Thursday, November 21, 2013

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS NOVEMBA 21, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

MAZUNGUMZO YA NYUKLIA YA IRAN YAANZA

017216860_35400_0aad8.jpg
Catherine Ashton Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja (kushoto) na Waziri wa mambo ya nje wa Iran Mohammad Javad Zarif wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari mjini Geneva baada ya kushindwa kufikiwa kwa makubaliano. (10.11.2013).
Mazungumzo magumu yanaanza leo kati ya Iran na mataifa makubwa kutafuta makubaliano kwa mpango wa nyuklia wa Iran ambayo pia yatawaridhisha wanasiasa wa msimamo mkali huko Marekani, Israel na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Mazungumzo hayo yanafanyika Geneva wakati kukiwa na hali ya mvutano inayoongezeka Mashariki ya Kati ambapo waziri wa mambo ya nje wa Iran akiishutumu Israel kwa kujaribu kuvuruga mchakato huo kufuatia mirupuko miwili ya mabomu iliouwa takriban watu 23 nje ya ubalozi wa Iran mjini Beirut hapo jana.Wizara ya mambo ya nje ya Iran imeilaumu Israel na mamluki wake kwa kuhusika na miripuko hiyo.
Israel imekanusha madai hayo na Waziri Mkuu wake Benjamin Netanyahu leo hii anatarajiwa kuendeleza kampeni yake dhidi ya kufikia makubaliano ya nyuklia na Iran wakati atakapokutana na Rais Vladimir Putin wa Urusi mjini Moscow.

WAZIRI NCHIMBI, MWAKYEMBE WAFANYA KIKAO NA WATENDAJI WAKUU WA WIZARA ZAO JIJINI DAR

bc_b7ac1.jpg
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto-meza kuu) akizungumza na Watendaji Wakuu wa wizara yake pamoja na wa Wizara ya Uchukuzi katika Kikao cha utendaji kazi cha kuimarisha uhusiano kati ya wizara hizo kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi jijini Dar es Salaam. Kulia (meza kuu) ni Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
cd_03534.jpg
Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe (kulia-meza kuu) akizungumza na Watendaji Wakuu wa wizara yake pamoja na wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika Kikao cha utendaji kazi cha kuimarisha uhusiano kati ya wizara hizo kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi jijini Dar es Salaam. Kushoto (meza kuu) ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
ab_64f21.jpg
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akizungumza na Watendaji Wakuu wa wizara yake pamoja na wa Wizara ya Uchukuzi (hawapo pichani) katika Kikao cha utendaji kazi cha kuimarisha uhusiano kati ya wizara hizo kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe. Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Wednesday, November 20, 2013

EMMANUEL ADEBAYOR AONESHA UTAJIRI WAKE, JUMBA LA KIFAHARI, MAGARI NA NDEGE

1
Mchezaji wa Tottenham Hotspur Emmanuel Adebayor ni mmoja kati ya wachezaji matajiri sana Africa na anamiliki nyumba kwao Togo,Ghana,UK na Marekani.

00
Adebayor mwenye miaka 29 ametoa picha zake zikionyesha magari yake ya kifahari, private jet na vitu vingine vingine.
,5
Enjoy picha 15 kutoka kwa Adebayor ambaye siku chache zilizopita alikuwa kwenye harusi ya Peter wa P Square pamoja na Diamond Platnums.

0

WATU ZAIDI YA 50 WAFUKIWA BAADA YA JENGO KUPOROMOKA AFRIKA KUSINI

131119173308 jengo laporomoka sa 304x171 bbc nocredit f5726
Watu wawili wamefariki na wengine takriban watu 50 kukwama kwenye vifusi baada ya paa ya jumba la maduka lililokuwa linajengwa kuporomoka nchini Afrika Kusini.
Inaarifiwa watu 29 wameweza kuokolewa.
Taarifa zinazohusianaAfrika Kusini
Madaktari kutoka kampuni ya kibinafsi ya Netcare 911 walifika kutoa huduma ya kwanza katika eneo hilo la Tongaat Kaskazini mwa mji wa Durban.
"Shughuli hii itachukua mda mrefu. Itatuchukua muda kuwafikia wale waliokwama," alisema msemaji wa kampuni hiyo.
Hata hivyo ni mapema mno kujua sababu ya kuporomoka kwa jengo hilo.
Inaarifiwa watu wengine 26 wamepelekwa hospitalini wakiwa na majereha mabaya.
CHANZO BBC SWAHILI

LIST YA WASANII WALIOLIPWA PESA NYINGI DUNIANI 2012 - 2013

1348009969_madonna-gaga-467
List mpya kutoka Forbes inahusisha wasanii waliolipwa pesa nyingi duniani kwa kipindi cha June 2012 hadi June 2013 ambapo pesa hizo zinatokana na mauzo ya album, show(tour) na vitu vingine.
Wakongwe bado wapo kwenye list na Justin Bieber pamoja na umri wake mdogo lakini bado ameendelea kubaki kwenye top 10 ya list hii. List kamili hii hapa.....

