia Gazeti la MTANZANIA kuwa  kuwepo kwa tukio hilo akiomba jina la mchungaji huyo lihifadhiwe kuepusha kuvuruga uchunguzi.
“Ni kweli tukio la aina hiyo lipo  lakini watu kama hawa siwezi kusema moja kwa moja ni Mchungaji  ndio muhusika hadi nipate vithibitisho vya kutosha ikiwa kuendesha kanisa kwani wengi wao wanatumia makanisa kama mwamvuli wa kujificha na kufanya biashara hii,”Alisema Nzowa.
Alisema kwa sasa watu hao wanashikiliwa na Jeshi hilo ambapo wawili kati yao si raia wa hapa nchini wakati upelelezi ukiendelea kabla ya kuweka hadharani ukweli wa mambo. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ANGALIA PICHA ZA MAPOKEZI YA MWILI WA ALIYEKUWA RAIS WA ZAMBIA, MICHAEL SATA

Mwili wa Rais wa Zambia, Michael Sata umewasili Zambia tayari kwa mazishi ambayo yamepangwa kufanyika November 11.

Mwili wa rais huyo umewasili uwanja wa ndege wa Kenneth Kaunda International Airport na kupelekwa Mulungushi International Conference Centre kwa ajili ya kuendelea na taratibu nyingine zilizopangwa na Serikali ya nchi hiyo kufanyika kabla ya mazishi.
Hizi ni picha 10 zikionyesha namna mapokezi yalivyokuwa katika jiji la Lusaka siku ya jana Novemba 1.
Sata4
Sata5 
Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBA 02, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KAMBI YA JESHI YAVAMIWA...!!!

wanajeshi katika kambi
Wanajeshi katika kambi ya jeshi ya Nyali iliopo mjini Mombasa pwani ya Kenya wamewaua kwa kuwapiga risasi watu 6 baada ya genge la wahalifu kuvamia kituo hicho cha jeshi mapema leo.
Inadaiwa kuwa kundi la watu 15 lilijaribu kuvamia kambi hiyo mwendo wa saa kumi na moja alfajiri ya jumapili.
Wanajeshi waliokuwa katika zamu waliweza kulidhibiti kundi hilo ambapo watu watano waliuawa huku askari mmoja akiweza kujeruhiwa kwa kukatwa na mapanga na wavamizi hao.
Kufikia sasa maafisa wa polisi wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha shambulizi jilo.
Hatahivyo wengi wanashuku watu hao huenda ni wanachama wa kundi la Mombasa Republican Council MRC.
Lakini msemaji wa kundi hilo Randu Nzai amekanusha habari hizo akisema kuwa kundi hilo halikuhusika kamwe. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC Swahili

WATU WA BENI WAANDAMANA

Ripoti zinasema kuwa maandamano yamefanywa katika mji wa Beni, mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo, baada ya mauaji ya karibuni yaliyofanywa na wapiganaji.
Kituo cha redio cha huko kinasema kuwa waandamanaji wanaodai ulinzi zaidi, wameshambulia sanamu ya Rais Joseph Kabila saa chache baada ya kujulikana kuwa watu 7 zaidi waliuwawa Jumamosi usiku.
Inakisiwa kuwa watu kama 100 wameuwawa katika eneo la Beni katika mwezi uliopita.
Wanaoshukiwa kufanya hayo ni wapiganaji wa ADF - kundi la wapiganaji Waislamu kutoka Uganda ambao sasa wanapigana na jeshi la Congo na askari wa Umoja wa Mataifa.
Alipozuru mji wa Beni Ijumaa, Rais Kabila aliahidi ulinzi zaidi kwa raia na aliomba kuwa kikosi cha Umoja wa Mataifa huko kizidishwe. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

Saturday, November 01, 2014

MTANGAZAJI BEN KIKO AFARIKI DUNIA



Ben Kiko enzi za uhai wake.
ALIYEKUWA mtangazaji maarufu wa Radio Tanzania, Ben Kiko, amefariki dunia usiku wa kuamkia jana Oktoba 31, 2014 akiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam alipokuwa akitibiwa.
Kiko amefariki baada ya kusumbuliwa na maradhi ya figo kwa muda mrefu. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. AMEN.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI NOVEMBA 01, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

