Juhudi za uokoji zinaendelea
siku ya pili Kaskazini mashariki mwa Afghanistan ambapo watu wapatao
elfu mbili wanasadikiwa kufa kutokana na maporomoko ya ardhi katika
maeneo ya vijiji kwenye mkoa wa Badakhshan.
Vijiji hivyo vimefunikwa na udongo wenye ukubwa
wa karibu mita kumi kwenda juu baada ya sehem ya mlima mmoja kuporomoja
kutokana na mvua kubwa zinazonyesha. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo TzSunday, May 04, 2014
Saturday, May 03, 2014
MWENGE WA UHURU WAWASHWA RASMI JANA MKOANI KAGERA,TAYARI KUKIMBIZWA KATIKA WILAYA 127
Makamu
wa Rais wa, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akiwasha Mwenge wa Uhuru wakati wa
Sherehe za uzinduzi wa mbio za Mwenge huo zilizofanyika kwenye Uwanja wa
Kaitaba, mjini Bukoba Mkoa wa Kagera leo. Mwenge huo unatarajia kuitimisha
mbio zake Oktoba 14 mkoani Tabora, ambapo zinatarajia kufungwa na Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete.
Makamu
wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Mwenge wa Uhuru, Kiongozi wa
mbio za Mwenge Taifa, Rachel Kasanda, baada ya kuuwasha rasmi wakati wa Sherehe
za uzinduzi wa mbio za Mwenge huo zilizofanyika kwenye Uwanja wa Kaitaba, mjini
Bukoba Mkoa wa Kagera jana. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
ABSALOM KIBANDA AFUNGUKA NDANI YAMAANDIMISHO YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI
Baadhi ya waandishi wa habari na
wadau kutoka asasi mbalimbali nchini wakifanya usajili kwenye kongamano
la siku moja lilioandiliwa kuadhimisha Uhuru wa vyombo vya Habari
Duniani 2014 lililofanyika jijini Arusha.
Na Waandishi Wetu, Arusha
Mwenyekiti wa Jukwaa la
Wahariri (TEF), Absalom Kibanda ametoa wito kwa waandishi wa habari
nchini kuyapa uzito matukio yanayowatokea waandishi wa habari na
kuyapigia kelele kwa nguvu zote ili kuyakomesha.
Kibanda aliyasema hayo
jana mjini Arusha katika kongamano lililoandaliwa kama sehemu ya
maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani na kuongeza
kwamba wakati umefika kwa waandishi wa habari kuondoa tofauti zao na
kuungana pamoja kuongeza nguvu waliyonayo kukabiliana na ukatili
unaoendelea dhidi ya waandishi wa habari katika miaka ya hivi karibuni.
“Baadhi ya wahariri
huwa hawayaandiki madhila yanayowasibu waandishi wa habari na kuyapa
uzito unaostahili aidha kwa huyapuuzia au kudharau kwa kuwa hayawahusu
moja kwa moja,” alisema Kibanda.
Aliongeza kwa kusema
kuwa vyombo vya habari mara nyingi vimekuwa vikinyooshewa vidole na
kulaumiwa kwa kutokufanya kazi kwa uadilifu jambo ambalo linatafsiriwa
kuwa ni la uonevu, vinatumiwa vibaya na hakuna anayesimama kuvitetea
kutokana na mchango wake mkubwa katika jamii. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
POLISI NIGERIA WAOMBA PICHA ZA WANAFUNZI
Polisi nchini Nigeria wamewataka wazazi wa wanafunzi wasichana zaidi ya 200 waliotekwa kuwasilisha picha za mabinti hao.
Wasichana hao walichukuliwa na watu wanaoshukiwa
kuwa wanamgambo wa Kiislam kutoka shuleni kwao katika jimbo la Borno
zaidi ya wiki mbili zilizopita.Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Subscribe to:
Posts (Atom)