Thursday, October 24, 2013

ZIARA YA WAZIRI MKUU MHE. MIZENGO PINDA CHENGDU - CHINA

IMG_0119
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda na mkewe Tunu wakipata maelezo kuhusu kiwanda cha kutengeneza maligafi za viwanda vya plastiki cha Hongda Chlor alkali Chemical Base cha Chengdu nchini China akiwa katika ziara ya kikazi Oktoba 22, 2013,. Kushoto ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Abdallah Kigoda. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) IMG_0427
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda akizungumza na viongozi wa kampuni ya Dalian International ya China kwenye hoteli ya Shangri-la, Chengdu akiwa ktika ziara nchini China. Oktoba 22, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
IMG_0496
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda akikagua eneo la Mradi wa umwagiliaji la Dujiangyan lililopo Chengdu nchini China akiwa kaika ziara nchini humo Oktoba 22,2013.(Picha naOfisi yaWairi Mkuu)
 IMG_0573
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda akitia saini kitabu cha wageni baada ya kutembelea mradi wa umwagiliaji wa Dujiangyan uliopo Chengdu nchini China akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo   Oktoba 22, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Monday, October 21, 2013

TUME YA WARIOBA YAOMBA MUDA ZAIDI

warioba_1_bc902.jpg
Tume ya Mabadiliko ya Katiba imeomba kuongezewa muda wa mwezi mmoja kutokana na ugumu wa kazi ya uchambuzi wa maoni yaliyotolewa na wananchi na asasi mbalimbali.
Tume hiyo inayoongozwa na Jaji Joseph Warioba ilitakiwa kufanya kazi kwa miezi 18 kwa mujibu wa Sura ya 83 ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.
Maana yake ni kuwa Tume hiyo iliyoanza kazi Mei 1, mwaka jana ilitakiwa kukamilisha kazi yake Novemba 1, mwaka huu.
Ikiwa maombi hayo ya Tume yatakubaliwa ina maana watatakiwa kukabidhi ripoti yake Desemba 1, mwaka huu.
Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Augustine Ramadhan aliliambia gazeti hili kwa simu jana kuwa wamepeleka serikalini maombi ya kuongezewa muda wa kufanya kazi.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU OKTOBA 21, 2013

DSC 0057 aae29
DSC 0058 6a210

Sunday, October 20, 2013

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOBA 20, 2013

.

.

KENYATTA ARUHUSIWA KUTOHUDHURIA BAADHI YA VIKAO VYA KESI


017113680_35400_1b04e.jpg
Mahakama ya ICC jana Ijumaa(18.10.2013)ilimruhusu kwa kiasi fulani Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kutohudhuria baadhi ya vikao vya kesi dhidi yake, ili kumpa muda wa kushughulikia majukumu ya kisiasa.
Kenyatta , ambaye alichaguliwa kuwa rais mwezi Machi mwaka huu, amekuwa akidai kwa muda mrefu sasa kuwa kesi hiyo mjini The Hague itazuwia uwezo wake wa kuiongoza nchi.
"Mahakama hiyo kimsingi inamuondolea Uhuru Kenyatta ulazima wa kuwapo wakati wote katika kesi dhidi yake inayoanza Novemba 12, imesema mahakama hiyo ya ICC katika taarifa, lakini ikasisitiza kuwa ni lazima afike kwa ajili ya ufunguzi wa kesi hiyo.
Majaji wamesema kuwa ruhusa ya Kenyatta inatolewa kwa misingi kwamba anaweze kutimiza majukumu aliyonayo kama rais wa Kenya, na sio kwasababu ya kutoa hadhi kwa kazi yake kama rais.
Atakuwapo wakati wa kutoa ushahidi
Mahakama hiyo iliyoko nchini Uholanzi pia inasisitiza kuwa Kenyatta anapaswa kuwapo wakati pande zote zitakapokuwa zinatoa taarifa zao za mwisho katika kesi hiyo, wakati wahanga wanatoa ushahidi wao na pia,iwapo kutakuwa na haja wakati wa kikao cha kutoa hukumu.