JEN TRAORE AJITANGAZA RAIS BURKINA FASO

Jenerali Honore Traore mkuu wa jeshi la Burkina Faso aliyejitangaza rais mpya wa nchi hiyo
Mkuu wa Jeshi la Burkina Faso Jenerali Honore Traore sasa amejitangaza kuwa rais baada ya aliyekuwa rais wa Burkina Faso Blaise Compaore kutangaza kujiuzulu.
Jenerali Traore ameshinikizwa na waandamanaji ambao walikuwa wanamtaka kuchukua usukani baada ya kuondoka kwa Bwana Compaore.
Bwana Compaore amesema kuwa amekubali kuondoka madarakani ili kutii matakwa ya waandamanaji ambao hawamtaki kuendelea kuongoza taifa hilo hata baada ya kutawala kwa miaka 27.
Bwana Compaore sasa ametaka uchaguzi mpya wa urais ufanyike baada ya siku 90.
Awali msemaji wa jeshi alikuwa amewaambia waandamanaji kuwa bwana Compaore hayuko tena madarakani huko Ouagadougou.
Maelfu ya waandamanji walikuwa wamerejea mabarabarani kwa siku ya pili
Hata hivyo hakubaini ikiwa afisa huyo wa kijeshi alikuwa akizungumza kwa niaba ya jeshi lote.
Jeshi lilisema kuwa litafanya mkutano na waandishi habari.
Siku ya Alhamisi waandamanaji waliokuwa wamekasirishwa na jitihada za rais za kuongeza muda wa uongozi wake baada ya kutawala kwa miaka 27 waliteketeza jengo la bunge na kuvamia kituo cha televisheni ya taifa.
Bwana Compaore alitupilia mbali jitihada za kubadilisha katiba ambayo ingemruhusu kuwania tena muhula mwingine kama rais lakini akasema kuwa angebaki madarakani kwa mwaka moja zaidi. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

WATAKA KIWANGO CHA KALORI KATIKA POMBE KITAJWE

Wataka pombe ionyeshe kiwango cha kalori kupunguza vitambi na unene wa kupitiliza
Pombe inatakiwa kuwa na nembo inayoonyesha kiwango cha kalori au kipimo cha joto litolewalo na chakula ili kupunguza vitambi au unene wa kupita kiasi.
Madaktari wa afya ya umma, wameonya kuwa glasi kubwa ya mvinyo inaweza kuwa na kiasi cha kalori 200- sawa na donati, aina ya maandazi.
Hata hivyo idadi kubwa ya watu hawajui madhara ya kula kiwango kikubwa cha kalori.
Waziri wa Afya Jane Ellison amesema "hatua kubwa" imefanyika kwa kuviwekea nembo vyakula, na kwa suala hilo serikali italiangalia.
Sekta ya vinywaji imesema imesema iko tayari kwa wazo hilo la kuweka nembo zenye kuonyesha kiasi cha kalori, lakini kuweka nembo zinazonyesha kiwango cha kilevi katika kinywaji ni muhimu zaidi.
Uingereza ni moja ya mataifa yenye watu wenye unene wa kupita kiasi duniani kwa kuwa na idadi ya karibu robo ya watu wazima kuwekwa katika kundi la wenye unene wa kupitiliza.
Vyakula tayari vinakuwa na taarifa za kiasi cha kalori kilichomo ndani yake, lakini pombe haimo katika sheria za Umoja wa Ulaya zinazotaka vyakula viwekewe nembo.
Mvinyo nao watakiwa kuonyesha kiwango cha kalori
Na Tume ya Ulaya inaangaliwa iwapo vinywaji viwekewe nembo yenye kuonyesha kiasi cha kalori kilichomo.
Utafiti uliofanywa na Chama cha Masuala ya Afya ya Jamii nchini Uingereza, umesema hatua hii itaungwa mkono na wanywaji nchini Uingereza.
Mkuu wa chama hicho cha RSPH, Shirley Cramer, ameiambia BBC: "Ni jambo la kushtusha kweli - asilimia 80% ya watu wazima hawana wazo la kujua kiasi cha kalori kilichomo katika kinywaji chochote na kama wanafikiri wana wazo hilo kwa ujumla wanakadiria kiasi cha chini mno."
"Itasaidia taifa kupunguza watu wenye unene wa kupitiliza na huenda kupunguza kupunguza unywaji wa pombe."

