Wednesday, November 20, 2013

LIST YA WASANII WALIOLIPWA PESA NYINGI DUNIANI 2012 - 2013

1348009969_madonna-gaga-467
List mpya kutoka Forbes inahusisha wasanii waliolipwa pesa nyingi duniani kwa kipindi cha June 2012 hadi June 2013 ambapo pesa hizo zinatokana na mauzo ya album, show(tour) na vitu vingine.
Wakongwe bado wapo kwenye list na Justin Bieber pamoja na umri wake mdogo lakini bado ameendelea kubaki kwenye top 10 ya list hii. List kamili hii hapa.....

1. Madonna – $125 million
2. Lady Gaga -  $80 million
3. Bon Jovi – $79 million
4. Toby Keith – $65 million
5. Coldplay – $64 million.
6.  Justin Bieber – $58 million
7. Taylor Swift – $55 million
8. Elton John – $54 million
9. Kenny Chesney – $53 million
9. Beyonce – $53 million (tie)

11. Sean “Diddy” Combs – $50 million
12. Sir Paul McCartney – $47 million
13. Calvin Harris – $46 million
14. Jennifer Lopez – $45 million
15. Roger Waters – $44 million
16. Muse – $43 million (tie)
16. Rihanna – $43 million (tie)
18. Jay Z – $42 million
18. One Direction – $42 million (tie)
20. Dr. Dre – $40 million
20. Red Hot Chili Peppers ($40 million, tie)
22. Rolling Stones – $39 million (tie)
22. Katy Perry – $39 million (tie)
24. Tim McGraw – $33 million (tie)
25. Pink – $32 million (tie)
25. Tiësto – $32 million (tie)

MSIMU WA SIKUKUU UMEWADIA TANGAZA BIASHARA YAKO NASI KWA BEI NAFUU

Kuza biashara yako msimu huu wa sikuu, kwa kutangaza na http://jambotz8.blogspot.com/

Piga simu no:- 0687 221198/ 0715 221198/ 0766 221198

MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 20, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

.

UFARANSA YAIPIGA UKRAINE 3-0 NA KUFUZU KOMBE LA DUNIA.

FRANCE_4c930.jpeg
Ufaransa imefanikiwa kufuzu kucheza Kombe la Dunia baada ya kuigeuzia kibao Ukraine na kuichapa mabao 3-0. Awali Ukraine ilishinda kwa mabao 2-0 ikiwa nyumbani na kuweka matumaini ya juu kusonga mbele katika mechi hiyo ya marudiano ugenini.
Lakini leo kwa mabao ya Mamadou Sakho aliyefunga mawili na Karim Benzema, Ufaransa imetinga fainali ya Kombe la Dunia. Ilionekana ni vigumu kwa Wafaransa kusonga mbele baada ya kufungwa mabao 2-0 katika mechi ya kwanza

Tuesday, November 19, 2013

KIWANDA CHA KUTENGENEZA VIYWAJI VIKALI CHAFUNGWA SHINYANGA

Kiwanda cha kutengeneza vinywaji cha Trully African kilichopo Mtanda Manispaa ya Shinyanga kimefungwa na Halmashauri ya mji huo kwa kutokidhi viwango vya ubora.... mengi kuhusu sakata hili endelea kusikiliza radio Faraja Fm na kutembelea mtanda huu wa jambotz8.blogspot.com.

Story na Steve Kanyeph na Isaac Edward Kisesa

MWANAFUNZI ANAYEDAI KUBAKWA NA KAPUYA HUYU HAPA AWEKEWA MTEGO NA KUBAINI MAMBO MAZITO

Denti anayedai kubakwa na Prof Kapuya akiongea na GPL.

MNYONGE mnyongeni haki yake mpeni, skandali ya kumbaka na kumwambukiza Ukimwi mwanafunzi, inamtafuna na kumuumiza Mbunge wa Urambo Magharibi (CCM), Juma Athuman Kapuya.
Kuhusu ukweli wa skendo hiyo, vyombo vya sheria vitazungumza lakini gazeti hili limejiridhisha pasipo shaka yoyote kuwa denti husika ni tapeli na anacheza rafu ili kumharibia Kapuya kwa maslahi yake.
Mbunge wa Urambo Magharibi (CCM), Profesa Juma Athuman Kapuya.
Gazeti hili, liliamua kumchunguza denti husika ili kumjua kiundani katika kutimiza ahadi ambayo Global Publishers Ltd, ilishaitoa kwenye Gazeti la Risasi, nakala ya Jumamosi iliyopita kuwa waandishi wake watafuatilia kinagaubaga na kuanika kila kitu kupitia magazeti yake, utekelezaji unaendelea.