1. Madonna – $125 million
2. Lady Gaga -  $80 million
3. Bon Jovi – $79 million
4. Toby Keith – $65 million
5. Coldplay – $64 million.
6.  Justin Bieber – $58 million
7. Taylor Swift – $55 million
8. Elton John – $54 million
9. Kenny Chesney – $53 million
9. Beyonce – $53 million (tie)

11. Sean “Diddy” Combs – $50 million
12. Sir Paul McCartney – $47 million
13. Calvin Harris – $46 million
14. Jennifer Lopez – $45 million
15. Roger Waters – $44 million
16. Muse – $43 million (tie)
16. Rihanna – $43 million (tie)
18. Jay Z – $42 million
18. One Direction – $42 million (tie)
20. Dr. Dre – $40 million
20. Red Hot Chili Peppers ($40 million, tie)
22. Rolling Stones – $39 million (tie)
22. Katy Perry – $39 million (tie)
24. Tim McGraw – $33 million (tie)
25. Pink – $32 million (tie)
25. Tiësto – $32 million (tie)

MSIMU WA SIKUKUU UMEWADIA TANGAZA BIASHARA YAKO NASI KWA BEI NAFUU

Kuza biashara yako msimu huu wa sikuu, kwa kutangaza na http://jambotz8.blogspot.com/

Piga simu no:- 0687 221198/ 0715 221198/ 0766 221198

MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 20, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

.

UFARANSA YAIPIGA UKRAINE 3-0 NA KUFUZU KOMBE LA DUNIA.

FRANCE_4c930.jpeg
Ufaransa imefanikiwa kufuzu kucheza Kombe la Dunia baada ya kuigeuzia kibao Ukraine na kuichapa mabao 3-0. Awali Ukraine ilishinda kwa mabao 2-0 ikiwa nyumbani na kuweka matumaini ya juu kusonga mbele katika mechi hiyo ya marudiano ugenini.
Lakini leo kwa mabao ya Mamadou Sakho aliyefunga mawili na Karim Benzema, Ufaransa imetinga fainali ya Kombe la Dunia. Ilionekana ni vigumu kwa Wafaransa kusonga mbele baada ya kufungwa mabao 2-0 katika mechi ya kwanza

Tuesday, November 19, 2013

KIWANDA CHA KUTENGENEZA VIYWAJI VIKALI CHAFUNGWA SHINYANGA

Kiwanda cha kutengeneza vinywaji cha Trully African kilichopo Mtanda Manispaa ya Shinyanga kimefungwa na Halmashauri ya mji huo kwa kutokidhi viwango vya ubora.... mengi kuhusu sakata hili endelea kusikiliza radio Faraja Fm na kutembelea mtanda huu wa jambotz8.blogspot.com.

Story na Steve Kanyeph na Isaac Edward Kisesa

MWANAFUNZI ANAYEDAI KUBAKWA NA KAPUYA HUYU HAPA AWEKEWA MTEGO NA KUBAINI MAMBO MAZITO

Denti anayedai kubakwa na Prof Kapuya akiongea na GPL.

MNYONGE mnyongeni haki yake mpeni, skandali ya kumbaka na kumwambukiza Ukimwi mwanafunzi, inamtafuna na kumuumiza Mbunge wa Urambo Magharibi (CCM), Juma Athuman Kapuya.
Kuhusu ukweli wa skendo hiyo, vyombo vya sheria vitazungumza lakini gazeti hili limejiridhisha pasipo shaka yoyote kuwa denti husika ni tapeli na anacheza rafu ili kumharibia Kapuya kwa maslahi yake.
Mbunge wa Urambo Magharibi (CCM), Profesa Juma Athuman Kapuya.
Gazeti hili, liliamua kumchunguza denti husika ili kumjua kiundani katika kutimiza ahadi ambayo Global Publishers Ltd, ilishaitoa kwenye Gazeti la Risasi, nakala ya Jumamosi iliyopita kuwa waandishi wake watafuatilia kinagaubaga na kuanika kila kitu kupitia magazeti yake, utekelezaji unaendelea.

JAMAA AUWA WAWILI NA KISHA KUJIUA YEYE MWENYEWE ILALA DAR LEO ASUBUHI

Mtu mmoja ambaye bado hajafahamika jina lake amewaua watu wawili kwa kuwapiga risasi ndani ya gari na kujeruhi mmoja kisha naye akajiua kwa risasi asubuhi hii jirani na Baa ya Wazee iliyopo Ilala, jijini Dar es Salaam!