Kiasi cha kalori:

Glasi kubwa ya 250ml ya mvinyo wenye kileo cha asilimia 8% ni kalori 170 Kiasi hicho hicho cha glasi ya 250ml ya mvinyo wenye kileo cha asilimia 14% ni kalori 230 Painti moja yenye asilimia 4% ya bia ni zaidi ya kalori 180. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Friday, October 31, 2014

MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 31, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PINDA ATAKA TANZANIA ISITEGEMEE WAFADHILI



Waziri Mkuu wa Tanzania, Mizengo Pinda

Suala la baadhi ya wafadhili wa TZ kubana au kuchelewesha fedha walizoahidi kusaidi bajeti ya nchi linaendelea kuiumiza serikali.
Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Mizengo Pinda, amesema umefika wakati sasa kwa Tanzania kujitegemea kwa mapato ya ndani kwa asilimia 100 badala ya kuegemea kwa wahisani ambao amedai wanakuwa na maslahi yao katika kusaidia.
Hivi karibuni wahisani wamesitisha kutoa fedha hizo kuishinikiza Tanzania kuchukua hatua dhidi ya upotevu wa mabilioni ya fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania katika mazingira yanayodaiwa kuwa ya rushwa.
Kiongozi huyo mwandamizi wa serikali ya Tanzania ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kurejea kutoka ziara ya ughaibuni ambako alihudhuria mikutano katika nchi mbali mbali akishughuli maswala kadhaa ikiwa ni pamoja na uwekezaji. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RAIS WA BURKINA FASO ASEMA ATAJIUZULU

Rais Blaise Compaore
Rais Blaise Compaore wa Burkina Faso amesema atajiuzulu baada ya miezi 12 ya serikali ya mpito.
Ameyasema hayo wakati akilihutubia taifa siku moja baada ya kutokea machafuko. Wakati ambao pia Mkuu wa Majeshi wa nchi hiyo ametangaza kuivunja serikali ya nchi hiyo.
Katika hotuba yake aliyoitoa kupitia kituo binafsi cha Televisheni, Rais Compaore amesema ameuelewa ujumbe uliotolewa na waandamanaji na kwamba ataondoka madarakani baada ya kumalizika kwa kipindi cha mpito cha miezi miezi kumi na mbili.
Wapinzani na waandamanaji nchini humo, waliandamana na kufanya vurugu kupinga kubadilishwa kwa katiba itakayomwongezea muda wa utawala Rais wa nchi hiyo Blaise Compaore, baada ya kuongoza nchi hiyo kwa miaka 27.
Wamemtaka rais huyo kujiuzulu mara moja. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KIVUMBI CHA LIGI KUU ENGLAND

Golikipa Simon Mignolet wa timu ya Liverpool ashindwa kuupangua mpira.
Kitimtim cha ligi kuu ya England kitaendelea tena kesho wakati ambapo mashabiki wa soka nchini humo na duniani kote watapata nafasi ya kuzishuhudia timu zao zikitafuta pointi tatu muhimu.
Newcastle Utd wataikaribisha Liverpool katika mchezo ambao utarushwa moja kwa moja kupitia idhaa ya Kiswahili ya BBC majira ya saa tisa unusu kwa saa za Afrika Mashariki.
Arsenal wao wataikaribisha Burnley, huku Chelsea nayo wakiialika QPR. Everton watakuwa nyumbani kucheza Swansea City. Hull City wataikabili Southampton. Michezo mingine ni itakayochezwa siku hiyo ya kesho ni kati ya Leicester City watakapo kwaana na West Brom, Huku Stoke City watakapoikabili West Ham utd.
Siku ya jumapili ni mpambano wa kukata na shoka ambapo Manchester United wataavaana na Manchester City mechi ambayo pia itatangazwa moja kwa moja na Idhaa ya Kiswahili ya BBC ,huku Tottenham watakapokwaana na Aston villa. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, October 29, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATANO OKTOBA 29, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BAN KI MOON KUTEMBELEA KAMBI YA DAADAB

Ban Ki Moon
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anatembelea kambi ya wakimbizi ya Daadab, nchini Kenya.
Hii ni mara ya kwanza kwa kingozi huyo mkubwa katika Umoja wa Mataifa kutembelea kambi hiyo kubwa ya wakimbizi.
Ban Ki Moon anatarajiwa kutathmini hali ya msongamano katika kambi hiyo na hali ya usalama ambayo imekuwa ikizorota mara kwa mara.
Aidha ripoti zinasema, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ataidhinisha kuondoka kwa baadhi wa wakimbizi wa kisomali waliojitolea kurudi nyumbani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...