JAMAA AUWA WAWILI NA KISHA KUJIUA YEYE MWENYEWE ILALA DAR LEO ASUBUHI

Mtu mmoja ambaye bado hajafahamika jina lake amewaua watu wawili kwa kuwapiga risasi ndani ya gari na kujeruhi mmoja kisha naye akajiua kwa risasi asubuhi hii jirani na Baa ya Wazee iliyopo Ilala, jijini Dar es Salaam!

Inadaiwa kuna gari ilikua inatoka ndani ya geti kutoka ikiwa na dereva mwanaume, abiria mwanamke mbele, na abiria wengine wawili wakiwa seat ya nyuma.

Pembeni hapo kulikua na jamaa kasimama. Inadaiwa alishushwa hapo dakika chache toka katika tax, walipotokeza abiria hao kupitia gari yao alitoa silaha yake na kupiga risasi gari akilenga zaidi abiria wa mbele pande zote kisha na nyuma. Baada ya kumaliza hapo muuaji huyo naye alijipiga risasi na kufariki hapo hapo.

Dereva na abiria wake wa mbele wamefariki dunia, huku abiria wa nyuma mmoja mama mtu mzima kajeruhiwa na risasi mgongoni na dada mwingine kujeruhiwa kwa kupigwa risasi mguuni.

Source: global publishers & Jamii Forums

WACHUNGAJI WAMKALIA KOONI MZEE WA UPAKO KUHUSU RAMBI RAMBI YA MAREHEMU MOSES KULOLA

WACHUNGAJI wa makanisa mbalimbali nchini wamemkalia kooni Mchungaji wa Kanisa la Maombezi, Antony Lusekelo maarufu kama Mzee wa Upako, kwa kumtaka atoe rambirambi aliyoahidi mbele ya umati wa watu siku ya kuaga mwili wa marehemu Askofu Moses Kulola Temeke, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mtu wa kamati iliyoratibu mazishi ya kiongozi huyo wa kanisa, viongozi wote wa dini walioahidi kutoa rambirambi hizo wametoa isipokuwa Lusekelo aliyeahidi kwa mbwembwe kutoa shilingi milioni 15.
Katibu Mkuu wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania, Mchungaji David Mwasota alisema anamheshimu Lusekelo kwani ni mtumishi wa Mungu, lakini ni bora angetimiza ahadi yake kama walivyofanya wenzake.

“Mzee wa Upako ni mtu mwenye jina kubwa kwenye jamii na kwa Mungu, hivyo anapaswa kuangalia kwa undani kile anachoahidi kwa muda unaotakiwa na amuache mke wa marehemu apumzike kwa kuwa ametokwa na mpendwa wake na bado hana nguvu,” alisema na kuongeza;

MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 19, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

KAGAME, MUSEVENI NA KENYATTA WASHTAKIWA KORTI YA JUMUIYA

kagamepx_deab7.jpg
Serikali za Rwanda, Uganda, Kenya na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, zimefunguliwa kesi katika Mahakama ya Afrika ya Mashariki, zikidaiwa kukiuka mkataba wa kuanzishwa kwa jumuiya hiyo.
Hatua hiyo inatokana na Serikali hizo kufanya vikao vitatu mfululizo na kuzitenga nchi za Tanzania na Burundi.
Walalamikaji katika kesi hiyo, ni Ally Msangi, David Makata na , John Adam, ambao ni Watanzania, wanaotetewa na wakili Mwandamizi, Jimm Obedi wa jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine, walalamikaji wamewaomba majaji katika mahakama hiyo, kutoa tamko la kusitisha utekelezaji wa maazimio yote ya vikao vya wakuu wa nchi hizo tatu.
Pia wameomba majaji watoe tamko la kukomesha kurejewa kwa vikao kama hivyo kinyume cha mkataba wa jumuiya hiyo.
Kesi hiyo ya aina yake, ilifunguliwa jana katika Mahakama ya Afrika ya Mashariki na kupokewa na Ofisa Masijala i katika mahakama hiyo, Boniface Ogoti.
Kufunguliwa kwa kesi hiyo, kunakuja siku kadhaa baada ya Rais Jakaya Kikwete kuzilalamikia nchi hizo, kuhusu kuitenga Tanzania kwa kufanya mikutano mbalimbali ya maendeleo ya nchi zao. Nchi nyingine iliyotengwa ni Burundi.
Kikao cha kwanza cha pamoja kilifanyika Aprili mjini Arusha kabla viongozi hao kukutana Juni 25 na 26 jijini Entebbe nchini Uganda, walidai kuwa na nia moja ya kurahisha mawasiliano katika nchi hizo.
Mkutano mwilingine ulifanyika mjini Kigali Rwanda Oktoba 28 ukiwajumuisha Rais Yoweri Museven wa Uganda, Uhuru Kenyatta (Kenya), Salva Kiir (Sudan Kusini) na Paul Kagame.
Wakili wa walalamikaji Obedi, alisema katika kesi ya msingi, wanawashtaki Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Rwanda, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Uganda,Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Kenya na Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo.

