Kesi ya wanablogu kumi waliokuwa wanakabiliwa na mashitaka ya ugaidi imeahairishwa hadi Agosti 20.
Kesi hiyo ilianza leo miezi mitatu baada ya tisa kati yao kukamatwa na polisi.
Mmoja wa wanablogu hao alishtakiwa bila kuwepo mahakamani.
Wanakabiliwa na mashitaka ya ugaidi chini ya sheria iliyoshutumiwa ya kupinga ugaidi.
Kesi hii imevutia hisia kubwa nje na ndani ya Ethiopia, hiyo basi hakukuwa na tofauti kubwa ilipoanza hivi leo.
Mahakama hiyo ilijazwa na raia wa Ethiopia,
wanahabari hali kadhalika maafisa wa kidiplomasia. Wote walioshitakiwa
walifika mahakamani. Mawakili walikuwa wamepinga kwa mapema mashitaka
hayo wakisema kuwa hayakuwa na msingi.
Hata hivyo mahakama ilikataa kuwaachilia kwa
dhamana wanablogu hao jinsi walivyokuwa wakitaka mawakili wao. Wote kumi
wameshitakiwa kwa kubuni kikundi haramu vile vile kushirikiana na
makundi ya upinzani yaliyopigwa marufuku ng’ambo na nchini.
Waendesha mashtaka walisema kuwa washtakiwa hao walipokea ufadhili na mafunzo ya kutengeneza vilipuzi.
Kitendo hicho cha kuwakamata wanablogu
kimesababisha serikali ya Ethiopia kushutumiwa kimataifa na kutaja kuwa
inatumia sheria dhidi ya ugaidi kukandamiza upinzani na uhuru wa vyombo
vya habari nchini humo.
Katika mahojiano ya hivi majuzi na BBC waziri
mkuu wa Ethiopia alikanusha madai ya kuwakandamiza wanahabari lakini
akasema kuwa serikali haitawavumilia wanablogu na wanaharakati
wanaonekana kushirikiana na makundi ya kigaidi nchini humo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz