Sunday, January 12, 2014

VIJUE VYAKULA 10 AMBAVYO MWANAUME ANATAKIWA KULA ILI KUONGEZA UWEZO WAKATI WA TENDO LA NDOA...!!!

Aina hizi za samaki zinazovuliwa baharini huwa na madini ya zink na chumvi ambayo yanatajwa kusaidia uzalisha wa vichocheo vinavyohamasisha msisimko wa mwili wakati wa tendo la ndoa.
 
2. POMEGRANATE
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Saturday, January 11, 2014

MTOTO WA AJABU... ANAKULA SUFULIA ZIMA LA WALI, ANAKUNYWA MAJI NDOO MOJA NA KUMALIZA MIKATE SABA KWA MKUPUO LAKINI HASHIBI...!!!

AMA kweli ukistaajabu ya Musa utayaona ya Farao, Andrea Marcus (13), mkazi wa Mbezi-Kibanda cha Mkaa, Dar anadaiwa kuwa wa ajabu kutokana na vitendo vyake.
Mtoto huyu amedaiwa kuwa ni wa kichawi kutokana na maajabu yafuatayo:

 
Mkazi wa Mbezi-Kibanda, Andrea Marcus.
Ana uwezo wa kula ubwabwa sufuria moja la familia, anamudu kunywa maji ndoo moja, ana uwezo wa kuingiza tumboni mikate mikubwa saba kwa mlo mmoja,  amewahi kula mchele (si ubwabwa) ndoo nzima. Mbaya zaidi baada ya kula milo hiyo huwa haoneshi ameshiba.
Maajabu mengine ambayo yanawashangaza watu wanaoishi naye ni jinsi anavyokula chakula kwa kumwaga chini kisha kukomba mpaka udongo.
“Sina amani ya moyo, naomba Watanzania wanisaidie, mwanangu ananiuma sana, hata kujisaidia ni hapohapo, chakula anakula kupita kiasi, kama nilivyosema hashibi na bado hali kama mwanadamu wa kawaida,” alisema mama wa mtoto huyo.

BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI LAIVA....!!!

 
Rais Jakaya Kikwete, anaweza kutangaza mabadiliko katika baraza lake la mawaziri wakati wowote kuanzia sasa.
Hatua hiyo inafuatia uteuzi wa mawaziri watatu kutenguliwa, mmoja kujiuzulu na mwingine kufariki dunia.

Desemba 20, mwaka jana, Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira iliwasilisha bungeni taarifa ya uchunguzi kuhusiana na athari zilizojitokeza katika Operesheni Tomokeza Ujangili iliyositishwa na serikali wakati wa Mkutano wa 13 wa Bunge kufuatilia malalamiko ya wananchi, wabunge na wadau.

Akiwasilisha ripoti hiyo, Mwenyekiti wa kamati hiyo, James Lembeli, alisema uchunguzi wao ulibaini kuwa operesheni hiyo iliendeshwa bila kufuata taratibu na matokeo yake kusababisha mateso kwa raia, vifo na upotevu wa mali hususani mifugo.

Baada ya ripoti hiyo kuwasilishwa, wabunge walichachamaa na kushinikiza mawaziri ambao wizara zao zilihusika katika utekelezaji wa operesheni hiyo wawajibike kisiasa au wawajibishwe.

Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, aliamua kujiuzulu wakati mjadala ukiendelea na siku hiyo baadaye Rais Kikwete, alikubaliana na mapendekezo ya wabunge kwa kutengua uteuzi wa mawaziri watatu, Dk. Emmanuel Nchimbi (Mambo ya Ndani ya Nchi); Mathayo David Mathayo (Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi) na Shamsi Vuai Nahodha (Ulinzi na JKT).