Monday, November 18, 2013

UFOO SARO: NI MIUJIZA YA MWENYEZI MUNGU TU NDIYO ILIYONIWEZESHA KUEPUKA KIFO.

Mwandishi wa habari wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro akisoma somo kwenye biblia  wakati wa ibada maalumu ya shukrani kwenye Kanisa la (KKKT ) Usharika wa Kibamba nje kidogo ya Jiji la Dare Salaam jana. Picha na Sanjito Msafiri.  
******
DAR ES SALAAM. 
MTANGAZAJI wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro ambaye alijeruhiwa kwa kupigwa risasi na mzazi mwenzake, Anthery Mushi, amefanya ibada na kusema: “Namshukuru Mungu kwa kumponya.”
Ni mara ya kwanza Saro kuzungumza tukio hilo tangu aliporuhusiwa kutoka Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu, MOI ya Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa.

Katika ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa la Kilutheli Tanzania (KKKT) Usharika wa Kibamba, Jimbo la Magharibi, Ufoo huku akitokwa na machozi na wakati mwingine kushindwa kuzungumza alisema: “Ni miujiza tu ya Mungu yeye kunifanya mimi kuwa hai leo.”

Mtangazaji huyo ambaye alilazwa kwa zaidi ya wiki mbili, aliwashukuru watu wote waliomtia moyo, kumsaidia kipindi chote alichokuwa mgonjwa.

'KACHAA' BALOTELLI AFURAHIA KUREJEA ENGLAND

balotel_94581.jpg
Siku za furaha: Mario Balotelli akiwa mwenye furaha wakati wa mazoezi ya Italia Uwanja wa Craven Cottage jana
'KACHAA' Mario Balotelli alikuwa mwenye furaha aliporejea England wakati mshambuliaji huyo wa AC Milan alipokuwa akifanya mazoezi na kikosi cha Italia Magharibi mwa London.
Balotelli aliichezea Manchester City kabla ya kutibuana na aliyekuwa kocha wa timu hiyo Roberto Mancini na wachezaji wenzake kadhaa hivyo kuondoka, lakini nyota huyo mwenye umri wa miaka 23, aliyeondoka Etihad miezi 10 iliyopita, alikuwa mtulivu jana.
Kikosi cha The Azurri kinaendelea na maandalizi ya Fainali za Kobe la Dunia mwakani nchini Brazil na leo usiku kitacheza mechi ya kirafiki na Nigeria, kwenye Uwanja wa Fulham, Craven Cottage.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 18, 2013

DSC 0080 9c6c1
DSC 0081 b7da2

Sunday, November 17, 2013

TAIFA STARS SASA KUIKABILI ZIMBABWE J4

Taifa Stars sasa inacheza na Zimbabwe mechi ya Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA)- FIFA Date itakayofanyika keshokutwa Jumanne (Novemba 19 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Awali Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ilikuwa icheze na Kenya (Harambee Stars), lakini Shirikisho la Mpira wa Miguu Kenya (FKF) lilituma taarifa jana jioni (Novemba 16 mwaka huu) likieleza kuwa timu yake haitacheza tena mechi hiyo.

Kikosi cha Zimbabwe chenye msafara wa watu 30 kinatarajia kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) kesho (saa 3 asubuhi) tayari kwa mechi hiyo itakayochezwa kuanzia saa 11 kamili jioni.

NIGERIA YA KWANZA KUKATA TIKETI YA BRAZIL 2014 BAADA YA KUIFUMUA ETHIOPIA 2-0

article-2508386-1973888200000578-737_634x423_5ac75.jpg
Timu ya taifa ya Nigeria imekua nchi ya kwanza ya Afrika kukata tiketi ya kecheza. Fainali za Kombe la Dunia mwakani baada ya ushindi wa mabao 2-0 nyumbani dhidi ya Ethiopia leo. Victor Moses alifunga kwa penalti dakika ya 20 na Victor Obinna akaongeza la pili dakika ya 82 kwa mpira wa adhabu, hivyo Super Eagles kufuzu kwa ushindi wa jumla wa 4-1, baada ya awali kushinda 2- mjini Addis Ababa mwezi uliopita katika mchezo wa kwanza

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...