MSHAHARA WA RAIS KAA LA MOTO


jk 17ab9
Siku chache baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe kutaja hadharani mishahara ya Rais Kikwete na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, serikali imekataa kuizungumzia mishahara hiyo.
Msimamo wa Serikali kutotaja mishahara ya viongozi wakuu unatofautiana na utamaduni wa nchi nyingine kama Marekani, Afrika Kusini, Ufaransa na Kenya ambazo mishahara ya wakuu wake huwekwa wazi kwa umma.
Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema akiwa wilayani Igunga Mkoani Tabora, alisema Rais Kikwete anapokea zaidi ya Sh30 milioni kwa mwezi (sawa na Sh360 milioni kwa mwaka) ikiwa ni marupuru na mshahara kwa mwezi bila kodi, huku Pinda akipokea Sh 26 milioni kwa mwezi.
Akizungumza na Mwananchi kwa simu jana, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina Kombani alisema kiongozi yeyote haruhusiwi kutaja mshahara wa mtu mwingine kwa kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria ya utumishi wa umma.
"Kuutaja mshahara wa mtu mwingine ni kinyume cha sheria na kosa, siyo utaratibu. Kwani wewe upo tayari watu waujue mshahara wako?" alihoji.

MATOKEO YA LIGI KUU YA UINGEREZA

2816039_orig_51785.jpg
Source: bongostaz

Friday, October 18, 2013

PAPII KOCHA, BABU SEYA...... NAFASI YA MWISHO, WANAHITAJI SALA NA DUA ZETU

 

Na Mwandishi Wetu

KITENDO cha Mahakama ya Rufaa kukubali kusikiliza marejeo ya hukumu ya kifungo cha maisha jela katika kesi iliyokuwa ikimkabili mwanamuziki Nguza Viking ‘Babu Seya’ na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ kimetafsiriwa kuwa ni kama wamepata nafasi ya mwisho ya kuweza kujinasua.


WARAKA WA PAPII KOCHA
Mahakama hiyo ilikubali ombi hilo hivi karibuni na kueleza kuwa marejeo hayo yanatarajiwa kusikilizwa Oktoba 30, mwaka huu ikiwa ni miezi kadhaa baada ya Papii Kocha kutuma waraka wa kuomba msamaha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu ndiye aliyekubali kuufikisha kwa JK hivyo kuna madai kuwa huenda waraka huo ndiyo umezaa matunda.
 
WARAKA UMEZAA MATUNDA?
“Unajua ule waraka ulikuwa na maneno ya kuumiza sana. Inawezekana kabisa kuwa ulimfikia JK akaagiza suala hilo liangaliwe upya. Haina maana kuwa JK anaingilia sheria. Nadhani wanasheria wana vipengele vingi ambavyo vinaruhusu marejeo ya rufaa hiyo. Kilichopo hapa ni namna ya kuzitafsiri sheria kisha kuona kama rufaa hiyo inaweza kusikilizwa.

SAKATA LA UFOO SARO LACHUKUA SURA MPYA UPANDE WA WAKWE...!!!



UTATA wa risasi umegubika tukio la kifo cha mzazi mwenzake na mwandishi wa habari wa ITV, Ufoo Saro, marehemu Anthery Mushi, aliyejiua kwa kujipiga risasi. Utata huo umeibuka baada ya ndugu wa marehemu Mushi kushangazwa na kuhoji mazingira ya kifo cha ndugu yao anayedaiwa kujipiga risasi mbili kidevuni na kupoteza maisha papo hapo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, jana Msemaji wa familia hiyo ambaye pia ni kaka wa marehemu, Isaya Mushi alisema familia imebaki kizani juu ya kifo cha ndugu yao na kwamba anayejua siri nzito juu ya kifo hicho ni mzazi mwenzake, Ufoo.

Isaya, alisema mazingira ya kifo cha Mushi ni ya kutatanisha kwani baada ya mwili wake kufanyiwa uchunguzi na madaktari, zilitolewa risasi mbili kichwani, huku wakihoji risasi ya pili.