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARI 11, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

RAIS AJIUZULU BAADA YA SHINIKIZO KALI

 Rais wa mpito wa Jamuhuri ya Afrika ya Kati, Michel Djotodia, amejiuzulu kufuatia shinikizo kali na kukosolewa kwa mwendo wake wa kujikokota katika kusuluhisha mgogoro wa kidini unaotokota nchini humo.
Hatma ya Djotodia ilikuwa swala kuu katika ajenda ya mkutano wa viongozi wa kikanda kuhusu mzozo unaoendelea nchini humo. Taarifa zinazohusiana Afrika, Siasa
Mkutano huo ulifanyika nchini Chad huku maelfu wakiendelea kutoroka nchini humo kutokana na ghasia.
Maelfu ya watu waliandamana leo katika barabara za mji mkuu Bangui kumtaka Rais Djotodia, ajiuzulu.
Rais Djotodia amekosolewa vikali kwa kukosa kumaliza mapigano ya kidini kati ya wakristo na waliokuwa waasi waisilamu ambao walimsaidia kuingia mamlakani kwa njia ya mapinduzi mwaka jana.
Baraza lote la mpito katika Jamuhuri ya Afrika ya kati limekwenda nchini Chad ambako viongozi wa Afrika wanakutana kujadili mzozo unaoendelea nchini humo.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Friday, January 10, 2014

CHADEMA HAPAKALIKI TIMUA TIMUA YAENDELEA... KATIBU WA WILAYA ASIMAMISHWA KAZI

  Kamati ya utendaji ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi, imemsimamisha Katibu wake, Jordan Membe, kwa madai ya kwenda kinyume na katiba ya Chama.

Habari kutoka wilayani humo zilizothibitishwa na uongozi wa chama hicho, ngazi ya wilaya na ile ya mkoa, zinaeleza Membe amesimamishwa kutokana na
kukiuka maadili ya uongozi, ikiwa ni pamoja na kujihusisha na masuala ya kuleta na
kusababisha vurugu ndani ya chama.

Baadhi ya wajumbe waliohudhuria kikao hicho, kilichofanyika makao makuu ya ofisi ya chama hicho, wilayani Nachingwea, ambao hawakupenda majina yao kuandikwa kwenye vyombo vya habari kwa madai sio wasemaji wa Chama, wameeleza kuwa Membe anadaiwa kusambaza waraka unaopinga kuondolewa kwa aliyekuwa Naibu Katibu mkuu, Zitto Zuberi Kabwe na wenzake.


Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

IGP ATANGAZA MABADILIKO MAKUBWA JESHI LA POLISI


Mkuu Mpya wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali, Ernest Mangu ameanza kazi kwa kutangaza mabadiliko ya mfumo wa jeshi hilo huku akiunda vitengo vipya kwa lengo kuongeza ufanisi katika kukabiliana na uhalifu.
Katika mabadiliko hayo, IGP Mangu amesema polisi wameanzisha kamisheni mpya tano ambazo ni Intelijensia, Utawala, Fedha na Ugavi, Upelelezi, Uchunguzi wa Kisayansi wa Kesi za Jinai na Polisi Jamii.
Mfumo huo mpya wa polisi ndiyo uliowezesha kuundwa kwa nafasi mpya ya Naibu IGP, ambayo mteule wake wa kwanza ni Abdulrahman Kaniki ambaye kabla ya hapo alikuwa Kamishna wa Uchunguzi wa Sayansi wa Makosa ya Jinai. Nafasi hiyo sasa inakaimiwa na watu waliokuwa chini yake.
Viongozi wengine katika safu hiyo ni Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Kamishna Issaya Mngulu, Kamishna wa Operesheni na Mafunzo, Paul Chagonja, Kamishna wa Fedha na Ugavi, Clodwig Mtweve, Kamishna wa Utawala, Thobiasi Andengenye na Kamishna wa Polisi Jamii, Mussa Ali Mussa. Naibu Kamishna wa Polisi, Diwani Athuman yeye anakaimu nafasi ya Kamisheni ya Intelijensia.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 10, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAJIBU YA UBALOZI WA TANZANIA CHINA JUU YA JACKIE CLIFF KUNASWA NA MADAWA YA KULEVYA HUKO MACAU/CHINA


J Cliff 1

Mwezi December 2013 taarifa zilitoka kwamba kuna binti wa Kitanzania mwenye umri wa miaka 28 aliekamatwa na dawa za kulevya huko Macao China ambapo baadhi ya taarifa zilizoripotiwa na Waandishi wa Tanzania zilisema aliekamatwa ni mrembo ambae amekua akionekana kwenye video kadhaa za wasanii wa bongofleva (Jackie Cliff).
Macao

Macao.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

WAFANYABIASHARA WA DAR WAGOMEA MASHINE ZA TRA TENA ... WAAMUA KUFUNGA MADUKA YAO




Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Thursday, January 09, 2014

SAMAKI MKUBWA AINGIA SEHEMU ZA SIRI ZA BINTI HUKO BUNDA ...!!!

MAISHA ya mwanafunzi wa kike mwenye umri wa miaka 12, (jina tunalihifadhi), anayesoma darasa la tano Shule ya Msingi Bwanza, Wilaya ya Bunda, mkoani Mara, yako hatarini baada ya kurukiwa na samaki aina ya sato, kuingia sehemu ya siri na kukimbilia tumbani.

Tukio hilo limetokea Januari mosi mwaka huu, saa 11 alfajiri,wakati mtoto huyo akichota maji katika Ziwa Victoria ili aweze kumwagilia bustani ya nyanya, vitunguu iliyopo kandokando ya ziwa hilo.

Akizungumza na Majira, kaka wa mtoto huyo (jina tunalihifadi), mwenye miaka 31, alisema tukio hilo limewashangaza wakazi wa Kijiji cha Bwanza na vitongoji vyake.

Alisema mdogo wake alikuwa akichota maji katika ziwa hilo akiwa amechuchumaa ndipo samaki huyo anayedaiwa kuwa mwenye ukubwa wa nchi nne, aliruka kutoka majini, kuingia sehemu yake ya siri na kukimbilia tumboni.

"Mdogo wangu alifanya jitihada za kumvuta ili aweze kumtoa lakini alikimbilia tumboni na kuanza kupata maumivu makali, kutokwa na damu nyingi baada ya kuparazwa na miba ya
mgongo wa samaki huyo.
 

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

GOOGLE YATAJA WATU MAARUFU WA TANZANIA AMBAO PICHA ZA ZILITAFUTWA SANA KWENYE MTANDAO MWAKA 2013

trends
Google trends imetoa list ya majina/maneno ambayo yametafutwa sana kwenye mtandao wa google search kwa mwaka 2013.
Dunia nzima ime-search sana jina la Nelson Mandela likifuatiwa na Paul Walker.
Upande wa Tanzania majina ya watu maarufu yaliyotafutwa sana kwa upande wa picha(image search) ni
Wema,Diamond na Wema Sepetu.
Kwa ujumla unaweza kusema jina lililotafutwa sana kwa upande wa image search kwenye google kwa mwaka 2013 ni Wema Sepetu
google

 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

BASI LA MTEI LACHOMWA MOTO NA WANANCHI LIKIWA SAFARINI

Screen Shot 2014-01-09 at 9.07.49 PM
Hii ni ajali ambayo imetokea njia Panda ya kwenda Arusha kama unatokea Singida, wakazi wa eneo hilo wamechoma moto basi la Mtei ambapo waandishi wameongea na miongoni mwa mashuhuda na abiria wa ajali hiyo na wametoa haya maelezo hapa chini.
mamtei
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARI 08, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAJINA ZAIDI 5,400 YAWANIA UJUMBE WA BUNGE LA KATIBA



Balozi Ombeni Sefue
********
Serikali imeanza mchakato wa kuchambua asasi na majina ambayo atakabidhiwa Rais, kuwa miongoni mwa wajumbe watakaounda Bunge maalumu la Katiba.

Akizungumza na NIPASHE jana, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alisema, jumla ya asasi 600 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, zimeshawasilisha mapendekezo yao ya majina takribani 5, 400, Ikulu.

Kuhusu kutaja baadhi ya majina ambayo asasi hizo zimeyependekeza kwenda Ikulu, Balozi Sefue, alisema ofisi hiyo haina ruhusa ya kufanya hivyo labda asasi zenyewe ziamue kufanya hivyo kupitia vyombo vya habari.

“Jumla ya asasi 600 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, zimeshaleta majina ya watu 5, 400 zilizoyapendekeza. Mapendekezo yaliyoletwa ni mengi, kwani katika idadi hii, wanaotakiwa ni 2001, hivyo kazi ipo,” alisema na kuongeza:

“Kuhusu majina yaliyopendekezwa, hatuna ruhusa ya kufanya hivyo, labda kwa ridhaa yao wenyewe wanaweza kutangaza kwenye vyombo vya habari. Na sasa kazi tunayoendelea nayo ni uchambuzi wa majina hayo ili tumpelekee Rais, ambaye ndiye atakayejua watakaopaswa kuwa miongoni mwa wajumbe wa Bunge la Katiba.” 
CHANZO: NIPASHE 

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...