Inadaiwa kuna gari ilikua inatoka ndani ya geti kutoka ikiwa na dereva mwanaume, abiria mwanamke mbele, na abiria wengine wawili wakiwa seat ya nyuma.

Pembeni hapo kulikua na jamaa kasimama. Inadaiwa alishushwa hapo dakika chache toka katika tax, walipotokeza abiria hao kupitia gari yao alitoa silaha yake na kupiga risasi gari akilenga zaidi abiria wa mbele pande zote kisha na nyuma. Baada ya kumaliza hapo muuaji huyo naye alijipiga risasi na kufariki hapo hapo.

Dereva na abiria wake wa mbele wamefariki dunia, huku abiria wa nyuma mmoja mama mtu mzima kajeruhiwa na risasi mgongoni na dada mwingine kujeruhiwa kwa kupigwa risasi mguuni.

Source: global publishers & Jamii Forums

WACHUNGAJI WAMKALIA KOONI MZEE WA UPAKO KUHUSU RAMBI RAMBI YA MAREHEMU MOSES KULOLA

WACHUNGAJI wa makanisa mbalimbali nchini wamemkalia kooni Mchungaji wa Kanisa la Maombezi, Antony Lusekelo maarufu kama Mzee wa Upako, kwa kumtaka atoe rambirambi aliyoahidi mbele ya umati wa watu siku ya kuaga mwili wa marehemu Askofu Moses Kulola Temeke, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mtu wa kamati iliyoratibu mazishi ya kiongozi huyo wa kanisa, viongozi wote wa dini walioahidi kutoa rambirambi hizo wametoa isipokuwa Lusekelo aliyeahidi kwa mbwembwe kutoa shilingi milioni 15.
Katibu Mkuu wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania, Mchungaji David Mwasota alisema anamheshimu Lusekelo kwani ni mtumishi wa Mungu, lakini ni bora angetimiza ahadi yake kama walivyofanya wenzake.

“Mzee wa Upako ni mtu mwenye jina kubwa kwenye jamii na kwa Mungu, hivyo anapaswa kuangalia kwa undani kile anachoahidi kwa muda unaotakiwa na amuache mke wa marehemu apumzike kwa kuwa ametokwa na mpendwa wake na bado hana nguvu,” alisema na kuongeza;

MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 19, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

KAGAME, MUSEVENI NA KENYATTA WASHTAKIWA KORTI YA JUMUIYA

kagamepx_deab7.jpg
Serikali za Rwanda, Uganda, Kenya na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, zimefunguliwa kesi katika Mahakama ya Afrika ya Mashariki, zikidaiwa kukiuka mkataba wa kuanzishwa kwa jumuiya hiyo.
Hatua hiyo inatokana na Serikali hizo kufanya vikao vitatu mfululizo na kuzitenga nchi za Tanzania na Burundi.
Walalamikaji katika kesi hiyo, ni Ally Msangi, David Makata na , John Adam, ambao ni Watanzania, wanaotetewa na wakili Mwandamizi, Jimm Obedi wa jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine, walalamikaji wamewaomba majaji katika mahakama hiyo, kutoa tamko la kusitisha utekelezaji wa maazimio yote ya vikao vya wakuu wa nchi hizo tatu.
Pia wameomba majaji watoe tamko la kukomesha kurejewa kwa vikao kama hivyo kinyume cha mkataba wa jumuiya hiyo.
Kesi hiyo ya aina yake, ilifunguliwa jana katika Mahakama ya Afrika ya Mashariki na kupokewa na Ofisa Masijala i katika mahakama hiyo, Boniface Ogoti.
Kufunguliwa kwa kesi hiyo, kunakuja siku kadhaa baada ya Rais Jakaya Kikwete kuzilalamikia nchi hizo, kuhusu kuitenga Tanzania kwa kufanya mikutano mbalimbali ya maendeleo ya nchi zao. Nchi nyingine iliyotengwa ni Burundi.
Kikao cha kwanza cha pamoja kilifanyika Aprili mjini Arusha kabla viongozi hao kukutana Juni 25 na 26 jijini Entebbe nchini Uganda, walidai kuwa na nia moja ya kurahisha mawasiliano katika nchi hizo.
Mkutano mwilingine ulifanyika mjini Kigali Rwanda Oktoba 28 ukiwajumuisha Rais Yoweri Museven wa Uganda, Uhuru Kenyatta (Kenya), Salva Kiir (Sudan Kusini) na Paul Kagame.
Wakili wa walalamikaji Obedi, alisema katika kesi ya msingi, wanawashtaki Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Rwanda, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Uganda,Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Kenya na Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...