Kwa mujibu wa wataalamu waliobobea katika silaha, ni vigumu mtu kujiua kwa risasi mbili katika eneo la kichwa kwa maelezo kuwa risasi moja inatosha kumaliza uhai wa mtu katika eneo hilo.

“Sisi kama familia bado tukio hili linatupa utata, hivyo tunaomba Jeshi la Polisi litumie busara katika kufanya uchunguzi wa kina kwani, Mushi haiwezekani akajipiga risasi kidevuni ikanasa kwenye ubongo, halafu akajipiga tena kidevuni upande wa kushoto… imetushangaza na hatuelewi tukio hili,” alisema Mushi.


Alisema wanafahamu fika maisha aliyoishi kijana wao kwani alikuwa ni mtaratibu, hivyo maamuzi aliyoyachukua yalikuwa magumu.

“Kijana wetu enzi za uhai wake alikuwa ni mtaratibu, hivyo maamuzi aliyoyachukua yalikuwa ni magumu mno na mwenye siri hiyo ni mzazi mwenzake Ufoo, tuna imani ataeleza,” alisema Mushi.

ASKARI JKT WATEMBEZA KICHAPO KWA RAIA


Msemaji wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Erick Komba
*******
Vurugu kubwa zilizopelekea mapambano makali kati ya wakazi wa kijiji cha Maramba wilayani Mkinga Mkoa wa Tanga na askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kikosi cha Maramba  na kusababisha watu 15  wakazi wa kijiji kujeruhiwa vibaya baada ya kupewa kipigo kutoka kwa askari hao.

Msemaji wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Erick Komba,  alithibitisha  kutokea kwa vurugu hizo ambazo zilianza baada ya kumalizika kwa mechi ya soka kati ya timu ya JKT Maramba na Maramba City inayoundwa na wakazi wa kijiji hicho.

Komba alisema viongozi wa JKT kikosi cha Maramba wapo katika harakati za kutafuta chanzo cha vurugu hizo na kwamba hakuna  athari iliyotokea wala wananchi kujeruhiwa katika mapambano hayo.

MUME AMKATA MKEWE MKONO KISA WIVU WA MAPENZI


Majeruhi Leah Clement (24), akiuguza jeraha lake wodini katika Hospitali Teule ya Wilaya Geita kwa madai ya kukatwa mkono wake wa kushoto na mumewe.(PICHA:RENATUS MASUGULIKO)
Mwanamke mkazi wa kijiji cha Nyamikoma Kata ya Bugarama Wilaya ya Geita, Leah Clement (24), anadaiwa kukatwa mkono wake wa kushoto na mumewe kutokana na wivu wa mapenzi.
Hivi sasa mwanamke huyo amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Geita akiendelea kupatiwa matibabu.
Aidha, mtuhumiwa wa ukatili huo, anadaiwa ametoroka na kwenda kujichimbia kwa `sangoma' kwa imani kwamba hatakamatwa.

Tukio hilo lilitokea Oktoba 9, mwaka huu saa 1:30  usiku katika kijiji cha Chifufu kata ya Bugarama wilayani Geita.

Imeelezwa kwamba mtuhumiwa huyo alikwenda jikoni kwa mkewe na kukuta akisonga ugali kisha akamvamia na kumshambulia kwa panga lengo likiwa ni kumkata shingo yake.

RIPOTI YA MO IBRAHIM: RWANDA, TANZANIA ZINA UTAWALA BORA ZAIDI EAC

Kagame Kikwete2
Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete (kushoto)  na Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame, nchi zao zimetajwa kuwa na utawala bora katika jumuiya ya Afrika mashariki
……………………………………………………………………………………………………………………………
Mahmoud Ahmad Arusha
Tasisi ya Mo Ibrahim juu ya Utawala Bora Afrika, imebaini nchi za Rwanda na Tanzania kuwa nchi zenye utawala bora zaidi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kati ya nchi 52 za kiafrika.
Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa Jumatatu na taasisis ya Mo Ibrahim imesema Rwanda imepata wastani wa asilimia 57.8 ikiwa ni zaidi ya wastani wa kiafrika wa asilimia 51.6.
Hii inamaanisha kwamba nchi hiyo imeboresha utawala bora kwa zaidi ya asilimia 10.9 tangu mwaka 2000, ikiwa nafasi ya kwanza kwa nchi za Afrika mashariki ikifuatiwa na Tanzania iliyoshika nafasi ya 17 barani Afrika kwa kupata asilimia 56.9 huku Uganda ikiwa ya tatu ECA kwa kuwa ya 18 kwa kupata asilimia 56. Kenya imekuwa ya 21 na kushika nafasi ya nne kwa kupata asilimia 53.6 huku Burundi iliyopata asilimia 43.8 ikishika nafasi tano kwa EAC.

MWANAFUNZI AUNGUZWA MAKALIO KISA KAPOTEZA MBUZI

Untitled 22
Mwanafunzi wa darasa la nne shule ya msingi Bukokwa,  Wilaya ya Sengerema  mkoani Mwanza Cristina John (13)  aliyeunguzwa na jiko la mkaa na dada yake Paulina John baada ya kupoteza Mbuzi aliyekuwa malishoni.
Untitled 33
Paulina John  aliyefanya unyama wa kumuunguza mdogo wake Cristina John bila huruma na hajachukuliwa hatua zozote za kisheria huku vyombo vya dola vipo na vinafanya kazi.(picha na Daniel Makaka, Sengerema).
Na. Daniel Makaka, Sengerema.
Mwanafunzi mmoja  aitwaye Cristina John  mwenye umri wa miaka 13, ambaye anasoma darasa la nne 4,  katika shule ya msingi Bukokwa iliyopo kata ya Nyakarilo wilayani Sengerema ameunguzwa  jiko lilokuwa na mkaa wa moto na dada yake.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Afisa mtendaji wa kijiji hicho Bwn. Timoth John  wakati akiongea na redio Sengerema hivi karibuni amesema kuwa, mtoto huyo ameunguzwa  na  jiko hilo lililokuwa na mkaa wa moto katika makalio yake ikiwemo sehemu zingine za mwili wake, kwakile kilichoelezwa kuwa  alipoteza mbuzi wakati akiwa amewapeleka malishoni.
 
Amefahamika kuwa tukio hilo limebainika baada ya  mtoto huyo kuomba msaada wa kupelekwa hospitalini kupatiwa matibabu, kutokana na  maumivu yaliyosababishwa na majeraha aliyoyapata.
 
Imeelezwa kuwa baada ya kutoa taarifa kwa wananchi wasamalia wema walimchukua na kumpeleka  katika zahanati ya kijiji hicho, na kupatiwa matibabu na baadaye taarifa hizo walizifikisha kwa Afisa mtendaji wa kijiji hicho, huku wakilaani kitendo hicho  kuwa ni cha kinyama na mhusika anapaswa kufikishwa katika vyombo vya dola.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 18, 2013



DSC 0012 f3426
DSC 0013 769e6

WAKIMBIZI WA SIRYA WATESEKA MISRI

AleppoCivilians_31072012_de2da.jpg
Shirika la kimataifa Amnesty International,linasema kuwa maafisa nchini Misri wanawazuilia mamia ya wakimbizi wa Syria katika mazingira mabaya sana.
Wakimbizi hao wanatoroka vita vinavyoendelea Syria.
Katika ripoti yake mpya, shirika hilo linasema kuwa idadi kubwa ya watoto wanazuiliwa wengi wakiwa hawana wazazi.
Kwa mujibu wa shirika hilo, baadhi ya wakimbizi wamezuiliwa katika vituo vya polisi ambako hali ni duni wengi wakiwa hawapati chakula wala matibabu kwa walio wagonjwa.
Linasema kuwa mjini Alexandria , mapacha wawili wenye mwaka mmoja walipatikana miongoni mwa wale waliozuiliwa.
Maafisa wa utawala bado hawajajibu tuhuma za shirika hilo.
Misri imekuwa ikikumbwa na vurugu za kisiasa tangu kuondolewa mamlakani kwa aliyekuwa Rais Hosni Mubarak mwaka 2011.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...